< 1 Corinthians 5 >
1 [Now I want to discuss another matter]. It has been {People have} reported to me, and I believe that it is true, that some people among you have been acting in a sexually immoral way, in a way that is so bad that not even (pagans/people who do not know about God) act that way. People tell me that a man is living with his stepmother (OR, his father’s other wife).
Yamkini habari imeenea ya kuwa miongoni mwenu kuna uzinzi ambao haujatokea hata miongoni mwa watu wasiomjua Mungu: Kwamba mtu anaishi na mke wa baba yake.
2 You should be sad about what that man is doing! He should have been expelled {[You] should have expelled him} from your congregation! [But you] have not [done that], so (how can you be proud, [thinking that you are spiritually mature?]/it is disgusting that you are proud, [thinking that you are spiritually mature]!) [RHQ]
Nanyi mwajivuna! Je, haiwapasi kuhuzunika na kumtenga na ushirika wenu mtu huyo aliyefanya mambo hayo?
3 As for me, I have already decided [how you should] punish that man. And even though I am away from you, my spirit is with you, and you should do as I would do if I were there with you.
Hata kama siko pamoja nanyi katika mwili, niko nanyi katika roho. Nami nimekwisha kumhukumu mtu huyo aliyetenda jambo hili, kama vile ningekuwepo.
4 [What I have decided is that] when you have gathered together with the authority [MTY] of our Lord Jesus, and my spirit is with you, and the power of our Lord Jesus [is with you],
Mnapokutana katika Jina la Bwana wetu Yesu nami nikiwepo pamoja nanyi katika roho na uweza wa Bwana Yesu ukiwepo,
5 you should hand that man over to Satan. Then Satan can injure/punish his body, in order that [he will turn away from his sinful behavior] and his spirit will be saved on the day when the Lord [returns] [MTY].
mkabidhini mtu huyu kwa Shetani, ili mwili wake uharibiwe, ili roho yake iokolewe katika siku ya Bwana.
6 It is not good that, [while you are letting that immoral man continue to be in your congregation], you are boasting [about being spiritually mature]. (You know that a small amount of yeast affects all the bread dough [MET] [into which it is put] {[a woman puts it]}./Do you not know that a small amount of yeast affects all the bread dough [MET] [into which it is put]?) [RHQ] [Similarly, one person who continues to sin will have a bad effect on all the congregation].
Majivuno yenu si mazuri. Je, hamjui ya kwamba chachu kidogo huchachusha donge zima la unga?
7 So, [just like we Jews] expel the old yeast [from our houses during the Passover celebration] in order that we may have a fresh batch of dough without yeast in it [MET], [you must expel such evil people from your congregation]. Do [that so that you can truly be holy people], as [I know that] you really are. Remember that Christ was sacrificed {sacrificed himself} [so that God could spare us from being punished for our sins, just like the Jews sacrificed lambs during] the [first] Passover celebration [so that God would spare their firstborn sons from being killed].
Ondoeni chachu ya kale ili mpate kuwa donge jipya lisilotiwa chachu, kama vile mlivyo. Kwa maana Kristo, Mwana-Kondoo wetu wa Pasaka amekwisha tolewa kuwa dhabihu.
8 So let us celebrate [the fact that God has freed us from being punished us for our sins] [MET], [just like the Jews] in [later years] celebrated Passover [to celebrate God freeing them from being slaves in Egypt. They made sure that there was] no old yeast in the dough. [They ate bread that] had no yeast in it. [Similarly], [we should make sure that there are no people in our congregations] [MET] [who act] maliciously [toward others] or [act] wickedly. Instead, [make sure] [MET] [that all those in our congregations are ones who act] sincerely and [speak] truthfully.
Kwa hiyo, tusiiadhimishe sikukuu hii, kwa chachu ya zamani, chachu ya nia mbaya na uovu, bali kwa mkate usiotiwa chachu, ndio weupe wa moyo na kweli.
9 In the previous letter that I wrote to you, I said that you should not associate with sexually immoral people.
Niliwaandikia katika waraka wangu kuwa msishirikiane na wazinzi.
10 I did not mean that you should not associate with unbelievers who are immoral, or who desire things that belong to others, or who (forcefully seize things that belong to others/are swindlers), or who worship idols. You would have to leave this world [to avoid all people] like that.
Sina maana kwamba msishirikiane na wazinzi wa ulimwengu huu, au wenye tamaa mbaya, wanyangʼanyi au waabudu sanamu. Kwa kufanya hivyo ingewalazimu mtoke ulimwenguni humu.
11 But now [I am stating clearly that] when I wrote, I [meant that] you should not associate with those who say that they are fellow believers, if they are sexually immoral or if they desire and forcefully seize things that belong to others, or worship idols, or slander others, or become drunk. You should not associate with people like that, and you should not even eat with them!
Lakini sasa nawaandikia kwamba msishirikiane na mtu yeyote anayejiita ndugu, hali akiwa ni mzinzi, au mwenye tamaa mbaya, mwabudu sanamu au msingiziaji, mlevi au mdhalimu. Mtu kama huyo hata msile naye.
12 It is certainly not [RHQ] my business to judge people who are not believers and who do not belong to [Christian congregations]. But it certainly is [RHQ] your business to judge those who are in [your congregation]!
Yanihusu nini kuwahukumu wale watu walio nje ya kanisa? Je, si mnapaswa kuwahukumu hao walio ndani?
13 God is the one who will judge those who are not believers. [Do as the Scriptures command]: “Expel the wicked person from your midst!”
Mungu atawahukumu hao walio nje. “Ninyi mwondoeni huyo mtu mwovu miongoni mwenu.”