< 1 Kings 12 >
1 All [HYP] the people of [northern] Israel went to Shechem [city] in order to appoint Rehoboam to be their king. So Rehoboam also went there.
Rehoboamu akaenda Shekemu, kwa kuwa Waisraeli wote walikuwa wamekwenda huko kumfanya yeye kuwa mfalme.
2 When Jeroboam, who was still in Egypt, heard about that, he returned from Egypt [to Israel].
Yeroboamu mwana wa Nebati aliposikia hili (alikuwa bado yuko Misri alikokuwa amekimbilia awe mbali na Mfalme Solomoni), akarudi kutoka Misri.
3 The [leaders of the northern tribes] summoned him, and they went together [to talk] to Rehoboam. They said to him,
Kwa hiyo wakatuma watu kumwita Yeroboamu, yeye na kusanyiko lote la Israeli wakamwendea Rehoboamu na kumwambia,
4 “Your father [Solomon] forced us to work very hard [MET] for him. If you (lighten these loads/do not force us to work that hard), and if you charge us less taxes than we were paying to him, we will serve you [faithfully].”
“Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini sasa tupunguzie kazi za kikatili na nira nzito aliyoweka juu yetu, nasi tutakutumikia.”
5 He replied, “Go away, and come back three days from now [and I will give you my answer].” So those leaders and Jeroboam left.
Rehoboamu akajibu, “Nendeni kwa muda wa siku tatu na kisha mnirudie.” Basi watu wakaenda zao.
6 Then King Rehoboam consulted the older men who had advised his father Solomon while he was still living. He asked them, “What shall I say to answer those men?”
Kisha Mfalme Rehoboamu akataka shauri kwa wazee ambao walimtumikia Solomoni baba yake wakati wa uhai wake akawauliza, “Mnanishauri nini katika kuwajibu watu hawa?”
7 They replied, “If you want to serve your people well, speak kindly to those men when you reply to them. If you do that, your people will always serve you faithfully.”
Wakajibu, “Kama leo utakuwa mtumishi wa watu hawa na kuwahudumia na kuwapa jibu linaloridhisha, watakuwa watumishi wako daima.”
8 But he ignored what the older men advised him to do. Instead, he consulted the younger men who had grown up with him, who were now (his advisors/the ones who told him what would be good to do).
Lakini Rehoboamu akakataa shauri alilopewa na wazee na akataka ushauri kwa vijana wanaume rika lake waliokuwa wakimtumikia.
9 He said to them, “What should I say to the men who are asking me to reduce the [work and taxes] that my father required from them?”
Akawauliza, “Ninyi ushauri wenu ni nini? Tutawajibuje watu hawa wanaoniambia, ‘Ifanye nyepesi nira baba yako aliyoweka juu yetu?’”
10 They replied, “This is what you should tell them: ‘My little finger is thicker than my father’s waist.
Wale vijana wa rika lake wakamjibu, “Waambie watu hawa waliokuambia, ‘Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini ifanye nira yetu nyepesi,’ kuwa, ‘Kidole changu kidogo ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu.
11 What I mean is that my father required you [to work hard and pay high taxes]. But I will make those loads heavier. [It was as though] my father whipped you, but [it will be as though] I will whip you with whips that have pieces of metal in them.’”
Baba yangu aliweka nira nzito juu yenu, mimi nitaifanya hata iwe nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.’”
12 So three days later, Jeroboam and all the leaders came to Rehoboam again, as he had told them to do.
Siku tatu baadaye, Yeroboamu na watu wote wakamrudia Rehoboamu, kama mfalme alivyokuwa amesema, “Rudini kwangu baada ya siku tatu.”
13 The king ignored the advice of the older men and spoke harshly to the Israeli leaders.
Mfalme akawajibu watu kwa ukatili. Akikataa shauri alilopewa na wazee,
14 [He told them what the younger men had advised.] He said, “My father put heavy burdens [of work and taxes] on you, but I will put heavier burdens on you. [It was as though] he beat you with whips, but I will beat you with whips that have pieces of metal in them!”
akafuata shauri la vijana wa rika lake na kusema, “Baba yangu alifanya nira yenu kuwa nzito, mimi nitaifanya kuwa nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.”
15 So the king did not pay any attention to the Israeli leaders. But this happened in order that what Yahweh wanted would occur, what he had told the prophet Ahijah about Jeroboam [becoming king of the ten tribes].
Kwa hiyo mfalme hakuwasikiliza watu, kwa kuwa jambo hili lilitoka kwa Bwana, ili kutimiza neno ambalo Bwana alikuwa amenena kwa Yeroboamu mwana wa Nebati kupitia Ahiya Mshiloni.
16 When the Israeli leaders realized that the king did not pay any attention to what they said, they shouted, “We do not [RHQ] want anything to do with this descendant of King David! We will not pay attention to what this grandson of Jesse says! You people of Israel, let’s go home! As for this descendant of David [MTY], he can rule his own kingdom [MTY]!” So the Israeli leaders returned to their homes.
Israeli wote walipoona kuwa mfalme amekataa kuwasikiliza, wakamjibu mfalme: “Tuna fungu gani kwa Daudi? Sisi hatuna urithi kwa mwana wa Yese. Nendeni kwenye mahema yenu, ee Israeli! Angalia nyumba yako mwenyewe, ee Daudi!” Hivyo Waisraeli wakaenda kwenye mahema yao.
17 And [after that, ] the [only Israeli] people whom Rehoboam ruled over were those who lived in the territory of [the tribe of] Judah.
Lakini kwa habari ya Waisraeli waliokuwa wakiishi katika miji ya Yuda, Rehoboamu akaendelea kuwatawala bado.
18 Then King Rehoboam sent Adoniram [to talk to the Israeli people]. Adoniram was the man who supervised [all the men who were] forced to work [for Rehoboam]. But the Israeli people killed him by throwing stones at him. When that happened, King Rehoboam quickly got in his chariot and escaped to Jerusalem.
Mfalme Rehoboamu akamtuma Adoramu, aliyekuwa msimamizi wa wale waliofanya kazi ngumu kwa kulazimishwa, lakini Israeli wote wakampiga kwa mawe hadi akafa. Hata hivyo, Mfalme Rehoboamu, akafanikiwa kuingia kwenye gari lake na kutorokea Yerusalemu.
19 Ever since that time, the people of [the northern tribes of] Israel have been rebelling against the descendants [MTY] of [King] David.
Hivyo Israeli wakaasi dhidi ya nyumba ya Daudi hadi leo.
20 When the Israeli people heard that Jeroboam had returned [from Egypt], they invited him to come to a meeting, and there they appointed him to be the king of Israel. Only the people of the tribes of Judah [and Benjamin] continued to be loyal to [the kings descended from King] [MTY] David.
Waisraeli wote waliposikia kwamba Yeroboamu amerudi, wakatuma watu na kumwita kwenye kusanyiko na kumfanya mfalme juu ya Israeli yote. Ni kabila la Yuda peke yake lililobaki kuwa tiifu kwa nyumba ya Daudi.
21 When Rehoboam arrived in Jerusalem, he gathered 180,000 of the best soldiers from the tribes [MTY] of Judah and Benjamin. He wanted them to fight against the northern tribes of [MTY] Israel [and defeat them], in order that he could [rule all the tribes of] his kingdom again.
Ikawa Rehoboamu alipofika Yerusalemu, akakusanya nyumba yote ya Yuda na kabila la Benyamini, wanaume wapiganaji 180,000, kufanya vita dhidi ya nyumba ya Israeli na kuurudisha tena ufalme kwa Rehoboamu mwana wa Solomoni.
22 But God spoke to the prophet Shemaiah and said this to him:
Lakini neno hili la Mungu likamjia Shemaya mtu wa Mungu:
23 “Go and tell this to [Solomon’s son] Rehoboam, the king of Judah, and to all the people of the tribes of Judah and Benjamin and the people from the northern tribe who live in Judah:
“Mwambie Rehoboamu mwana wa Solomoni mfalme wa Yuda, na nyumba yote ya Yuda na Benyamini, na watu wengine wote,
24 ‘Yahweh says that you must not go to fight against your own relatives, the people of Israel. All of you must go home. What has happened is what Yahweh wanted to happen.’” [So Shemaiah went and told that to them, ] and they all paid attention to what Yahweh had commanded them to do, and they went home.
‘Hili ndilo asemalo Bwana: Msipande kupigana dhidi ya ndugu zenu, Waisraeli. Nendeni nyumbani, kila mmoja wenu, kwa kuwa hili nimelitenda mimi.’” Kwa hiyo wakalitii neno la Bwana na kurudi nyumbani, kama Bwana alivyokuwa ameagiza.
25 Then Jeroboam’s workers built [walls around] Shechem [city] in the hilly area [where the descendants] of Ephraim [lived], and he ruled from there for a while. He and his workers then left there and went to Peniel [town], and they built walls around that town.
Kisha Yeroboamu akajenga Shekemu akaizungushia ngome katika nchi ya vilima ya Efraimu na akaishi huko. Akatoka huko, akaenda akajenga Penueli.
26 Then Jeroboam said to himself, “If my people [continue to] go to Jerusalem and offer sacrifices to Yahweh at the temple there, soon they will again become loyal to Rehoboam, the king of Judah [DOU], and they will kill me.”
Yeroboamu akawaza moyoni mwake, “Sasa inawezekana ufalme ukarudi katika nyumba ya Daudi.
Kama watu hawa watapanda kwenda kutoa dhabihu katika Hekalu la Bwana huko Yerusalemu, mioyo yao itamrudia bwana wao, Rehoboamu mfalme wa Yuda. Wataniua mimi na kurudi kwa Mfalme Rehoboamu.”
28 So he consulted [his advisors, and then he did what they suggested]. He [told his workers to] make gold [statues of] two calves. Then he said to the people, “You have been going to Jerusalem [to worship] for a long time. It is a big trouble for you to continue going there. You people of Israel, look! These statues are the gods that brought our [ancestors] up from Egypt! [So you can worship these, here!]”
Baada ya kutafuta shauri, mfalme akatengeneza ndama wawili wa dhahabu. Akawaambia watu, “Ni gharama kubwa kwenu kukwea kwenda Yerusalemu. Hii hapa miungu yenu, ee Israeli, iliyowapandisha kutoka Misri.”
29 He [told his workers to] place one of the statues in Bethel [city in the south] and one in Dan [city in the north].
Ndama mmoja akamweka Betheli na mwingine Dani.
30 So [what Jeroboam did caused] the people [to] sin. Some of them went and worshiped the calf at Bethel, and others went and worshiped the other calf at Dan.
Nalo jambo hili likawa dhambi, watu wakawa wanaenda hadi Dani kumwabudu huyo aliyewekwa huko.
31 [Moses had declared that only men from the tribe of Levi would be priests, but] Jeroboam also told his workers to build shrines on hilltops, and then he appointed men who were not from the tribe of Levi to be priests.
Yeroboamu akajenga madhabahu mahali pa juu pa kuabudia miungu na kuwateua makuhani kutoka watu wa aina zote, ijapokuwa hawakuwa Walawi.
32 He also appointed Adonijah and two priests, Elishama and Jehoram. They had a celebration at the end of October, like the celebration [of Living in Temporary Shelters] that occurred in Judah [each year]. On the altar [that they built] in Bethel, he offered sacrifices to the gold statues of calves that they had made, and he stationed the priests there at the shrines that his workers had built.
Pia Yeroboamu akaweka sikukuu katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, kama sikukuu iliyokuwa ikifanyika huko Yuda, na akatoa dhabihu juu ya madhabahu. Akafanya hivyo huko Betheli akitoa dhabihu kwa ndama alizotengeneza. Huko Betheli akawaweka makuhani, na pia katika sehemu za juu za kuabudia miungu alizozitengeneza.
33 Jeroboam went up to that altar on that day in October which he himself had chosen. There on that altar he burned incense [to be a sacrifice]. And he declared that the people should celebrate that festival [on that same day every year].
Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, mwezi aliouchagua mwenyewe, alitoa dhabihu juu ya madhabahu aliyokuwa amejenga huko Betheli. Kwa hiyo akaweka sikukuu kwa ajili ya Waisraeli na akapanda madhabahuni kutoa sadaka.