< 2 Peter 2 >

1 BUT there were false prophets in the world, as also among you there will be false teachers, they who introduce heresies of destruction, and, the Lord who bought them denying, bring upon themselves swift destruction.
Lakini pia waliinuka manabii wa uongo miongoni mwa watu, kama vile watakavyokuwako walimu wa uongo miongoni mwenu. Wataingiza mafundisho yasiyopatana na kweli kwa siri, hata kumkana Bwana wa pekee aliyewanunua, na hivyo kujiletea wenyewe maangamizi ya haraka.
2 And many will go after their wickedness; they, on account of whom the way of truth will be blasphemed.
Hata hivyo, wengi watafuata njia zao za ufisadi, na kwa ajili yao njia ya kweli itatukanwa.
3 And with fraudulency of deceptive words will they make merchandise of you; they, whose judgment (denounced) before tarrieth not, and whose destruction doth not sleep.
Nao katika tamaa zao mbaya, walimu hawa watajipatia faida kwenu kwa hadithi walizotunga wenyewe. Lakini hukumu imekwisha kutangazwa dhidi yao tangu zamani, wala uangamivu wao haujalala usingizi.
4 For if Aloha upon the angels who sinned was not lenient, but in chains of darkness shut them in the deeps, and delivered them to be kept to the judgment of pain; (Tartaroō g5020)
Kwa maana, kama Mungu hakuwasamehe malaika walipotenda dhambi, bali aliwatupa kuzimu katika vifungo vya giza wakae humo mpaka ije hukumu; (Tartaroō g5020)
5 and on the former world was not lenient, but Nuch, who was the eighth preacher of righteousness, he preserved, when the deluge came upon the world of the wicked;
kama hakuusamehe ulimwengu wa kale alipoleta gharika juu ya watu wale wasiomcha Mungu, bali akamhifadhi Noa, mhubiri wa haki, pamoja na watu wengine saba;
6 the cities of Sadum and of Omuro he burned, and with overthrow condemned them, while an example to the wicked who should be he set them;
kama aliihukumu miji ya Sodoma na Gomora kwa kuiteketeza kwa moto ikawa majivu, na kuifanya kuwa kielelezo kwa yale yatakayowapata wale wasiomcha Mungu;
7 also Lut the righteous, who was bruised with the impure conversation of the lawless, he delivered;
na kama alimwokoa Loti, mtu mwenye haki, ambaye alihuzunishwa na maisha machafu ya watu wapotovu
8 -for in sight and in hearing, while (that) just (man) dwelt among them, from day to day, his righteous soul by their lawless works was tortured; -
(kwa sababu yale matendo mapotovu aliyoyaona na kuyasikia huyo mtu mwenye haki alipoishi miongoni mwao yalimhuzunisha siku baada ya siku):
9 the Lord knoweth how to deliver from affliction them who fear him, but the evil unto the day of judgment to be tormented will he reserve.
ikiwa hivyo ndivyo, basi Bwana anajua jinsi ya kuwaokoa wamchao Mungu kutoka majaribu, na kuwaweka waasi katika adhabu hadi siku ya hukumu.
10 But most those who after the flesh follow the concupiscence of impurity, and of authority are contemptuous; daring and arrogant, (and) who by greatness are not moved while they blaspheme:
Hii ni hakika hasa kwa wale wanaofuata tamaa mbaya za mwili na kudharau mamlaka. Kwa ushupavu na kwa kiburi, watu hawa hawaogopi kunena mabaya dhidi ya viumbe vya mbinguni.
11 whereas angels, who in power and strength are (so much) greater than they, bring not against them a judgment of blasphemy.
Lakini hata malaika, ingawa wana nguvu na uwezo zaidi, hawaleti mashtaka mabaya dhidi ya viumbe kama hao mbele za Bwana.
12 But these, as the dumb animals, by nature (ordained) to the knife and to destruction, blaspheming what they know not, in their own destruction will be destroyed;
Lakini watu hawa hukufuru katika mambo wasiyoyafahamu. Wao ni kama wanyama wasio na akili, viumbe wanaotawaliwa na hisia za mwili, waliozaliwa ili wakamatwe na kuchinjwa. Hawa nao kama wanyama wataangamizwa pia.
13 while they in whom is iniquity the wages of iniquity shall receive. They repute as pleasure the luxury which is in the day. Blemishes (are they), full of spots, who delighting in their refreshments are luxurious:
Watalipwa madhara kwa ajili ya madhara waliyowatendea wengine. Huhesabu kuwa ni fahari kufanya karamu za ulevi na ulafi mchana peupe. Wao ni mawaa na dosari, wakijifurahisha katika anasa zao wanaposhiriki katika karamu zenu.
14 having eyes full of adultery, and sins which cease not, alluring souls that are not established. An heart have they which is disciplined in covetousness; sons of malediction,
Wakiwa na macho yaliyojaa uzinzi, kamwe hawaachi kutenda dhambi. Huwashawishi wale wasio imara. Wao ni hodari kwa kutamani; ni wana wa laana!
15 who, forsaking the straight way, have erred, and gone in the way of Belam bar Beur, who the wages of iniquity loved. But he had reproof of his transgression;
Wameiacha njia iliyonyooka, wakapotoka na kuifuata njia ya Balaamu mwana wa Beori aliyependa mshahara wa uovu.
16 (for) the dumb ass which spake with the voice of man rebuked the madness of the prophet.
Lakini kwa ajili ya uovu wake, alikemewa na punda, mnyama asiyejua kusema, akaongea akitumia sauti ya mwanadamu na kuzuia wazimu wa huyo nabii.
17 These are wells without water, clouds driven from above, unto whom the blackness of darkness is reserved.
Watu hawa ni chemchemi zisizo na maji, na ukungu upeperushwao na tufani. Giza nene limewekwa tayari kwa ajili yao.
18 For while they speak scoffing words of vanity, they allure with impure desires of the flesh those who almost escaped from them who have their conversation in error.
Kwa maana wao hunena maneno makuu mno ya kiburi cha bure, na kwa kuvutia tamaa mbaya za asili ya mwili, huwashawishi watu ambao ndipo tu wamejiondoa miongoni mwa wale wanaoishi katika ufisadi.
19 And liberty to them they promise, while they (themselves) are the servants of corruption; for the thing by which a man is overcome, to that he is subject.
Huwaahidi uhuru hao waliowanasa, wakati wao wenyewe ni watumwa wa ufisadi: kwa maana mtu ni mtumwa wa kitu chochote kinachomtawala.
20 For if they have escaped from the pollutions of the world through the knowledge of our Lord and Saviour Jeshu Meshiha, with those very things entangled they are again over-come, their end becomes worse than the beginning.
Kama wameukimbia upotovu wa dunia kwa kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo, kisha wakanaswa tena humo na kushindwa, hali yao ya mwisho ni mbaya zaidi kuliko ile ya kwanza.
21 For it had been more tolerable for them not to have known the way of righteousness, than, when they knew, to turn backward from the holy commandment delivered to them.
Ingelikuwa afadhali kwao kama wasingeliijua kamwe njia ya haki, kuliko kuijua kisha wakaiacha ile amri takatifu waliyokabidhiwa.
22 But it hath happened to them according to the true proverb, that The dog hath turned unto his vomit; the sow which had washed into the wallow of the mire.
Imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli isemayo: “Mbwa huyarudia matapiko yake mwenyewe,” tena, “Nguruwe aliyeoshwa hurudi kugaagaa matopeni.”

< 2 Peter 2 >