< 1 Kings 6 >

1 480 years after the Israeli people left Egypt, during the fourth year that Solomon ruled Israel, early in May, Solomon’s workers began to build the temple.
Kwa hiyo Sulemani akaanza kulijenga hekalu. Hii ilikuwa mwaka wa 480 baada ya wana wa Israeli kutoka katika nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa utawala wa Sulemani huko Israeli, katika mwezi wa Ziv, ambao ndio mwezi wa pili.
2 Inside, [the main part of] the temple was 90 feet long, 30 feet wide, and 45 feet high.
Hekalu ambalo mfalme Sulemani alimjengea BWANA lilikuwa na urefu wa mita 27, na upana wa mita 9, na kimo cha mita 13. 5.
3 The entrance room was 15 feet long and 30 feet wide, just as wide as the main part of the temple.
Na ukumbi uliokuwa mbele ya hekalu ulikuwa na urefu wa mita 9 na upana wa mita 4. 5 sawa na upana wa sehemu kuu ya hekalu.
4 There were windows in [the walls of] the temple. The windows were narrower on the outside than on the inside.
Lile hekalu alilitengenezea madirisha ambayo fremu zake kwa nje yalifanya yaonekane membamba kuliko ile sehemu ya ndani.
5 Against the two sides and against the back of the temple walls, they built a structure/building that had rooms in it. [This structure had three levels/stories and each was 7-1/2 feet high].
Na ukuta wa nyumba aliuzungushia vyumba kuzunguka pande zake, kushikamana na vyumba vya nje na vya ndani ya hekalu. Akajenga vyumba katika pande zote.
6 [Each room in] the lowest level/story was 7-1/2 feet wide. [Each room in] the middle level/story was nine feet wide. [The rooms in] the top level/story were 10-1/2 feet wide. The wall of the temple at the top level/story was thinner than the wall at the middle level/story, and the wall of the middle level/story was thinner than the wall at the bottom level/story. The result was that the rooms could be supported by the wall underneath them, and did not require wooden beams to support them.
Kile chumba cha chini kilikuwa na upana wa mita 2. 3, kile cha kati kilikuwa na upana wa mita 2. 8. na kile cha tatu kilikuwa na upana wa mita 3. 2. upande wa nje akaupunguza ukuta wa nyumba pande zote, ili boriti zisishikamane ukutani mwa nyumba.
7 The huge stones for [the foundation of] the temple were cut and shaped at the quarry [to become very smooth]. The result was that while the workers were building the temple there was no noise, because they did not use hammers or chisels or any other iron tools there.
Hekalu lilijengwa kwa mawe yaliyokuwa yamechongwa chimboni. Hakuna nyundo, wala shoka au chombo chochote cha chuma kilisikika wakati hekalu lilipokuwa likjengwa.
8 The entrance to the bottom level/story [of that attached structure] was on the south side of the temple. There were stairs from the bottom level/story to the middle and top level/story.
Upande wa kusini wa hekalu kulikuwa na lango la chini, ambalo mtu hupanda kwa madaraja mpaka juu kwenye chumba cha kati, na kutoka chumba cha kati hadi chumba cha tatu.
9 So Solomon’s [workers] finished building the [framework of the] temple. They made the ceiling from cedar beams and boards.
Kwa hiyo Sulemani akalijenga hekalu mpaka akalimaliza, akalifunika hekalu kwa boriti na mbao za mwerezi.
10 They built the structure that had three levels/stories, that was against the walls of the temple. Each level/story was 7-1/2 feet high, and was joined to the temple with cedar beams.
Akajenga vyumba vya pembeni mwa hekalu, kila upande mita 2. 3 kwenda juu. Navyo vikaunganishwa na hekalu kwa mbao za mierezi.
11 Then Yahweh said this to Solomon:
Neno la BWANA likamjia Sulemani, likisema,
12 “[I want to tell you] about this temple that you are building. If you continually obey all my statutes and laws and commands, I will do for you what I promised to your father David.
“Kuhusu hili hekalu ambalo unajenga, kama utatatembea katika maagizo yangu na kuhukumu kwa haki, na kutunza amri zangu na kuishi kwa hizo, ndipo ntakapozithibitisha ahadi zangu na wewe ambazo niliziahidi kwa baba yako Daudi.
13 I will live among the Israeli people, [in this temple, ] and I will never abandon them.”
Nitaishi kati ya watu wa Israeli nami sitawatupa.”
14 Solomon’s [workers] finished building the temple.
Kwa hiyo Sulemani akalijenga hekalu mpaka akalimaliza.
15 On the inside, they lined/covered the walls with cedar boards. They lined/covered them from the floor to the ceiling. They made the floor from cypress boards.
Kisha akajenga kuta za ndani za hekalu kwa mbao za mwerezi. Kuanzia sakafu ya hekalu hadi boriti za juu, kwa ndani akazifunika kwa miti, na akaifunika sakafu kwa mbao za miberoshi.
16 Inside the back part of the temple they built an inner room, called the Very Holy Place. It was 30 feet long. All the walls of this room were lined with cedar boards.
Alijenga mita 9 ndani ya hekalu kwa mbao za miberoshi kutoka sakafuni hadi juu. Hiki ni chumba cha ndani, cha patakatifu sana.
17 In front of the Very Holy Place there was a room that was 60 feet long.
Ule ukumbu mkuu, ulikuwa mahali pakatifu amabao ulikuwa mbele ya patakatifu sana, ulikuwa wa mita 18. hapo kulikwa na mbao za mwerezi ndani ya hekalu, zilizokuwa zimechongwa kwa sura ya vibuyu na maua yaliyochanua.
18 The cedar [boards on the walls] inside the temple were decorated with carvings of gourds and flowers. [The walls were] completely covered with cedar boards, with the result that the stones [of the walls behind them] could not be seen.
Zote zilikuwa za mierezi kwa ndani. Hapakuonekana chochote ndani kilichokuwa kimetengenezwa kwa mawe.
19 At the back of the temple they made the Very Holy Place, where the Sacred Chest would be put.
Sulemani alitengeneza kile chumba cha ndani kwa lengo la kuweka sanduku la agano la BWANA.
20 That room was 30 feet long, 30 feet wide, and 30 feet high. They covered the walls with [very thin sheets of] pure gold. [For burning incense] they also made an altar of cedar [boards].
Kile chumba cha ndani kilikuwa na upana wa mita 9, na kimo cha mita 9. Sulemani alizifunika kuta kwa dhabahu na madhabahu aliifunika kwa mbao za mierezi.
21 Solomon told them to cover the other walls inside the temple with [very thin sheets of] pure gold and to fasten gold chains across the entrance to the Very Holy Place.
Sulemani alifunika ndani ya hekalu kwa dhahabu safi na akaweka mikufu ya dhahabu iliyopita mbele ya chumba cha ndani, na kulifunika eneo la mbele kwa dhabahu.
22 They covered all the walls of the temple and the altar that was outside the Very Holy Place with [very thin sheets of] gold.
Akalisakafia kwa dhahabu eneo lote la ndani mpaka akamaliza hekalu lote. Pia akalisakafia kwa dhahabu madhahabu yote ya chumba cha ndani.
23 Inside the Very Holy Place, they made from olive tree wood [large statues of] two creatures with wings. Each one was 15 feet tall.
Sulemani akatengeneza makerubi mawili kwa mbao za mizeituni, kila moja lilikuwa na kimo cha mita 4. 5 kwa ajili ya chumba cha ndani.
24 They each were the same size and had the same shape. They each had two wings [which were spread out]. Each wing was 7-1/2 feet long, with the result that the distance between the outer ends of the two wings was 15 feet.
Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa mita 2. 3. Kwa hiyo kutoka ncha ya bawa moja hadi ncha ya bawa lingine kulikuwa na umbali wa mita 4. 5. Yule
kerubi mwingine naye alikuwa na bawa lenye kipimo cha mita 4. 5 Makerubi hawa walikuwa wanafanana kwa umbo na kwa vipimo.
Kimo cha kerubi mmoja kilikuwa mita 4. 5 na yule wa pili alikuwa hivyo hivyo.
27 They put those statues next to each other in the Very Holy Place so that the wing of the one touched the one wing of the other in the center of the room, and the outer wings touched the walls.
Sulemani aliwaweka hao kerubi kwenye chumba cha patakatifu sana. Bawa moja la kerubi lilikuwa limeenea kiasi kwamba bawa moja liligusa ukuta huu na bawa la yule wa pili nalo liligusa ukuta wa upande mwingine. Hayo mabawa yalikuwa yanakutana katikati ya chumba cha patakatifu sana.
28 They covered the statues with [very thin sheets of] gold.
Sulemani aliwafunika hao kerubi kwa dhahabu.
29 [Solomon told them to] decorate the walls of the main room and the Very Holy Place by carving representations of winged creatures and palm trees and flowers.
Akazinakshi kuta zote kwa sura za makerubi, miti ya mitende, na maua yaliyochanua, kwa vyumba vya nje na vya ndani.
30 They also covered the floor of both rooms with [very thin sheets of] gold.
Sulemani akalisakafia hekalu kwa dhahabu, kwa vyumba vyote vya ndani na vya nje.
31 They made a set of doors from olive tree wood, and placed them at the entrance to the Very Holy Place. The doorposts joined at the top to form a pointed arch.
Sulemani akatengeneza milango ya mbao za mizeituni kwenye lango la kuingia ndani. Aliweka vizingiti na miimo kwenye pande tano.
32 The doors were decorated by carving on them representations of winged creatures, palm trees, and flowers. All of these things were covered with [very thin sheets of] gold.
Kwa hiyo akatengeneza na milango miwili ya mizeituni, na akainakshi kwa makerubi, na mitende, na maua yaliyochanua. Akasakafia kwa dhahabu na akatandaza dhahabu kwenye makerubi na kwenye mitende.
33 They made a rectangular door frame from olive tree wood, and put it [between the entrance room and] the main room.
Kwa njia hii, akalitengenezea hekalu miimo miwili ya mbao za mizeituni yenye pande nne
34 They made two folding doors from cypress wood [and fastened them to the door frame].
na milango miwili ya mbao za mierezi. Zile mbao mbili za mlango mmoja zilikuwa zikijikunja na mbao mbili za mlango wa pili nazo zilikuwa zikijikunja pia.
35 The doors were also decorated with wood carvings of winged creatures, palm trees, and flowers, and they were also covered evenly with [very thin sheets of] gold.
Akazinakshi kwa makerubi, mitende, na maua yaliyochanua, na pia akazisakafia kwa dhahabu juu ya zile nakshi.
36 They built a courtyard in front of the temple. The walls around the courtyard were made of cedar and stone; to make the walls, between each layer of cedar beams they put down two layers of stone.
Akalijengs Korido la ndani kwa safu tatu za mawe ya kuchongwa na safu moja ya mhimili wa mierezi.
37 They laid the foundation of the temple of Yahweh in early May, in the fourth year [that Solomon ruled].
Msingi wa hekalu ulijengwa katika mwaka wa nne, wa mwezi wa Ziv.
38 In the eleventh year [that he ruled], in the middle of October, they finished building the temple and all of its parts, doing exactly what Solomon told them to do. It required seven years to build it.
Mwaka wa kumi na moja mwezi wa Buli, ambao ndio mwezi wa nane, sehemu zote za hekalu zilimalizika na sharti zake zote. Sulemani alilijenga hekalu kwa miaka saba.

< 1 Kings 6 >