< Psalms 53 >

1 to/for to conduct upon Mahalath Maskil to/for David to say foolish in/on/with heart his nothing God to ruin and to abhor injustice nothing to make: do good
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi. Utenzi wa Daudi. Mpumbavu anasema moyoni mwake, “Hakuna Mungu.” Wameharibika, na njia zao ni za uovu kabisa, hakuna hata mmoja atendaye mema.
2 God from heaven to look upon son: child man to/for to see: see there be prudent to seek [obj] God
Mungu anawachungulia wanadamu chini kutoka mbinguni aone kama wako wenye akili, wowote wanaomtafuta Mungu.
3 all his to turn together to corrupt nothing to make: do good nothing also one
Kila mmoja amegeukia mbali, wameharibika wote pamoja, hakuna atendaye mema. Naam, hakuna hata mmoja!
4 not to know to work evil: wickedness to eat people my to eat food: bread God not to call: call to
Je, watendao mabaya kamwe hawatajifunza: wale ambao huwala watu wangu kama watu walavyo mkate, hao ambao hawamwiti Mungu?
5 there to dread dread not to be dread for God to scatter bone to camp you be ashamed for God to reject them
Hapo waliingiwa na hofu kuu, ambapo hapakuwa cha kutetemesha. Mungu alitawanya mifupa ya wale waliokushambulia; uliwaaibisha, kwa sababu Mungu aliwadharau.
6 who? to give: if only! from Zion salvation Israel in/on/with to return: rescue God captivity people his to rejoice Jacob to rejoice Israel
Laiti wokovu wa Israeli ungalikuja kutoka Sayuni! Wakati Mungu arejeshapo wafungwa wa watu wake, Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi!

< Psalms 53 >