< Mark 7 >

1 AND there gathered to him Pharishee and Sophree, who had come from Urishlem;
Mafarisayo na baadhi ya waandishi ambao walikuwa wametokea Yerusalemu walikusanyika kumzunguka yeye.
2 and they saw some of his disciples eating bread with their hands not washed; and they complained.
Na waliona kuwa baadhi ya wanafunzi wake walikula mkate kwa mikono najisi; ambayo haikuoshwa.
3 For all the Jihudoyee and Pharishee, unless they carefully wash their hands, do not eat, because they hold the tradition of the elders;
(kwa Mafarisayo na Wayahudi wote hawali mpaka wameosha mikono yao vizuri; wanashikilia utamaduni wa wazee. Wakati
4 and (coming) from the market, unless they lave, they eat not. And many other of those (things) there are which they have received to observe, (as) the baptisms of cups, and of measures, and of brasen utensils, and of beds.
Mafarisayo wanaporudi kutoka mahali pa soko, hawali mpaka wameoga kwanza. Na kuna sheria zingine ambazo wanazifuata kabisa, ikiwa ni pamoja na kuosha vikombe, masufuria, vyombo vya shaba, na hata viti vinavyotumika wakati wa chakula.)
5 And the Sophree and Pharishee questioned him, Why do not your disciples walk according to the tradition of the elders; but, while their hands are not washed, eat bread?
Mafarisayo na waandishi walimuuliza Yesu, “Kwa nini wanafunzi wako hawaishi kulingana na tamaduni za wazee, kwani wanakula mkate pasipo kunawa mikono?”
6 But he said to them, Well prophesied concerning you Eshaia the prophet, you hypocrites; as it is written, This people with their lips honour me, but their heart is very far from me.
Lakini yeye aliwaambia, “Isaya alitabiri vizuri kuhusu ninyi wanafiki, aliandika, 'Watu hawa wananiheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali na mimi.
7 But in vain do they reverence me while they teach the teachings of the commandments of men.
Wananifanyia ibaada zisizo na maana, wakifundisha sheria za wanadamu kama mapokeo yao.'
8 For you have abandoned the commandment of God and hold the tradition of men, as the baptisms of cups and measures, and many things like these.
Mmeiacha sheria ya Mungu na kushikilia kwa wepesi tamaduni za wanadamu.”
9 He said to them (moreover), You decently suppress the commandment of God, that you may establish your tradition.
Na akasema kwao, “Mmeikataa amri ya Mungu kwa urahisi ili kwamba mtunze tamaduni zenu!
10 For Musha hath said, Honour thy father and thy mother; and whosoever curseth father and mother, the death he shall die.
Kwa kuwa Musa alisema, 'mheshimu baba yako na mama yako,' na 'Yeye asemaye mabaya juu ya baba yake au mama yake hakika atakufa.'
11 But you say, If a man shall say to his father, or to his mother, My oblation, (be that) whatever from me thou mayest profit;
Lakini mnasema, 'kama mtu akisema kwa baba yake au mama, “Msaada wowote ambao mngepokea kutoka kwangu ni hazina ya Hekalu,”' (hiyo ni kusema kwamba, 'imetolewa kwa Mungu')
12 and you permit him not to do any thing for his father and his mother.
hivyo haumruhusu kufanya jambo lolote kwa ajili ya baba au mama yake.
13 But you reject the word of Aloha for the sake of the tradition which you have delivered: and many similar (observances) to these you practise.
Mnaifanya amri ya Mungu kuwa bure kwa kuleta tamaduni zenu. Na mambo mengi ya jinsi hiyo mnayoyafanya.”
14 And Jeshu called the whole multitude, and said to them, Hear me, all of you, and understand:
Aliwaita makutano tena na kuwaambia, “Mnisikilize mimi, ninyi nyote, na mnielewe.
15 It is not that which is without the man, and which entereth into him, that can defile him: but that which proceedeth from him, that defileth a man.
Hakuna chochote kutoka nje ya mtu ambacho chaweza kumchafua mtu kiingiapo kwake. Bali ni kile kimtokacho mtu ndicho kimchafuacho.
16 He who hath ears to hear, let him hear.
(Zingatia: mstari huu, “kama mtu yeyote ana masikio ya kusikia, na asikie” haumo kwenye nakala za kale).
17 But when Jeshu had gone into the house (apart) from the multitude, his disciples asked him concerning that parable.
Yesu alipowaacha makutano na kuingia nyumbani, wanafunzi wake wakamwuliza kuhusu mfano huo.
18 He said to them, How dull are even you! Know you not, that nothing from without that entereth a man can defile him,
Yesu akasema, “Na ninyi pia bado hamjaelewa? Hamuoni kwamba chochote kimuingiacho mtu hakiwezi kumchafua,
19 because it entereth not into his heart, but into his belly, and is cast out in the purgation which all food purgeth?
kwa sababu hakiwezi kwenda kwenye moyo wake, lakini kinaingia katika tumbo lake na kisha kinapita kwenda chooni.” Kwa maelezo haya Yesu alivifanya vyakula vyote kuwa safi.
20 But that which proceedeth from a man, that polluteth a man.
Alisema, “Ni kile ambacho kinamtoka mtu ndicho kimchafuacho.
21 For from within, from the heart of the sons of men, go forth evil thoughts, adultery, fornication, robbery, murder,
Kwa kuwa hutoka ndani ya mtu, nje ya moyo, hutoka mawazo maovu, zinaa, wizi, mauaji,
22 rapacity, malice, fraud, obscenity, an evil eye, blasphemy, vain-glory, folly;
uasherati, tamaa mbaya, uovu, udanganyifu, kujamiiana, wivu, kashfa, majivuno, ujinga.
23 all these evils come from within, and they defile a man.
Maovu haya yote yanatoka ndani, ndiyo yale yamchafuayo mtu.”
24 FROM thence Jeshu arose and went to the confine of Tsur and of Tsaidon, and entered into a certain house: and he was unwilling that any man should know of him, but he could not conceal.
Aliamka kutoka pale na kuondoka kwenda katika mkoa wa Tiro na Sidoni. Aliingia ndani na hakutaka mtu yeyote ajue kuwa alikuwa hapo, lakini haikuwezekana kumficha.
25 For immediately heard a certain woman concerning him, whose daughter had an unclean spirit; and she came, (and) fell before his feet.
Lakini ghafla mwanamke, ambaye mtoto wake mdogo alikuwa na roho mchafu, alisikia habari zake, akaja, na akaanguka miguuni pake.
26 But that woman was a Gentile of Phuniki of Suria, and she prayed of him to cast out the demon from her daughter.
Mwanamke huyo alikuwa Myunani, wa kabila la Kifoeniki. Alimsihi yeye amfukuze pepo kutoka kwa binti yake.
27 But Jeshu said to her, Let the children first be filled; for it is not well to take the bread of the children and cast it to the dogs.
Yesu akamwambia mwanamke, “Waache watoto walishwe kwanza, kwa kuwa sio sawa kuuchukua mkate wa watoto na kuwatupia mbwa.”
28 But she answering said to him, Yes, my Lord, yet the dogs also from beneath the table eat the crumbs of the children.
Lakini mwanamke akamjibu na kusema, “Ndiyo Bwana, hata mbwa chini ya meza hula mabaki ya chakula cha watoto.”
29 Jeshu saith to her, Go; on account of that word, the demon hath gone forth from thy daughter.
Akamwambia, “Kwa kuwa umesema hivi, uko huru kwenda. Pepo ameshamtoka binti yako.”
30 And she went to her house, and found her daughter lying on the couch, and the demon had gone out from her.
Mwanamke alirudi nyumbani kwake na akamkuta binti yake amelala kitandani, na pepo alikuwa amemtoka.
31 Jeshu again departed from the confine of Tsur and of Tsaidon, and came to the sea of Galila, on the confine of the Ten Cities;
Yesu alitoka tena nje ya mkoa wa Tiro na kupitia Sidoni kuelekea Bahari ya Galilaya mpaka kanda ya Dikapolisi.
32 and they brought to him a blind man, a stammerer, and besought him to lay upon him the hand.
Na wakamletea mtu aliyekuwa kiziwi na alikuwa hawezi kuzungumza vizuri, walimsihi Yesu aweke mikono juu yake.
33 And he took him aside from the crowd by himself, and put his fingers in his ears, and spat, and touched his tongue.
Alimtoa nje ya kusanyiko kwa siri, na akaweka vidole vyake kwenye masikio yake, na baada ya kutema mate, aligusa ulimi wake.
34 And he looked up to heaven, and sighed, and said to him, Be opened:
Alitazama juu mbinguni, akahema na kumwambia, “Efata,” hiyo ni kusema “funguka!”
35 and in that hour his ears were opened, and the bond of his tongue was loosed, and he spake plainly.
Na muda ule ule masikio yakafunguka, na kilichokuwa kimezuia ulimi kiliharibiwa na akaweza kuongea vizuri.
36 And he charged them that to no man they should tell this. But so much as he charged them, they the more proclaimed it;
Na aliwaamuru wasimwambie mtu yeyote. Lakini kadri alivyowaamuru, ndivyo walivyotangaza habari hizo kwa wingi.
37 and they were exceedingly astonished, and said, He doeth every thing well; the deaf he maketh to hear, and them who spoke not, to speak.
Hakika walishangazwa, na kusema, “Amefanya kila kitu vizuri. Hata amewafanya viziwi kusikia na mabubu kuongea.”

< Mark 7 >