< Revelation 12 >
1 AND a great sign was seen in heaven; a woman clothed with the sun, and the moon beneath her feet, and upon her head a crown of twelve stars.
Ishara kuu ilionekana mbinguni: mwanamke aliyefunikwa na jua, na akiwa na mwezi chini ya miguu yake; na taji ya nyota kumi na mbili ilikuwa juu ya kichwa chake.
2 And having in her womb, she cried, and was in travail, and was pained to give birth.
Alikuwa na mimba na alikuwa analia kwa ajili ya maumivu ya kuzaa—katika uchungu wa kujifungua.
3 And I saw another sign in heaven; and behold a great dragon of fire, which had seven heads and ten horns, and upon his heads seven diadems.
Na ishara nyingine ilionekana mbinguni: Tazama! Kulikuwa na joka mwekundu mkubwa ambaye alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na kulikuwa na taji saba kwenye vichwa vyake.
4 And his tail drew the third of the stars of heaven, and cast them to the earth. And the dragon stood before the woman when she was about to give birth, that when she had given birth he might devour her son.
Mkia wake ulikokota theluthi moja ya nyota mbinguni na kuzitupa chini duniani. Joka alisimama mbele ya mwanamke aliyekuwa anakaribia kuzaa, ili kwamba wakati anazaa, apate kummeza mtoto wake.
5 And she gave birth to a male child, who is to rule all nations with a rod of iron; and her son was rapt unto Aloha and unto his throne.
Alimzaa mwana, mtoto wa kiume, ambaye atayatawala mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Mtoto wake alinyakuliwa juu kwa Mungu na kwenye kiti chake cha enzi,
6 And the woman fled into the desert, where she had a place prepared of Aloha, that there they might nourish her, DAYS A THOUSAND AND TWO HUNDRED AND SIXTY.
na mwanamke alikimbilia nyikani, mahali ambapo Mungu alikuwa ameandaa eneo kwa ajili yake, ili aweze kuhudumiwa kwa siku 1, 260.
7 And there was war in heaven. And Mikoel and his angels to fight with the dragon; and the dragon and his angels warred.
Sasa kulikuwa na vita mbinguni. Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka; naye joka mkubwa na malaika zake wakapigana nao.
8 And they could not prevail, and their place was found no more in heaven.
Lakini joka hakuwa na nguvu za kutosha kushinda. Kwa hiyo haikuwepo tena nafasi mbinguni kwa ajili yake na malaika zake.
9 And the great dragon was cast down, the old serpent, who is called the Deceiver, and the Adversary, which seduceth the whole habitable world. And he was cast upon the earth, and his angels with him were cast.
Joka mkubwa—yule nyoka wa zamani aitwaye ibilisi au Shetani ambaye hudanganya - dunia nzima akatupwa chini katika dunia, na malaika zake wakatupwa chini pamoja naye.
10 And I heard a great voice in heaven saying, Now is there salvation and strength, And the kingdom of our God, And the power of his Meshiha; Because the accuser of our brethren is cast down, Who accused them before Aloha day and night.
Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mbinguni: “Sasa wokovu umekuja, nguvu—na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake. Kwa kuwa mshitaki wa ndugu zetu ametupwa chini—ambaye aliwashitaki mbele za Mungu wetu mchana na usiku.
11 And they overcame him by the blood of the Lamb, And by the word of his testimony. But they loved not their lives unto death.
Walimshinda kwa damu ya Mwanakondoo na kwa neno la ushuhuda wao, kwa maana hawakupenda sana maisha yao, hata kufa.
12 Wherefore let the heavens be glad, And those who dwell in them. Woe to the earth and to the sea! Because the deceiver hath gone down to you, Having great indignation, Knowing that little time is to him.
Kwa hiyo, shangilieni, ninyi mbingu, na wote mnaokaa ndani yake. Lakini ole wa nchi na bahari kwa sababu mwovu ameshuka kwenu. Amejawa na hasira kali, kwa sababu anajua kwamba ana muda mchache tu.
13 And when the dragon saw that he was cast down upon the earth, he pursued the woman which gave birth to the son.
Wakati joka alipotambua kuwa ametupwa chini kwenye nchi, alimfuata mwanamke ambaye alikuwa amezaa mtoto wa kiume.
14 And there were given to the woman two wings of a great eagle, that she might fly into the desert unto her place, where she was to be nourished A TIME, AND TIMES, AND THE DIVIDING OF A TIME, from the face of the serpent.
Lakini mwanamke alipewa mabawa mawili ya tai mkubwa, ili kwamba aweze kuruka hadi kwenye eneo lililoandaliwa kwa ajili yake kule jangwani, eneo ambalo angeweza kutunzwa, kwa wakati, nyakati na nusu wakati-mahali asipoweza kupafikia huyo nyoka.
15 And the serpent cast forth from his mouth after the woman waters like a river, as that she might be carried off by the river which he would make.
Nyoka alimwaga maji kutoka mdomoni mwake kama mto, ili afanye gharika ya kumgharikisha.
16 And the earth succoured the woman, and the earth opened her mouth, and swallowed the river which the dragon had cast forth from his mouth.
Lakini ardhi ilimsaidia mwanamke. Ilifunua kinywa chake na kuumeza mto alioutema joka kutoka kinywani mwake.
17 And the dragon raged against the woman, and went to make war with those of the rest of her seed which kept the commandments of Aloha, and had the testimony of Jeshu.
Kisha joka akamkasirikia mwanamke naye aliondoka na kufanya vita na uzao wake wote—wale wanaotii amri za Mungu na kushikilia ushuhuda kuhusu Yesu.