< 1 Chronicles 18 >

1 Some time later, David’s [army] attacked the army of Philistia and defeated them. They captured Gath [city] and the surrounding villages.
Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Gathi pamoja na vijiji vinavyouzunguka kutoka utawala wa Wafilisti.
2 His [army] also defeated [the army of] the Moab [people-group]. The people were forced to accept David as their ruler, and also to pay money [each year to David’s government, in order that David’s army would protect them].
Pia Daudi akawashinda Wamoabu, wakawa watumishi wake, nao wakawa wanamletea ushuru.
3 David’s [army] also fought against [the army of] Hadadezer, the king of [the] Zobah [region in Syria] near Hamath [city], when Hadadezer was trying to establish control over the area near the Euphrates River.
Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mfalme wa Soba, hadi Hamathi, wakati alikwenda kuimarisha utawala wake katika Mto Frati.
4 David’s [army] captured 1,000 of Hadadezer’s chariots, 7,000 chariot-drivers, and 20,000 soldiers. They hamstrung/crippled most of their horses; there were only 100 horses that they did not cripple.
Daudi akateka magari ya vita 1,000 miongoni mwa magari yake, waendesha hayo magari ya kukokotwa na farasi 7,000 na askari wa miguu 20,000. Daudi akakata mishipa ya miguu ya nyuma ya farasi wote wakokotao magari, ila akabakiza 100.
5 When the army of Syria came from Damascus [city] to help Hadadezer’s [army], David’s soldiers killed 22,000 of them.
Waaramu wa Dameski, walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
6 Then David stationed groups of his soldiers in Damascus, and the people of Syria were forced to accept David as their ruler, and to pay to David’s government [each year] the payment/tax that he demanded. And Yahweh enabled David’s [army] to win battles everywhere they went.
Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski. Basi Waaramu wakawa watumwa wa Daudi, na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
7 David soldiers took the gold shields that were carried by the officers of Hadadezer’s [army] and brought them to Jerusalem.
Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
8 They also brought from Tebah (OR, Tibhath) and Cun, two towns that belonged to Hadadezer, a lot of bronze, which [David’s son] Solomon [later] used to make the huge bronze basin and the pillars and other bronze items [for the temple].
Kutoka miji ya Tibhathi na Kuni, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Daudi akatwaa shaba nyingi sana, ambayo Solomoni aliitumia kutengenezea ile Bahari ya shaba, zile nguzo na vifaa mbalimbali vya shaba.
9 When Tou, the king of Hamath [city in Syria], heard that David’s [army] had defeated the entire army of King Hadadezer,
Tou mfalme wa Hamathi aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri mfalme wa Soba,
10 he sent his son Hadoram to King David, to greet him and (congratulate him/tell him that he was happy) about his defeating Hadadezer’s army, which had been fighting [the army of] Tou. Hadoram brought to David many items/gifts made of gold, silver, and bronze.
akamtuma mwanawe, Hadoramu kwa Mfalme Daudi ili kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Mfalme Hadadezeri, kwa kuwa alikuwa amepigana vita mara nyingi na Tou. Hadoramu akamletea Daudi vifaa mbalimbali vya dhahabu, fedha na shaba.
11 King David dedicated those things to Yahweh, like he had done with the silver and gold that his soldiers had taken from [the] Edom and Moab [people-groups], and from the Ammon people-group and from the people of Philistia, and from [the descendants of] Amalek.
Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu aliyokuwa ameitwaa katika mataifa yote haya: Edomu na Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki.
12 [One of David’s army commanders, ] Abishai, whose mother was Zeruiah, went with his army and killed 18,000 soldiers from Edom in the Salt Valley.
Abishai mwana wa Seruya akawaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
13 Then David stationed groups of his soldiers there in Edom, and the people of Edom were forced to accept David as their king and to pay money to David’s government [every year]. And Yahweh enabled David’s [army] to win battles wherever they went.
Akaweka kambi za askari walinzi huko Edomu, nao Waedomu wote wakawa watumishi wa Daudi. Bwana akampa Daudi ushindi kila alipokwenda.
14 David ruled over all the Israeli people, and he always did for them what was just and fair.
Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
15 Zeruiah’s son Joab was the chief army commander. Jehoshaphat the son of Ahilud was the record-keeper.
Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
16 Zadok the son of Ahitub and Ahimelech the son of Abiathar were the Supreme Priests. Shavsha was the official secretary.
Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Shausha alikuwa mwandishi;
17 Benaiah the son of Jehoiada ruled over the Kereth and Peleth groups [who were David’s bodyguards]. And David’s sons were his most important officials.
naye Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa maafisa wakuu katika utumishi wa mfalme.

< 1 Chronicles 18 >