< Acts 5 >
1 AND a certain man whose name was Hanania, with his wife whose name was Shaphira, sold a field,
Hivyo, mtu mmoja aliyeitwa Anania, na Safira mkewe, waliuza sehemu ya mali,
2 and took from its value and concealed, while his wife consented, and brought of it silver and laid before the feet of the apostles.
na akaficha sehemu ya fedha waliyouza (mke wake pia alilijua hili), na akaleta sehemu iliyobakia na kuiweka kwenye miguu ya mitume.
3 And Shemun said to him, Hanania, how hath Satana thus filled thine heart that thou shouldest lie to the Spirit of Holiness, and conceal from the silver of the price of the field?
Lakini Petro akasema, “Anania, kwa nini shetani ameujaza moyo wako kusema uongo kwa Roho Mtakatifu na kuficha sehemu ya mali ya shamba?
4 Was it not thine own until it should be sold? and when it was sold thou hadst yet power over the price of it. Why hast thou laid up in thy heart to do this thing? Thou hast not lied unto men, but unto Aloha!
Wakati lilipokuwa halijauzwa, halikuwa ni mali yako? Na baada ya kuuzwa, halikuwa chini ya uamuzi wako? Ilikuwaje uwaze jambo hili moyoni mwako? Hujawadanganya wanadamu, bali umemdanganya Mungu.”
5 And when Hanania heard these words he fell and died. And there was great fear upon all those who heard.
Katika kusikia maneno haya, Anania alidondoka chini na akakata roho. Na hofu kubwa iliwajia wote waliolisikia hili.
6 And they who were young men among them arose and composed him, carried him forth and buried him.
Vijana wakaja mbele na kumtia katika sanda, na kumpeleka nje na kumzika.
7 And after there had been three hours, his wife also entered, not knowing what had been done.
Baada ya masaa matatu hivi, mke wake aliingia ndani, asijue ni nini kilichokuwa kimetokea.
8 Shemun said to her, Tell me if for these prices you sold the field? But she said, Yes: for these prices.
Petro akamwambia, “Niambie, kama mliuza shamba kwa thamani hiyo.” Akasema, “Ndiyo, kwa thamani hiyo.”
9 Shemun said to her, Why have you agreed to tempt the Spirit of the Lord? Lo, the feet of the buriers of thy husband are at the door, and they will carry thee out!
Kisha Petro akamwambia, “Inakuwaje kwamba mmepatana kwa pamoja kumjaribu Roho wa Bwana? Angalia, miguu ya wale waliomzika mme wako iko mlangoni, na watakubeba na kukupeleka nje.”
10 And at once she fell before their feet and died. And those young men entered and found her dead, and they laid her out, and brought her forth and buried her by the side of her husband.
Ghafla akadondoka miguuni pa Petro, akakata roho, na wale vijana wakaja ndani wakamkuta ameshakufa. Wakambeba kumpeleka nje, na kumzika karibu na mmewe.
11 And there was great fear upon all the church and in all them who heard.
Hofu kubwa ikaja juu ya kanisa zima, na juu ya wote walioyasikia mambo haya.
12 AND by the hand of the apostles were done great signs and mighty works among the people: and all gathered together at the portico of Shelemun.
Ishara nyingi na maajabu vilikuwa vinatokea miongoni mwa watu kupitia mikono ya mitume. Walikuwa pamoja katika ukumbi wa Sulemani.
13 And from the others not a man dared to come near them; but the people magnified them.
Lakini, hakuna mtu mwingine tofauti aliyekuwa na ujasiri wa kuambatana nao; hata hivyo, walipewa heshima ya juu na watu.
14 And the more were they who believed added to the Lord, an assemblage of men and of women;
Na pia, waamini wengi walikuwa wakiongezeka kwa Bwana, idadi kubwa ya wanaume na wanawake,
15 so that into the streets they brought forth the diseased lying on beds, that, when Shemun should come, even his shadow might overshadow them.
kiasi kwamba hata waliwabeba wagonjwa mitaani, na kuwalaza vitandani na kwenye makochi, ili kwamba Petro akiwa anapita, kivuli chake kiweze kushuka juu yao.
16 But there came many to them from the other cities round about Urishlem, bringing the diseased and those who had unclean spirits: and they were healed, all of them.
Hapo pia, idadi kubwa ya watu walikuja kutoka miji iliyozunguka Yerusalem, wakiwaleta wagonjwa na wote waliopagawa na roho wachafu, na wote waliponywa.
17 And the chief of the priests, and they who were with him, who were of the doctrine of the Zadukoyee, were filled with envy,
Lakini kuhani mkuu aliinuka, na wote waliokuwa pamoja naye (ambao ni wa dhehebu la masadukayo); na walijawa na wivu
18 and they laid hands on the apostles, and apprehended and bound them in the house of the bound.
wakanyosha mikono yao kuwakamata mitume na kuwaweka ndani ya gereza la jumla.
19 Then in the night the angel of the Lord opened the gate of the house of the bound, and brought them forth, and said to them,
Na wakati wa usiku malaika wa Bwana akaifungua milango ya gereza na kuwaongoza nje na kusema,
20 Go stand in the temple and speak to the people all these words of salvation.
“Nendeni, mkasimame hekaluni na kuwaambia watu maneno yote ya Uzima huu.”
21 And they went forth in the time of morning, and entered the temple, and taught. But the chief of the priests and they who were with him arose (and) convoked their associates and the elders of Israel, and sent to the house of the bound to bring the apostles.
Waliposikia hili, waliingia hekaluni wakati wa kupambazuka na kufundisha. Lakini, kuhani mkuu alikuja na wote waliokuwa naye, na kuitisha baraza lote kwa pamoja, na wazee wote wa watu wa Israeli, na kuwatuma gerezani ili kuwaleta mitume.
22 And when they who were sent from them went, they found them not (in) the house of the bound; and they returned, and came,
Lakini watumishi waliokwenda, hawakuwakuta gerezani, walirudi na kutoa taarifa,
23 and said, We found the house of the bound shut carefully, and the keepers standing at the gates: and we opened, but no man found we there.
“Tumekuta gereza limefungwa vizuri salama, na walinzi wamesimama langoni, lakini tulipokuwa tukifungua, hatukuona mtu ndani.”
24 And when the chief priests and rulers of the temple heard these words, they were astounded by them, and reasoned, what this was.
Sasa wakati jemedari wa hekalu na makuhani wakuu waliposikia maneno haya, waliingiwa na shaka kubwa kwa ajili yao wakiwaza litakuwaje jambo hili.
25 And one came and declared to them, Those men whom you shut up in the house of the bound, behold, they are standing in the temple and teaching the people.
Kisha mmoja akaja na kuwaambia, “Watu mliowaweka gerezani wamesimama hekaluni na wanafundisha watu.”
26 Then went the rulers with the satellites to bring them, not with violence, for they feared lest the people should stone them;
Hivyo jemedari alienda pamoja na watumishi, na wakawaleta, lakini bila ya kufanya vurugu, kwa sababu waliwaogopa watu wangeweza kuwapiga kwa mawe.
27 and when they had brought them they made them stand before all the assembly, and the chief of the priests began to say to them,
Walipokwisha kuwaleta, waliwaweka mbele ya baraza. Kuhani mkuu aliwahoji
28 Did we not commanding command you, that you should teach no man in this name? But, behold, you have filled Urishlem with your doctrine, and you will to bring upon us the blood of this man!
akisema, “Tuliwaamuru msifundishe kwa jina hili, na bado mmeijaza Yerusalemu kwa fundisho lenu, na kutamani kuleta damu ya mtu huyu juu yetu.”
29 SHEMUN answered with the apostles and said to them, Aloha must we obey rather than men.
Lakini Petro na mitume wakajibu, “Lazima tumtii Mungu kuliko watu.
30 The God of our fathers hath raised up Jeshu whom you killed and hanged on the tree.
Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu, mliyemuua, kwa kumtundika juu ya mti.
31 Him hath Aloha constituted a Prince and a Saviour, and elevated him at his right hand, to give repentance and remission of sins unto Israel.
Mungu alimtukuza katika mkono wake wa kuume, na kumfanya kuwa Mkuu na mwokozi, kutoa toba kwa Israeli, na msamaha wa dhambi.
32 And we are witnesses of these words, and the Spirit of Holiness himself, whom Aloha hath given to them who believe in him.
Sisi ni mashahidi wa mambo haya, na Roho Mtakatifu, ambaye Mungu amemtoa kwa wale wanaomtii.”
33 And when they heard these words they were transported with rage, and were mindful to kill them.
Wajumbe wa baraza waliposikia hivi, walishikwa na hasira wakataka kuwaua mitume.
34 And one of the Pharishee arose, whose name was Gamaliel, a doctor of the law, and honoured by all the people, and commanded to take the apostles without a little time.
Lakini pharisayo aliyeitwa Gamalieli, mwalimu wa sheria, aliyeheshimiwa na watu wote, alisimama na kuwaamuru mitume wachukuliwe nje kwa muda mfupi.
35 And he said to them, Men, sons of Israel, beware of yourselves, and consider what it behoves you to do concerning these men.
Kisha akawaambia, “Wanaume wa Israeli, iweni makini sana na kile mnachopendekeza kuwafanyia watu hawa.
36 For before this time arose Thuda, and said of himself that he was something great, and there went after him four hundred men: and he was slain, and they who went after him were scattered and became as nothing.
Kwa sababu, zamani zilizopita, Theuda aliinuka na kujidai kuwa mtu mkuu, na idadi ya watu, wapata mia nne walimfuata. Aliuawa, na wote waliokuwa wanamtii walitawanyika na kupotea.
37 Afterward arose Jihuda Galiloya in the days when men were enregistered for the head-silver, and tempted much people after him; and he died, and all they who went after him were scattered.
Baada ya mtu huyu, Yuda mgalilaya, aliinuka siku zile za kuandikwa sensa, akavuta watu wengi nyuma yake. Naye pia alipotea na wote waliokuwa wakimtii walitawanyika.
38 And now I say to you, keep aloof from these men, and dismiss them; for if from men be this imagination and this work, it will be dissolved and end;
Sasa nawaambia, jiepusheni na watu hawa na muwaache wenyewe, kwa sababu, kama mpango huu au kazi hii ni ya watu itatupwa.
39 but if it be from Aloha, there is no power in your hands to bring it to an end: lest you should be found to have arisen against Aloha.
Lakini kama ni ya Mungu, hamtaweza kuwazuia; mnaweza mkajikuta hata mnashindana na Mungu.” Hivyo, walishawishika na maneno yake.
40 And they were persuaded by him, and called the apostles, and scourged them, and commanded them that they should not teach in the name of Jeshu, and loosed them.
Kisha, waliwaita mitume ndani na kuwachapa na kuwaamuru wasinene kwa jina la Yesu, na wakawaacha waende zao.
41 And they went out from before them, rejoicing to be worthy for the sake of the Name to be ill treated.
Waliondoka mbele ya baraza wakifurahi kwa sababu wamehesabiwa kuwa wamestahili kuteseka na kutoheshimiwa kwa ajili ya Jina hilo.
42 And they ceased not daily to teach in the temple, and in the house, and to preach concerning our Lord Jeshu Meshiha.
Kwa hiyo, kila siku, ndani ya hekalu na kutoka nyumba hadi nyumba waliendelea kufundisha na kuhubiri Yesu kuwa ni Masihi.