< Psalms 17 >
1 prayer to/for David to hear: hear [emph?] LORD righteousness to listen [emph?] cry my to listen [emph?] prayer my in/on/with not lips deceit
Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
2 from to/for face your justice: judgement my to come out: come eye your to see uprightness
Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
3 to test heart my to reckon: visit night to refine me not to find to plan not to pass: trespass lip my
Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
4 to/for wages man in/on/with word lips your I to keep: guard way violent
Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
5 to grasp step my in/on/with track your not to shake beat my
Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
6 I to call: call to you for to answer me God to stretch ear your to/for me to hear: hear word my
Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
7 be distinguished kindness your to save to seek refuge from to arise: attack in/on/with right your
Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
8 to keep: guard me like/as pupil daughter eye in/on/with shadow wing your to hide me
Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
9 from face: before wicked this to ruin me enemy my in/on/with soul: life to surround upon me
kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
10 fat their to shut lip their to speak: speak in/on/with majesty
Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
11 step our now (to turn: surround us *Q(K)*) eye their to set: make to/for to stretch in/on/with land: soil
Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
12 likeness his like/as lion to long to/for to tear and like/as lion to dwell in/on/with hiding
Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
13 to arise: rise [emph?] LORD to meet [emph?] face of his to bow him to escape [emph?] soul my from wicked sword your
Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
14 from man hand: power your LORD from man from lifetime/world portion their in/on/with life (and to treasure your *Q(K)*) to fill belly: womb their to satisfy son: child and to rest remainder their to/for infant their
Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
15 I in/on/with righteousness to see face your to satisfy in/on/with to awake likeness your
Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.