< 2 Corinthians 11 >

1 BUT I could desire that you could tolerate me a little that I may speak foolishly.
Nahisi kwamba mngevumiliana na mimi katika baadhi ya upumbavu. Lakini kwa kweli mnavumiliana na mimi.
2 Nevertheless tolerate me, for I am zealous towards you with the zeal of Aloha; for I have betrothed you to one man, a pure virgin, whom I would bring unto the Meshiha.
Kwa kuwa ni mwenye wivu kuhusu ninyi. Nina wivu wa Mungu kwa ajili yenu, tangu nilipowaahidi ninyi kwenye ndoa ya mume mmoja. Niliahidi kuwaleta ninyi kwa Kristo kama bikra safi.
3 But I fear lest, as the serpent deceived 'Hava by his guile, so your minds may be corrupted from the simplicity that is toward the Meshiha.
Lakini ninaogopa kwamba kwa namna fulani, kama nyoka alivyomdanganya Eva kwa hila yake, mawazo yenu yanaweza kupotoshwa mbali kutoka kwenye ibada halisi na safi kwa Kristo.
4 For if he who hath come to you shall preach to you another Jeshu, whom we have not preached, or you receive another Spirit which you have not received or another gospel which you have not accepted, you would have been well persuaded.
Kwa kuwa kwa mfano kwamba mtu fulani akaja na kutangaza Yesu mwingine tofauti na yule tuliyewahubiri. Au kwa mfano kwamba mkapokea roho mwingine tofauti na yule mliyempokea. Au kwa mfano kwamba mkapokea injili nyingine tofauti na ile mliyoipokea. Mkavumilia mambo haya vema inatosha!
5 For I consider that I am nothing inferior to those apostles who are most excellent.
Kwa kuwa nadhani kwamba mimi si miongoni mwa walio duni kwa hao wanaoitwa mitume-bora.
6 For if I am rude in my speech, I yet am not in my knowledge; but in every thing we are manifest among you.
Lakini hata kama mimi sijafundishwa katika kutoa hotuba, siko hivyo katika maarifa. Kwa kila namna na katika mambo yote tumelifanya hili kujulikana kwenu.
7 Or, offending have I offended in humbling myself that you may be exalted, and have gratuitously preached to you the gospel of Aloha?
Je, nilifanya dhambi kwa kujinyenyekeza mwenyewe ili ninyi muweze kuinuliwa? Kwa kuwa nilihubiri kwa uhuru injili ya Mungu kwenu.
8 And other churches have I despoiled, receiving of them expenses, for your service.
Nilinyang'anya makanisa mengine kwa kupokea msaada kutoka kwao ili kwamba ningeweza kuwahudumia ninyi.
9 And being come among you, I burdened no man of you; for my want the brethren who came from Makedunia supplied: and in every thing have I kept myself, and will keep, that I may not be burdensome to you.
Wakati nilipokuwa nanyi na nilikuwa katika uhitaji, sikumlemea yeyote. Kwa kuwa mahitaji yangu yalitoshelezwa na ndugu waliokuja kutoka Makedonia. Katika kila kitu nimejizuia mwenyewe kutokuwa mzigo kwenu, na nitaendelea kufanya hivyo.
10 The truth of the Meshiha is in me, that this boasting shall not be abolished respecting me in the regions of Akaia.
Kama kweli ya Kristo ilivyo ndani yangu, huku kujisifu kwangu, hakutanyamazishwa katika sehemu za Akaya.
11 Why? because I love you not? Aloha himself knoweth!
Kwa nini? Kwa sababu siwapendi? Mungu anajua nawapenda.
12 But I do this, and also will do it, to cut off the occasion of them who seek an occasion, that in the thing in which they boast they may be found as we are.
Lakini kile ninachokifanya, nitakifanya pia. Nitakifanya ili kwamba niweze kuzuia nafasi ya wale wanaotamani nafasi ya kuwa kama tulivyo katika kile kile wanachojivunia.
13 For these are apostles of falsehood and workers of deceits, assimilating themselves to the apostles of the Meshiha.
Kwa kuwa watu wale ni mitume wa uongo na watendakazi wadanganyifu. Wanajigeuza wenyewe kama mitume wa Kristo.
14 Nor in this may we wonder, if Satana himself be transformed into an angel of light.
Na hii haishangazi, kwa kuwa hata Shetani hujigeuza mwenyewe kama malaika wa nuru.
15 Nor is it a great thing if his ministers also are transformed into ministers of righteousness; -whose end will be according to their works.
Hii haina mshangao mkubwa kama watumishi wake pia kujigeuza wenyewe kama watumishi wa haki. Hatma yao itakuwa kama matendo yao yastahilivyo.
16 BUT I say again, Let no man think of me as a fool; or if otherwise, let him receive me as a fool, that I also may boast a little.
Nasema tena: Basi na asiwepo mtu yeyote anayefikiri mimi ni mpumbavu. Lakini kama mkifanya, nipokeeni mimi kama mpumbavu ili niweze kujisifu kidogo.
17 The thing which I (now) speak, I do not speak in our Lord, but as in foolishness in this place of boasting.
Kile ninachosema kuhusu huku kujiamini kwa kujivuna hakuhukumiwi na Bwana, lakini nazungumza kama mpumbavu.
18 Because many boast in the flesh, I also will boast.
Kwa vile watu wengi hujivuna kwa jinsi ya mwili, nitajivuna pia.
19 For you are content to listen to the feebleminded, you yourselves being wise.
Kwa kuwa mlichukuliana kwa furaha na wapumbavu, ninyi wenyewe mna busara!
20 For you are ruled by one who subjugates you, and by one who devours you, and by one who takes away from you, and by one who exalts himself over you, and by one who smites you on your faces!
Kwa kuwa mnachukuliana na mtu kama akikutia utumwani, kama husababisha mgawanyiko kati yenu, kama akiwatumia ninyi kwa faida yake, kama akijiweka juu hewani, au kama akiwapiga usoni.
21 As in abasement I speak; as though we were weak through defectiveness of mind, I speak. In whatever any man dareth, I also dare.
Nitasema kwa aibu yetu kwamba sisi tukuwa dhaifu sana kufanya hivyo. Na bado kama yeyote akijivuna— nazungumza kama mpumbavu— mimi pia nitajivuna.
22 If they are Ebroyee, so am I; if they are Isroloyee, so am I; if they are the seed of Abraham, so am I;
Je, wao ni Wayahudi? Na mimi ni hivyo. Je, wao ni Waisraeli? Na mimi ni hivyo. Je, wao ni uzao wa Abrahamu? Na mimi ni hivyo.
23 if they are ministers of the Meshiha, -I speak with defectiveness of mind, -I exceed then! In labours I exceed them, in stripes I exceed them, in chains I exceed them, in deaths many times.
Je, wao ni watumishi wa Kristo? (Nanena kama nilirukwa na akili zangu. ) Mimi ni zaidi. Nimekuwa hata katika kazi ngumu zaidi, mbali zaidi ya kuwa vifungoni, katika kupigwa kupita vipimo, katika kukabili hatari nyingi za kifo.
24 From the Jihudoyee, five times, forty (stripes) wanting one have I devoured;
Kutoka kwa Wayahudi nimepokea mara tano “mapigo arobaini kutoa moja.”
25 three times with staves have I been beaten, once was I stoned, three times have I been in shipwreck, a day and a night without a ship have I been in the sea.
Mara tatu nilipigwa kwa fimbo. Mara moja nilipigwa mawe. Mara tatu nilinusurika melini. Nimetumia usiku na mchana katika bahari wazi.
26 In journeys many, in danger of rivers, in danger of robbers, in danger from my own race, in danger from the Gentiles; I have been in danger in cities, I have been in danger in the waste, in danger by sea, in danger from false brethren;
Nimekuwa katika safari za mara kwa mara, katika hatari za mito, katika hatari za majambazi, katika hatari kutoka kwa watu wangu mwenyewe, katika hatari kutoka kwa watu wa mataifa, katika hatari ya mji, katika hatari ya jangwa, katika hatari ya bahari, katika hatari kutoka kwa ndugu waongo.
27 in labour and weariness, in much watching, in hunger and thirst, in much fasting, in cold and in nakedness;
Nimekuwa katika kazi ngumu na katika maisha magumu, katika usiku mwingi wa kutolala, katika njaa na kiu, mara nyingi katika kufunga, katika baridi na uchi.
28 besides the aboundings and the gathering which are upon me daily even my care which is for all the churches.
Mbali na kila kitu kingine, kuna msukumo wa kila siku juu yangu wa wasiwasi wangu kwa ajili ya makanisa.
29 Who is weak, and I am not weak? Who is offended, and I burn not?
Nani ni dhaifu, na mimi siyo dhaifu? Nani amesababisha mwingine kuanguka dhambini, na mimi siungui ndani?
30 If I must boast in my infirmities, I will boast.
Kama ni lazima nijivune, nitajivunia kuhusu kile kinachoonyesha udhaifu wangu.
31 Aloha, the Father of our Lord Jeshu Meshiha, the Blessed for ever and ever, knoweth that I lie not. (aiōn g165)
Mungu na Baba wa Bwana Yesu, yeye ambaye anatukuzwa milele, anajua kwamba mimi sidanganyi. (aiōn g165)
32 In Darmsuk the great force of Aretos the king kept the city of the Darmsukoyee to apprehend me.
Kule Dameski, mkuu wa mkoa chini ya mfalme Areta alikuwa akiulinda mji wa Dameski ili kunikamata.
33 And from a window in a basket they sent me from the wall, and I was delivered from his hands.
Lakini niliwekwa kikapuni, kupitia dirishani katika ukuta, na nikanusurika kutoka mikononi mwake.

< 2 Corinthians 11 >