< 1 Chronicles 20 >

1 [In that region], kings usually went [with their armies] to fight [their enemies] (in the springtime/when the cold season ended). But that year, David [did not do that. Instead, he] stayed in Jerusalem, and he sent [his commander] Joab [to lead the army]. Joab took his troops. They [crossed the Jordan River and] ruined the land of the Ammon people-group. Then they went to Rabbah, [the capital city, ] and surrounded it. David stayed in Jerusalem [for a while. But later he took more troops and went to help] Joab. Their armies attacked Rabbah and destroyed it.
Mwanzoni mwa mwaka mpya, wakati ambapo wafalme huenda vitani, Yoabu aliliongoza jeshi. Aliangamiza nchi ya Waamoni, na akaenda Raba na kuuzingira, lakini Daudi alibaki Yerusalemu. Yoabu akashambulia Raba na kuuacha ukiwa magofu.
2 Then David took the crown from the head of the king of Rabbah (OR, from the head of their god Milcom) and put it on his own head. It [was very heavy; it] weighed (75 pounds/34 kg.), and it had many very valuable stones [fastened to it]. They also took many other valuable things from the city.
Daudi akachukua taji kutoka kwa kichwa cha mfalme wao, lililokuwa na uzito wa talanta moja ya dhahabu, nayo ilizungushiwa vito vya thamani. Ikawekwa juu ya kichwa cha Daudi. Alichukua nyara nyingi kutoka mjini huo.
3 Then they brought the people out of the city and forced them to [work for their army, ] using saws and iron picks and axes. David’s soldiers did this in all the cities of the Ammon people-group. Then David and all of his army returned to Jerusalem.
Akawatoa watu waliokuwa humo, akawaweka wafanye kazi kwa misumeno, sululu za chuma na mashoka. Daudi akafanya hivi kwa miji yote ya Waamoni. Kisha Daudi na jeshi lake lote wakarudi Yerusalemu.
4 Later, [David’s army] fought a battle with the army of Philistia, at Gezer [city]. During the battle Sibbecai, from Hushah [clan], killed Sippai, one of the descendants of the Rapha [giants]. So the armies of Philistia were defeated.
Baada ya muda, kulitokea vita dhidi ya Wafilisti, huko Gezeri. Wakati huo Sibekai, Mhushathi, akamuua Sipai, aliyekuwa mmoja wa wazao wa Warefai, nao Wafilisti wakashindwa.
5 In another battle against the soldiers of Philistia, Elhanan, the son of Jair, killed Lahmi, the [younger] brother of [the giant] Goliath from Gath [town], who had a spear which was as thick as a weaver’s rod.
Katika vita vingine na Wafilisti, Elhanani mwana wa Yairi alimuua Lahmi nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.
6 There was another battle near Gath. A (huge man/giant) was there who had six fingers on each hand and six toes on each foot. He was descended from [the] Rapha [giants].
Katika vita vingine tena, vilivyopiganwa huko Gathi, kulikuwako na mtu mmoja mkubwa mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita katika kila mguu: jumla vidole ishirini na vinne. Yeye alikuwa pia mzao wa Mrefai.
7 When he made fun of the soldiers of Israel, Jonathan, the son of David’s [older] brother Shimea, killed him.
Alipowadhihaki Israeli, Yonathani, mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akamuua.
8 Those were some of the descendants of [the] Rapha [giants] who had lived in Gath, who were killed [MTY] by David and his soldiers.
Hawa walikuwa ndio wazao wa Warefai huko Gathi, nao walianguka kwa mikono ya Daudi na watu wake.

< 1 Chronicles 20 >