< Revelation 21 >

1 AND I saw new heavens and a new earth: for the first heaven and the first earth had gone, and the sea was no more.
Kisha nikaona mbingu mpya na dunia mpya. Mbingu ile ya kwanza na dunia ile ya kwanza vilikuwa vimetoweka, nayo bahari pia haikuweko tena.
2 And the holy city, Urishlem the new, I saw descending from heaven from Aloha, prepared as the bride is decked for her husband.
Nikaona mji mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka kwa Mungu mbinguni. Ulikuwa umetayarishwa vizuri kama bibi arusi aliyepambwa tayari kukutana na mumewe.
3 And I heard a great voice from heaven, saying, Behold, the tabernacle of Aloha is with men; and he will dwell with them, and they shall be his people; and Aloha himself will be with them, and will be their God.
Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka katika kiti cha enzi ikisema, “Tazama! Mungu amefanya makao yake kati ya watu. Atakaa kati yao, nao watakuwa watu wake, naye atakuwa Mungu wao.
4 And every tear shall be wiped away from their eyes, and death shall be no more; nor sorrow, nor clamour, nor pain, shall be any more; for the former things are passed away.
Yeye atayafuta machozi yao yote; maana hakutakuwako tena na kifo, wala uchungu, wala kilio, wala maumivu; maana ile hali ya kale imepita!”
5 And He who sat upon the throne said, Behold, I make all things new. And he said, Write: for these are the faithful and true words of Aloha.
Kisha yule aliyeketi juu ya kiti cha enzi akasema, “Tazama, nafanya yote mapya.” Tena akaniambia, “Andika hili, maana maneno haya ni ya kuaminika na ya kweli!”
6 And he said to me, I am Olaph and Thau, the Beginning and the End. To him who thirsteth I will give of the water of life freely.
Kisha akaniambia, “Yametimia! Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Aliye na kiu nitampa kinywaji cha bure kutoka katika chemchemi ya maji ya uzima.
7 He who overcometh shall inherit these; and I will be to him Aloha, and he shall be my son.
Yeyote atakayeshinda atapokea hiki, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.
8 But the fearful, and the faithless, and sinners, and the unclean, and murderers, and fornicators, and sorcerers, and servers of idols, and all liars, (shall have) their portion in the lake which burneth with fire and sulphur; which is the second death. (Limnē Pyr g3041 g4442)
Lakini watu waoga, wasioamini, wapotovu, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, na waongo wote, mahali pao patakuwa ndani ya lile ziwa linalowaka moto na kiberiti; hicho ndicho kifo cha pili.” (Limnē Pyr g3041 g4442)
9 And one of the seven angels who had the seven vials full of the seven last plagues, came and spake with me. saying, Come, I will show thee the bride, the wife of the Lamb.
Kisha mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na yale mabakuli saba yaliyokuwa yamejaa mabaa saba ya mwisho, akaja na kuniambia, “Njoo! Mimi nitakuonyesha bibi arusi, mkewe Mwanakondoo!”
10 And he led me in spirit upon a great and high mountain, and showed me the holy city Urishlem, descending from heaven from Aloha;
Basi, Roho akanikumba, naye malaika akanipeleka juu ya mlima mrefu sana. Akanionyesha mji mtakatifu, ukishuka kutoka kwa Mungu mbinguni,
11 having the glory of Aloha, as the clearness of light, like a stone of great price, as the stone Jaspon, resembling crystallos;
uking'aa kwa utukufu wa Mungu. Mwangaza wake ulikuwa kama wa jiwe la thamani kubwa kama yaspi, angavu kama kioo.
12 having a wall great and high, which had twelve gates, and names written upon them, which are the names of the twelve tribes of the sons of Israel.
Ulikuwa na ukuta mrefu na mkubwa, wenye milango kumi na miwili, na malaika wanangojea kumi na wawili. Majina ya wangoja milango kumi na mawili ya Israeli yalikuwa yameandikwa juu ya milango hiyo.
13 On the east three gates, and on the north three gates, and on the south three gates, and on the west three gates.
Kila upande ulikuwa na milango mitatu: upande wa mashariki, milango mitatu, kaskazini milango mitatu, kusini milango mitatu na magharibi milango mitatu.
14 And the wall of the city had twelve foundations; and upon them the twelve names of the twelve apostles of the Lamb.
Kuta za mji huo zilikuwa zimejengwa juu ya mawe ya msingi kumi na mawili, na juu ya mawe hayo yalikuwa yameandikwa majina na mitume kumi na wawili wa Mwanakondoo.
15 And he who talked with me had a measure, a rod of gold, that he might measure the city and the gates and the walls thereof.
Basi, yule malaika aliyekuwa anasema nami alikuwa na kijiti cha dhahabu cha kupimia, kwa ajili ya kuupima huo mji, milango yake na kuta zake.
16 And the city was set four-square, and the length of it was as the breadth: and he measured the city with the rod, upon twelve stadia of twelve thousand. And the length and the breadth and the height of it are equal.
Mji wenyewe ulikuwa wa mraba, upana na urefu wake sawa. Basi, malaika akaupima mji huo kwa kijiti chake: ulikuwa na urefu, upana na urefu wa kwenda juu, kama kilomita elfu mbili na mia nne.
17 And he measured the wall of it, an hundred and forty and four measures of the cubits of a man, that is, of the angel.
Kisha akaupima ukuta wake pia; nao ulikuwa mita sitini kwa kipimo cha macho cha kibinadamu ambacho malaika alitumia.
18 And the structure of the wall of it is (of) jaspis, and the city is of pure gold, like pure brightness.
Ukuta huo ulikuwa umejengwa kwa mawe mekundu ya thamani, na mji wenyewe ulikuwa umejengwa kwa dhahabu safi, angavu kama kioo.
19 And the foundations of the wall of the city were adorned with every precious stone: the first foundation was of jaspis, the second sathphiros, the third caledon, the fourth zmoragdo,
Mawe ya msingi wa ukuta huo yalikuwa yamepambwa kwa kila aina ya mawe ya thamani. Jiwe la kwanza la msingi lilikuwa jiwe la thamani jekundu, la pili yakuti samawati, la tatu kalkedoni, la nne zamaradi,
20 the fifth sardonicos, the sixth sardion, the seventh crisuthilos, the eighth berulla, the ninth topadion, the tenth chrosoposius, the eleventh hyacinthos, the twelfth amuthistos.
la tano sardoniki, la sita akiki, la saba krisolito, la nane zabarijadi, la tisa topazi, la kumi krisopraso, la kumi na moja yasinto, na la kumi na mbili amethisto.
21 And the twelve gates are twelve pearls, each of every one of the gates (a pearl), and each of every one of the pearls (a gate). And the wide street of the city was of pure gold as the brightness of light.
Na ile milango kumi na miwili ilikuwa lulu kumi na mbili; kila mlango ulikuwa umetengenezwa kwa lulu moja. Barabara kuu ya mji ilikuwa imetengenezwa kwa dhahabu safi, angavu kama kioo.
22 And a temple I saw not in it; for the Lord, the Omnipotent, is the temple thereof and the Lamb.
Sikuona hekalu katika mji huo, maana Bwana Mungu Mwenye Uwezo na yule Mwanakondoo ndio Hekalu lake.
23 And the city hath no need of the sun nor of the moon to enlighten it; for the glory of Aloha illuminateth it, and the light thereof is the Lamb.
Mji huo hauhitaji jua wala mwezi kuangazia, maana utukufu wa Mungu huuangazia, na taa yake ni yule Mwanakondoo.
24 And the nations of the saved walk by the light of it, and the kings of the earth bring their glory and the honour of the nations into it.
Watu wa mataifa watatembea katika mwanga wake, na wafalme wa dunia watauletea utajiri wao.
25 And the gates of it shall not be shut by day, for night is not there.
Milango ya mji huo itakuwa wazi mchana wote; maana hakutakuwa na usiku humo.
26 And they shall bring the glory and honour of the nations into it;
Fahari na utajiri wa watu wa mataifa utaletwa humo ndani.
27 and nothing shall enter into it that defileth, nor that worketh uncleanness; but they who are written in the book of life of the Lamb.
Lakini hakuna chochote kilicho najisi kitakachoingia humo; wala mtu yeyote atendaye mambo ya kuchukiza au ya uongo hataingia humo. Ni wale tu walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwanakondoo ndio watakaoingia ndani.

< Revelation 21 >