< Mark 1 >
1 beginning the/this/who gospel Jesus Christ son (the/this/who *ko*) God
Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
2 (as/just as *N(k)O*) to write in/on/among (the/this/who Isaiah *NO*) (the/this/who *N(k)O*) (prophet *N(K)O*) look! (I/we *KO*) to send the/this/who angel: messenger me before face you which to prepare the/this/who road you (before you *K*)
Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie; yeye atakutayarishia njia yako.
3 voice/sound: voice to cry out in/on/among the/this/who deserted to make ready the/this/who road lord: God Straight to do/make: do the/this/who path it/s/he
Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni mapito yake.”
4 to be John (the/this/who *no*) to baptize in/on/among the/this/who deserted and to preach baptism repentance toward forgiveness sin
Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba ni lazima watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
5 and to depart to/with it/s/he all the/this/who Judea country and the/this/who Jerusalem all and to baptize by/under: by it/s/he in/on/among the/this/who Jordan river to agree the/this/who sin it/s/he
Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
6 (and *no*) to be (then *k*) the/this/who John to put on hair camel and belt/sash/girdle made of leather about the/this/who loins it/s/he and to eat locust and honey wild
Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
7 and to preach to say to come/go the/this/who strong me after me which no to be sufficient to stoop/bend down to loose the/this/who leather strap the/this/who sandal it/s/he
Naye alihubiri akisema, “Baada yangu anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.
8 I/we (on the other hand *k*) to baptize you (in/on/among *ko*) water it/s/he then to baptize you in/on/among spirit/breath: spirit holy
Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
9 and to be in/on/among that the/this/who day to come/go Jesus away from Nazareth the/this/who Galilee and to baptize toward the/this/who Jordan by/under: by John
Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani.
10 and immediately to ascend (out from *N(k)O*) the/this/who water to perceive: see to split the/this/who heaven and the/this/who spirit/breath: spirit (as/when *N(k)O*) dove to come/go down (toward *N(k)O*) it/s/he
Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa.
11 and voice/sound: voice to be out from the/this/who heaven you to be the/this/who son me the/this/who beloved in/on/among (you *N(K)O*) to delight
Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
12 and immediately the/this/who spirit/breath: spirit it/s/he to expel toward the/this/who deserted
Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani,
13 and to be (there *k*) in/on/among the/this/who deserted forty day to test/tempt: tempt by/under: by the/this/who Satan and to be with/after the/this/who wild animal and the/this/who angel to serve it/s/he
akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamtumikia.
14 (and *o*) with/after then the/this/who to deliver the/this/who John to come/go the/this/who Jesus toward the/this/who Galilee to preach the/this/who gospel (the/this/who kingdom *K*) the/this/who God
Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema,
15 and to say that/since: that to fulfill the/this/who time/right time and to come near the/this/who kingdom the/this/who God to repent and to trust (in) in/on/among the/this/who gospel
“Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!”
16 (and *no*) (to pass *N(k)O*) (then *k*) from/with/beside the/this/who sea the/this/who (Sea of) Galilee to perceive: see Simon and Andrew the/this/who brother (it/s/he *k*) (the/this/who *o*) (Simon *no*) (to cast *N(k)O*) (net *k*) in/on/among the/this/who sea to be for fisherman
Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu.
17 and to say it/s/he the/this/who Jesus come after me and to do/make: do you to be fisherman a human
Yesu akawaambia, “Nifuateni nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu.”
18 and immediately to release: leave the/this/who net (it/s/he *k*) to follow it/s/he
Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
19 and to advance (from there *k*) little/few to perceive: see James the/this/who the/this/who Zebedee and John the/this/who brother it/s/he and it/s/he in/on/among the/this/who boat to complete the/this/who net
Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
20 and immediately to call: call it/s/he and to release: leave the/this/who father it/s/he Zebedee in/on/among the/this/who boat with/after the/this/who hired worker to go away after it/s/he
Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
21 and to enter toward Capernaum and immediately the/this/who Sabbath to enter toward the/this/who synagogue to teach
Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika Sunagogi, akaanza kufundisha.
22 and be astonished upon/to/against the/this/who teaching it/s/he to be for to teach it/s/he as/when authority to have/be and no as/when the/this/who scribe
Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama walimu wao wa Sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.
23 and (immediately *NO*) to be in/on/among the/this/who synagogue it/s/he a human in/on/among spirit/breath: spirit unclean and to yell
Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu,
24 to say (ha!/aha! *K*) which? me and you Jesus Nazareth to come/go to destroy me to know you which? to be the/this/who holy the/this/who God
akapaaza sauti, “Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: wewe ni Mtakatifu wa Mungu!”
25 and to rebuke it/s/he the/this/who Jesus to say to muzzle and to go out out from it/s/he
Yesu akamkemea, “Nyamaza! Mtoke mtu huyu.”
26 and to convulse it/s/he the/this/who spirit/breath: spirit the/this/who unclean and (to call *N(k)O*) voice/sound: voice great to go out out from it/s/he
Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.
27 and to astonish (all *N(k)O*) so to debate to/with (themself *N(k)O*) to say which? to be this/he/she/it (which? the/this/who *k*) teaching (the/this/who *k*) new (this/he/she/it that/since: that *k*) according to authority and the/this/who spirit/breath: spirit the/this/who unclean to command and to obey it/s/he
Watu wote wakashangaa, wakaulizana, “Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
28 (and *no*) to go out (then *k*) the/this/who hearing it/s/he immediately (everywhere *NO*) toward all the/this/who region the/this/who Galilee
Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika wilaya ya Galilaya.
29 and immediately out from the/this/who synagogue (to go out to come/go *NK(O)*) toward the/this/who home Simon and Andrew with/after James and John
Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.
30 the/this/who then mother-in-law Simon to recline be feverish and immediately to say it/s/he about it/s/he
Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.
31 and to come near/agree to arise it/s/he to grasp/seize the/this/who hand (it/s/he *ko*) and to release: leave it/s/he the/this/who fever (immediately *K*) and to serve it/s/he
Yesu akamwendea huyo mama, akamshika mkono, akamwinua. Na ile homa ikamwacha, akaanza kuwatumikia.
32 evening then to be when (to set *N(k)O*) the/this/who sun to bear/lead to/with it/s/he all the/this/who badly to have/be and the/this/who be demonised
Jioni, jua lilipokwisha tua, wakamletea Yesu wagonjwa wote na watu waliopagawa na pepo.
33 and to be all the/this/who city to gather to/with the/this/who door
Watu wote wa mji ule wakakusanyika nje ya mlango.
34 and to serve/heal much badly to have/be various illness and demon much to expel and no to release: permit to speak the/this/who demon that/since: since to perceive: know it/s/he (Christ to exist *O*)
Naye Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa mbalimbali; aliwafukuza pepo wengi, lakini hakuwaruhusu kusema kitu maana walikuwa wanamjua yeye ni nani.
35 and early at night greatly to arise to go out and to go away toward deserted place and there to pray
Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
36 and (to seek *N(k)O*) it/s/he (the/this/who *ko*) Simon and the/this/who with/after it/s/he
Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
37 and (to find/meet *N(k)O*) it/s/he (and *no*) to say it/s/he that/since: that all to seek you
Walipomwona wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta.”
38 and to say it/s/he to bring (from elsewhere *NO*) toward the/this/who to have/be village in order that/to and there to preach toward this/he/she/it for (to go out *N(k)O*)
Yesu akawaambia, “Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo.”
39 and (to come/go *N(k)O*) to preach (toward the/this/who synagogue *N(k)O*) it/s/he toward all the/this/who Galilee and the/this/who demon to expel
Basi, akaenda kila mahali Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
40 and to come/go to/with it/s/he leprous to plead/comfort it/s/he and to kneel (it/s/he *ko*) and to say it/s/he that/since: that if to will/desire be able me to clean
Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba, “Ukitaka, waweza kunitakasa!”
41 (the/this/who *k*) (and *N(k)O*) (Jesus *k*) (to pity *NK(O)*) to stretch out the/this/who hand it/s/he to touch and to say it/s/he to will/desire to clean
Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, “Nataka, takasika!”
42 and (to say it/s/he *K*) immediately to go away away from it/s/he the/this/who leprosy and to clean
Mara ukoma ukamwacha mtu huyo, akatakasika.
43 and be agitated it/s/he immediately to expel it/s/he
Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwonya vikali,
44 and to say it/s/he to see: see nothing nothing to say but to go you to show the/this/who priest and to bring to about the/this/who cleansing you which to order Moses toward testimony it/s/he
“Usimwambie mtu yeyote jambo hili, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani; kisha utoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona.”
45 the/this/who then to go out be first to preach much and to publish abroad the/this/who word so never again it/s/he be able plainly toward city to enter but out/outside(r) (upon/to/against *N(k)O*) deserted place to be and to come/go to/with it/s/he (from all sides *N(k)O*)
Lakini huyo mtu akaenda, akaanza kueneza habari hiyo kila mahali na kusema mambo mengi hata Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote waziwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande.