Aionian Verses

But I say unto you, that he who is angry against his brother rashly, is obnoxious to the judgment; and he who shall say to his brother, Thou empty one! is liable to the council; and every one who shall say, Thou fool! is liable to the gihano of fire. (Geenna g1067)
Lakini mimi nawaambieni, yeyote anayemkasirikia ndugu yake, lazima ahukumiwe. Anayemdharau ndugu yake atapelekwa mahakamani. Anayemwita ndugu yake: Pumbavu atastahili kuingia katika moto wa Jehanamu. (Geenna g1067)
But if thy right eye cause thee to offend, root it out and cast it from thee: it is better to thee that one of thy members should perish, than that thy whole body should fall into gihano. (Geenna g1067)
Basi, kama jicho lako la kulia linakukosesha, ling'oe ukalitupe mbali. Afadhali zaidi kwako kupoteza kiungo kimoja cha mwili wako, kuliko mwili wako wote kutupwa katika moto wa Jehanamu. (Geenna g1067)
And if thy right hand cause thee to offend, cut it off and cast it from thee; for it is better to thee that one from thy members should perish, rather than thy whole body should fall into gihano. (Geenna g1067)
Na kama mkono wako wa kulia unakukosesha, ukate ukautupe mbali. Afadhali zaidi kupoteza kiungo kimoja cha mwili, kuliko mwili wako wote uende katika moto wa Jehanamu. (Geenna g1067)
And fear not them who kill the body, but the soul cannot kill; but fear rather One who the soul and the body can destroy in gihano. (Geenna g1067)
Msiwaogope wale wauao mwili, lakini hawawezi kuiua roho. Afadhali zaidi kumwogopa yule awezaye kuuangamiza mwili pamoja na roho katika moto wa Jehanamu. (Geenna g1067)
And thou, Kaphernachum, who unto heaven art exalted, unto Shiul shalt be brought down; for if in Sadum had been done those miracles which have been done in thee, it would have stood until this day. (Hadēs g86)
Na wewe Kafarnaumu, je, utajikweza mpaka mbinguni? Utaporomoshwa mpaka Kuzimu! Maana, kama miujiza iliyofanyika kwako ingalifanyika kule Sodoma, mji huo ungalikuwako mpaka hivi leo. (Hadēs g86)
And every one who shall speak a word against the Son of man, it shall be forgiven him; but every one who against the Spirit of Holiness shall speak, it shall not be forgiven to him, neither in this world nor in the world to come. (aiōn g165)
Tena, asemaye neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa, lakini yule asemaye neno la kumpinga Roho Mtakatifu, hatasamehewa, wala katika ulimwengu huu, wala katika ulimwengu ujao. (aiōn g165)
That sown the place of thorns, is he who heareth the word, but the anxious thought of this world and the illusions of riches stifle the word in him, and he is without fruits. (aiōn g165)
Ile mbegu iliyoanguka kati ya miti ya miiba, ni mfano wa mtu asikiaye huo ujumbe, lakini wasiwasi wa ulimwengu huu na anasa za mali huusonga ujumbe huo, naye hazai matunda. (aiōn g165)
The adversary who sowed them is Satana; the harvest is the consummation of the world; the reapers are the angels. (aiōn g165)
Adui aliyepanda yale magugu ni Ibilisi. Mavuno ni mwisho wa nyakati na wavunaji ni malaika. (aiōn g165)
As, therefore, the zizania are gathered and burned in the fire, so shall it be in the completion of this world. (aiōn g165)
Kama vile magugu yanavyokusanywa kuchomwa moto, ndivyo itakavyokuwa mwishoni mwa nyakati; (aiōn g165)
Thus shall it be at the consummation of the world. The angels shall go forth, and separate the evil from among the just, (aiōn g165)
Ndivyo itakavyokuwa mwishoni mwa nyakati: malaika watatokea, watawatenganisha watu wabaya na watu wema, (aiōn g165)
Also I say unto thee, that thou art Kipha, and upon this rock will I build my church, and the gates of Sheul shall not prevail against her. (Hadēs g86)
Nami nakwambia: wewe ni Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala kifo chenyewe hakitaweza kulishinda. (Hadēs g86)
but woe to the man by whom the causes of offence shall come! If, then, thine hand or thy foot shall be a cause of offence to thee, cut it off, and cast it from thee; for it is good for thee that thou enter into life lame or mutilated; and not that, having two hands or two feet, thou fall into the fire of eternity. (aiōnios g166)
“Kama mkono au mguu wako ukikukosesha, ukate na kuutupa mbali nawe. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima bila mkono au mguu, kuliko kutupwa katika moto wa milele ukiwa na mikono miwili na miguu yako miwili. (aiōnios g166)
And if thine eye be a cause of offence to thee, dig it out, and cast it from thee; good (it is) for thee that with one eye thou enter into life; and not that, having two eyes, thou fall into the gihâna of fire. (Geenna g1067)
Na kama jicho lako likikukosesha, ling'oe na kulitupa mbali nawe. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa chongo, kuliko kutupwa katika moto wa Jehanamu ukiwa na macho yako yote mawili. (Geenna g1067)
AND one came and approached and said to him, Good teacher, what of good shall I do, that I may have the life of eternity? (aiōnios g166)
Mtu mmoja alimjia Yesu, akamwuliza, “Mwalimu, nifanye kitu gani chema ili niupate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
And every man who hath relinquished houses, or brethren, or sisters, or father, or mother, or wife, or children, or lands, on account of my name, shall receive a hundred-fold, and shall inherit the life of eternity, (aiōnios g166)
Na kila aliyeacha nyumba, au ndugu, au dada, au baba, au mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili yangu, atapokea mara mia zaidi, na kupata uzima wa milele. (aiōnios g166)
and he saw a certain fig-tree in the way, and came to it, but found nothing thereon but leaves only; and he said, Let there be no fruit upon thee again for ever. And immediately that fig-tree withered. (aiōn g165)
Akauona mtini mmoja kando ya njia, akauendea; lakini aliukuta hauma chochote ila majani matupu. Basi akauambia, “Usizae tena matunda milele!” Papo hapo huo mtini ukanyauka. (aiōn g165)
Woe to you, scribes and Pharishee, hypocrites! because you go over sea and dry (land) to make one proselyte; and when you have done it, you make him doubly more a son of gihana than yourselves. (Geenna g1067)
“Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnasafiri baharini na nchi kavu ili kumpata mtu mmoja afuate dini yenu. Mnapompata, mnamfanya astahili maradufu kwenda katika moto wa Jehanamu kuliko ninyi wenyewe. (Geenna g1067)
Serpents, birth of vipers! how will you escape from the judgment of gihana? (Geenna g1067)
Enyi kizazi cha nyoka wenye sumu! Mnawezaje kuiepa hukumu ya moto wa Jehanamu? (Geenna g1067)
And while Jeshu sat upon the mount of Olives, his disciples drew near and said between themselves and him, Tell us when these things shall be; and what is the sign of thy coming and of the consummation of the world. (aiōn g165)
Yesu alipokuwa ameketi juu ya mlima wa Mizeituni, wanafunzi walimwendea faraghani, wakamwuliza, “Twambie mambo haya yatatukia lini? Ni ishara gani itakayoonyesha kuja kwako na mwisho wa nyakati?” (aiōn g165)
Then shall he say also unto them on his left hand, Go from me, accursed, into the fire of eternity, which was prepared for the accuser and for his angels. (aiōnios g166)
“Kisha atawaambia wale walio upande wake wa kushoto, Ondokeni mbele yangu enyi mliolaaniwa! Nendeni katika moto wa milele aliotayarishiwa Ibilisi na malaika wake. (aiōnios g166)
And these shall go away into the torment which is eternal, and the just into the life which is eternal. (aiōnios g166)
Basi, hawa watakwenda kwenye adhabu ya milele, lakini wale waadilifu watakwenda kwenye uzima wa milele.” (aiōnios g166)
And teach them to observe all things whatsoever I have commanded you. And, behold, I am with you all the days, until the consummation of the world. Amen. (aiōn g165)
Wafundisheni kushika maagizo yote niliyowapeni. Nami nipo pamoja nanyi siku zote; naam, mpaka mwisho wa nyakati.” (aiōn g165)
but whosoever shall blaspheme against the Spirit of Holiness hath no remission for ever, but is condemned to the judgment that is eternal. (aiōn g165, aiōnios g166)
lakini anayesema mabaya dhidi ya Roho Mtakatifu, hatasamehewa kamwe; ana hatia ya dhambi ya milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
and the care of this world, and the deceptiveness of wealth, and the remainder of other lusts, entering, choke the word, and it is without fruits. (aiōn g165)
lakini wasiwasi wa ulimwengu huu, anasa za mali na tamaa za kila namna huwaingia na kulisonga hilo neno, nao hawazai matunda. (aiōn g165)
But if thy hand offend thee, cut it off: better for thee mutilated to go into life, than having two hands to go into gihana; (Geenna g1067)
Mkono wako ukikukosesha, ukate! Afadhali kuingia kwenye uzima bila mkono mmoja, kuliko kuwa na mikono miwili na kwenda katika moto wa Jehanamu. (Geenna g1067)
And if thy foot offend thee, cut it off: better for thee to go into life lame, than having two feet to fall into gihana: (Geenna g1067)
Na mguu wako ukikukosesha, ukate! Afadhali kuingia katika uzima bila mguu mmoja, kuliko kuwa na miguu yote miwili na kutupwa katika moto wa Jehanamu. (Geenna g1067)
And if thine eye offend thee, root it out: better for thee that with one eye thou enter the kingdom of Aloha, than having two eyes to fall into the gihana of fire: (Geenna g1067)
Na jicho lako likikukosesha, ling'oe! Afadhali kuingia katika utawala wa Mungu ukiwa na jicho moja tu, kuliko kuwa na macho yako yote mawili na kutupwa katika moto wa Jehanamu. (Geenna g1067)
AND as he journeyed in the way, one ran, fell upon his knees, and asked him, saying, Good Teacher, what shall I do that I may inherit eternal life? (aiōnios g166)
Yesu alipoanza tena safari yake, mtu mmoja alimjia mbio, akapiga magoti mbele yake, akamwuliza, “Mwalimu mwema, nifanyeje ili niupate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
who shall not receive a hundred-fold now in this time, houses, and brethren, and sisters, and mothers, and children, and fields, with persecution; and in the world which cometh the life that is eternal. (aiōn g165, aiōnios g166)
atapokea mara mia zaidi wakati huu wa sasa nyumba, ndugu, dada, mama, watoto na mashamba pamoja na mateso; na katika wakati ujao atapokea uzima wa milele. (aiōn g165, aiōnios g166)
And he said to it, Henceforth and for ever man from thee fruit shall not eat. And his disciples heard. (aiōn g165)
Hapo akauambia mtini, “Tangu leo hata milele mtu yeyote asile matunda kwako.” Nao wanafunzi wake walisikia maneno hayo. (aiōn g165)
And he shall reign over the house of Jakub for ever, and of his kingdom there shall be no end. (aiōn g165)
Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
As he spake with our fathers, With Abraham and with his seed for ever. (aiōn g165)
Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele.” (aiōn g165)
As he spake by the mouth of his holy prophets, Who have been from of old, (aiōn g165)
Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu, (aiōn g165)
And they besought from him that he would not cast them out to go into the abyss. (Abyssos g12)
Hao pepo wakamsihi asiwaamuru wamtoke na kwenda kwenye shimo lisilo na mwisho. (Abyssos g12)
And thou, Kapher-nachum, which unto heaven art lifted up, unto Shiul shalt thou be abased. (Hadēs g86)
Na wewe Kafarnaumu, unataka kujikweza mpaka mbinguni? La; utaporomoshwa mpaka Kuzimu.” (Hadēs g86)
AND, behold, a certain Sophra stood up to try him, saying, Malphona, what shall I do to inherit everlasting life? (aiōnios g166)
Baadaye mwalimu mmoja wa Sheria alisimama akamwuliza akitaka kumtega, “Mwalimu, nifanye nini ili nipate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
but I will show you whom you shall fear; Him who, after he hath killed, hath power to cast into gihana, yes, I say to you, Fear this (one). (Geenna g1067)
Nitawaonyesheni yule ambaye ni lazima kumwogopa: mwogopeni yule ambaye baada ya kuua ana uwezo wa kumtupa mtu katika moto wa Jehanamu. Naam, ninawaambieni, mwogopeni huyo. (Geenna g1067)
And praised our Lord the house-chief who was unjust, in that he had done wisely; for the sons of this world are wiser than the sons of light in this their generation. (aiōn g165)
“Basi, yule bwana akamsifu huyo karani asiye mwaminifu, kwa kuwa alitumia busara. Kwa maana watu wa dunia hii wana busara zaidi na mambo yao kuliko watu wa mwanga.” (aiōn g165)
Also I say unto you, Make to you friends from this wealth of unrighteousness, that, when perfect, they may receive you into the tabernacles of eternity. (aiōnios g166)
Naye Yesu akaendelea kusema, “Nami nawaambieni, jifanyieni marafiki kutokana na mali ya dunia, ili zitakapowaishieni, mweze kupokewa nao katika makao ya milele. (aiōnios g166)
And, tormented in shiul, he lifted up his eyes afar, and seeth Abraham, and Loózar in his bosom. (Hadēs g86)
Huyo tajiri, alikuwa na mateso makali huko kuzimu, akainua macho yake, akamwona Abrahamu kwa mbali na Lazaro karibu naye. (Hadēs g86)
AND one of the rulers asked him, saying, Good Teacher, what shall I do that I may inherit eternal life? (aiōnios g166)
Kiongozi mmoja, Myahudi, alimwuliza Yesu, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niweze kuupata uzima wa milele?” (aiōnios g166)
and shall not receive by two-fold (as) many in this time, and in the world that cometh the life that is eternal. (aiōn g165, aiōnios g166)
atapokea mengi zaidi wakati huu wa sasa, na kupokea uzima wa milele wakati ujao.” (aiōn g165, aiōnios g166)
Jeshu saith to them, The sons of this world take wives, and women become (the wives) of men: (aiōn g165)
Yesu akawaambia, “Watu wa nyakati hizi huoa na kuolewa; (aiōn g165)
but they who of that world are worthy, and of the resurrection which is from among the dead, take not wives, neither do women become (the wives) of men. (aiōn g165)
lakini wale ambao Mungu atawawezesha kushiriki ule wakati wa ufufuo, hawataoa wala kuolewa. (aiōn g165)
that every man who believeth in him might not perish, but have the life which is eternal. (aiōnios g166)
ili kila anayemwamini awe na uzima wa milele. (aiōnios g166)
For so loved Aloha the world, as his Son, the Only-begotten, he would give, that every one who believeth in him might not perish, but have the life which is eternal. (aiōnios g166)
Maana Mungu aliupenda ulimwengu hivi hata akamtoa Mwana wake wa pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. (aiōnios g166)
He who believeth in the Son hath the life which is eternal; and he who obeyeth not the Son shall not see life, but the wrath of Aloha remaineth on him. (aiōnios g166)
Anayemwamini Mwana anao uzima wa milele; asiyemtii Mwana hatakuwa na uzima wa milele, bali ghadhabu ya Mungu hubaki juu yake.” (aiōnios g166)
but every one who shall drink of the waters that I will give him shall never thirst; but those waters that I shall give him shall be in him a fountain of waters, that shall spring forth to the life of eternity. (aiōn g165, aiōnios g166)
Lakini atakayekunywa maji nitakayompa mimi, hataona kiu milele. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji ya uzima na kumpatia uzima wa milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
And he who reapeth receiveth wages, and gathereth fruit unto life eternal; and the sower and the reaper shall rejoice together. (aiōnios g166)
Mvunaji anapata mshahara wake, na anakusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele; hivyo mpandaji na mvunaji watafurahi pamoja. (aiōnios g166)
Amen, amen, I say to you, He who heareth my word and believeth on him who sent me, hath the life that is eternal, and into condemnation he cometh not, but hath passed from death unto life. (aiōnios g166)
“Kweli nawaambieni, anayesikia neno langu, na kumwamini yule aliyenituma, anao uzima wa milele. Hatahukumiwa kamwe, bali amekwisha pita kutoka kifo na kuingia katika uzima. (aiōnios g166)
Investigate the scriptures; for in them you think you have the life that is eternal, and they testify of me. (aiōnios g166)
Ninyi huyachunguza Maandiko Matakatifu mkidhani kwamba ndani yake mtapata uzima wa milele; na kumbe maandiko hayohayo yananishuhudia! (aiōnios g166)
Work not (for) the food which perisheth, but (for) the food that endureth unto the life that is eternal, which the Son of man shall give to you: for this hath the Father sealed, (even) Aloha. (aiōnios g166)
Msikishughulikie chakula kiharibikacho; kishugulikieni chakula kidumucho kwa ajili ya uzima wa milele. Mwana wa Mtu ambaye Baba amemthibitisha atawapeni chakula hicho.” (aiōnios g166)
For this is the will of my Father, that every one who seeth the Son and believeth on him, shall have the life that is eternal, and I will raise him at the last day. (aiōnios g166)
Maana anachotaka Baba yangu ndicho hiki: kila amwonaye Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele; nami nitamfufua Siku ya mwisho.” (aiōnios g166)
AMEN, amen, I say to you, Whosoever believeth in me hath the life which is eternal. (aiōnios g166)
Kweli, nawaambieni, anayeamini anao uzima wa milele. (aiōnios g166)
I am the bread of life that from heaven hath descended; and if man shall eat of this bread, he shall live for ever; and the bread that I will give is my body, which for the life of the world I give. (aiōn g165)
Mimi ni mkate hai ulioshuka kutoka mbinguni. Mtu yeyote akila mkate huu ataishi milele. Na mkate nitakaompa ni mwili wangu ninaoutoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.” (aiōn g165)
He who eateth of my body, and drinketh of my blood, hath the life which is eternal, and I will raise him at the last day. (aiōnios g166)
Anayekula mwili wangu na kunywa damu yangu anao uzima wa milele nami nitamfufua siku ya mwisho. (aiōnios g166)
This is the bread which hath descended from heaven. Not as was the manna that your fathers ate, and are dead; he who eateth of this bread shall live for ever. (aiōn g165)
Basi, huu ndio mkate ulioshuka kutoka mbinguni; si kama mana waliyokula babu zetu, wakafa. Aulaye mkate huu ataishi milele.” (aiōn g165)
Shemun Kipha answered and said, My Lord, unto whom shall we go? thou hast the words of eternal life; (aiōnios g166)
Simoni Petro akamjibu, “Bwana, tutakwenda kwa nani? Wewe unayo maneno yaletayo uzima wa milele. (aiōnios g166)
And the servant abideth not for ever in the house, but the Son for ever abideth. (aiōn g165)
Mtumwa hana makao ya kudumu nyumbani, lakini mwana anayo makao ya kudumu. (aiōn g165)
Amen, amen, I say to you, That he who my word keepeth, death shall not see for ever. (aiōn g165)
Kweli nawaambieni, anayeuzingatia ujumbe wangu hatakufa milele.” (aiōn g165)
The Jihudoyee say to him, Now we know that thou hast a devil. Abraham is dead, and the prophets; and thou sayest, that he who thy word keepeth, death shall not taste for ever. (aiōn g165)
Basi, Wayahudi wakasema, “Sasa tunajua kweli kwamba wewe ni mwendawazimu! Abrahamu alikufa, na manabii pia walikufa, nawe wasema ati, Anayeuzingatia ujumbe wangu hatakufa milele! (aiōn g165)
From of old it hath not been heard that a man hath opened the eyes of one born blind. (aiōn g165)
Tangu mwanzo wa ulimwengu haijasikika kwamba mtu ameyafumbua macho ya mtu aliyezaliwa kipofu. (aiōn g165)
and I give to them the life which is eternal, and they shall not perish for ever, and no man shall snatch them from my hands. (aiōn g165, aiōnios g166)
Mimi nawapa uzima wa milele; nao hawatapotea milele, wala hakuna mtu atakayeweza kuwatoa mkononi mwangu. (aiōn g165, aiōnios g166)
And every one who liveth and believeth in me, for ever shall not die. Believest thou this? (aiōn g165)
na kila anayeishi na kuniamini, hatakufa kamwe. Je, waamini hayo?” (aiōn g165)
He who loveth his life shall lose it; and he who hateth his life in this world shall keep it to the life which is eternal. (aiōnios g166)
Anayependa maisha yake, atayapoteza; anayeyachukia maisha yake katika ulimwengu huu, atayaweka kwa ajili ya uzima wa milele. (aiōnios g166)
The people said to him, We have heard from the law that the Meshicha for ever abideth: how sayest thou that the Son of man is to be lifted up? Who is this Son of man? (aiōn g165)
Basi, umati huo ukamjibu, “Sisi tunaambiwa na Sheria yetu kwamba Kristo atadumu milele. Wawezaje basi, kusema ati Mwana wa Mtu anapaswa kuinuliwa? Huyo Mwana wa Mtu ni nani?” (aiōn g165)
And I know that his commandments are life everlasting: these therefore which I speak, as said to me my Father, so I speak. (aiōnios g166)
Nami najua kuwa amri yake huleta uzima wa milele. Basi, mimi nasema tu yale Baba aliyoniagiza niyaseme.” (aiōnios g166)
Shemun Kipha saith to him, Never shalt thou wash for me my feet. Jeshu saith to him, If I do not wash thee, thou hast with me no part. (aiōn g165)
Petro akamwambia, “Wewe hutaniosha miguu kamwe!” Yesu akamjibu, “Nisipokuosha hutakuwa na uhusiano nami tena.” (aiōn g165)
and I will pray of my Father, and another Paraclete will he give you, who will be with you for ever, (aiōn g165)
Nami nitamwomba Baba naye atawapeni Msaidizi mwingine, atakayekaa nanyi milele. (aiōn g165)
As thou hast given him power over all flesh, that to all whom thou hast given him he should give the life which is eternal. (aiōnios g166)
Maana ulimpa Mwanao mamlaka juu ya watu wote ili awape uzima wa milele wote hao uliompa. (aiōnios g166)
But this is the life which is eternal, that they know thee, who art the true Aloha, and Him whom thou hast sent, Jeshu Meshicha. (aiōnios g166)
Na uzima wa milele ndio huu: kukujua wewe uliye peke yako Mungu wa kweli, na kumjua Yesu Kristo uliyemtuma. (aiōnios g166)
For thou wilt not leave my soul in Shiul, Nor give thy Saint to see corruption. (Hadēs g86)
kwa kuwa hutaiacha roho yangu katika kuzimu, wala kumruhusu mtakatifu wako aoze. (Hadēs g86)
And he foresaw and spake concerning, the resurrection of the Meshiha, that He would not be left in Shiul, nor would his body see corruption. (Hadēs g86)
Daudi aliona kabla mambo yatakayofanywa na Mungu na hivyo akasema juu ya ufufuo wa Kristo wakati aliposema: Hakuachwa kuzimu, mwili wake haukuoza. (Hadēs g86)
whom the heavens must receive until the completion of the times of all those which Aloha hath spoken by the mouth of his holy prophets, who (have been) from of old. (aiōn g165)
Ni lazima yeye abaki huko mbinguni mpaka utakapofika wakati wa kurekebishwa vitu vyote, kama Mungu alivyosema kwa njia ya manabii wake watakatifu wa tangu zamani. (aiōn g165)
But Paulos and Bar Naba said to them openly, To you it behoved first to speak the word of Aloha; but because you repel it from you, and determine against yourselves that you are not worthy of eternal life, behold, we turn to the Gentiles. (aiōnios g166)
Hata hivyo, Paulo na Barnaba waliongea kwa uhodari zaidi, wakasema, “Ilikuwa ni lazima neno la Mungu liwafikieni ninyi kwanza; lakini kwa kuwa mmelikataa na kujiona hamstahili uzima wa milele, basi, tunawaacheni na kuwaendea watu wa mataifa mengine. (aiōnios g166)
And when the Gentiles heard, they rejoiced and glorified Aloha; and they believed who were disposed unto eternal life. (aiōnios g166)
Watu wa mataifa mengine waliposikia jambo hilo walifurahi, wakausifu ujumbe wa Mungu; na wale waliokuwa wamechaguliwa kupata uzima wa milele, wakawa waumini. (aiōnios g166)
Saith the Lord, who doeth all these. Known from eternity are the works of Aloha. (aiōn g165)
Ndivyo asemavyo Bwana, aliyefanya jambo hili lijulikane tangu kale. (aiōn g165)
For the occult things of Aloha from the foundations of the world, unto his creatures by intelligence are apparent, and his power and his Godhead eternal, that they may be without excuse. (aïdios g126)
Tangu Mungu alipoumba ulimwengu, uwezo wake wa milele na uungu wake, ingawa havionekani kwa macho, vinafahamika wazi. Watu wanaweza kuyajua mambo hayo kutokana na vitu hivyo alivyoumba Mungu. Kwa hiyo hawana njia yoyote ya kujitetea! (aïdios g126)
And they changed the truth of Aloha into a lie, and worshipped and served the creatures rather than their Creator, to whom be praises and blessings for ever and ever. Amen. (aiōn g165)
Wanaubadili ukweli juu ya Mungu kwa uongo; wanaheshimu na kuabudu kiumbe badala ya Muumba mwenyewe, ambaye ndiye astahiliye sifa milele! Amina. (aiōn g165)
To them who seek, in perseverance of good works, glory and honour and incorruption, he giveth eternal life; (aiōnios g166)
Wale wanaozingatia kutenda mema, kutafuta utukufu na heshima ya Mungu na kutokufa, watapata uzima wa milele. (aiōnios g166)
that as sin hath reigned in death, so grace might reign in righteousness unto the life which is eternal, by the hand of our Lord Jeshu Meshiha. (aiōnios g166)
Kama vile dhambi ilivyotawala kwa kifo, kadhalika neema inatawala kwa njia ya uadilifu, na kuleta uzima wa milele kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu. (aiōnios g166)
And now made free from sin, and become servants to Aloha, you have holy fruits, of which the end is the life of eternity. (aiōnios g166)
Lakini sasa, mmekwisha kombolewa kutoka utumwa wa dhambi na mmekuwa watumishi wa Mungu; faida mliyo nayo sasa ni utakatifu, na matokeo yake ni uzima wa milele. (aiōnios g166)
For the wages of sin is death; and the gift of Aloha the life of eternity by our Lord Jeshu Meshiha. (aiōnios g166)
Kwa maana mshahara wa dhambi ni kifo; lakini zawadi anayotoa Mungu ni uzima wa milele katika kuungana na Kristo Yesu, Bwana wetu. (aiōnios g166)
and the fathers; and from whom appeared the Meshiha in the flesh, who is Aloha over all: his be praises and benedictions to the age of ages. Amen. (aiōn g165)
Wao ni wajukuu wa mababu, naye Kristo, kadiri ya ubinadamu wake, ametoka katika ukoo wao. Mungu atawalaye juu ya yote, na atukuzwe milele! Amina. (aiōn g165)
And who shall descend into the deep of Sheul, And bring up the Meshiha from among the dead? (Abyssos g12)
wala usiseme: Nani atashuka mpaka Kuzimu (yaani, kumleta Kristo kutoka kwa wafu).” (Abyssos g12)
For Aloha hath included them all in disobedience, that upon all he might show mercy. (eleēsē g1653)
Maana Mungu amewafunga watu wote katika uasi wao ili wapate kuwahurumia wote. (eleēsē g1653)
For all is of him, and all in him, and all by him. To him be praises and benedictions unto the age of ages. Amen. (aiōn g165)
Kwa maana vitu vyote vyatoka kwake, vyote vipo kwa uwezo wake na kwa ajili yake. Utukufu na uwe kwake hata milele! Amina. (aiōn g165)
And be not likened unto this world, but be changed by the renewing of your minds, that you may discern what is the will of Aloha, good, and acceptable, and perfect. (aiōn g165)
Msiige mitindo ya ulimwengu huu, bali Mungu afanye mabadiliko ndani yenu kwa kuzigeuza fikira zenu. Hapo ndipo mtakapoweza kuyajua mapenzi ya Mungu, kutambua jambo lililo jema, linalompendeza na kamilifu. (aiōn g165)
TO ALOHA, who is able to confirm you in my gospel which is proclaimed concerning Jeshu the Meshiha, through revelation of the mystery, which from the times of the ages was hidden, (aiōnios g166)
Basi, sasa na tumsifu Mungu! Yeye anaweza kuwaimarisheni katika ile Habari Njema niliyohubiri juu ya ujumbe wa Yesu Kristo, na katika ile siri iliyofunuliwa na ambayo ilikuwa imefichika kwa karne nyinyi zilizopita. (aiōnios g166)
but is revealed in this time by means of the scriptures of the prophets, and by the commandment of the Everlasting Aloha is made known to all the nations for the obedience of faith; (aiōnios g166)
Lakini, sasa ukweli huo umefunuliwa kwa njia ya maandiko ya manabii; na kwa amri ya Mungu wa milele umedhihirisha kwa mataifa yote ili wote waweze kuamini na kutii. (aiōnios g166)
(to Him) who alone is wise, BE GLORY BY JESHU MESHIHA, UNTO THE AGE OF AGES. AMEN. (aiōn g165)
Kwake Mungu aliye peke yake mwenye hekima, uwe utukufu kwa njia ya Yesu Kristo, milele na milele! Amina. (aiōn g165)
Where is the wise? Where is the scribe? Or where is the disputer of this world? Hath not. Aloha made foolish the wisdom of this world? (aiōn g165)
Yu wapi basi, mwenye hekima? Yu wapi basi, mwalimu wa Sheria? Naye bingwa wa mabishano wa nyakati hizi yuko wapi? Mungu ameifanya hekima ya ulimwengu kuwa upumbavu. (aiōn g165)
But we speak wisdom among the perfect: not the wisdom of this world, nor the authorities of this world, which are abolished; (aiōn g165)
Hata hivyo, sisi tunatumia lugha ya hekima kwa wale waliokomaa kiroho; lakini hekima hiyo si ya hapa duniani, wala si ya watawala wa dunia hii ambao wako katika mkumbo wa kupotea. (aiōn g165)
but we speak the wisdom of Aloha in the mystery which was hidden, and which Aloha predetermined from before the worlds unto our glorification; (aiōn g165)
Hekima tunayotumia ni hekima ya siri ya Mungu, hekima iliyofichika, ambayo Mungu aliiazimia tangu mwanzo kwa ajili ya utukufu wetu. (aiōn g165)
which not one of the authorities of this world hath known; for if they had known it, the Lord of glory they would not have crucified. (aiōn g165)
Ni hekima ambayo watawala wa dunia hii hawakuielewa; maana wangalielewa, hawangalimsulubisha Bwana wa utukufu. (aiōn g165)
Let no man deceive himself. Whoever among you supposeth himself wise in this world, let him become foolish, that he may be wise. (aiōn g165)
Msijidanganye! Mtu yeyote miongoni mwenu akijidhania mwenye hekima mtindo wa kidunia, heri awe mjinga kusudi apate kuwa na hekima ya kweli. (aiōn g165)
On this account, if meat cause my brother to stumble, I will never (more) eat flesh, that I may not cause my brother to stumble. (aiōn g165)
Kwa hiyo, ikiwa chakula husababisha kuanguka kwa ndugu yangu, sitakula nyama kamwe, nisije nikamfanya ndugu yangu aanguke katika dhambi. (aiōn g165)
For all these which happened to them were unto us an example, and were written for our instruction, upon whom come the ends of the world. (aiōn g165)
Basi, mambo hayo yaliyowapata wao ni kielelezo kwa wengine, na yaliandikwa ili kutuonya sisi, ambao mwisho wa nyakati unatukabili. (aiōn g165)
Where is thy sting, Death? and where is thy victory Shiul? (Hadēs g86)
“Kifo, ushindi wako uko wapi? Uwezo wako wa kuumiza uko wapi?” (Hadēs g86)
(to) them whose minds the god of this world hath blinded because they believe not; lest the light of the gospel of the glory of Meshiha, who is the image of Aloha, should arise upon them. (aiōn g165)
Hao hawaamini kwa sababu yule mungu wa ulimwengu huu amezitia giza akili zao wasipate kuuona wazi mwanga wa Habari Njema ya utukufu wa Kristo, ambaye ni mfano kamili wa Mungu. (aiōn g165)
For the affliction of this time, while small and light, a glory without end for ever and ever prepareth for us. (aiōnios g166)
Taabu tunayopata ni kidogo, tena ya muda tu: lakini itatupatia utukufu upitao matazamio yote, utukufu ambao hauna mwisho. (aiōnios g166)
While we look not on these which are seen, but at those which are unseen. For the seen are of time, but the unseen are of eternity. (aiōnios g166)
Hivyo tunatazamia kwa makini si vitu vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Maana vinavyoonekana ni vya muda tu; lakini vile visivyoonekana ni vya milele. (aiōnios g166)
FOR we know that if our earthly house of this body were dissolved, we have nevertheless a building that is by Aloha; a house which is not made with hands, in the heaven, eternal. (aiōnios g166)
Maana tunajua kwamba hema hii ambayo ndani yake tunaishi sasa hapa duniani, yaani mwili wetu, itakapong'olewa, Mungu atatupa makao mengine mbinguni, nyumba ya milele isiyotengenezwa kwa mikono. (aiōnios g166)
As it is written, He hath dispersed and given to the poor, And his righteousness standeth for ever. (aiōn g165)
Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Yeye hutoa kwa ukarimu, huwapa maskini, wema wahudumu milele.” (aiōn g165)
Aloha, the Father of our Lord Jeshu Meshiha, the Blessed for ever and ever, knoweth that I lie not. (aiōn g165)
Mungu na Baba wa Bwana Yesu—jina lake litukuzwe milele—yeye anajua kwamba sisemi uongo. (aiōn g165)
who gave himself for our sins to deliver us from this evil world, according to the will of Aloha our Father: (aiōn g165)
Kristo alijitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na mapenzi ya Mungu wetu na Baba, ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu mbaya wa sasa. (aiōn g165)
to whom be glory to the age of ages. Amen. (aiōn g165)
Kwake yeye uwe utukufu milele! Amina. (aiōn g165)
He who in the flesh soweth, from the flesh corruption reapeth; and he who in the Spirit soweth, from the Spirit the life that is eternal shall reap. (aiōnios g166)
Apandaye katika tamaa za kidunia, atavuna humo uharibifu; lakini akipanda katika Roho, atavuna kutoka kwa Roho uzima wa milele. (aiōnios g166)
and powers, and mighty ones, and rulers, and above every name that is named, not only in this world, but also in (that) to come; (aiōn g165)
Huko, Kristo anatawala juu ya kila tawala, mamlaka, enzi na ukuu; anatawala juu ya kila cheo kiwezacho kutajwa katika ulimwengu huu na katika ulimwengu ujao. (aiōn g165)
in which from the first you walked according to the worldliness of this age, and according to the will of the prince of the power of the air, of that Spirit who urgeth in the sons of disobedience; (aiōn g165)
Wakati ule mliishi kufuatana na mtindo mbaya wa ulimwengu huu, mkawa mnamtii mtawala wa pepo wenye nguvu wa anga, pepo ambao huwatawala sasa watu wasiomtii Mungu. (aiōn g165)
that he might show to the ages to come the greatness of the riches of his grace and his goodness, which hath been upon us in Jeshu the Meshiha. (aiōn g165)
Ndivyo alivyopenda kuonyesha kwa watu wa nyakati za baadaye, ukuu wa neema yake aliyotujalia kwa ukarimu katika kuungana kwetu na Kristo Yesu. (aiōn g165)
which are not searched; and to bring to light unto all men what is the dispensation of the mystery which was hidden from the ages in Aloha, who created all: (aiōn g165)
tena niwaangazie watu wote waone jinsi mpango wa Mungu uliofichika unavyotekelezwa. Mungu aliye Muumba wa vitu vyote alificha siri hiyo yake tangu milele, (aiōn g165)
that which he prepared from of old, and which he hath executed by Jeshu our Lord, (aiōn g165)
Mungu alifanya jambo hilo kufuatana na azimio lake la milele ambalo amelifanya kwa njia ya Kristo Bwana wetu. (aiōn g165)
to Him be glory in his church, by Jeshu Meshiha, in all ages, for ever and ever. Amen. (aiōn g165)
kwake Mungu uwe utukufu katika kanisa na katika Kristo Yesu, nyakati zote, milele na milele! Amina. (aiōn g165)
For your wrestling is not with flesh and blood (only), but with princes, and with powers, and with the possessors of this dark world, and with the evil spirits who are under heaven. (aiōn g165)
Maana vita vyenu si vita kati yetu na binadamu, bali ni vita dhidi ya jeshi ovu la ulimwengu wa roho; tunapigana na watawala, wakuu na wenye nguvu wanaomiliki ulimwengu huu wa giza. (aiōn g165)
To Aloha our Father be praise and glory to the age of ages. Amen. (aiōn g165)
(parallel missing)
that mystery which was hidden from ages and generations, but now hath been revealed unto his saints. (aiōn g165)
ambao ni siri aliyowaficha binadamu wote tangu milele, lakini sasa amewajulisha watu wake. (aiōn g165)
For these in the judgment will be punished (with) the perdition of eternity, from the presence of our Lord, and from the glory of his power; (aiōnios g166)
Adhabu yao itakuwa kuangamizwa milele na kutengwa mbali na utukufu wake mkuu, (aiōnios g166)
But our Lord Jeshu Meshiha himself, and Aloha our Father, who hath loved us, and given us everlasting consolation, and a good hope through grace, (aiōnios g166)
Tunamwomba Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu ambaye alitupenda, na kwa neema yake akatujalia faraja ya milele na tumaini jema, (aiōnios g166)
But for this he had compassion upon me, that in me first Jeshu Meshiha might show all long-suffering, as an exhibition for them who should believe in him unto everlasting life. (aiōnios g166)
lakini Mungu alinionea huruma, ili Kristo aonyeshe uvumilivu wake wote kwangu mimi, kama mfano kwa wale wote ambao baadaye watamwamini na kupokea uzima wa milele. (aiōnios g166)
But to the King who is eternal, incorruptible, and unseen, who is one Aloha, be honour and glory for ever and ever. Amen. (aiōn g165)
Kwake yeye aliye Mfalme wa milele na asiyekufa, yeye aliye Mungu pekee—kwake viwe heshima na utukufu milele na milele! Amina. (aiōn g165)
And contend in the good agony of faith, and lay hold of the life which is eternal, unto which thou art called, and hast confessed a good confession before many witnesses. (aiōnios g166)
Piga mbio kadiri uwezavyo katika shindano la mbio za imani, ukajipatie tuzo la uzima wa milele, uliloitiwa wakati ulipokiri imani yako mbele ya mashahidi wengi. (aiōnios g166)
he who only is incorruptible, and (who) dwelleth in light which no man can approach; whom no man of men hath seen, nor is able to see: to him be honour and power for ever and ever. Amen. (aiōnios g166)
Yeye peke yake anaishi milele, katika mwanga usioweza kukaribiwa na mtu. Hakuna mtu aliyepata kumwona au awezaye kumwona. Kwake iwe heshima na uwezo wa milele! Amina. (aiōnios g166)
The rich of this world instruct, that they be not uplifted in their minds, nor be trustful upon riches which have no security, but upon Aloha the living, who giveth to us all abundantly for our comfort; (aiōn g165)
Waamuru watu walio matajiri katika mambo ya maisha ya sasa, wasijivune, wasiweke tumaini lao katika mali isiyoweza kutegemewa; bali wamtegemee Mungu, ambaye kwa ukarimu hutupatia vitu vyote tuvifurahie. (aiōn g165)
who hath saved us, and called us with an holy calling; not according to our works, but according to his will, and that grace of his which was given to us in Jeshu Meshiha before the time of the worlds, (aiōnios g166)
Yeye alituokoa, akatuita tuwe watu wake yeye mwenyewe, si kwa sababu ya matendo yetu wenyewe bali kwa sababu ya kusudi lake na neema yake. Alitujalia neema hiyo katika Kristo Yesu kabla mwanzo wa nyakati; (aiōnios g166)
Therefore I endure every thing on account of the elect, that they also may find salvation in Jeshu Meshiha, with the glory that is eternal. (aiōnios g166)
na hivyo navumilia kila kitu kwa ajili ya wateule wa Mungu, ili wao pia wapate ukombozi upatikanao kwa njia ya Yesu Kristo, na ambao huleta utukufu wa milele. (aiōnios g166)
for Dema hath left me, and hath loved this world, and is gone to Thessalonika; Krispos to Galatia, Titos to Dalmatia; (aiōn g165)
Dema ameupenda ulimwengu huu akaniacha na kwenda zake Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia, na Tito amekwenda Dalmatia. (aiōn g165)
And my Lord will deliver me from every evil work, and will save me into his kingdom, which is in heaven. To Him be glory for ever and ever. Amen. (aiōn g165)
Bwana ataniokoa na mambo yote maovu, na kunichukua salama mpaka katika Utawala wake wa mbinguni. Kwake uwe utukufu milele na milele! Amina. (aiōn g165)
unto the hope of eternal life, which Aloha the true counselled before the times of the ages, (aiōnios g166)
ambayo msingi wake ni tumaini la kupata uzima wa milele. Mungu ambaye hasemi uongo, alituahidia uzima huo kabla ya mwanzo wa nyakati, (aiōnios g166)
and teacheth us to deny wickedness and the lusts of the world, and to live in this world in purity, and in rectitude, and in the fear of Aloha, (aiōn g165)
Neema hiyo yatufunza kuachana na uovu wote na tamaa za kidunia; tuwe na kiasi, tuishi maisha adili na ya kumcha Mungu katika ulimwengu huu wa sasa, (aiōn g165)
that by his grace we might be justified, and be made heirs according to the hope of the life which is eternal. (aiōnios g166)
ili kwa neema yake tupate kukubaliwa kuwa waadilifu na kuupokea uzima wa milele tunaoutumainia. (aiōnios g166)
But, perhaps, for this he passed away for an hour, that thou mayest hold him for ever; (aiōnios g166)
Labda Onesimo aliondoka kwako kwa kitambo tu, kusudi uweze tena kuwa naye daima. (aiōnios g166)
whom he constituted the heir of every thing, and by whom he made the worlds; (aiōn g165)
lakini siku hizi za mwisho, amesema nasi kwa njia ya Mwanae. Yeye ndiye ambaye kwa njia yake Mungu aliumba ulimwengu na akamteua avimiliki vitu vyote. (aiōn g165)
But concerning the Son he hath said, Thy throne, Aloha, (is) for ever and ever, a right sceptre (is) the sceptre of thy kingdom. (aiōn g165)
Lakini kumhusu Mwana, Mungu alisema: “Utawala wako ee Mungu, wadumu milele na milele! Wewe wawatawala watu wako kwa haki. (aiōn g165)
So, too, in another place he saith, Thou art the Priest for ever, after the likeness of Malki-Zedek. (aiōn g165)
Alisema pia mahali pengine: “Wewe ni kuhani milele, kufuatana na utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.” (aiōn g165)
And so was he perfected, and became unto all them who obey him the Cause of eternal salvation; (aiōnios g166)
Na alipofanywa mkamilifu, akawa chanzo cha wokovu wa milele kwa wale wote wanaomtii, (aiōnios g166)
and for the doctrine of ablution and of imposition of the hand, and for the resurrection from the place of the dead, and for the judgment which is eternal? (aiōnios g166)
mafundisho juu ya ubatizo na kuwekewa mikono; ufufuo wa wafu na hukumu ya milele. (aiōnios g166)
and have tasted the good word of Aloha, and the power of the world to come, (aiōn g165)
walikwisha onja wema wa neno la Mungu na nguvu za ulimwengu ujao, (aiōn g165)
where Jeshu hath first entered for us, and become the Priest for ever in the likeness of MALKI-ZEDEK. (aiōn g165)
Yesu ametangulia kuingia humo kwa niaba yetu, na amekuwa kuhani mkuu milele, kufuatana na utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki. (aiōn g165)
For he testifieth concerning him, Thou art a Priest for evermore according to the likeness of Malki-Zedek. (aiōn g165)
Maana Maandiko yasema: “Wewe ni kuhani milele, kufuatana na utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.” (aiōn g165)
For they were made priests without an oath; but this with an oath: as he said unto him by the hand of David, The Lord hath sworn and will not lie, that thou art the Priest for ever in the likeness of Malki-Zedek. (aiōn g165)
Lakini Yesu alifanywa kuhani kwa kiapo wakati Mungu alipomwambia: “Bwana ameapa, wala hataigeuza nia yake: Wewe ni kuhani milele.” (aiōn g165)
But because this (one) standeth for ever, his priesthood passeth not away. (aiōn g165)
Lakini Yesu si kama wao, yeye anaishi milele; ukuhani wake hauondoki kwake. (aiōn g165)
For the law constituted infirm men priests; but the word of the oath, which was subsequent to the law, (hath constituted) THE SON perfect for evermore. (aiōn g165)
Sheria ya Mose huwateua watu waliokuwa dhaifu kuwa makuhani wakuu; lakini ahadi ya Mungu aliyoifanya kwa kiapo na ambayo imefika baada ya sheria imemteua Mwana ambaye amefanywa mkamilifu milele. (aiōn g165)
Nor entered he with the blood of goats and calves, but with the blood of himself he entered once the holy place, and hath found eternal redemption. (aiōnios g166)
Yeye aliingia Mahali Patakatifu mara moja tu, tena hakuwa amechukua damu ya mbuzi wala ng'ombe, bali aliingia kwa damu yake yeye mwenyewe, akatupatia ukombozi wa milele. (aiōnios g166)
how much more then shall the blood of the Meshiha, who, by the Eternal Spirit, himself hath offered without spot unto Aloha, purify our conscience from dead works, to serve the Aloha the Living? (aiōnios g166)
Lakini, kwa damu ya Kristo, mambo makuu zaidi hufanyika! Kwa nguvu za Roho wa milele, Kristo alijitolea mwenyewe dhabihu kamilifu kwa Mungu. Damu yake itatutakasa dhamiri zetu kutokana na matendo yaletayo kifo, ili tupate kumtumikia Mungu aliye hai. (aiōnios g166)
For this was he made the Mediator of the new covenant, that by his death he might become the ransom for those who had transgressed against the first covenant, (and) that they might receive the promise, they, who are called unto the inheritance which is eternal. (aiōnios g166)
Kwa hiyo, Kristo ndiye aliyeratibisha agano jipya ili wale walioitwa na Mungu wazipokee baraka za milele walizoahidiwa. Watazipata, kwani kifo kimetokea ambacho huwakomboa watu kutoka yale makosa waliyofanya wakati wa lile agano la kale. (aiōnios g166)
otherwise he would have been obligated many times to suffer from the beginning of the world. But now, in the end of the world, once hath he offered himself, that by his sacrifice he might abolish sin. (aiōn g165)
maana ingalikuwa hivyo, Kristo angalipaswa kuteswa mara nyingi tangu kuumbwa ulimwengu. Lakini sasa nyakati hizi zinapokaribia mwisho wake, yeye ametokea mara moja tu, kuondoa dhambi kwa kujitoa yeye mwenyewe dhabihu. (aiōn g165)
For by faith we perceive that the worlds were ordained by the word of Aloha, and (how) these (things) which are seen were from those which are not seen. (aiōn g165)
Kwa imani sisi tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu; vitu vinavyoonekana kutoka vitu visivyoonekana. (aiōn g165)
Jeshu Meshiha is yesterday, and to-day, and for ever. (aiōn g165)
Yesu Kristo ni yuleyule, jana, leo na milele. (aiōn g165)
But the God of peace, who brought up from the house of the dead the great Shepherd of the flock, by the blood of the eternal covenant, who is Jeshu Meshiha, our Lord, (aiōnios g166)
Mungu amemfufua Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ni Mchungaji Mkuu wa kondoo kwa sababu ya kumwaga damu yake iliyothibitisha agano la milele. (aiōnios g166)
make you perfect in every good work, that ye may do his will, and effect in you whatever is good before him, by Jeshu Meshiha: to him be glory unto the age of ages. Amen. (aiōn g165)
Mungu wa amani awakamilishe katika kila tendo jema ili mtekeleze mapenzi yake; yeye na afanye ndani yetu kwa njia ya Kristo yale yanayompendeza mwenyewe. Utukufu uwe kwake, milele na milele! Amina. (aiōn g165)
and the tongue is a fire, a world of sin, like a forest is the tongue itself among our members; it defileth all of our body, and burneth the course of our generations which run (forward) as a wheel, and kindleth also itself with fire. (Geenna g1067)
Hali kadhalika ulimi ni kama moto. Umejaa maovu chungu nzima, unayo nafasi yake katika miili yetu na hueneza ubaya katika nafsi zetu zote. Huteketeza maisha yetu yote kwa moto utokao Jehanamu kwenyewe. (Geenna g1067)
as men who are regenerated, not by a perishable seed, but by that which is imperishable, by the living word of Aloha which abideth for ever. (aiōn g165)
Maana kwa njia ya neno hai la Mungu, ninyi mmezaliwa upya, si kama watoto wa baba awezaye kufa, bali baba asiyekufa milele. (aiōn g165)
but the word of our God abideth for ever; and this is that word which is preached unto you. (aiōn g165)
Lakini neno la Bwana hudumu milele.” Neno hilo ni hiyo Habari Njema iliyohubiriwa kwenu. (aiōn g165)
Whoever shall speak, as the word of Aloha let him speak and whoever ministereth, (he shall minister) as from the power which Aloha giveth to him, that in every thing which you do Aloha may be glorified through Jeshu Meshiha, whose are the glory and honour to the age of ages. Amen. (aiōn g165)
Anayesema kitu, maneno yake na yawe kama maneno ya Mungu; anayetumika anapaswa kutumikia kwa nguvu anayojaliwa na Mungu, ili katika mambo yote, Mungu atukuzwe kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye utukufu na nguvu ni vyake milele na milele! Amina. (aiōn g165)
But the God of grace, who hath called us to his eternal glory by Jeshu Meshiha, will give to us while we endure these few afflictions to be strengthened, and confirmed, and established in him for ever. (aiōnios g166)
Lakini mkisha teseka muda mfupi, Mungu aliye asili ya neema yote na ambaye anawaiteni muushiriki utukufu wake wa milele katika kuungana na Kristo, yeye mwenyewe atawakamilisheni na kuwapeni uthabiti, nguvu na msingi imara. (aiōnios g166)
To Him be glory and dominion and honour unto the age of ages. Amen. (aiōn g165)
Kwake uwe uwezo milele! Amina. (aiōn g165)
for so abundantly shall be given to you the entrance of the eternal kingdom of our Lord and our Saviour Jeshu Meshiha. (aiōnios g166)
Kwa namna hiyo mtafaulu kupewa haki kamili ya kuingia katika Utawala wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. (aiōnios g166)
For if Aloha upon the angels who sinned was not lenient, but in chains of darkness shut them in the deeps, and delivered them to be kept to the judgment of pain; (Tartaroō g5020)
Malaika walipotenda dhambi, Mungu hakuwahurumia, bali aliwatupa katika moto wa Jehanamu ambako wamefungwa wakingojea Siku ile ya Hukumu. (Tartaroō g5020)
But increase in grace, and in the knowledge of our Lord and our Saviour Jeshu Meshiha, and (of) Aloha the Father, Whose be glory both now, and in all time, and to the days eternal. Amen. (aiōn g165)
Lakini endeleeni kukua katika neema na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo. Utukufu uwe kwake, sasa na hata milele! Amina. (aiōn g165)
And the life was manifested, and we have seen, and testify, and preach to you the eternal life which was with the Father, and was manifested to us. (aiōnios g166)
Uzima huo ulipotokea sisi tuliuona na sasa tunasema habari zake na kuwaambieni juu ya uzima huo wa milele uliokuwa kwa Baba na uliodhihirishwa kwetu. (aiōnios g166)
And the world passeth, (both) it and its lusts; but he who doeth the will of Aloha, continueth for ever. (aiōn g165)
Ulimwengu pamoja na vitu vyake vyote vyenye kutamanika unapita; lakini mtu atendaye atakalo Mungu, anaishi milele. (aiōn g165)
And this is the promise which he promised to us, eternal life. (aiōnios g166)
Na ahadi aliyotuahidia sisi ndiyo hii: uzima wa milele. (aiōnios g166)
For every one who hateth his brother is a man-killer; and we know that in no man-killer can abide the life which is eternal. (aiōnios g166)
Kila anayemchukia ndugu yake ni muuaji; nanyi mnajua kwamba muuaji yeyote yule hana uzima wa milele ndani yake. (aiōnios g166)
And this is the testimony, That the life which is eternal, Aloha hath given to us, and this life is in his Son. (aiōnios g166)
Na, ushahidi wenyewe ndio huu: Mungu alitupatia uzima wa milele, na uzima huo uko kwa Bwana. (aiōnios g166)
These I have written to you, that you may know that you have the life which is eternal, who believe in the name of the Son of Aloha. (aiōnios g166)
Nawaandikieni mpate kujua kwamba mnao uzima wa milele ninyi mnaoamini kwa jina la Mwana wa Mungu. (aiōnios g166)
And we know that the Son of Aloha hath come, and hath given us knowledge to know the truth, and to be in him in the truth, in his Son Jeshu the Meshiha. This is Aloha the true, and the life which is eternal. (aiōnios g166)
Twajua pia kwamba Mwana wa Mungu amekuja, akatupa elimu ili tumjue Mungu wa kweli; tuishi katika muungano na Mungu wa kweli—katika muungano na Mwanae, Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli, na huu ndio uzima wa milele. (aiōnios g166)
on account of the truth which abideth in us, and is with us for ever; (aiōn g165)
kwa sababu ukweli unakaa nasi milele. (aiōn g165)
And the angels who kept not their primacy, but left their habitation, unto the judgment of the great day in chains unknown, under darkness, he hath kept. (aïdios g126)
Na, malaika ambao hawakuridhika na cheo chao, wakayaacha makao yao ya asili, Mungu amewafunga gizani kwa minyororo ya milele wahukumiwe Siku ile kuu. (aïdios g126)
As Sadum and Omuro, and the cities which were around them, which in manner of them committed fornication, and went after other flesh, are lying under everlasting fire, condemned unto judgment. (aiōnios g166)
Kumbukeni pia Sodoma na Gomora, na miji ya kandokando yake; wenyeji wake walifanya kama wale malaika; walifanya uzinzi na mambo yaliyo kinyume cha maumbile, wakapewa hukumu ya moto wa milele, iwe onyo kwa watu wote. (aiōnios g166)
turbulent waves of the sea, which, by their foaming, manifest their shame; erring stars, unto whom the blackness of darkness that is eternal is reserved. (aiōn g165)
Watu hao ni kama mawimbi makali ya bahari, na matendo yao ya aibu yanaonekana dhahiri kama vile mapovu ya mawimbi. Wao ni kama nyota zinazotangatanga, ambao Mungu amewawekea mahali pao milele katika giza kuu. (aiōn g165)
ourselves in the love of Aloha to keep, while looking for the mercy of our Lord Jeshu Meshiha unto our eternal salvation. (aiōnios g166)
na kubaki katika upendo wa Mungu, mkiwa mnamngojea Bwana wetu Yesu Kristo awapeni uzima wa milele kwa huruma yake. (aiōnios g166)
Be glory, and dominion, and honour, and grandeur, both now and in all ages. Amen. (aiōn g165)
kwake yeye aliye peke yake Mungu, Mkombozi wetu, uwe utukufu, ukuu, nguvu na mamlaka kwa njia ya Kristo Bwana wetu, tangu zama zote, sasa na hata milele! Amina. (aiōn g165)
and hath made us a priestly kingdom unto Aloha and his Father; to whom be glory and dominion for ever and ever. Amen. (aiōn g165)
akatufanya sisi kuwa ufalme wa makuhani, tumtumikie Mungu, Baba yake. Kwake Yesu Kristo uwe utukufu na nguvu, milele na milele! Amina. (aiōn g165)
and who liveth and who have been dead; and, behold, I am alive for ever and ever. Amen! And I have the keys of death and of Sheul. (aiōn g165, Hadēs g86)
Mimi ni yeye aliye hai! Nilikuwa nimekufa, lakini, tazama, sasa ni mzima milele na milele. Ninazo funguo za kifo na Kuzimu. (aiōn g165, Hadēs g86)
And when those living-ones give glory and honour and thanks unto Him who sitteth upon the throne, to Him who liveth for ever and ever, (aiōn g165)
Kila mara viumbe vinne vilipoimba nyimbo za kumtukuza, kumheshimu na kumshukuru huyo aliyeketi juu ya kiti cha enzi, ambaye anaishi milele na milele, (aiōn g165)
the four and twenty presbyters fell before Him who sitteth upon the throne, and worshipped Him who liveth for ever and ever, and cast their crowns before the throne, saying, (aiōn g165)
wale wazee ishirini na wanne hujiangusha mbele ya huyo aliyeketi juu ya kiti cha enzi na kumwabudu huyo ambaye anaishi milele na milele; na huziweka taji zao mbele ya kiti cha enzi wakisema: (aiōn g165)
And every creature which is in heaven, and on earth, And under the earth, and in the sea, And all them which are therein. And I heard him who sat upon the throne saying: To the Lamb let there be given blessing, and honour, and glory, and praise, and dominion, for ever and ever. (aiōn g165)
Nikasikia viumbe vyote mbinguni, duniani, chini kuzimuni na baharini—viumbe vyote ulimwenguni—vikisema: “Kwake yeye aketiye katika kiti cha enzi, na kwa Mwanakondoo, iwe sifa na heshima na utukufu na enzi milele na milele.” (aiōn g165, questioned)
And I saw a green horse, and he who sat upon him had the name of Death, and Shiul followed after him. And there was given to him power over the fourth of the earth, to kill with the sword, and with famine, and with death, and with the toothed beast of the earth. (Hadēs g86)
Nami nikatazama, na kumbe alikuwapo farasi mmoja hapo, rangi yake kijivu. Na jina la mpanda farasi wake lilikuwa kifo, na Kuzimu alimfuata nyuma. Hao walipewa mamlaka juu ya robo moja ya dunia, wawaue watu kwa upanga, njaa, tauni na kwa wanyama wakali wa dunia. (Hadēs g86)
saying, Amen. Blessing, and glory, and wisdom, and thanksgiving, And honour, and might, and power, To our God, for ever and ever. Amen. (aiōn g165)
wakisema, “Amina! Sifa, utukufu, hekima, shukrani, heshima, uwezo na nguvu viwe kwa Mungu wetu, milele na milele! Amina!” (aiōn g165)
AND the Fifth angel sounded. And I saw a star which fell from heaven unto the earth and there was given to him the key of the pit of the abyss. (Abyssos g12)
Kisha malaika wa tano akapiga tarumbeta yake. Nami nikaona nyota iliyokuwa imeanguka juu ya nchi kutoka mbinguni. Nayo ikapewa ufunguo wa shimo la Kuzimu. (Abyssos g12)
And he opened the pit of the abyss, and smoke ascended from the pit, as the smoke of a burning furnace; and the sun was darkened, and the air, from the smoke of the pit. (Abyssos g12)
Basi, nyota hiyo ikafungua shimo la Kuzimu, kukatoka moshi wa tanuru kubwa. Jua na anga vikatiwa giza kwa moshi huo wa Kuzimu. (Abyssos g12)
And they had a king over them, the angel of the abyss, and his name in Hebrew is Abadon; but in Javanith his name is Apolon. (Abyssos g12)
Tena wanaye mfalme anayewatawala, naye ndiye malaika wa kuzimu; jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kigiriki ni Apolioni, yaani mwangamizi. (Abyssos g12)
and sware by Him who liveth for ever and ever, who created heaven and those who are in it, and the earth and those that are in it, and the sea and those that are in it, That time no more shall be; (aiōn g165)
akaapa kwa jina la Mungu aishiye milele na milele, Mungu aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, bahari na vyote vilivyomo, dunia na vyote vilivyomo. Akasema, “Wakati wa kusubiri zaidi umekwisha! (aiōn g165)
And when they shall have completed their testimony, the beast of prey, which ascended from the abyss, will make war against them, and overcome them, (Abyssos g12)
Lakini wakisha maliza kutangaza ujumbe huo, mnyama atokaye shimoni kuzimu atapigana nao, atawashinda na kuwaua. (Abyssos g12)
And the Seventh angel sounded. And there were voices and thunders, saying, The kingdom of the world Is of our Lord, and of his Meshiha; And he will reign for ever and ever! (aiōn g165)
Kisha malaika wa saba akapiga tarumbeta yake. Na sauti kuu zikasikika mbinguni zikisema, “Sasa utawala juu ya ulimwengu ni wa Bwana wetu na Kristo wake. Naye atatawala milele na milele!” (aiōn g165)
And I saw another angel flying through heaven, who with blood had the everlasting gospel to preach to them who dwell on the earth, and unto every nation and tribe, and tongue and people; (aiōnios g166)
Kisha nikamwona malaika mwingine anaruka juu angani akiwa na Habari Njema ya milele ya Mungu, aitangaze kwa watu wote waishio duniani, kwa mataifa yote, makabila yote, watu wa lugha zote na rangi zote. (aiōnios g166)
And the smoke of their torment For ever and ever will ascend. And they have no rest day and night Who worship the beast of prey and his image. (aiōn g165)
Moshi wa moto unaowatesa kupanda juu milele na milele. Watu hao waliomwabudu huyo mnyama na sanamu yake, na kutiwa alama ya jina lake, hawatakuwa na nafuu yoyote usiku na mchana.” (aiōn g165)
And one of the four living-ones gave to the seven angels SEVEN VIALS of gold, which were full of the wrath of Aloha, who liveth for ever and ever. (aiōn g165)
Kisha, mmojawapo wa vile viumbe vinne akawapa hao malaika saba mabakuli ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu, aishiye milele na milele. (aiōn g165)
The beast of prey which thou seest, was, and is not; and will ascend from the abyss, and go into perdition: and they who dwell on the earth will admire, they whose name is not written in the book of life from the foundations of the world, while they see the beast of prey, who was, and is not, and draweth nigh. (Abyssos g12)
Huyo mnyama uliyemwona alikuwa hai hapo awali, lakini sasa amekufa. Hata hivyo, karibu sana atapanda kutoka shimoni kuzimu, lakini ataangamizwa. Wanaoishi duniani watashangaa; naam, watu wote ambao majina yao hayakupata kuandikwa katika kitabu cha uzima tangu mwanzo wa ulimwengu, watashangaa kumwona huyo mnyama ambaye hapo awali, aliishi, kisha akafa na sasa anatokea tena! (Abyssos g12)
And the second time they said, Halleluia! And her smoke went up for ever and ever. (aiōn g165)
Wakasema, “Asifiwe Mungu! Moshi wa moto unaoteketeza mji huo utapanda juu milele na milele!” (aiōn g165)
And the beast of prey was taken, and the false prophet with him who wrought signs before him, with which he deluded them who received the signature of the beast of prey, and them who worshipped his image; and living they were both cast into the lake of fire which burneth with sulphur. (Limnē Pyr g3041 g4442)
Lakini huyo mnyama akachukuliwa mateka, pamoja na nabii wa uongo aliyekuwa akifanya miujiza mbele yake. (Kwa miujiza hiyo, alikuwa amewapotosha wale waliokuwa na chapa ya huyo mnyama, na ambao walikuwa wameiabudu sanamu yake.) Huyo mnyama pamoja na huyo nabii walitupwa wote wawili, wakiwa wazimawazima, ndani ya ziwa linalowaka moto wa kiberiti. (Limnē Pyr g3041 g4442)
AND I saw an angel descending from heaven, having the key of the abyss, and a great chain in his hand. (Abyssos g12)
Kisha nikamwona malaika mmoja anashuka kutoka mbinguni akiwa na ufunguo wa kuzimu na mnyororo mkubwa mkononi mwake. (Abyssos g12)
and cast him into the abyss, and shut and sealed over him, that he should no more seduce the nations, until the thousand years be completed: but after them he will be loosed a little time. (Abyssos g12)
Malaika akalitupa Kuzimu, akaufunga mlango wa kuingilia huko na kuutia mhuri ili lisiweze tena kuyapotosha mataifa mpaka hapo miaka elfu moja itakapotimia. Lakini baada ya miaka hiyo ni lazima lifunguliwe tena, lakini kwa muda mfupi tu. (Abyssos g12)
And the accuser who seduced them was cast into the lake of fire and of sulphur, as was also the beast of prey and the false prophet; and they will be tormented day and night for ever and ever. (aiōn g165, Limnē Pyr g3041 g4442)
Ibilisi, aliyekuwa anawapotosha, akatupwa ndani ya ziwa linalowaka moto wa kiberiti, walimo yule mnyama na yule nabii wa uongo, nao watateswa mchana na usiku, milele na milele. (aiōn g165, Limnē Pyr g3041 g4442)
And the sea gave up the dead which were in it, and death and shiul gave up the dead which were in them. And they were judged every one according to their works. (Hadēs g86)
Bahari ikawatoa nje wafu waliokuwa ndani yake; kifo na kuzimu vikawatoa nje wafu waliokuwa ndani yao. Kila mmoja akahukumiwa kufuatana na matendo yake. (Hadēs g86)
And death and shiul were cast into the lake of fire, which is the second death. (Hadēs g86, Limnē Pyr g3041 g4442)
Kisha kifo na kuzimu vikatupwa ndani ya ziwa la moto. Ziwa hili la moto ndicho kifo cha pili. (Hadēs g86, Limnē Pyr g3041 g4442)
And if a man was not found written in the Book of Life, he was cast into the lake of fire. (Limnē Pyr g3041 g4442)
Mtu yeyote ambaye jina lake halikupatikana limeandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika ziwa la moto. (Limnē Pyr g3041 g4442)
But the fearful, and the faithless, and sinners, and the unclean, and murderers, and fornicators, and sorcerers, and servers of idols, and all liars, (shall have) their portion in the lake which burneth with fire and sulphur; which is the second death. (Limnē Pyr g3041 g4442)
Lakini watu waoga, wasioamini, wapotovu, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, na waongo wote, mahali pao patakuwa ndani ya lile ziwa linalowaka moto na kiberiti; hicho ndicho kifo cha pili.” (Limnē Pyr g3041 g4442)
And night shall be no more: nor any need have they of the light of a lamp, or the light of the sun; for the Lord God enlighteneth them, and they will reign for ever and ever. (aiōn g165)
Usiku hautakuwako tena, wala hawatahitaji mwanga wa taa au wa jua, maana Bwana Mungu atawaangazia, nao watatawala milele na milele. (aiōn g165)

ESE > Aionian Verses: 200
SWH > Aionian Verses: 199