< 2 Corinthians 1 >
1 PAULOS, apostle of Jeshu Meshiha, by the will of Aloha; and Timotheos a brother: to the church of Aloha which is in Kurinthos, and to all the saints who are in all Akaia.
Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu, kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, na kwa waumini wote walioko katika mkoa wote wa Akaya.
2 Grace be with you and peace, from Aloha our Father, and from our Lord Jeshu Meshiha.
Neema na iwe kwenu na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
3 Blessed be Aloha, the Father of our Lord Jeshu Meshiha, the Father of mercies, and the God of all consolation, who consoleth us in all our afflictions,
Na asifiwe Mungu na Baba wa Bwana Yesu Kristo. Yeye ni Baba wa rehema na Mungu wa faraja yote.
4 that we may be able to console those who are in all afflictions by that consolation by which we are consoled of Aloha.
Mungu hutufariji sisi katika mateso yetu yote, ili kwamba tuweze kuwafariji wale walio katika mateso. Tunawafariji wengine kwa faraja ileile ambayo Mungu alitumia kutufariji sisi.
5 For as the sufferings of the Meshiha abound in us, so, through the Meshiha, our consolation aboundeth also.
Kwa kuwa kama vile mateso ya Kristo huongezeka kwa ajili yetu, vile vile faraja yetu huongezeka kupitia Kristo.
6 But if we are afflicted, it is for your consolation and for your salvation that we be afflicted: and if we are consoled, it is that you may be consoled, that there may be in you perseverance to endure those sufferings which we also suffer.
Lakini kama tunataabishwa, ni kwa ajili ya faraja yenu na wokovu wenu. Na kama tunafarijiwa, ni kwa ajili ya faraja yenu. Faraja yenu inafanya kazi kikamilifu mnaposhiriki mateso kwa uvumilivu kama sisi pia tunavyoteseka.
7 And our hope concerning you is steadfast: for we know that if you participate in the sufferings, you also participate in the consolation.
Na ujasiri wetu juu yenu ni thabiti. Tunajua kwamba kama vile ambavyo mnashiriki mateso, vile vile mnashiriki faraja.
8 FOR I would have you to know, my brethren, of the affliction that befell us in Asia: for we were greatly pressed beyond our strength, until our life was nigh to be dissolved,
Kwa kuwa hatutaki ninyi muwe wajinga, ndugu, kuhusu matatizo tuliyokuwa nayo huko Asia. Tulionewa zaidi ya vile tuwezavyo kubeba, kana kwamba hatukuwa hata na tumaini la kuishi tena.
9 and because of these we had concluded (for) death; that we should not have hope in ourselves, but in Aloha, who raiseth the dead:
Kweli, tulikuwa na hukumu ya kifo juu yetu. Lakini hiyo ilikuwa ni kutufanya sisi tusiweke tumaini juu yetu wenyewe, badala yake tuweke tumaini katika Mungu, afufuaye wafu.
10 who from deaths of violence delivered us, and who will again, we trust, deliver us,
Alituokoa sisi kutoka hayo maafa ya mauti, na atatuokoa tena. Tumeweka ujasiri wetu katika yeye ya kwamba atatuokoa tena.
11 through the help of your prayers for us; that his gift towards us may be a benefit effected for many, and many may praise him on our behalf.
Atafanya hivi kama vile ninyi pia mtusaidiavyo kwa maombi yenu. Hivyo wengi watatoa shukurani kwa niaba yetu kwa ajili ya upendeleo wa neema tuliyopewa sisi kupitia maombi ya wengi.
12 For our glorying is this, the testimony of our conscience, that in simplicity and purity, and by the grace of Aloha, we are conversant in the world; and not with the wisdom of the flesh, and especially with you yourselves.
Tunajivunia hili: ushuhuda wa dhamiri yetu. Kwa kuwa ni katika nia safi na usafi wa Mungu kwamba tulienenda wenyewe katika dunia. Tumefanya hivi hasa na ninyi, na sio katika hekima ya ulimwengu, lakini badala yake ni katika neema ya Mungu.
13 For we write no other (things) to you than those which you know and acknowledge, and which I am confident you will acknowledge unto the end:
Hatuwaandikii chochote ambacho hamwezi kukisoma au kuelewa. Ninaujasiri
14 even as you have in part acknowledged that we are your glorying, as you also are ours in the day of our Lord Jeshu Meshiha.
kwamba kwa sehemu mumekwisha kutuelewa. Na ninaujasiri kwamba katika siku ya Bwana Yesu tutakuwa sababu yenu kwa ajili ya kiburi chenu, kama vile mtakavyokuwa kwetu.
15 And in this confidence I have willed from the first to come to you, that doubly you may receive benefit,
Kwa sababu nilikuwa na ujasiri kuhusu hili, nilitaka kuja kwenu kwanza, ili kwamba muweze kupokea faida ya kutembelewa mara mbili.
16 and that I may pass by you to Makedunia, and again from Makedunia I may come to you, and you may lead me forth unto Jihud.
Nilikuwa napanga kuwatembelea wakati nikielekea Makedonia. Tena nilitaka kuwatembelea tena wakati nikirudi kutoka Makedonia, na kisha ninyi kunituma mimi wakati nikielekea Uyahudi.
17 This then that I have purposed, have I purposed boastingly? or are they things of the flesh that I purpose, that I should have in them Yes, yes, or No, no?
Nilipokuwa nafikiria namna hii, je, nilikuwa nasitasita? Je ninapanga mambo kulingana na viwango vya kibinadamu, ili kwamba niseme “Ndiyo, ndiyo” na “Hapana, hapana” kwa wakati mmoja?
18 Faithful is Aloha that our word with you was not Yes and No.
Lakini kama vile Mungu alivyo mwaminifu, hatusemi vyote “Ndiyo” na “Hapana.”
19 For the Son of Aloha, Jeshu Meshiha, who by us hath been preached unto you, by me and by Sylvanas and by Timotheos, was not Yes and No, but it was Yes in him.
Kwa kuwa mwana wa Mungu, Yesu Kristo, ambaye Silvano, Timotheo na mimi tulimtangaza miongoni mwenu, siyo “Ndiyo” na “Hapana.” Badala yake, yeye wakati wote ni “Ndiyo.”
20 For all the promises of Aloha in him, in the Meshiha, are Yes; for which by him we give Amen to the glory of Aloha.
Kwa kuwa ahadi zote za Mungu ni “Ndiyo” katika yeye. Hivyo pia kupitia yeye tunasema “Amina” kwa utukufu wa Mungu.
21 But Aloha himself confirmeth us with you in the Meshiha, who himself hath anointed us,
Sasa ni Mungu ambaye hututhibitisha sisi pamoja nanyi katika Kristo, na alitutuma sisi.
22 and hath sealed us, and given us the earnest-pledge of his Spirit in our hearts.
Aliweka muhuri juu yetu na alitupa Roho katika mioyo yetu kama dhamana ya kile ambacho angetupatia baadaye.
23 BUT I testify to Aloha on my soul that because I am sparing of you, I have not come to Kurinthos.
Badala yake, namsihi Mungu kunishuhudia mimi kwamba sababu iliyonifanya nisije Korintho ni kwamba nisiwalemee ninyi.
24 Not because we are lords of your faith, but are helpers of your joy; for by faith you stand.
Hii sio kwa sababu tunajaribu kudhibiti jinsi imani yenu inavyotakiwa kuwa. Badala yake, tunafanya pamoja nanyi kwa ajili ya furaha yenu, kama mnavyosimama katika imani yenu.