< 1 Kings 11 >

1 King Solomon married many foreign women. First he married the daughter of the king of Egypt. He also married women from the Heth people-group and from the Moab, Ammon, and Edom people-groups, and from Sidon [city].
Hata hivyo, Mfalme Solomoni akawapenda wanawake wengi wa kigeni zaidi, mbali na binti Farao: wanawake wa Wamoabu, Waamoni, Waedomu, Wasidoni na Wahiti.
2 He married them even though Yahweh had commanded the Israeli people, “Do not marry people from those areas, because if you do that, they will surely persuade you [IDM] to worship the gods that they worship!”
Walitoka katika mataifa ambayo Bwana aliwaambia Waisraeli, “Msije mkaoana nao, kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu mgeukie miungu yao.” Hata hivyo, Solomoni akakaza kuwapenda.
3 Solomon married 700 women who were kings’ daughters. He also had 300 wives who were his slaves/servants. And his wives caused him to turn away [from worshiping God].
Alikuwa na wake 700 mabinti wa uzao wa kifalme, na masuria 300, nao wake zake wakampotosha.
4 By the time that Solomon became old, they had persuaded him to worship the gods from their countries. He was not completely dedicated/committed to Yahweh his God like his father [SYN] David had been.
Kadiri Solomoni alivyozidi kuzeeka, wake zake wakaugeuza moyo wake kuelekea miungu mingine, na moyo wake haukujitolea kikamilifu kwa Bwana Mungu wake, kama ulivyokuwa moyo wa Daudi baba yake.
5 Solomon worshiped Astarte, the goddess that the people of Sidon [worshiped], and he worshiped Molech, the disgusting god that the Ammon people-group [worshiped].
Solomoni akafuata Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, na Moleki mungu aliyekuwa chukizo la Waamoni.
6 That’s how Solomon did things that Yahweh said were evil. He did not conduct his life like his father David had done; he did not conduct his life as Yahweh wanted him to.
Kwa hiyo Solomoni akafanya uovu machoni pa Bwana; hakumfuata Bwana kikamilifu kama alivyofanya Daudi baba yake.
7 On the hill to the east of Jerusalem he built a place to worship Chemosh, the disgusting god that the Moab people-group [worshiped], and a place to worship Molech, the disgusting god that the Ammon people-group [worshiped].
Kwenye kilima mashariki mwa Yerusalemu, Solomoni akajenga mahali pa juu kwa ajili ya Kemoshi chukizo la Wamoabu, na kwa Moleki mungu chukizo la Waamoni.
8 He also built places where all his foreign wives could burn incense and offer sacrifices to the gods from their own countries.
Akafanya hivyo kwa wake zake wote wa kigeni, ambao walifukiza uvumba na kutoa dhabihu kwa miungu yao.
9 Even though Yahweh, the God whom the Israelis [worshiped], had appeared to Solomon two times, and had commanded him to not worship foreign gods, Solomon refused to obey Yahweh. So Yahweh was angry with Solomon,
Bwana akamkasirikia Solomoni kwa sababu moyo wake uligeuka mbali na Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye alikuwa amemtokea mara mbili.
Ingawa alikuwa amemkataza Solomoni kufuata miungu mingine, Solomoni hakutii amri ya Bwana.
11 and said to him, “You have chosen to break the agreement that I made with you and to disobey what I commanded you. So I am surely not going to allow you to rule all of your kingdom. I am going to allow one of your officials to rule it.
Kwa hiyo Bwana akamwambia Solomoni, “Kwa kuwa hii ndiyo hali yako na hukushika Agano langu na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme kutoka kwako na kumpa mmoja wa walio chini yako.
12 But, because of [what I promised] your father David, I will allow you to rule all your kingdom while you are still [living]. [After you die], I will not allow your son to rule the whole kingdom [MTY].
Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi baba yako, sitafanya jambo hili wakati wa uhai wako. Nitaurarua kutoka mikononi mwa mwanao.
13 But I will not take all the kingdom away from him. Instead, I will allow him to rule one tribe [besides the tribe of Judah], because of what I promised to David, who served me [well], and because [I want David’s descendants to rule in] Jerusalem, [where my temple is located].”
Lakini pia sitaurarua ufalme wote kutoka kwake, bali nitampa kabila moja kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu na kwa ajili ya Yerusalemu, ambao nimeuchagua.”
14 Yahweh caused Hadad, from the family of the kings in the Edom people-group, to rebel against Solomon.
Kisha Bwana akamwinua adui dhidi ya Solomoni, Hadadi, Mwedomu, kutoka ukoo wa ufalme wa Edomu.
15 What happened was that previously, when David’s [army] had conquered the Edom people-group, his army commander Joab had gone there to [help] bury the [Israeli soldiers] who had been killed [in the battle]. Joab and his army remained in the Edom area for six months, and during that time they killed all the males of that area.
Huko nyuma wakati Daudi alipokuwa akipigana na Edomu, Yoabu jemadari wa jeshi, aliyekuwa amekwenda kuzika waliouawa, alikuwa amewaua wanaume wote waliokuwako Edomu.
Yoabu na Waisraeli wote walikaa huko kwa miezi sita, mpaka walipomaliza kuwaangamiza wanaume wote huko Edomu.
17 Hadad was a young child [at that time], and he had escaped to Egypt, along with some of his father’s servants from the Edom area.
Lakini Hadadi, akiwa bado mvulana mdogo, alikimbilia Misri akiwa na baadhi ya maafisa wa Kiedomu waliokuwa wakimhudumia baba yake.
18 They [went to the] Midian [region], and then they went to [the desert area at] Paran. Some other men joined them there. Then they all traveled to Egypt and went to see the king of Egypt. The king gave Hadad some land and ordered his servants to give him some food regularly.
Wakaondoka Midiani wakaenda Parani. Basi wakichukua pamoja nao wanaume kutoka Parani, wakaenda Misri, kwa Farao mfalme wa Misri, ambaye alimpa Hadadi nyumba, ardhi na akampatia chakula.
19 The king liked Hadad. As a result he gave him the sister of his own wife, Queen Tahpenes, to be Hadad’s wife.
Farao akapendezwa sana na Hadadi hata akampa ndugu wa mkewe mwenyewe, Malkia Tapenesi, ili aolewe na Hadadi.
20 Later Hadad’s wife gave birth to a son named Genubath. The sister of Tahpenes (raised him/brought him up) in the palace, where he lived with the king’s sons.
Huyo ndugu wa Tapenesi akamzalia mwana aliyeitwa Genubathi, ambaye alilelewa na Tapenesi katika jumba la kifalme. Huko Genubathi aliishi pamoja na watoto wa Farao mwenyewe.
21 While Hadad was in Egypt, he heard that David had died [EUP], and that Joab, the commander of David’s army, was also dead. So he said to the king of Egypt, “Please allow me to return to my own country.”
Alipokuwa huko Misri, Hadadi alisikia kwamba Daudi amepumzika na baba zake na ya kwamba pia Yoabu aliyekuwa jemadari wa jeshi amekufa. Ndipo Hadadi akamwambia Farao, “Niruhusu niende ili niweze kurudi katika nchi yangu.”
22 But the king said to him, “Why do you want to go back to your country? Is there something that you lack that you want me to give to you?” Hadad replied, “No, but please just allow me to go.” [So the king allowed him to leave, and he returned to his own country and became the king of Edom].
Farao akauliza, “Umekosa nini hapa, kwamba unataka kurudi katika nchi yako?” Hadadi akajibu, “Hakuna, lakini niruhusu niende!”
23 God also caused another man named Rezon, the son of Eliada, to rebel against Solomon. Rezon had run away from his master, King Hadadezer of [the] Zobah [area north of Damascus].
Mungu akamwinua adui mwingine dhidi ya Solomoni, Rezoni mwana wa Eliada, ambaye alikuwa amemkimbia bwana wake Hadadezeri, mfalme wa Soba.
24 Rezon then became the leader of a group of outlaws. That happened after David’s [army had defeated Hadadezer and] had [also] killed all [his soldiers]. Rezon and his men went to Damascus and started to live there, and [the people there] appointed him to be their king.
Akawakusanya watu, naye akawa kiongozi wa kundi la waasi, wakati Daudi alipoangamiza majeshi ya Soba; waasi walikwenda Dameski, mahali walipokaa na kumiliki.
25 All during the time that Solomon was alive, while Rezon was ruling [not only Damascus but all of] Syria, he was an enemy of Israel and caused trouble for Israel like Hadad did.
Rezoni alikuwa adui wa Israeli kwa muda wote alioishi Solomoni, ukiongezea matatizo yaliyosababishwa na Hadadi. Kwa hiyo Rezoni akatawala katika Aramu na alikuwa mkatili kwa Israeli.
26 Another man who rebelled against [IDM] Solomon was one of his officials named Jeroboam, the son of Nebat. He was from Zeredah [town] in [the region where the tribe of] Ephraim [lives]. His mother was a widow named Zeruah.
Pia, Yeroboamu mwana wa Nebati aliasi dhidi ya mfalme. Alikuwa mmoja wa maafisa wa Solomoni, Mwefraimu kutoka Sereda, ambaye mama yake alikuwa mjane aliyeitwa Serua.
27 This is what happened. Solomon’s workers were filling in the land/ground on the east side of Jerusalem and repairing the walls [around the city].
Haya ndiyo maelezo ya jinsi alivyomwasi mfalme: Solomoni alikuwa amejenga Milo naye akawa ameziba mwanya katika ukuta wa mji wa Daudi baba yake.
28 Jeroboam was a very capable young man. So, when Solomon saw that he worked very hard, he appointed him to supervise all the men who were forced to work in the areas where the tribes of Manasseh and Ephraim live.
Basi Yeroboamu alikuwa mtu shujaa na hodari, naye Solomoni alipoona jinsi kijana alivyofanya kazi yake, akamweka kuwa kiongozi wa kazi yote ya mikono ya nyumba ya Yosefu.
29 One day when Jeroboam was walking alone along the road outside of Jerusalem, the prophet Ahijah from Shiloh [city] met him. Ahijah was wearing a new robe,
Karibu na wakati ule Yeroboamu alikuwa anatoka nje ya Yerusalemu, Ahiya nabii Mshiloni akakutana naye njiani, akiwa amevaa joho jipya. Hawa wawili walikuwa peke yao mashambani,
30 which he took off and tore into twelve pieces.
naye Ahiya akachukua joho jipya alilokuwa amevaa akalirarua vipande kumi na viwili.
31 He said to Jeroboam, “Take ten of these pieces for yourself, because Yahweh, the God whom we Israelis [worship], says to you, ‘I am going to tear the kingdom from Solomon, and I am going to enable you to become the ruler of ten of the tribes [of Israel].
Kisha akamwambia Yeroboamu, “Chukua vipande kumi kwa ajili yako, kwa kuwa hivi ndivyo Bwana, Mungu wa Israeli asemavyo: ‘Tazama, ninakwenda kuuchana ufalme kutoka mikononi mwa Solomoni na kukupa wewe makabila kumi.
32 Solomon’s [descendants] will still rule one tribe (OR, two tribes), because of [what I promised] David, a man who served me [very well], and because of Jerusalem, the city that I have chosen from all the cities in Israel [to be the city where my people will worship me].
Lakini kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi na mji wa Yerusalemu, ambao nimeuchagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli, atakuwa na kabila moja.
33 I am going to do this because Solomon has rejected me and has been worshiping Astarte, the goddess that the people of Sidon worship, Chemosh, the god that the Moab people-group worship, and Milcom, the god that the Ammon people-group worship. He has not conducted his life as I wanted him to. He has not obeyed my statutes and laws, like his father David did.
Nitafanya hivi kwa sababu wameniacha mimi na kuabudu Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, Kemoshi mungu wa Wamoabu, na Moleki mungu wa Waamoni, nao hawakwenda katika njia zangu ili kufanya yaliyo sawa machoni pangu, wala kushika amri na sheria zangu kama Daudi, babaye Solomoni, alivyofanya.
34 ‘But I will not take the entire kingdom away from him. I will enable him to rule [Judah] all during the years that he is alive. I will do that because of [what I promised to do for] David, whom I chose [to be the king], and who served me [well], and who always obeyed my commandments and laws.
“‘Lakini sitauondoa ufalme wote kutoka mikononi mwa Solomoni, nimemfanya mtawala siku zote za maisha yake kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, niliyemchagua na ambaye aliyatunza maagizo na amri zangu.
35 But I will take the [other] ten tribes of his kingdom and give them to you [to rule].
Nitauondoa ufalme kutoka mikononi mwa mwanawe na kukupa wewe makabila kumi.
36 I will allow Solomon’s son to rule one tribe, in order that descendants [MET] of David will always rule in Jerusalem, the city that I have chosen to be the place where [my people worship] me [MTY].
Nitampa mwanawe kabila moja ili kwamba Daudi mtumishi wangu awe na taa mbele zangu daima katika Yerusalemu, mji ambao nimeuchagua kuweka Jina langu.
37 I will enable you to become the king of Israel, and you will rule over all the territory that you want to.
Hata hivyo, kukuhusu wewe Yeroboamu, nitakutwaa, nawe utatawala juu ya yote yale moyo wako unayotamani, utakuwa mfalme juu ya Israeli.
38 If you obey all that I command you to do, and conduct your life as I want you to, and if you do what I say is right by obeying my laws and commandments like David did, I will help you. I will make sure that your descendants will rule after you [die], like I [promised to] do for David.
Ikiwa utafanya kila nitakalokuamuru, kuenenda katika njia zangu na kufanya yaliyo sawa mbele za macho yangu kwa kuzishika amri zangu na maagizo yangu kama alivyofanya Daudi mtumishi wangu, nitakuwa pamoja nawe. Nitakujengea ufalme utakaodumu kama ule niliomjengea Daudi, nami nitakupa Israeli.
39 Because of [Solomon’s sins], I will punish David’s descendants, but I will not continue to punish them forever.’”
Nitawatesa wazao wa Daudi kwa ajili ya hili, lakini siyo milele.’”
40 Solomon [found out what Ahijah told Jeroboam], so he tried to kill Jeroboam. But Jeroboam escaped and went to Egypt. He went to Shishak, the king of Egypt, and stayed with him until after Solomon died.
Solomoni akajaribu kumuua Yeroboamu, lakini Yeroboamu akakimbilia Misri, kwa Mfalme Shishaki, naye akakaa huko mpaka Solomoni alipofariki.
41 [A record of] all the other things that Solomon did, and all the wise things that he [said and wrote], was written in the Book Telling what Solomon Did.
Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, yote aliyoyafanya na hekima aliyoionyesha, je hayakuandikwa yote katika kitabu cha matendo cha Solomoni?
42 He was the king in Jerusalem who ruled over all of Israel for 40 years.
Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
43 Then Solomon died [EUP], and was buried in the [part of Jerusalem called] ‘The City of David’. And his son Rehoboam became the king.
Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 1 Kings 11 >