< Malachi 2 >

1 and now to(wards) you [the] commandment [the] this [the] priest
“Sasa onyo hili ni kwa ajili yenu, enyi makuhani.
2 if not to hear: hear and if not to set: consider upon heart to/for to give: give glory to/for name my to say LORD Hosts and to send: depart in/on/with you [obj] [the] curse and to curse [obj] blessing your and also to curse her for nothing you to set: consider upon heart
Kama hamtasikiliza, na kama hamtaki kuielekeza mioyo yenu kuheshimu Jina langu, nitatuma laana juu yenu, nami nitalaani baraka zenu. Naam, nimekwisha kuzilaani, kwa sababu hamkuielekeza mioyo yenu kuniheshimu mimi,” Asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
3 look! I to rebuke to/for you [obj] [the] seed: children and to scatter refuse upon face your refuse feast your and to lift: bear [obj] you to(wards) him
“Kwa sababu yenu nitawakatilia mbali wazao wenu. Nitazipaka nyuso zenu mavi, mavi ya dhabihu zenu. Nanyi mtafukuzwa pamoja nazo mtoke mbele zangu.
4 and to know for to send: depart to(wards) you [obj] [the] commandment [the] this to/for to be covenant my with Levi to say LORD Hosts
Nanyi mtajua kuwa nimewapelekea onyo hili ili kwamba Agano langu na Lawi lipate kuendelea,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
5 covenant my to be with him [the] life and [the] peace and to give: give them to/for him fear and to fear: revere me and from face: because name my to to be dismayed he/she/it
“Agano langu lilikuwa pamoja naye, agano la uhai na amani, nami nilimpa yote, ili aniche na kuniheshimu, naye akaniheshimu na kusimama akilicha Jina langu.
6 instruction truth: true to be in/on/with lip his and injustice not to find in/on/with lips his in/on/with peace and in/on/with plain to go: walk with me and many to return: repent from iniquity: crime
Fundisho la kweli lilikuwa kinywani mwake, wala hakuna uongo wowote uliopatikana katika midomo yake. Alitembea nami katika amani na unyofu, naye akawageuza wengi kutoka dhambini.
7 for lips priest to keep: guard knowledge and instruction to seek from lip his for messenger LORD Hosts he/she/it
“Kwa maana yapasa midomo ya kuhani kuhifadhi maarifa. Tena kutoka kinywani mwake watu wangepaswa kutafuta mafundisho, kwa sababu yeye ni mjumbe wa Bwana Mwenye Nguvu Zote.
8 and you(m. p.) to turn aside: turn aside from [the] way: conduct to stumble many in/on/with instruction to ruin covenant [the] Levi to say LORD Hosts
Lakini mmegeuka mkaiacha njia, na kwa mafundisho yenu mmesababisha wengi kujikwaa. Mmevunja agano na Lawi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
9 and also I to give: make [obj] you to despise and low to/for all [the] people like/as lip: according which nothing you to keep: obey [obj] way: conduct my and to lift: kindness face: kindness in/on/with instruction
“Kwa hiyo nimewasababisha ninyi kudharauliwa na kufedheheshwa mbele ya watu wote, kwa sababu hamkufuata njia zangu, bali mmeonyesha upendeleo katika mambo ya sheria.”
10 not father one to/for all our not God one to create us why? to act treacherously man: anyone in/on/with brother: compatriot his to/for to profane/begin: profane covenant father our
Je, sote hatuna Baba mmoja? Hatukuumbwa na Mungu mmoja? Kwa nini basi tunalinajisi Agano la baba zetu kwa kukosa uaminifu kila mmoja kwa mwenzake?
11 to act treacherously Judah and abomination to make in/on/with Israel and in/on/with Jerusalem for to profane/begin: profane Judah holiness LORD which to love: lover and rule: to marry daughter god foreign
Yuda amevunja uaminifu. Jambo la kuchukiza limetendeka katika Israeli na katika Yerusalemu: Yuda amepanajisi mahali patakatifu apendapo Bwana, kwa kuoa binti wa mungu mgeni.
12 to cut: eliminate LORD to/for man which to make: do her to rouse and to answer from tent Jacob and to approach: bring offering to/for LORD Hosts
Kwa maana kwa mtu yeyote atendaye jambo hili, Bwana na amkatilie mbali kutoka hema za Yakobo, hata kama huwa anamletea Bwana Mwenye Nguvu Zote sadaka.
13 and this second to make: do to cover tears [obj] altar LORD weeping and groaning from nothing still to turn to(wards) [the] offering and to/for to take: recieve acceptance from hand: power your
Kitu kingine mnachokifanya: Mnaifurikisha madhabahu ya Bwana kwa machozi. Mnalia na kuugua kwa sababu yeye haziangalii tena sadaka zenu wala hazikubali kwa furaha kutoka mikononi mwenu.
14 and to say upon what? upon for LORD to testify between you and between woman: wife youth your which you(m. s.) to act treacherously in/on/with her and he/she/it consort your and woman: wife covenant your
Mnauliza, “Kwa nini?” Ni kwa sababu Bwana ni shahidi kati yako na mke wa ujana wako, kwa sababu umevunja uaminifu naye, ingawa yeye ni mwenzako, mke wa agano lako la ndoa.
15 and not one to make and remnant spirit to/for him and what? [the] one to seek seed: children God and to keep: guard in/on/with spirit your and in/on/with woman: wife youth your not to act treacherously
Je, Bwana hakuwafanya wao kuwa mmoja? Katika mwili na katika roho wao ni wa Mungu. Kwa nini wawe mmoja? Kwa sababu Mungu alikuwa akitafuta mzao mwenye kumcha Mungu. Kwa hiyo jihadharini wenyewe katika roho zenu, mtu asivunje uaminifu kwa mke wa ujana wake.
16 for to hate to send: divorce to say LORD God Israel and to cover violence upon clothing his to say LORD Hosts and to keep: guard in/on/with spirit your and not to act treacherously
“Ninachukia kuachana,” asema Bwana, Mungu wa Israeli, “pia nachukia mtu anayejivika jeuri kama vazi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. Kwa hiyo jihadharini wenyewe katika roho zenu, wala msije mkavunja uaminifu.
17 be weary/toil LORD in/on/with word your and to say in/on/with what? be weary/toil in/on/with to say you all to make: do bad: evil pleasant in/on/with eye: seeing LORD and in/on/with them he/she/it to delight in or where? God [the] justice
Mmemchosha Bwana kwa maneno yenu. Nanyi mnauliza, “Tumemchosha kwa namna gani?” Mmemchosha kwa kusema, “Wote watendao mabaya ni wema machoni pa Bwana, naye anapendezwa nao” au “Mungu wa haki yuko wapi?”

< Malachi 2 >