< John 2 >

1 AND on the third day there was a feast in Kotna, a city of Galila; and the mother of Jeshu was there:
Baada ya siku tatu, kulikuwa na arusi huko Kana ya Galilaya na mama yake Yesu alikuwa huko.
2 and Jeshu and his disciples were called to the feast.
Yesu na wanafunzi wake walikuwa wamealikwa katika arusi.
3 And the wine failed, and his mother saith to him, to Jeshu, They have no wine.
Wakati walipoishiwa na divai, mama yake Yesu akamwambia, “Hawana divai.”
4 Jeshu saith to her, What (is it) to me and to thee, woman? Not yet hath come mine hour.
Yesu akajibu, “Mwanamke hiyo inanihusu nini mimi? Muda wangu mimi bado haujatimia.”
5 His mother saith to the servitors, Whatever he telleth you, do.
Mama yake akawambia watumishi, “Chochote atakachowambia fanyeni.”
6 Now there were six waterpots of stone set there, unto the purification of the Jihudoyee, which contained each two quarantals or three.
Basi kulikuwa na mitungi sita ya mawe pale iliyowekwa kwa ajili ya kunawa katika sikukuu za Wayahudi, kila moja lilikuwa na ujazo wa nzio mbili tatu.
7 Jeshu saith to them, Fill these water-pots with waters; and they filled them to the top.
Yesu akawambia, “Ijazeni maji mitungi ya mawe.” Wakajaza hadi juu.
8 He saith to them, Draw now, and carry to the chief of the guests. And they carried.
Kisha akawambia wale watumishi, “Chukueni kiasi sasa na mpeleke kwa muhudumu mkuu wa meza.” Wakafanya kama walivyoagizwa.
9 And when that chief of the guests had tasted those waters which were made wine, and knew not whence it was, (but the servitors knew, who had filled them with waters, ) the chief of the guests called the bridegroom,
Mhudumu mkuu aliyaonja yale maji yaliyokuwa yamebadilika na kuwa divai, ila hakujua yalikotoka (lakini watumishi waliochota maji walijua yalikotoka). Kisha akamwita bwana harusi na
10 and said to him, Every man at first the good wine produceth, and when they are satisfied, then that which is inferior; but thou hast kept the good wine until now.
kumwambia, “Kila mmoja huanza kuwahudumia watu divai nzuri na wakiishalewa huwapa divai isiyo nzuri. Lakini wewe umeitunza divai nzuri hadi sasa”
11 This is the first sign that Jeshu wrought in Kotna of Galila, and manifested his glory; and his disciples believed in him.
Muujiza huu wa Kana ya Galilaya, ulikuwa ndio mwanzo wa ishara za miujiza aliyoifanya Yesu, akifunua utukufu wake, hivyo wanafunzi wake wakamwamini.
12 AFTER this he went to Kapher-nachum, he and his mother and his brethren and his disciples. And they were there a few days.
Baada ya hii, Yesu, mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake walienda katika mji wa Kapernaum na wakaa huko kwa siku chache.
13 And the petscha of the Jihudoyee was nigh, and Jeshu went up to Urishlem.
Basi Pasaka ya Wayahudi ilikuwa imekaribia, hivyo Yesu akaenda Yerusalemu.
14 And he found in the temple those who sold oxen and sheep and doves, and the money-changers sitting.
Akawakuta wauzaji wa ng'ombe, kondoo, na njiwa ndani ya Hekalu. Pia na wabadilisha fedha walikuwa wameketi ndani ya Hekalu.
15 And he made him a scourge of cord, and drove them all from the temple, and the sheep and the oxen and the money-changers; and he shed their money, and their tables he overturned.
Yesu akatengeneza mjeledi wenye vifundo, akawatoa wote walikuwemo katika hekalu, ikijumuisha ng'ombe na kondoo. Akamwaga fedha za wabadili fedha na kuzipindua meza zao.
16 And to those who sold doves he said, Take these hence; make not the house of my Father a house of merchandise.
Kwa wauzaji wa njiwa akawambia, “Toeni vitu hivi mbali na mahali hapa, acheni kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa mahali pa soko.”
17 And his disciples remembered that it was written, The zeal of thy house hath devoured me.
Wanafunzi wake wakakumbuka kuwa ilikuwa imeandikwa, “Wivu wa nyumba yako utanila.”
18 The Jihudoyee answered and said to him, What sign showest thou to us, as these things thou doest?
Wakuu wa Kiyahudi wakajibu, wakamwambia, Ni ishara ipi utakayoionyesha kwa sababu unayafanya mambo haya?”
19 Jeshu answered, Destroy this temple, and in three days I will raise it.
Yesu akawajibu, libomoeni Hekalu hili nami nitalijenga baada ya siku tatu.”
20 The Jihudoyee say to him, Forty-and six years was this temple being built, and wilt thou in three days raise it?
Kisha wakuu wa Wayahudi wakasema, “Iligharimu miaka arobaini na sita kujenga hekalu hili nawe unasema utalijenga kwa siku tatu?”
21 But he spake of the temple of his body.
Ingawa, yeye aliongea hekalu akimaanisha mwili wake.
22 But when he was risen from the house of the dead, his disciples remembered that this he had said; and they believed the scriptures, and the word which Jeshu had spoken.
Hivyo baadaye baada ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu, wanafunzi wake wakakumbuka kuwa alisema hivyo, wakaamini maandiko na kauli hii ambayo Yesu alikuwa amekwisha kuisema.
23 WHILE Jeshu was in Jerusalem at the petscha, at the feast, Many believed in him who saw the signs which he wrought.
Basi alipokuwa Yerusalemu wakati wa Pasaka, wakati wa sikukuu watu wengi waliamini jina lake, walipoona ishara ya miujiza aliyoifanya.
24 But he, Jeshu, did not confide himself to them, because he knew every man,
Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wanadamu wote.
25 and needed not that any should testify to him concerning any man, because he knew what is in man.
Hakuhitaji mtu yeyote kumwambia kuhusu walivyo wanadamu kwa sababu alijua kilichokuwamo ndani yao.

< John 2 >