< Matthew 25 >

1 Then may the kingdom of heaven be shadowed forth by ten virgins, who took their lamps and went out to meet the bridegroom and bride.
Ndipo ufalme wa mbinguni utafananishwa na wanawali kumi waliochukua taa zao na kuondoka kwenda kumpokea bwana harusi.
2 And five of them were wise, and five were foolish.
Watano miongoni mwao walikuwa wapumbavu na watano wengine walikuwa werevu.
3 And the foolish took their lamps, but took no oil with them.
Wanawali wapumbavu walipochukua taa zao, hawakuchukua mafuta yoyote.
4 But the wise took oil in vessels, with their lamps.
Bali wanawali welevu walichukua vyombo vyenye mafuta pamoja na taa zao.
5 And while the bridegroom delayed, they all became sleepy and fell asleep.
Sasa wakati bwana harusi amechelewa kufika, wote walishikwa usingizi na wakalala.
6 And at midnight there was an outcry: Behold, the bridegroom cometh; go ye out to meet him.
Lakini wakati wa usiku wa manane kulikuwa na yowe, 'Tazama, bwana harusi! Tokeni nje mkampokee.'
7 Then all those virgins arose, and trimmed their lamps.
Ndipo hao wanawali waliamka wote na kuwasha taa zao.
8 And the foolish said to the wise; Give us of your oil; for, behold, our lamps have gone out.
Wale wapumbavu waliwaambia wale welevu, 'Mtupatie sehemu ya mafuta yenu kwa sababu taa zetu zinazimika.'
9 The wise answered and said: We must refuse, lest there should not be enough for us and for you: but go ye to them that sell, and buy for yourselves.
Lakini wale welevu waliwajibu na kuwaambia, 'Kwa kuwa hayatatutosha sisi na ninyi, badala yake nendeni kwa wanaouza mjinunulie kiasi kwa ajili yenu.'
10 And while they went to buy, the bridegroom came; and they that were ready, went with him into the house of the nuptials, and the door was shut.
Wakati wameenda huko kununua, Bwana harusi alifika, na wote waliokuwa tayari walienda naye kwenye sherehe ya harusi, na mlango ulifungwa.
11 And at length came also the other virgins, and said: Our lord, our lord, open to us.
Baadaye wale wanawali wengine pia walifika na kusema, 'Bwana, bwana, tufungulie.'
12 But he answered, and said to them: Verily I say to you, I know you not.
Lakini alijibu na kusema, 'Kweli nawaambia, Mimi siwajui.'
13 Watch, therefore, seeing ye know not the day nor the hour.
Kwa hiyo angalieni, kwa kuwa hamjui siku au saa.
14 For, as a man that took a journey, called his servants and delivered to them his property;
Kwa kuwa ni sawa na mtu alipotaka kusafiri kwenda nchi nyingine. Aliwaita watumwa wake na kuwakabidhi utajiri wake.
15 to one he gave five talents; to another, two; and to another, one: to each, according to his ability: and he immediately departed.
Mmoja wao alimpatia talanta tano, mwingine alimpa mbili, na yule mwingine alimpa talanta moja. Kila mmoja alipokea kiasi kulingana na uwezo wake, na yule mtu alisafari kwenda zake.
16 Then he that received five talents, went and traded with them, and gained five more.
Mapema yule aliyepokea talanta tano alienda kuziwekeza, na kuzalisha talanta zingine tano.
17 And likewise: the one of two talents, by trading gained two more.
Vilevile yule aliyepokea talanta mbili, alizalisha zingine mbili.
18 But he that received one, went and digged in the earth, and hid his lord's money.
Lakini mtumwa aliyepokea talanta moja, alienda zake, akachimba shimo ardhini, na kuificha fedha ya bwana wake.
19 And after a long time, the lord of those servants came, and received account from them.
Na baada ya muda mrefu, bwana wa watumwa hao alirudi na kutengeneza mahesabu nao.
20 And he who had received the five talents, came and brought five others; and said, My lord, thou gavest me five talents; behold, I have gained by trading five more to them.
Yule mtumwa aliyepokea talanta tano alikuja na kuleta talanta zingine tano, akasema, 'Bwana, ulinipa talanta tano. Tazama, nimepata faida ya talanta zingine tano.'
21 His lord said to him: Well done! good and faithful servant: thou hast been faithful with a little; I will set thee over much: enter thou into the joy of thy lord.
Bwana wake alimwambia, 'Hongera, mtumwa mzuri na mwaminifu! Umekuwa mwaminifu kwa vitu vidogo. Nitakupa madaraka juu ya vitu vingi. Ingia katika furaha ya bwana wako.'
22 And he of the two talents came, and said: My lord, thou gavest me two talents; behold, I have by trading gained two more to them.
Mtumwa aliyepokea talanta mbili alikuja na kusema, 'Bwana, ulinipa talanta mbili. Tazama, nimepata faida ya talanta zingine mbili,'
23 His lord said to him: Well done! good and faithful servant: thou hast been faithful with a little; I will set thee over much: enter thou into the Joy of thy lord.
Bwana wake alimwambia, 'Hongera, mtumwa mzuri na mwaminifu! Umekuwa mwaminifu kwa vitu vichache. Nitakupa madaraka juu ya vitu vingi. Ingia katika furaha ya bwana wako.'
24 And he also that received the one talent, came and said: My lord, I knew thee, that thou art a hard man, reaping where thou hast not sowed, and gathering where thou hast not scattered;
Baadaye mtumwa aliyepokea talanta moja alikuja na kusema, 'Bwana, najua kuwa wewe ni mtu mkali. Unachuma mahali ambapo hukupanda, na unavuna mahali ambapo hukusia.
25 and I was afraid, and I went and hid thy talent in the earth. Behold, thou hast what is thine.
Mimi niliogopa, nikaenda zangu na kuificha talanta yako katika udongo. Tazama, unayo hapa ile iliyo yako.'
26 His lord answered, and said to him: Wicked and slothful servant! Thou knewest me, that I reap where I have not sowed, and gather where I have not scattered!
Lakini bwana wake alijibu na kusema, 'Wewe mtumwa mwovu na mzembe, ulijua kwamba ninachuma mahali ambapo sijapanda na kuvuna mahali ambapo sikusia.
27 Thou oughtest to have cast my money into the exchange; and I might have come and demanded my property with its interest.
Kwahiyo ulipaswa kuwapa fedha yangu watu wa benki, na wakati wa kurudi kwangu ningeipokea ile yangu pamoja na faida.
28 Take therefore the talent from him, and give it to him that hath ten talents.
Kwa hiyo mnyang'anyeni hiyo talanta na mpeni yule mtumwa aliye na talanta kumi.
29 For, to him that hath, shall be given, and he shall have more; but from him that hath not, even what he hath shall be taken away.
Kila mtu aliye nacho, ataongezewa zaidi-hata kwa kuzidishiwa sana. Lakini kwa yeyote asiye na kitu, hata alicho nacho atanyang'anywa.
30 And cast ye the unprofitable servant into the outer darkness: there will be weeping and gnashing of teeth.
Mtupeni nje gizani huyo mtumwa asiyefaa, ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.'
31 And when the Son of man shall come in his glory, and all his holy angels with him, then will he sit upon the throne of his glory.
Wakati Mwana wa Adamu atakapokuja katika utukufu wake, na malaika wote pamoja naye, ndipo atakapokaa juu ya kiti chake cha utukufu.
32 And before him will be gathered all nations; and he will separate them one from another, as a shepherd severeth the sheep from the goats.
Mataifa yote yatakusanyika mbele zake, naye atawatenganisha watu, kama vile mchungaji anavyowatenganisha kondoo na mbuzi.
33 And he will place the sheep on his right hand, and the goats on his left.
Atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, bali mbuzi atawaweka mkono wa kushoto.
34 Then will the king say to those on his right hand: Come, ye blessed of my Father; inherit the kingdom that was prepared for you from the foundation of the world.
Kisha mfalme atawaambia wale walio mkono wake wa kulia, 'Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme ulioandaliwa kwa ajili yenu tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu.
35 For I was hungry, and ye gave me food; I was thirsty, and ye gave me drink; I was a stranger, and ye took me home;
Kwa kuwa nilikuwa na njaa na mlinipa chakula; Nilikuwa mgeni na mlinikaribisha;
36 I was naked, and ye clothed me; I was sick, and ye visited me; I was in prison, and ye came to me.
Nilikuwa uchi, na mlinivika nguo; Nilikuwa mgonjwa na mkanitunza; Nilikuwa kifungoni na mkaniijia.'
37 Then will the righteous say to him: Our Lord, when saw we thee hungry, and fed thee? or thirsty, and gave thee drink?
Ndipo wenye haki watamjibu na kumwambia, 'Bwana, lini tulikuona ukiwa na njaa, na kukulisha? Au una kiu na tukakupa maji?
38 And when saw we thee a stranger, and took thee home? or naked, and clothed thee?
Na lini tulikuona ukiwa mgeni, na tukakukaribisha? Au ukiwa uchi na tukakuvisha nguo?
39 And when saw we thee sick, or in prison, and came to thee?
Na lini tulikuona ukiwa mgonjwa, au katika kifungo, na tukakujia?
40 And the king will answer, and say to them: Verily I Say to you, That inasmuch as ye did so to one of these my little brothers, ye did so to me.
Na mfalme atawajibu na kuwaambia, 'Kweli nawaambia, mlichotenda hapa kwa mmoja wa ndugu zangu wadogo, mlinitendea mimi.'
41 Then will he say also to them on his left hand: Go from me, ye accursed, into everlasting fire, which was prepared for the Calumniator and his angels, (aiōnios g166)
Ndipo atawaambia hao walio mkono wake wa kushoto, 'Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, nendeni katika moto wa milele ulioandaliwa kwa ajili ya shetani na malaika zake, (aiōnios g166)
42 For I was hungry, and ye gave me no food; and I was thirsty, and ye gave me no drink;
kwa sababu nilikuwa na njaa lakini hamkunipa chakula; Nilikuwa na kiu lakini hamkunipa maji;
43 and I was a stranger, and ye took me not home; and I was naked, and ye clothed me not; and I was sick and in prison, and ye did not visit me.
Nilikuwa mgeni lakini hamkunikaribisha; nikiwa uchi lakini hamkunipa mavazi; nikiwa mgonjwa na nikiwa kifungoni, lakini hamkunitunza.'
44 Then will they also answer and say: Our Lord, when saw we thee hungry, or thirsty, or a stranger, or naked, or sick, or in prison, and did not minister to thee?
Ndipo wao pia watamjibu na kusema, 'Bwana, lini tulikuona ukiwa na njaa, au una kiu, au u mgeni, au ukiwa uchi, au ukiwa mgonjwa, au ukiwa mfungwa, na hatukukuhudumia?
45 Then will he answer, and say to them: Verily I say to you, That in as much as ye did not so to one of these little ones, ye did not so to me.
Kisha atawajibu na kusema, 'Kweli nawaambia, kile ambacho hamkutenda kwa mmoja wa hawa wadogo, hamkunitendea mimi.'
46 And these will go into everlasting torment, and the righteous into everlasting life. (aiōnios g166)
Hawa watakwenda katika adhabu ya milele bali wenye haki katika uzima wa milele.” (aiōnios g166)

< Matthew 25 >