< Numbers 1 >

1 and to speak: speak LORD to(wards) Moses in/on/with wilderness (Wilderness of) Sinai in/on/with tent meeting in/on/with one to/for month [the] second in/on/with year [the] second to/for to come out: come them from land: country/planet Egypt to/for to say
Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
2 to lift: count [obj] head: count all congregation son: descendant/people Israel to/for family their to/for house: household father their in/on/with number name all male to/for head their
“Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
3 from son: aged twenty year and above [to] all to come out: regular army: war in/on/with Israel to reckon: list [obj] them to/for army their you(m. s.) and Aaron
Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
4 and with you to be man man to/for tribe man head: leader to/for house: household father his he/she/it
Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
5 and these name [the] human which to stand: stand with you to/for Reuben Elizur son: child Shedeur
Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
6 to/for Simeon Shelumiel son: child Zurishaddai
kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
7 to/for Judah Nahshon son: child Amminadab
kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
8 to/for Issachar Nethanel son: child Zuar
kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
9 to/for Zebulun Eliab son: child Helon
kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
10 to/for son: child Joseph to/for Ephraim Elishama son: child Ammihud to/for Manasseh Gamaliel son: child Pedahzur
kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
11 to/for Benjamin Abidan son: child Gideoni
kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
12 to/for Dan Ahiezer son: child Ammishaddai
kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
13 to/for Asher Pagiel son: child Ochran
kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
14 to/for Gad Eliasaph son: child Deuel
kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
15 to/for Naphtali Ahira son: child Enan
kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
16 these (to call: call to *Q(K)*) [the] congregation leader tribe father their head: leader thousand: clan Israel they(masc.)
Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
17 and to take: take Moses and Aaron [obj] [the] human [the] these which to pierce in/on/with name
Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
18 and [obj] all [the] congregation to gather in/on/with one to/for month [the] second and to beget upon family their to/for house: household father their in/on/with number name from son: aged twenty year and above [to] to/for head their
wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
19 like/as as which to command LORD [obj] Moses and to reckon: list them in/on/with wilderness (Wilderness of) Sinai
kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
20 and to be son: descendant/people Reuben firstborn Israel generation their to/for family their to/for house: household father their in/on/with number name to/for head their all male from son: aged twenty year and above [to] all to come out: regular army: war
Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
21 to reckon: list their to/for tribe Reuben six and forty thousand and five hundred
Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
22 to/for son: descendant/people Simeon generation their to/for family their to/for house: household father their to reckon: list his in/on/with number name to/for head their all male from son: aged twenty year and above [to] all to come out: regular army: war
Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
23 to reckon: list their to/for tribe Simeon nine and fifty thousand and three hundred
Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
24 to/for son: descendant/people Gad generation their to/for family their to/for house: household father their in/on/with number name from son: aged twenty year and above [to] all to come out: regular army: war
Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
25 to reckon: list their to/for tribe Gad five and forty thousand and six hundred and fifty
Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
26 to/for son: descendant/people Judah generation their to/for family their to/for house: household father their in/on/with number name from son: aged twenty year and above [to] all to come out: regular army: war
Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
27 to reckon: list their to/for tribe Judah four and seventy thousand and six hundred
Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
28 to/for son: descendant/people Issachar generation their to/for family their to/for house: household father their in/on/with number name from son: aged twenty year and above [to] all to come out: regular army: war
Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
29 to reckon: list their to/for tribe Issachar four and fifty thousand and four hundred
Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
30 to/for son: descendant/people Zebulun generation their to/for family their to/for house: household father their in/on/with number name from son: aged twenty year and above [to] all to come out: regular army: war
Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
31 to reckon: list their to/for tribe Zebulun seven and fifty thousand and four hundred
Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
32 to/for son: descendant/people Joseph to/for son: descendant/people Ephraim generation their to/for family their to/for house: household father their in/on/with number name from son: aged twenty year and above [to] all to come out: regular army: war
Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
33 to reckon: list their to/for tribe Ephraim forty thousand and five hundred
Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
34 to/for son: descendant/people Manasseh generation their to/for family their to/for house: household father their in/on/with number name from son: aged twenty year and above [to] all to come out: regular army: war
Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
35 to reckon: list their to/for tribe Manasseh two and thirty thousand and hundred
Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
36 to/for son: descendant/people Benjamin generation their to/for family their to/for house: household father their in/on/with number name from son: aged twenty year and above [to] all to come out: regular army: war
Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
37 to reckon: list their to/for tribe Benjamin five and thirty thousand and four hundred
Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
38 to/for son: descendant/people Dan generation their to/for family their to/for house: household father their in/on/with number name from son: aged twenty year and above [to] all to come out: regular army: war
Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
39 to reckon: list their to/for tribe Dan two and sixty thousand and seven hundred
Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
40 to/for son: descendant/people Asher generation their to/for family their to/for house: household father their in/on/with number name from son: aged twenty year and above [to] all to come out: regular army: war
Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
41 to reckon: list their to/for tribe Asher one and forty thousand and five hundred
Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
42 son: descendant/people Naphtali generation their to/for family their to/for house: household father their in/on/with number name from son: aged twenty year and above [to] all to come out: regular army: war
Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
43 to reckon: list their to/for tribe Naphtali three and fifty thousand and four hundred
Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
44 these [the] to reckon: list which to reckon: list Moses and Aaron and leader Israel two ten man man one to/for house: household father his to be
Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
45 and to be all to reckon: list son: descendant/people Israel to/for house: household father their from son: aged twenty year and above [to] all to come out: regular army: war in/on/with Israel
Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
46 and to be all [the] to reckon: list six hundred thousand and three thousand and five hundred and fifty
Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
47 and [the] Levi to/for tribe father their not to reckon: list in/on/with midst their
Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
48 and to speak: speak LORD to(wards) Moses to/for to say
Bwana alikuwa amemwambia Mose:
49 surely [obj] tribe Levi not to reckon: list and [obj] head: count their not to lift: count in/on/with midst son: descendant/people Israel
“Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
50 and you(m. s.) to reckon: overseer [obj] [the] Levi upon tabernacle [the] testimony and upon all article/utensil his and upon all which to/for him they(masc.) to lift: bear [obj] [the] tabernacle and [obj] all article/utensil his and they(masc.) to minister him and around to/for tabernacle to camp
Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
51 and in/on/with to set out [the] tabernacle to go down [obj] him [the] Levi and in/on/with to camp [the] tabernacle to arise: establish [obj] him [the] Levi and [the] be a stranger [the] approaching to die
Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
52 and to camp son: descendant/people Israel man: anyone upon camp his and man: anyone upon standard his to/for army their
Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
53 and [the] Levi to camp around to/for tabernacle [the] testimony and not to be wrath upon congregation son: descendant/people Israel and to keep: guard [the] Levi [obj] charge tabernacle [the] testimony
Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
54 and to make: do son: descendant/people Israel like/as all which to command LORD [obj] Moses so to make: do
Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.

< Numbers 1 >