< Matthew 4 >
1 Then Jesus was led up into the wilderness by the Spirit to be tempted by the devil.
Kisha Yesu akaongozwa na Roho Mtakatifu kwenda nyikani ili akajaribiwe na ibilisi.
2 After fasting for forty days and forty nights, he was hungry.
Baada ya kufunga siku arobaini usiku na mchana, hatimaye akaona njaa.
3 Then the tempter came up to him and said, “If yoʋ are the Son of God, command these stones to become bread.”
Mjaribu akamjia na kumwambia, “Ikiwa wewe ndiye Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yawe mikate.”
4 But Jesus answered, “It is written, ‘Man shall not live by bread alone, but by every word that comes from the mouth of God.’”
Lakini Yesu akajibu, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.’”
5 Then the devil took him to the holy city, set him on the pinnacle of the temple,
Ndipo ibilisi akamchukua Yesu mpaka mji mtakatifu na kumweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu,
6 and said to him, “If yoʋ are the Son of God, throw yoʋrself down, for it is written, ‘He will command his angels concerning yoʋ,’ and, ‘In their hands they will lift yoʋ up, so that yoʋ do not strike yoʋr foot against a stone.’”
akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini. Kwa kuwa imeandikwa: “‘Atakuagizia malaika zake, nao watakuchukua mikononi mwao ili usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’”
7 Jesus said to him, “Again it is written, ‘Yoʋ shall not put the Lord yoʋr God to the test.’”
Yesu akamjibu, “Pia imeandikwa: ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”
8 Again, the devil took him to a very high mountain and showed him all the kingdoms of the world and their glory.
Kwa mara nyingine, ibilisi akamchukua Yesu mpaka kwenye kilele cha mlima mrefu na kumwonyesha falme zote za dunia na fahari zake,
9 And he said to him, “All these things I will give yoʋ, if yoʋ will fall down and worship me.”
kisha akamwambia, “Nitakupa hivi vyote kama ukinisujudia na kuniabudu.”
10 Then Jesus said to him, “Get behind me, Satan! For it is written, ‘Yoʋ shall worship the Lord yoʋr God, and him only shall yoʋ serve.’”
Yesu akamwambia, “Ondoka mbele yangu, Shetani! Kwa maana imeandikwa, ‘Mwabudu Bwana Mungu wako, na umtumikie yeye peke yake.’”
11 Then the devil left him, and behold, angels came and ministered to him.
Ndipo ibilisi akamwacha, nao malaika wakaja na kumhudumia.
12 Now when Jesus heard that John had been put in prison, he withdrew to Galilee.
Yesu aliposikia kwamba Yohana Mbatizaji alikuwa ametiwa gerezani, alirudi Galilaya.
13 And leaving Nazareth, he went and dwelt at Capernaum by the sea, in the region of Zebulun and Naphtali,
Akaondoka Nazareti akaenda kuishi Kapernaumu, mji ulioko karibu na bahari, katika mipaka ya nchi ya Zabuloni na Naftali,
14 so that what had been spoken by the prophet Isaiah might be fulfilled:
ili kutimiza unabii wa nabii Isaya, kama alivyosema:
15 “Land of Zebulun and land of Naphtali, way of the sea, beyond the Jordan, Galilee of the Gentiles,
“Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, kwenye njia ya kuelekea baharini, ngʼambo ya Yordani, Galilaya ya watu wa Mataifa:
16 the people sitting in darkness have seen a great light, and on those sitting in the region and shadow of death light has dawned.”
watu wale waliokaa gizani wameona nuru kuu; nao wale walioishi katika nchi ya uvuli wa mauti, nuru imewazukia.”
17 From that time Jesus began to preach, “Repent, for the kingdom of heaven has drawn near.”
Tangu wakati huo, Yesu alianza kuhubiri akisema: “Tubuni, kwa maana Ufalme wa Mbinguni umekaribia.”
18 As Jesus was walking by the Sea of Galilee, he saw two brothers, Simon (who is called Peter) and Andrew his brother, casting a net into the sea, for they were fishermen.
Yesu alipokuwa anatembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea ndugu yake. Walikuwa wakizitupa nyavu zao baharini kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
19 Jesus said to them, “Follow me, and I will make you fishers of men.”
Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
20 So they immediately left their nets and followed him.
Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
21 Going on from there, he saw two other brothers, James the son of Zebedee and John his brother, in the boat with their father Zebedee, mending their nets, and he called them.
Alipoendelea mbele kutoka pale, akawaona ndugu wengine wawili, Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa wamekaa kwenye mashua pamoja na baba yao Zebedayo, wakizitengeneza nyavu zao. Yesu akawaita.
22 So they immediately left the boat and their father and followed him.
Nao mara wakaiacha mashua yao, pamoja na baba yao, wakamfuata.
23 Then Jesus went throughout all of Galilee, teaching in their synagogues, preaching the gospel of the kingdom, and healing every disease and every sickness among the people.
Yesu akapita katika Galilaya yote, akifundisha katika masinagogi yao, akihubiri habari njema za Ufalme, na akiponya kila ugonjwa na kila aina ya maradhi miongoni mwa watu.
24 So the news about him went out into all of Syria, and the people brought to him all who were sick with various diseases, those suffering severe pain, the demon-possessed, epileptics, and paralytics. And he healed them.
Kwa hiyo sifa zake zikaenea sehemu zote za Shamu, nao watu wakamletea wote waliokuwa na magonjwa mbalimbali na maumivu, waliopagawa na pepo wachafu, wenye kifafa na waliopooza, naye akawaponya.
25 And large crowds followed him from Galilee, the Decapolis, Jerusalem, Judea, and from beyond the Jordan.
Makutano makubwa ya watu yakawa yanamjia kutoka Galilaya, Dekapoli, Yerusalemu, Uyahudi na kutoka ngʼambo ya Mto Yordani.