< Numbers 15 >

1 and to speak: speak LORD to(wards) Moses to/for to say
Bwana akamwambia Mose,
2 to speak: speak to(wards) son: descendant/people Israel and to say to(wards) them for to come (in): come to(wards) land: country/planet seat your which I to give: give to/for you
“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Baada ya ninyi kuingia katika nchi ninayowapa kama nyumbani,
3 and to make: offer food offering to/for LORD burnt offering or sacrifice to/for to wonder vow or in/on/with voluntariness or in/on/with meeting: festival your to/for to make aroma soothing to/for LORD from [the] cattle or from [the] flock
nanyi mkitoa sadaka za kuteketezwa kwa moto, kutoka makundi ya ngʼombe au kondoo, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, ikiwa ni sadaka za kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum ama sadaka ya hiari au sadaka ya sikukuu zenu,
4 and to present: bring [the] to present: bring offering his to/for LORD offering fine flour tenth to mix in/on/with fourth [the] hin oil
ndipo yeye aletaye sadaka yake ataiweka mbele za Bwana sadaka ya nafaka, sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta.
5 and wine to/for drink offering fourth [the] hin to make: offer upon [the] burnt offering or to/for sacrifice to/for lamb [the] one
Pamoja na kila mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, andaa robo ya hini ya divai kwa sadaka ya kinywaji.
6 or to/for ram to make: offer offering fine flour two tenth to mix in/on/with oil third [the] hin
“‘Pamoja na kondoo dume andaa sadaka ya nafaka ya sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na theluthi moja ya hini ya mafuta,
7 and wine to/for drink offering third [the] hin to present: bring aroma soothing to/for LORD
na theluthi moja ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Vitoe kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
8 and for to make: offer son: young animal cattle burnt offering or sacrifice to/for to wonder vow or peace offering to/for LORD
“‘Unapoandaa fahali mchanga kama sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum au sadaka ya amani kwa Bwana,
9 and to present: bring upon son: young animal [the] cattle offering fine flour three tenth to mix in/on/with oil half [the] hin
leta pamoja na huyo fahali sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na nusu ya hini ya mafuta.
10 and wine to present: bring to/for drink offering half [the] hin food offering aroma soothing to/for LORD
Pia utaleta nusu ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Itakuwa sadaka iliyoteketezwa kwa moto, harufu nzuri inayompendeza Bwana.
11 thus to make: do to/for cattle [the] one or to/for ram [the] one or to/for sheep in/on/with lamb or in/on/with goat
Kila fahali au kondoo dume, kila mwana-kondoo au mbuzi mchanga, atatayarishwa kwa njia hii.
12 like/as number which to make: offer thus to make: do to/for one like/as number their
Fanyeni hivi kwa ajili ya kila mmoja, kwa kadiri ya wingi wa mtakavyoandaa.
13 all [the] born to make: do thus [obj] these to/for to present: bring food offering aroma soothing to/for LORD
“‘Kila mmoja ambaye ni mzawa ni lazima afanye vitu hivi kwa njia hii hapo aletapo sadaka ya kuteketezwa kwa moto kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
14 and for to sojourn with you sojourner or which in/on/with midst your to/for generation your and to make: offer food offering aroma soothing to/for LORD like/as as which to make: do so to make: do
Kwa vizazi vijavyo, wakati wowote mgeni au mtu mwingine yeyote anayeishi miongoni mwenu aletapo sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana, ni lazima afanye sawasawa kabisa na jinsi mnavyofanya ninyi.
15 [the] assembly statute one to/for you and to/for sojourner [the] to sojourn statute forever: enduring to/for generation your like/as you like/as sojourner to be to/for face: before LORD
Jumuiya itakuwa na sheria hizo hizo kwenu na kwa mgeni aishiye miongoni mwenu; hii ni amri ya kudumu kwa vizazi vijavyo. Ninyi na mgeni mtakuwa sawa mbele za Bwana:
16 instruction one and justice: judgement one to be to/for you and to/for sojourner [the] to sojourn with you
Sheria hizo hizo na masharti hayo hayo hayo, yatawahusu ninyi na mgeni aishiye miongoni mwenu.’”
17 and to speak: speak LORD to(wards) Moses to/for to say
Bwana akamwambia Mose,
18 to speak: speak to(wards) son: descendant/people Israel and to say to(wards) them in/on/with to come (in): come you to(wards) [the] land: country/planet which I to come (in): bring [obj] you there [to]
“Sema na Waisraeli na uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapeleka
19 and to be in/on/with to eat you from food: bread [the] land: country/planet to exalt contribution to/for LORD
nanyi mkala chakula cha nchi hiyo, toeni sehemu ya chakula hicho kama sadaka kwa Bwana.
20 first: beginning dough your bun to exalt contribution like/as contribution threshing floor so to exalt [obj] her
Toeni andazi kutoka kwa malimbuko ya chakula chenu kitokacho katika ardhi, na mkitoe kama sadaka kutoka sakafu ya kupuria nafaka.
21 from first: beginning dough your to give: give to/for LORD contribution to/for generation your
Kwa vizazi vyote vijavyo hamna budi kutoa sadaka hii kwa Bwana kutoka kwa malimbuko ya unga wenu.
22 and for to wander and not to make: do [obj] all [the] commandment [the] these which to speak: speak LORD to(wards) Moses
“‘Basi kama pasipo kukusudia umeshindwa kushika mojawapo katika amri hizi ambazo Bwana alimpa Mose,
23 [obj] all which to command LORD to(wards) you in/on/with hand: by Moses from [the] day which to command LORD and further to/for generation your
amri yoyote ya Bwana kwenu kupitia Mose, tangu siku ile Bwana alipowapa na inaendelea hadi vizazi vyote vijavyo;
24 and to be if from eye: appearance [the] congregation to make: do to/for unintentionally and to make: offer all [the] congregation bullock son: young animal cattle one to/for burnt offering to/for aroma soothing to/for LORD and offering his and drink offering his like/as justice: judgement and he-goat goat one to/for sin: sin offering
ikiwa hili limefanyika pasipo kukusudia bila jumuiya kuwa na habari nalo, basi jumuiya yote itatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya kuteketezwa ikiwa harufu nzuri inayompendeza Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka na ya kinywaji zilizoamriwa kwayo, na mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
25 and to atone [the] priest upon all congregation son: descendant/people Israel and to forgive to/for them for unintentionally he/she/it and they(masc.) to come (in): bring [obj] offering their food offering to/for LORD and sin: sin offering their to/for face: before LORD upon unintentionally their
Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya jumuiya yote ya Kiisraeli, nao watasamehewa, kwa kuwa haikuwa makusudi nao wamemletea Bwana sadaka iliyoteketezwa kwa moto na sadaka ya dhambi kwa ajili ya kosa lao.
26 and to forgive to/for all congregation son: descendant/people Israel and to/for sojourner [the] to sojourn in/on/with midst their for to/for all [the] people in/on/with unintentionally
Jumuiya yote ya Kiisraeli pamoja na wageni waishio miongoni mwao watasamehewa, kwa sababu watu wote walihusika katika kosa lile lisilokusudiwa.
27 and if soul: person one to sin in/on/with unintentionally and to present: bring goat daughter year her to/for sin: sin offering
“‘Lakini kama mtu mmoja peke yake akitenda dhambi pasipo kukusudia, ni lazima alete mbuzi mke wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
28 and to atone [the] priest upon [the] soul: person [the] to go astray in/on/with to sin in/on/with unintentionally to/for face: before LORD to/for to atone upon him and to forgive to/for him
Kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule aliyekosa kwa kufanya dhambi pasipo kukusudia, upatanisho utakapofanywa kwa ajili yake, atasamehewa.
29 [the] born in/on/with son: descendant/people Israel and to/for sojourner [the] to sojourn in/on/with midst their instruction one to be to/for you to/for to make: do in/on/with unintentionally
Sheria hiyo moja itamhusu kila mmoja ambaye ametenda dhambi pasipo kukusudia, awe Mwisraeli mzawa ama mgeni.
30 and [the] soul: person which to make: do in/on/with hand to exalt from [the] born and from [the] sojourner [obj] LORD he/she/it to blaspheme and to cut: eliminate [the] soul: person [the] he/she/it from entrails: among people her
“‘Lakini yeyote ambaye amefanya dhambi kwa dharau awe mzawa au mgeni, anamkufuru Bwana, naye mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
31 for word LORD to despise and [obj] commandment his to break to cut: eliminate to cut: eliminate [the] soul: person [the] he/she/it iniquity: crime her in/on/with her
Kwa sababu amelidharau neno la Bwana na kuvunja amri zake, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali; hatia yake inabaki juu yake.’”
32 and to be son: descendant/people Israel in/on/with wilderness and to find man to gather tree: stick in/on/with day [the] Sabbath
Waisraeli walipokuwa jangwani, mtu mmoja alikutwa akikusanya kuni siku ya Sabato.
33 and to present: bring [obj] him [the] to find [obj] him to gather tree: stick to(wards) Moses and to(wards) Aaron and to(wards) all [the] congregation
Wale waliomkuta akikusanya kuni wakamleta kwa Mose, Aroni na kusanyiko lote,
34 and to rest [obj] him in/on/with custody for not to declare what? to make: do to/for him
nao wakamweka kifungoni, kwa sababu haikufahamika kwa wazi kwamba afanyiwe nini.
35 and to say LORD to(wards) Moses to die to die [the] man to stone [obj] him in/on/with stone all [the] congregation from outside to/for camp
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Huyo mtu ni lazima afe. Kusanyiko lote lazima limpige mawe nje ya kambi.”
36 and to come out: send [obj] him all [the] congregation to(wards) from outside to/for camp and to stone [obj] him in/on/with stone and to die like/as as which to command LORD [obj] Moses
Hivyo kusanyiko likamtoa nje ya kambi na kumpiga mawe hadi akafa, kama Bwana alivyomwamuru Mose.
37 and to say LORD to(wards) Moses to/for to say
Bwana akamwambia Mose,
38 to speak: speak to(wards) son: descendant/people Israel and to say to(wards) them and to make to/for them tassel upon wing garment their to/for generation their and to give: put upon tassel [the] wing cord blue
“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Kwa vizazi vyote vijavyo jifanyieni vifundo katika pindo za mavazi yenu vikiwa na uzi wa buluu kwenye kila kifundo.
39 and to be to/for you to/for tassel and to see: see [obj] him and to remember [obj] all commandment LORD and to make [obj] them and not to spy after heart your and after eye your which you(m. p.) to fornicate after them
Mtakuwa mkivitazama vifundo hivyo ili mpate kukumbuka amri zote za Bwana, ili mpate kuzitii msije mkajitia uzinzi wenyewe kwa kuzifuata tamaa za mioyo yenu na za macho yenu.
40 because to remember and to make: do [obj] all commandment my and to be holy to/for God your
Ndipo mtakumbuka kuzitii amri zangu zote nanyi mtawekwa wakfu kwa Mungu wenu.
41 I LORD God your which to come out: send [obj] you from land: country/planet Egypt to/for to be to/for you to/for God I LORD God your
Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa Misri niwe Mungu wenu. Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu.’”

< Numbers 15 >