< Luke 6 >

1 IT was on the shabath, while Jeshu was walking among the corn, and his disciples gathered the ears, and rubbed in their hands and ate (them).
Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano, na wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakaondoa punje zake kwa mikono, wakala.
2 But some of the Pharishee said to them, Why do you a thing which it is not lawful on the shabuth to do?
Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato?”
3 Jeshu answered and said to them, And this have you not read, what David did when he hungered, and they who were with him?
Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma jinsi alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
4 that he went into the house of Aloha, and the bread of the table of the Lord he took, ate, and gave to them who were with him, that (bread) which was not lawful to eat, except by the priests only?
Yeye aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akachukua ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu, akala na kuwapa wenzake. Kisheria, ni makuhani tu peke yao ndio walioruhusiwa kula mikate hiyo.”
5 And he said to them, That the Lord of the shabath is the Son of man.
Hivyo akawaambia, “Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato.”
6 And it was on another shabath (that) he entered into the synagogue, and taught. And there was a man whose right hand was dried:
Siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia katika sunagogi, akafundisha. Mle ndani mlikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
7 and the Sophree and Pharishee watched him, if he would heal on the shabath, that they might accuse him.
Walimu wa Sheria na Mafarisayo walitaka kupata kisingizio cha kumshtaki Yesu na hivyo wakawa wanangojea waone kama angemponya mtu siku ya Sabato.
8 But he knew their thoughts, and said to the man whose hand was dried, Rise (and) come into the midst of the assembly.
Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Inuka, simama katikati.” Yule mtu akaenda akasimama katikati.
9 And when he had come and stood, Jeshu said to them, I ask you which is lawful to do on the shabath, good or evil, life to save or to destroy?
Kisha Yesu akawaambia, “Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?”
10 And he beheld them all, and said to him, Stretch forth thine hand: and he stretched it forth, and his hand was restored as its fellow.
Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, “Nyosha mkono wako.” Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.
11 But they were filled with envy, and spake one with another what they should do with Jeshu.
Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.
12 BUT it was in those days that Jeshu went forth into a mountain to pray; and there remained he all night in the prayer of Aloha.
Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akimwomba Mungu.
13 And when the day brake, he called his disciples, and chose from them twelve, those whom he named Apostles,
Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume:
14 Shemun, he whose name was Kipha, and Andreas his brother, and Jacub, and Juchanon, and Philipos, and Bar Tholmai,
Simoni (ambaye Yesu alimpa jina Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo na Yohane, Filipo na Bartholomayo,
15 and Mathai, and Thoma, and Jakub bar Chalphai, and Shemun who was called the Zealous,
Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo na Simoni (aliyeitwa Zelote),
16 and Jihuda bar Jakub, and Jihuda Scaruta, he who was the traitor.
Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.
17 And Jeshu descended with them, and stood in the plain, and a great assembly of his disciples and a multitude of people from all Jehud, and from Urishlem, and from the sea-coast of Tsur and Tsaidon,
Baada ya kushuka mlimani pamoja na mitume, Yesu alisimama mahali palipokuwa tambarare. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati wa watu waliotoka pande zote za Yudea na Yerusalemu na pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walifika kumsikiliza Yesu na kuponywa magonjwa yao.
18 who had come to hear his words, and to be healed of their diseases; and they who were vexed by unclean spirits, and they were healed.
Aliwaponya pia wote waliokuwa wanasumbuliwa na pepo wachafu.
19 And all the multitudes sought to approach to him, for the power went forth from him, and all of them he healed.
Watu wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa inatoka ndani yake na kuwaponya wote.
20 AND he lifted up his eyes upon his disciples, and said, Blessed are you poor, for yours is the kingdom of Aloha.
Yesu akawageukia wanafunzi wake, akasema: “Heri ninyi mlio maskini, maana Ufalme wa Mungu ni wenu.
21 Blessed are you who hunger now, for you shall be satisfied. Blessed are you who weep now, for you shall laugh.
Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
22 Blessed are you when the sons of man hate you, and separate you, and revile you, and cast out your name as evil, for the sake of the Son of man.
“Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
23 Rejoice in that day, and exult, for your reward is great in heaven; for thus did they to your fathers the prophets.
Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
24 But woe to you (who are) rich, because you have received your consolation.
Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
25 Woe to you (who are) full, for you shall hunger. Woe to you who laugh now, for you shall weep and lament.
Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
26 Woe to you when the sons of men shall speak well of you, for so did to the prophets of falsity their fathers.
Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
27 But I say to you who hear, Love your adversaries, and do good to those who hate you,
“Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
28 and bless those who execrate you, and pray for those who lead you by violence.
Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
29 And to one who striketh you on your cheek, offer to him the other: and whosoever taketh your cloak, forbid him not your coat also.
Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
30 To every one who asketh of you give; and from him who taketh of yours demand not (again).
Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
31 And as you will that the sons of man should do to you, so do you also to them.
Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.
32 For if you love them who love you, what is your grace? for sinners also love those who love them.
“Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda ninyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.
33 And if you do good to those who benefit you, what is your grace? for the sinners also thus do.
Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo!
34 And if you lend to them from whom you expect to be recompensed, what is your grace? for sinners also lend to sinners, that they might be profited.
Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!
35 But love your adversaries, and do good to them, and lend, and cut not off the hope of any one; and great shall be your reward, and you shall be the children of the Most High; for he is benign to the evil and to the ungrateful.
Ila nyinyi wapendeni adui zenu, na kuwatendea mema; kopesheni bila kutazamia malipo, na tuzo lenu litakuwa kubwa, nanyi mtakuwa watoto wa Mungu aliye juu. Kwa maana yeye ni mwema kwa wale wasio na shukrani na walio wabaya.
36 Be you therefore merciful, as also your Father is merciful.
Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.
37 JUDGE not, and you shall not be judged; condemn not, and you shall not be condemned; release, and you shall be released;
“Msiwahukumu wengine, nanyi hamtahukumiwa; msiwalaumu wengine, nanyi hamtalaumiwa; wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
38 give, and it shall be given to you; in good measure, compressed, redundant, shall they pour into your bosoms. For in that measure you mete, it shall be measured to you.
Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu.”
39 And he spake to them a parable: How can the blind lead the blind, and not fall into the ditch?
Akawaambia mfano huu: “Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwenzake? La! Wote wataanguka shimoni.
40 The disciple than his master is not greater; but every man who is perfect shall be as his master.
Mwanafunzi hamshindi mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi akisha hitimu huwa kama mwalimu wake.
41 For why behold you the rod that is in the eye of your brother, but the rafter in your (own) eye is not seen by you?
Unawezaje kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwenzio, usione boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
42 Or how can you say to your brother, My brother, permit (that) I pull out the rod that is in your eye, and behold the rafter in your own eye is not seen by you? Hypocrite! first take out the rafter from your own eye, and then shall you see to take out the rod that is in the eye of your brother.
Au, unawezaje kumwambia mwenzako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi katika jicho lako, na huku huioni boriti iliyoko katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, na hivyo utaona sawasawa kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilicho katika jicho la ndugu yako.
43 A good tree maketh not evil fruits; also an evil tree maketh not good fruits:
“Mti mwema hauzai matunda mabaya, wala mti mbaya hauzai matunda mazuri.
44 for every tree by its fruits is known. For how gather they from thorns figs? neither also from the bramble do they gather in grapes.
Watu huutambua mti kutokana na matunda yake. Ni wazi kwamba watu hawachumi tini katika michongoma, wala hawachumi zabibu katika mbigili.
45 The good man, from the good treasures which are in his heart, bringeth forth good things; and the evil man, from the evil treasures which are in his heart, bringeth forth evil things; for from the adundancies of the heart the lips speak.
Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka katika hazina bora iliyo moyoni mwake; na mtu mbaya hutoa yaliyo mabaya katika hazina mbaya iliyo moyoni mwake, kwa maana mtu huongea kutokana na yale yaliyojaa moyoni mwake.
46 Why call you me, My Lord, my Lord, and the things which I say do not?
“Mbona mwaniita Bwana, Bwana, na huku hamtimizi yale ninayosema?
47 Every man who cometh to me and heareth my words, and doeth them, I will show you to whom he is like.
Nitawapeni mfano unaofaa kuonyesha alivyo yeyote yule anayekuja kwangu, akasikia maneno yangu na kuyatimiza:
48 He is like a man who built a house, and digged deep, and laid the foundations upon the rock: but when there was an inundation, the inundation beat against that house, and it could not shake it, for its foundations were set upon a rock.
Huyo anafanana na mtu ajengaye nyumba, ambaye amechimba chini na kuweka msingi wake juu ya mwamba; kukatokea mafuriko ya mto, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa imara.
49 And he who heareth and doeth not, is like a man who built his house upon the dust, without a foundation: and when the river beat against it, it immediately fell, and the ruin was great of that house.
Lakini yeyote anayesikia maneno yangu lakini asifanye chochote, huyo anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo, bila msingi. Mafuriko ya mto yakatokea, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, ikaanguka na kuharibika kabisa!”

< Luke 6 >