< Mark 7 >

1 Now the Pharisees and some of the scribes who had come from Jerusalem were gathered around Jesus.
Mafarisayo na baadhi ya waandishi ambao walikuwa wametokea Yerusalemu walikusanyika kumzunguka yeye.
2 When they saw some of his disciples eating bread with hands that were defiled (that is, unwashed), they criticized them.
Na waliona kuwa baadhi ya wanafunzi wake walikula mkate kwa mikono najisi; ambayo haikuoshwa.
3 (For none of the Pharisees or Jews eat unless they wash their hands properly, holding to the tradition of the elders.
(kwa Mafarisayo na Wayahudi wote hawali mpaka wameosha mikono yao vizuri; wanashikilia utamaduni wa wazee. Wakati
4 And when they come from the marketplace, they do not eat unless they have washed. There are also many other traditions they observe, such as the washing of cups, pots, copper vessels, and dining couches.)
Mafarisayo wanaporudi kutoka mahali pa soko, hawali mpaka wameoga kwanza. Na kuna sheria zingine ambazo wanazifuata kabisa, ikiwa ni pamoja na kuosha vikombe, masufuria, vyombo vya shaba, na hata viti vinavyotumika wakati wa chakula.)
5 Now the Pharisees and the scribes asked Jesus, “Why do yoʋr disciples not walk according to the tradition of the elders, but eat bread with unwashed hands?”
Mafarisayo na waandishi walimuuliza Yesu, “Kwa nini wanafunzi wako hawaishi kulingana na tamaduni za wazee, kwani wanakula mkate pasipo kunawa mikono?”
6 He answered them, “Isaiah prophesied rightly about you hypocrites, as it is written, ‘This people honors me with their lips, but their heart is far from me.
Lakini yeye aliwaambia, “Isaya alitabiri vizuri kuhusu ninyi wanafiki, aliandika, 'Watu hawa wananiheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali na mimi.
7 They worship me in vain, teaching as doctrines the commandments of men.’
Wananifanyia ibaada zisizo na maana, wakifundisha sheria za wanadamu kama mapokeo yao.'
8 For you have neglected the commandment of God and are holding to the tradition of men, such as various washings of pots and cups. And you do many other similar things such as these.”
Mmeiacha sheria ya Mungu na kushikilia kwa wepesi tamaduni za wanadamu.”
9 Then he said to them, “You have a fine way of setting aside the commandment of God so that you may keep your tradition!
Na akasema kwao, “Mmeikataa amri ya Mungu kwa urahisi ili kwamba mtunze tamaduni zenu!
10 For Moses said, ‘Honor yoʋr father and yoʋr mother,’ and, ‘Whoever speaks evil of his father or mother must surely die.’
Kwa kuwa Musa alisema, 'mheshimu baba yako na mama yako,' na 'Yeye asemaye mabaya juu ya baba yake au mama yake hakika atakufa.'
11 But you teach that it is acceptable for a man to say to his father or mother, ‘Whatever benefit yoʋ might have received from me is Corban’” (that is, a gift devoted to God).
Lakini mnasema, 'kama mtu akisema kwa baba yake au mama, “Msaada wowote ambao mngepokea kutoka kwangu ni hazina ya Hekalu,”' (hiyo ni kusema kwamba, 'imetolewa kwa Mungu')
12 “In this way you no longer permit him to do anything for his father or his mother,
hivyo haumruhusu kufanya jambo lolote kwa ajili ya baba au mama yake.
13 thus nullifying the word of God by your tradition that you have handed down. And you do many similar things such as these.”
Mnaifanya amri ya Mungu kuwa bure kwa kuleta tamaduni zenu. Na mambo mengi ya jinsi hiyo mnayoyafanya.”
14 Then Jesus called over the entire crowd and said to them, “Listen to me, all of you, and understand:
Aliwaita makutano tena na kuwaambia, “Mnisikilize mimi, ninyi nyote, na mnielewe.
15 There is nothing outside of a person that can defile him by going into him, but the things that come out of a person are what defile him.
Hakuna chochote kutoka nje ya mtu ambacho chaweza kumchafua mtu kiingiapo kwake. Bali ni kile kimtokacho mtu ndicho kimchafuacho.
16 If anyone has ears to hear, let him hear.”
(Zingatia: mstari huu, “kama mtu yeyote ana masikio ya kusikia, na asikie” haumo kwenye nakala za kale).
17 After Jesus had left the crowd and gone into a house, his disciples asked him about the parable.
Yesu alipowaacha makutano na kuingia nyumbani, wanafunzi wake wakamwuliza kuhusu mfano huo.
18 He said to them, “So are you also without understanding? Do you not understand that whatever goes into a person from the outside cannot defile him?
Yesu akasema, “Na ninyi pia bado hamjaelewa? Hamuoni kwamba chochote kimuingiacho mtu hakiwezi kumchafua,
19 For it does not go into his heart but into his stomach; then it goes out into the latrine, thus purifying all foods.”
kwa sababu hakiwezi kwenda kwenye moyo wake, lakini kinaingia katika tumbo lake na kisha kinapita kwenda chooni.” Kwa maelezo haya Yesu alivifanya vyakula vyote kuwa safi.
20 He also said, “It is what comes out of a person that defiles a person.
Alisema, “Ni kile ambacho kinamtoka mtu ndicho kimchafuacho.
21 For from within, from the hearts of men, come evil thoughts, adultery, fornication, murder,
Kwa kuwa hutoka ndani ya mtu, nje ya moyo, hutoka mawazo maovu, zinaa, wizi, mauaji,
22 theft, covetousness, wickedness, deceit, sensuality, envy, slander, pride, and foolishness.
uasherati, tamaa mbaya, uovu, udanganyifu, kujamiiana, wivu, kashfa, majivuno, ujinga.
23 All these evil things come from within and defile a person.”
Maovu haya yote yanatoka ndani, ndiyo yale yamchafuayo mtu.”
24 Then Jesus rose from there and went away to the region of Tyre and Sidon. He went into a house and did not want anyone to know it, yet he could not escape notice.
Aliamka kutoka pale na kuondoka kwenda katika mkoa wa Tiro na Sidoni. Aliingia ndani na hakutaka mtu yeyote ajue kuwa alikuwa hapo, lakini haikuwezekana kumficha.
25 For a woman whose little daughter had an unclean spirit heard about him and came and fell at his feet.
Lakini ghafla mwanamke, ambaye mtoto wake mdogo alikuwa na roho mchafu, alisikia habari zake, akaja, na akaanguka miguuni pake.
26 (This woman was a Greek, a Syrophoenician by birth.) She asked Jesus to cast the demon out of her daughter.
Mwanamke huyo alikuwa Myunani, wa kabila la Kifoeniki. Alimsihi yeye amfukuze pepo kutoka kwa binti yake.
27 But Jesus said to her, “Let the children first be filled, for it is not good to take the children's bread and throw it to the dogs.”
Yesu akamwambia mwanamke, “Waache watoto walishwe kwanza, kwa kuwa sio sawa kuuchukua mkate wa watoto na kuwatupia mbwa.”
28 She answered him, “Yes, Lord, yet even the dogs under the table eat the children's crumbs.”
Lakini mwanamke akamjibu na kusema, “Ndiyo Bwana, hata mbwa chini ya meza hula mabaki ya chakula cha watoto.”
29 Then he said to her, “Because of this reply, yoʋ may go; the demon has come out of yoʋr daughter.”
Akamwambia, “Kwa kuwa umesema hivi, uko huru kwenda. Pepo ameshamtoka binti yako.”
30 And when she went to her house, she found the demon gone and her daughter lying in bed.
Mwanamke alirudi nyumbani kwake na akamkuta binti yake amelala kitandani, na pepo alikuwa amemtoka.
31 Then Jesus came back from the region of Tyre and Sidon and went to the Sea of Galilee, within the region of the Decapolis.
Yesu alitoka tena nje ya mkoa wa Tiro na kupitia Sidoni kuelekea Bahari ya Galilaya mpaka kanda ya Dikapolisi.
32 Some people brought to him a deaf man who had a speech impediment, and they begged him to lay his hand on the man.
Na wakamletea mtu aliyekuwa kiziwi na alikuwa hawezi kuzungumza vizuri, walimsihi Yesu aweke mikono juu yake.
33 So Jesus took him aside privately, away from the crowd. Then he put his fingers into the man's ears, spit, and touched the man's tongue.
Alimtoa nje ya kusanyiko kwa siri, na akaweka vidole vyake kwenye masikio yake, na baada ya kutema mate, aligusa ulimi wake.
34 And looking up to heaven, he sighed and said to him, “Ephphatha” (that is, “Be opened”).
Alitazama juu mbinguni, akahema na kumwambia, “Efata,” hiyo ni kusema “funguka!”
35 Immediately the man's ears were opened, the impediment of his tongue was removed, and he began speaking clearly.
Na muda ule ule masikio yakafunguka, na kilichokuwa kimezuia ulimi kiliharibiwa na akaweza kuongea vizuri.
36 Then Jesus ordered them not to tell anyone. But as much as he ordered them not to do so, they proclaimed it all the more.
Na aliwaamuru wasimwambie mtu yeyote. Lakini kadri alivyowaamuru, ndivyo walivyotangaza habari hizo kwa wingi.
37 And they were completely astonished, saying, “He has done all things well. He even makes the deaf hear and the mute speak.”
Hakika walishangazwa, na kusema, “Amefanya kila kitu vizuri. Hata amewafanya viziwi kusikia na mabubu kuongea.”

< Mark 7 >