< Luke 23 >
1 And the whole company of them arose, and carried him before Pilate.
Mkutano wote wakasimama, wakampeleka Yesu mbele ya Pilato.
2 And they began to accuse him, and said: We have found this man seducing our people, and forbidding to pay the capitation money to Caesar, and declaring himself to be king Messiah.
Wakaanza kumshutumu, wakisema, “Tumemkuta mtu huyu akipotosha taifa letu, kwa kukataza tusitoe kodi kwa Kaisari, na akisema kwamba yeye mwenyewe ni Kristo, Mfalme.”
3 And Pilate interrogated him, and said to him: Art thou king of the Jews? He said to him: Thou hast said.
Pilato akamuuliza, akisema, “Je wewe ni Mfalme wa Wayahudi?” Na Yesu akamjibu akisema, “Wewe wasema hivyo”.
4 And Pilate said to the chief priests and the company: I find no crime upon this man.
Pilato akamuambia kuhani mkuu na makutano, “Sioni kosa kwa mtu huyu”.
5 And they vociferated, and said: He raiseth disturbance among our people, by teaching in all Judaea, commencing from Galilee, and quite to this place.
Lakini wao wakasisitiza, wakisema, “Amekuwa akiwachochea watu, akifundisha katika Uyahudi yote, kuanzia Galilaya na sasa yuko hapa.”
6 And Pilate, when he heard the name Galilee, inquired if the man were a Galilean.
Pilato aliposikia haya, akaulizia kama mtu huyo ni wa Galilaya?
7 And having learned that he was from under Herod's jurisdiction, he sent him to Herod; for he was at Jerusalem on those days.
Alipotambua kuwa alikuwa chini ya utawala wa Herode, akampeleka Yesu kwa Herode, ambaye naye alikuwa Yerusalemu kwa siku hizo.
8 And Herod rejoiced greatly when he saw Jesus, for he had been desirous to see him for a long time, because he had heard many things of him, and he hoped to see some sign from him.
Herode alipomuona Yesu, alifurahi sana kwasababu alitaka kumuona kwa siku nyingi. Alisikia habari zake na alitamani kuona moja ya miujiza ikifanywa na yeye.
9 And he asked him many questions; but Jesus gave him no reply.
Herode alimhoji Yesu kwa maneno mengi, lakini Yesu hakumjibu chochote.
10 And the chief priests and Scribes stood up, and accused him vehemently.
Makuhani wakuu pamoja na waandishi walisimama kwa ukali wakimshitaki.
11 And Herod and his warriors contemned him. And when he had mocked him, he clothed him in a purple robe, and sent him to Pilate.
Herode pamoja na maaskari wake, walimtukana na kumdhihaki, na kumvika mavazi mazuri, kisha akamrudisha Yesu kwa Pilato.
12 And on that day, Pilate and Herod became friends to each other; for there had previously been enmity between them.
Herode na Pilato wakawa marafiki kuanzia siku hiyo, (kabla ya hapo walikuwa maadui).
13 And Pilate called the chief priests and the rulers of the people,
Pilato akawaita pomoja makuhani wakuu na watawala na umati wa watu,
14 and said to them: Ye have brought this man before me, as a disturber of your people; and lo, I have examined him before you, and I find in the man no crime, among all that ye charge upon him.
Akawaambia, “Mmeniletea mtu huyu kama mtu anaye waongoza watu wafanye mabaya, na tazama, baada ya kuwa nimemhoji mbele yenu, sikuona kosa kwa mtu huyu kuhusu mambo yote ambayo ninyi mnamshitaki yeye.
15 Neither yet Herod: for I sent him to him, and lo, nothing deserving death hath been done by him.
Hapana, wala Herode, kwa maana amemrudisha kwetu, na tazama hakuna chochote alichokifanya kinachostahili adhabu ya kifo.
16 I will therefore chastise him, and release him.
Kwahiyo basi nitamuadhibu na kumuachilia.
17 For it was a custom, that he should release one at the festival.
(Sasa, Pilato anawajibika kumuachilia mfungwa mmoja kwa wayahudi wakati wa sikukuu).
18 And all the company vociferated, and said: Away with this man; and release to us Barabbas.
Lakini wote wakapiga kelele pamoja, wakisema, “Mwondoe huyo, na tufungulie Baraba!”
19 He was one who had been thrown into prison, on account of a sedition and murder which had occurred in the city.
Baraba alikuwa ni mtu ambaye amewekwa gerezani kwa sababu ya uasi fulani katika jiji na kwa kuua.
20 And Pilate, being disposed to release Jesus, conversed with them again.
Pilato akawaambia tena, akitamani kumwachilia Yesu.
21 But they cried out, and said: Crucify him; crucify him.
Lakini wao wakapiga kelele, wakisema, “Msulibishe, msulibishe.”
22 And he said to them the third time: But, what evil hath he done? I find no crime in him deserving of death. I will scourge him, therefore, and release him.
Akawauliza kwa mara ya tatu, “kwa nini, huyu mtu amefanya maovu gani? Sikupata kosa linalostahili adhabu ya kifo kwake. Kwahiyo nitakapo maliza kumuadhibu nitamuachilia.”
23 But they were urgent, with a loud voice; and demanded of him, that they might crucify him.
Lakini wakasisitiza kwa sauti ya juu, wakitaka asulubiwe. Na sauti zao zikamshawishi Pilato.
24 And Pilate decreed, that their request be granted.
Hivyo Pilato akaamua kuwapatia matakwa yao.
25 And he released to them him, who for sedition and murder had been cast into prison, for whom they petitioned; and he delivered up Jesus to their pleasure.
Akamuachilia yule waliyemtaka ambaye alifungwa kwa kusababisha ghasia na kuua. Lakini akamtoa Yesu kwa matakwa yao.
26 And as they led him away, they seized Simon the Cyrenian, coming from the fields. and laid upon him the cross, to bear it after Jesus.
Walipokuwa wakimpeleka, walimkamata mtu mmoja aitwaye Simoni wa Ukirene, akitokea katika nchi, wakamtwika msalaba ili abebe, akimfuata Yesu.
27 And there followed after him a great multitude of people; and those women also who wailed and lamented over him.
umati mkubwa wa watu, na wanawake ambao walihuzunika na kuomboleza kwa ajili yake, walikuwa wakimfuata.
28 And Jesus turned to them, and said to them: Daughters of Jerusalem, weep not for me; but weep rather for yourselves, and for your children.
Lakini akawageukia, Yesu akawaambia, 'Mabinti wa Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni ninyi wenyewe na kwa ya ajili watoto wenu.
29 For lo, the days are coming, in which they will say: Happy the barren, and the wombs that never bore, and the breasts that never nursed.
Tazama, siku zinakuja ambazo watasema, “Wamebarikiwa walio tasa na matumbo yasiyozaa, na matiti ambayo hayakunyonyesha.
30 Then will they begin to say to the mountains, Fall upon us! and to the hills, Cover us!
Ndipo watakapo anza kuiambia milima, 'Tuangukieni,' na vilima, 'Mtufunike.'
31 For if they do these things in a green tree, what will be in the dry?
Maana kama wakifanya mambo haya ikiwa mti mbichi, itakuwaje ukiwa mkavu?”
32 And there went along with him two others, malefactors, to be crucified.
wanaume wengine, wahalifu wawili, walipelekwa pamoja naye ili wauwawe.
33 And when they came to a certain place which is called a Skull, they crucified him there; and the two malefactors, the one on his right hand, and the other on his left.
Walipofika mahali paitwapo Fuvu la kichwa, ndipo wakamsulubisha pamoja na wale wahalifu, mmoja upande wa kulia na mwingine upande wa kushoto.
34 And Jesus said: Father, forgive them; for they know not what they do. And they divided his garments, casting a lot upon them.
Yesu alisema, “Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. “Nao wakapiga kura, kugawa mavazi yake.
35 And the people stood and looked on; and the rulers also derided him, and said: He quickened others; let him quicken himself, if he is the Messiah, the chosen of God.
Watu walikuwa wamesimama wakiangalia huku watawala wakimdhihaki, wakisema, “Aliwaokoa wengine. Sasa ajiokoe mwenyewe, kama yeye ni Kristo wa Mungu, mteule”.
36 And the soldiers like wise mocked him, coming to him and offering him vinegar,
Askari pia walimdharau, walimkaribia yeye na wakumpa siki,
37 and saying to him: If thou art the king of the Jews, quicken thyself.
wakisema, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi jiokoe mwenyewe”
38 And there was likewise a superscription over him, written in Greek, and Latin, and Hebrew: THIS IS THE KING OF THE JEWS.
Kulikuwa pia na alama juu yake iliyoandikwa “HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI.”
39 And one of the malefactors who were crucified with him, reproached him, and said: If thou art the Messiah, rescue thyself, and rescue us.
Mmoja wa wahalifu aliyesulubishwa alimtukana akisema, “Wewe si Kristo? jiokoe mwenyewe na sisi”
40 But his fellow Malefactor rebuked him, said to him: Art thou not afraid even of God, seeing thou art under the same sentence?
Lakini yule mwingine akajibu, akimkemea na akisema, “Je wewe humuogopi Mungu, nawe uko katika hukumu hiyo hiyo?
41 And we justly; for we have a retribution according to our deserts, and according to our deeds; but nothing hateful hath been done by him.
Sisi tupo hapa kwa haki, kwa maana sisi tunapokea kile tunachostahili kwa matendo yetu. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya.”
42 And he said to Jesus: My Lord, remember me, when thou comest into thy kingdom.
Na aliongeza, “Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.”
43 Jesus said to him: Verily I say to you, That this day thou shalt be with me in paradise.
Yesu akamwambia, “Amini nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”
44 And it was about the sixth hour; and darkness was over all the land, until the ninth hour.
Hapo ilikuwa karibu saa ya sita, giza likaja juu ya nchi yote hadi saa ya tisa,
45 And the sun was darkened, and the curtain of the door of the temple was rent through its middle.
Mwanga wa jua ulizimika. Kisha pazia la hekalu likagawanyika katikati kuanzia juu.
46 And Jesus cried with a loud voice, and said: My Father, into thy hand I commit my spirit. Thus he spake, and expired.
Akilia kwa sauti kuu, Yesu alisema, “Baba mikononi mwako naiweka roho yangu,” baada ya kusema haya, akafa.
47 And when the centurion saw what occurred, he glorified God and said: Certainly, this was a righteous man.
Wakati Akida alipoona yaliyotendeka alimtukuza Mungu akisema, “Hakika huyu alikuwa mtu mwenye haki.”
48 And all the multitudes who had assembled at this spectacle, on seeing what occurred, returned, smiting upon their breasts.
Wakati umati wa watu waliokuja pamoja kushuhudia walipoona mambo yaliyofanyika, walirudi huku wakipiga vifua vyao.
49 And there were standing at a distance, all they that knew Jesus, and those women who came with him from Galilee; and they beheld these things.
Lakini marafiki zake, na wanawake waliomfuata toka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiangalia hayo mambo.
50 And there was a certain man, whose name was Joseph, a counsellor, from Ramath a city of Judaea, who was a good man and righteous;
Tazama, palikuwepo na mtu aitwaye Yusufu, ambaye ni mmoja wa baraza, mtu mzuri na mwenye haki,
51 and he had not consented to their decision and deed; and he was waiting for the kingdom of God.
(alikuwa hajakubaliana na maamuzi au matendo yao), kutoka Armathaya, mji wa Kiyahudi, ambao ulikua ukisubiria ufalme wa Mungu.
52 This man went to Pilate, and begged the body of Jesus.
Mtu huyu, alimkaribia Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
53 And he took it down, and wrapped it in a winding-sheet of linen; and laid it in an excavated sepulchre, in which no one had hitherto been laid.
Alimshusha, na akauzungushia sanda, na akaumweka katika kaburi lililokuwa limechongwa katika jiwe, ambalo hakuna aliyewahi kuzikwa.
54 And it was the day of preparation, and the sabbath began to dawn.
Ilikuwa ni siku ya maandalizi, na Sabato inakaribia.
55 And those women who came with him from Galilee, approached, and viewed the sepulchre, and the manner in which the body was deposited.
Wanawake, waliokuja nao kutoka Galilaya, walimfuata, na wakaona kaburi na jinsi mwili wake ulivyolazwa.
56 And they returned, and prepared perfumes and aromatics; and they rested on the sabbath, as it is commanded.
Walirudi na kuanza kuandaa manukato na marashi. Kisha siku ya sabato walipumzika kwa mujibu wa sheria.