< Psalms 31 >
1 to/for to conduct melody to/for David in/on/with you LORD to seek refuge not be ashamed to/for forever: enduring in/on/with righteousness your to escape me
Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. In wewe, Yahwe, nakimbilia usalama; usiniache niaibishwe. Katika haki yako uniokoe.
2 to stretch to(wards) me ear your haste to rescue me to be to/for me to/for rock security to/for house: home fortress to/for to save me
Unisikie; uniokoe haraka; uwe mwamba wangu wa usalama, ngome ya kuniokoa.
3 for crag my and fortress my you(m. s.) and because name your to lead me and to guide me
Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu; kwa hiyo kwa ajili ya jina lako, uniongoze na unielekeze.
4 to come out: send me from net this to hide to/for me for you(m. s.) security my
Unitoe katika mtego ambao wameuficha kwa ajili yangu, kwa kuwa wewe ni usalama wangu.
5 in/on/with hand your to reckon: overseer spirit my to ransom [obj] me LORD God truth: faithful
Mikononi mwako naikabidhi roho yangu; nawe utaniokoa, Yahwe, mwenye kuaminika.
6 to hate [the] to keep: look at vanity vanity: vain and I to(wards) LORD to trust
Ninawachukia wale wanaotumikia miungu isiyo na maana, bali ninaamini katika Yahwe.
7 to rejoice and to rejoice in/on/with kindness your which to see: see [obj] affliction my to know in/on/with distress soul my
Nitafurahi na kushangilia katika uaminifu wa agano lako, kwa kuwa uliyaona mateso yangu; wewe uliijua dhiki ya moyo wangu.
8 and not to shut me in/on/with hand: power enemy to stand: stand in/on/with broad foot my
Wewe haujaniweka kwenye mkono wa maadui zangu. Nawe umeiweka miguu yangu mahali pa wazi papana.
9 be gracious me LORD for to constrain to/for me to waste in/on/with vexation eye my soul my and belly: body my
Uniurumie, Yahwe, kwa maana niko katika dhiki; macho yangu yanafifia kwa huzuni pamoja na moyo wangu na mwili wangu.
10 for to end: expend in/on/with sorrow life my and year my in/on/with sighing to stumble in/on/with iniquity: crime my strength my and bone my to waste
Kwa kuwa maisha yangu yamechoshwa kwa huzuni na miaka yangu kwa kuugua kwangu. Nimekuwa dhaifu kwa sababu ya dhambi zangu, na mifupa yangu inachakaa.
11 from all to vex me to be reproach and to/for neighboring my much and dread to/for to know my to see: see me in/on/with outside to wander from me
Kwa sababu ya maadui zangu wote, watu wananibeza; majirani zangu wanaishangaa hali yangu, na wale wanao nifahamu wanashtuka. Wale wanionao mitaani hunikimbia.
12 to forget like/as to die from heart to be like/as article/utensil to perish
Nimesahaulika kama mtu aliye kufa ambaye hakuna mtu anaye mfikiria. Niko kama chungu kilicho pasuka.
13 for to hear: hear slander many terror from around: side in/on/with to found they unitedness upon me to/for to take: take soul: life my to plan
Kwa maana nimesikia minong'ono ya wengi, habari za kutisha kutoka pande zote kwa pamoja wamepanga njama kinyume na mimi. Wao wanapanga njama ya kuniua.
14 and I upon you to trust LORD to say God my you(m. s.)
Bali mimi ninakuamini wewe, Yahwe; Ninasema, “Wewe ni Mungu wangu.”
15 in/on/with hand your time my to rescue me from hand enemy my and from to pursue me
Hatima yangu iko mikononi mwako. Uniokoe mikononi mwa maadui zangu na wale wanao nifukuzia.
16 to light [emph?] face your upon servant/slave your to save me in/on/with kindness your
Nuru ya uso wako imuangazie mtumishi wako; uniokoe katika uaminifu wa agano lako.
17 LORD not be ashamed for to call: call to you be ashamed wicked to silence: silent to/for hell: Sheol (Sheol )
Usiniache niaibishwe, Yahwe; kwa maana ninakuita wewe! Waovu waaibishwe! Na wanyamaze kimya kuzimuni. (Sheol )
18 be dumb lips deception [the] to speak: speak upon righteous arrogant in/on/with pride and contempt
Na inyamazishwe midomo midanganyifu ambayo husema maneno mabaya kuhusu watu wenye haki huku wakiwa na kiburi na dharau.
19 what? many goodness your which to treasure to/for afraid your to work to/for to seek refuge in/on/with you before son: child man
Uzuri wako ni wa namna gani nao umeuhifadhii kwa ajili ya wale wanao kuheshimu sana, ambao wewe huufanya kwa ajili ya wale ambao hukimbilia kwako kwa ajili ya usalama mbele ya watoto wote wa wanadamu!
20 to hide them in/on/with secrecy face your from conspiracy man to treasure them in/on/with booth from strife tongue
Katika makao ya uwepo wako, wewe huwaficha mbali na njama za watu. Wewe huwaficha mahali salama na ndimi zenye vurugu.
21 to bless LORD for to wonder kindness his to/for me in/on/with city siege
Atukuzwe Yahwe, kwa maana yeye alinionesha maajabu ya uaminifu wa agano lake mahali nilipoishi.
22 and I to say in/on/with to hurry I to cut off from before eye: seeing your surely to hear: hear voice supplication my in/on/with to cry I to(wards) you
Ingawa kwa haraka zangu nilisema, “Nimeondolewa machoni pako,” bali wewe ulisikia kusihi kwangu nilipokulilia wewe.
23 to love: lover [obj] LORD all pious his faithful to watch LORD and to complete upon remainder to make: do pride
Enyi wafuasi waaminifu, mpendeni Yahwe, Yahwe huwalinda waaminifu, lakini huwalipa wakaidi ipasavyo.
24 to strengthen: strengthen and to strengthen heart your all [the] to wait: hope to/for LORD
Iweni imara na jasiri, ninyi nyote mnao mwamini Mungu kuwasaidia.