< 1 Chronicles 27 >
1 This is a list of the Israeli men who served the king in the army. Some were leaders of families, some were commanders of 100 men, some were commanders of 1,000 men, and some were their officers. There were 24,000 men [DOU] in each group. Each group served one month of each year.
Hii ndiyo orodha ya Waisraeli: viongozi wa jamaa, majemadari wa maelfu, majemadari wa mamia na maafisa wao, waliomtumikia mfalme kwa lolote lililohusu vikosi vya jeshi vilivyokuwa zamu mwezi baada ya mwezi katika mwaka mzima. Kila kikosi kimoja kilikuwa na watu 24,000.
2 Jashobeam, the son of Zabdiel, was in charge of the group that served during the first month [of each year].
Msimamizi wa kikosi cha kwanza kwa mwezi wa kwanza alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Kulikuwa na watu 24,000 katika kikosi chake.
3 He was a descendant of Perez, and he was the commander of all the army officers during the first month of each year.
Yeye alikuwa mzao wa Peresi, na mkuu wa maafisa wote wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
4 Dodai, from the clan of Ahohi, was the commander of the group that served during the following/second month of each year. Mikloth was his (assistant/chief officer).
Msimamizi wa kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai Mwahohi. Miklothi ndiye alikuwa kiongozi wa kikosi chake. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
5 Benaiah, the son of Jehoiada the Supreme Priest, was the commander of the group that served during the following/third month.
Jemadari wa kikosi cha tatu kwa mwezi wa tatu alikuwa Benaya mwana wa kuhani Yehoyada. Ndiye alikuwa mkuu wa kikosi chake kilichokuwa na watu 24,000.
6 He was the one who was a mighty warrior among David’s thirty greatest soldiers, and he was their leader. His son Ammizabad was his assistant.
Huyu ndiye yule Benaya aliyekuwa shujaa miongoni mwa wale Thelathini na ndiye alikuwa juu yao hao Thelathini. Mwanawe Amizabadi ndiye alikuwa mkuu katika kikosi chake.
7 Asahel, Joab’s [younger] brother, was [the commander of the group that served] during the following/fourth month. Asahel’s son Zebadiah became the commander after Asahel [was killed].
Jemadari wa nne kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli nduguye Yoabu, mwanawe Zebadia ndiye aliingia mahali pake kwenye uongozi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
8 The commander for the following/fifth month was Shamhuth, a descendant of Izrah.
Jemadari wa kikosi cha tano kwa mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi Mwizrahi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
9 The commander for the following/sixth month was Ira the son of Ikkesh from Tekoa [town].
Jemadari wa kikosi cha sita kwa mwezi wa sita alikuwa Ira, mwana wa Ikeshi Mtekoa. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
10 The commander for the following/seventh month was Helez, a member of the Pelon [clan] from the tribe of Ephraim.
Jemadari wa kikosi cha saba kwa mwezi wa saba alikuwa Helesi Mpeloni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
11 The commander for the following/eighth month was Sibbecai, a descendant of Zerah from Hushah [town].
Jemadari wa nane kwa mwezi wa nane, alikuwa Sibekai Mhushathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
12 The commander for the following/ninth month was Abiezer from Anathoth [city] in the tribe of Benjamin.
Jemadari wa tisa kwa mwezi wa tisa alikuwa Abiezeri Mwanathothi wa Wabenyamini. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
13 The commander for the following/tenth month was Maharai, a descendant of Zerah from Netophath [town].
Jemadari wa kumi kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai Mnetofathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
14 The commander for the following/eleventh month was Benaiah from Pirathon [town] in the tribe of Ephraim.
Jemadari wa kumi na moja kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaya Mpirathoni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
15 The commander for the last month [of each year] was Heldai, a descendant of Othniel from Netophath [town].
Jemadari wa kumi na mbili kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Heldai Mnetofathi kutoka jamaa ya Othnieli. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
16 This is a list of the administrators of the [twelve] tribes [DOU] of Israel: Eliezer, the son of Zicri, was the administrator of the tribe of Reuben. Shephatiah, the son of Maacah, was the administrator of the tribe of Simeon.
Maafisa waliokuwa wanaoongoza makabila ya Israeli walikuwa: Kwa Wareubeni: Eliezeri mwana wa Zikri; kwa Wasimeoni: Shefatia mwana wa Maaka;
17 Hashabiah, the son of Kemuel, was the administrator of the tribe of Levi. Zadok was the administrator of the tribe of Aaron.
kwa Walawi: Hashabia mwana wa Kemueli; kwa Aroni: Sadoki;
18 Elihu, David’s [older] brother, was the administrator of the tribe of Judah. Omri, the son of Michael, was the administrator of the tribe of Issachar.
kwa Yuda: Elihu, nduguye Daudi; kwa Waisakari: Omri mwana wa Mikaeli;
19 Ishmaiah, the son of Obadiah, was the administrator of the tribe of Zebulun. Jerimoth, the son of Azriel, was the administrator of the tribe of Naphtali.
kwa Wazabuloni: Ishmaya mwana wa Obadia; kwa Wanaftali: Yeremothi mwana wa Azrieli;
20 Hoshea, the son of Azaziah, was the administrator of the tribe of Ephraim. Joel, the son of Pedaiah, was the administrator of the tribe of the [western] half of the tribe of Manasseh.
kwa Waefraimu: Hoshea mwana wa Azazia; kwa nusu ya kabila la Manase: Yoeli mwana wa Pedaya;
21 Iddo, the son of Zechariah, was the administrator of the [eastern] half of the tribe of Manasseh, in [the] Gilead [region]. Jaasiel, the son of Abner, was the administrator of the tribe of Benjamin.
kwa nusu nyingine ya kabila la Manase huko Gileadi: Ido mwana wa Zekaria; kwa Wabenyamini: Yaasieli mwana wa Abneri;
22 Azarel, the son of Jeroham, was the administrator of the tribe of Dan. Those were the leaders over the tribes of Israel.
kwa Wadani: Azareli mwana wa Yerohamu. Hao ndio waliokuwa maafisa wa makabila ya Israeli.
23 [When] David [told Joab to count the men of Israel, he] did not [tell him to] count the men who were less then 20 years old, because Yahweh had promised [many years previously] that there would be as many [people] in Israel as there are stars in the sky.
Daudi hakuwahesabu watu waliokuwa chini ya miaka ishirini, kwa sababu Bwana alikuwa ameahidi kuwafanya Israeli kuwa wengi kama nyota za angani.
24 Joab [and his helpers] started to count the men of Israel, but they did not finish counting them [because Joab knew that Yahweh was angry about their being counted]. Yahweh punished [MTY] the people of Israel because of this counting, and as a result the total number of Israeli men [able to serve in the army] was not written on the scroll about King David’s [rule].
Yoabu mwana wa Seruya alianza kuwahesabu watu lakini hakumaliza. Kwa sababu ya kuwahesabu watu, hasira ya Mungu iliwaka juu ya Israeli, nayo hiyo hesabu yao haikuingizwa katika kitabu cha kumbukumbu za Mfalme Daudi.
25 Azmaveth, the son of Adiel, was in charge of the king’s storehouses. Jonathan, the son of Uzziah, was is charge of the storehouses in various towns and villages in Israel, and also in charge of the watchtowers.
Azmawethi mwana wa Adieli ndiye alikuwa msimamizi wa hazina za mfalme. Msimamizi wa hazina katika mashamba, miji, vijiji na kwenye ngome alikuwa Yonathani mwana wa Uzia.
26 Ezri the son of Kelub was in charge of the workers who farmed the land [that belonged to the king].
Ezri mwana wa Kelubu alikuwa msimamizi wa wafanyakazi waliolima katika mashamba.
27 Shimei from Ramath [town] was in charge of the king’s vineyards. Zabdi from Shepham [town] was in charge of storing the wine from the [grapes produced in] vineyards.
Shimei Mramathi alikuwa msimamizi wa mashamba ya mizabibu. Zabdi Mshifmi alikuwa msimamizi wa zabibu, utengenezaji na uhifadhi wa divai katika mapipa makubwa.
28 Baal-Hanan from Geder [city] was in charge of storing the olive oil.
Baal-Hanani Mgederi ndiye alikuwa mwangalizi wa mashamba ya mfalme ya mizeituni na mikuyu katika tambarare za vilima vya magharibi. Yoashi alikuwa msimamizi wa ghala za mafuta ya zeituni.
29 Shitrai from the Sharon Plain was in charge of the herds of cattle that (grazed/ate grass) there. Shaphat the son of Adlai was in charge of the cattle in the valleys.
Shitrai Msharoni alikuwa msimamizi wa makundi ya ngʼombe waliojilisha huko Sharoni. Shafati mwana wa Adlai alikuwa msimamizi wa yale makundi ya ngʼombe yaliyokuwa makondeni.
30 Obil, a descendant of Ishmael, was in charge of the camels. Jehdeiah from Meronoth [town] was in charge of the donkeys.
Obili Mwishmaeli alikuwa msimamizi wa ngamia. Yedeya Mmeronothi alikuwa msimamizi wa punda.
31 Jaziz, a descendant of Hagar, was in charge of the [king’s] flocks of sheep. All of those officials were in charge of the things that belonged to King David.
Yazizi Mhagri alikuwa msimamizi wa makundi ya kondoo na mbuzi. Hawa wote ndio waliokuwa maafisa wasimamizi wa mali alizokuwa nazo Mfalme Daudi.
32 David’s uncle Jonathan was a wise counselor for him. Jehiel, the son of Hacmoni, taught the king’s sons.
Yonathani mjomba wa Daudi alikuwa mshauri, mtu mwenye ufahamu mkubwa na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakmoni alikuwa akiwahudumia wana wa mfalme.
33 Ahithophel was the king’s official counselor.
Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme. Hushai Mwariki alikuwa rafiki wa mfalme.
34 Hushai from the Ark people-group was the king’s special friend. Benaiah’s son Jehoiada became the king’s advisor after Ahithophel died, and later Abiathar became his advisor. Joab was the chief commander of the army.
Baada ya Ahithofeli, Yehoyada mwana wa Benaya aliingia mahali pake kama mshauri wa mfalme pamoja na Abiathari. Yoabu alikuwa ndiye jemadari wa majeshi ya mfalme.