< Leviticus 6 >
1 and to speak: speak LORD to(wards) Moses to/for to say
Bwana akamwambia Mose:
2 soul: person for to sin and be unfaithful unfaithfulness in/on/with LORD and to deceive in/on/with neighbor his in/on/with deposit or in/on/with security hand or in/on/with robbery or to oppress [obj] neighbor his
“Kama mtu yeyote akitenda dhambi, naye si mwaminifu kwa Bwana kwa kumdanganya jirani yake kuhusu kitu fulani alichokabidhiwa, au kimeachwa chini ya utunzaji wake, au kimeibwa, au kama akimdanganya,
3 or to find something lost and to deceive in/on/with her and to swear upon deception upon one from all which to make: do [the] man to/for to sin in/on/with them
au akiokota mali iliyopotea na akadanganya, au kuapa kwa uongo, au kama akitenda dhambi yoyote ambayo watu waweza kuitenda;
4 and to be for to sin and be guilty and to return: rescue [obj] [the] violence which to plunder or [obj] [the] oppression which to oppress or [obj] [the] deposit which to reckon: overseer with him or [obj] [the] something lost which to find
wakati akitenda dhambi hizo na kuwa mwenye hatia, ni lazima arudishe kile alichokuwa amekiiba au amekichukua kwa dhuluma, au alichokuwa amekabidhiwa, au mali iliyokuwa imepotea akaipata,
5 or from all which to swear upon him to/for deception and to complete [obj] him in/on/with head: first his and fifth his to add upon him to/for which he/she/it to/for him to give: give him in/on/with day guiltiness his
au chochote alichokuwa amekiapia kwa uongo. Lazima akirudishe kikamilifu, na aongeze sehemu ya tano ya thamani yake, vyote ampe mwenye mali siku ile anapeleka sadaka yake ya hatia.
6 and [obj] guilt (offering) his to come (in): bring to/for LORD ram unblemished from [the] flock in/on/with valuation your to/for guilt (offering) to(wards) [the] priest
Kisha kama adhabu lazima amletee kuhani, yaani kwa Bwana, kama sadaka yake ya hatia, kondoo dume asiye na dosari na mwenye thamani kamili kutoka kundi lake.
7 and to atone upon him [the] priest to/for face: before LORD and to forgive to/for him upon one from all which to make: do to/for guiltiness in/on/with her
Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana, naye atasamehewa kwa kosa lolote katika mambo hayo aliyoyatenda yaliyomfanya kuwa na hatia.”
8 and to speak: speak LORD to(wards) Moses to/for to say
Bwana akamwambia Mose:
9 to command [obj] Aaron and [obj] son: child his to/for to say this instruction [the] burnt offering he/she/it [the] burnt offering upon hearth upon [the] altar all [the] night till [the] morning and fire [the] altar to burn in/on/with him
“Mpe Aroni na wanawe agizo hili: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa: Sadaka ya kuteketezwa itabaki kwenye moto juu ya madhabahu usiku kucha, mpaka asubuhi, nao moto lazima uwe unaendelea kuwaka juu ya madhabahu.
10 and to clothe [the] priest garment his linen and undergarment linen to clothe upon flesh his and to exalt [obj] [the] ashes which to eat [the] fire [obj] [the] burnt offering upon [the] altar and to set: put him beside [the] altar
Kisha kuhani atavaa mavazi yake ya kitani, pamoja na nguo za ndani za kitani mwilini wake, na aondoe majivu ya sadaka ya kuteketezwa ambayo moto umeteketeza juu ya madhabahu, na kuyaweka kando ya madhabahu.
11 and to strip [obj] garment his and to clothe garment another and to come out: send [obj] [the] ashes to(wards) from outside to/for camp to(wards) place pure
Kisha atayavua mavazi haya na kuvaa mengine, naye achukue yale majivu nje ya kambi na kuyapeleka mahali palipo safi kwa kawaida ya ibada.
12 and [the] fire upon [the] altar to burn in/on/with him not to quench and to burn: burn upon her [the] priest tree: wood in/on/with morning in/on/with morning and to arrange upon her [the] burnt offering and to offer: burn upon her fat [the] peace offering
Moto ulio juu ya madhabahu lazima uwe unaendelea kuwaka, kamwe usizimike. Kila asubuhi kuhani ataongeza kuni na kupanga sadaka ya kuteketezwa juu ya moto, na kuteketeza mafuta ya sadaka za amani juu yake.
13 fire continually to burn upon [the] altar not to quench
Moto lazima uendelee kuwaka juu ya madhabahu mfululizo, kamwe usizimike.
14 and this instruction [the] offering to present: bring [obj] her son: child Aaron to/for face: before LORD to(wards) face: before [the] altar
“‘Haya ndiyo masharti ya sadaka ya nafaka: Wana wa Aroni wataileta mbele za Bwana, mbele za madhabahu.
15 and to exalt from him in/on/with handful his from fine flour [the] offering and from oil her and [obj] all [the] frankincense which upon [the] offering and to offer: burn [the] altar aroma soothing memorial her to/for LORD
Kuhani atachukua konzi ya unga laini na mafuta, pamoja na uvumba wote ulioko juu ya sadaka ya nafaka, ateketeze sehemu ya kumbukumbu juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
16 and [the] to remain from her to eat Aaron and son: child his unleavened bread to eat in/on/with place holy in/on/with court tent meeting to eat her
Aroni na wanawe watakula sehemu iliyobaki, lakini italiwa bila kutiwa chachu mahali patakatifu, nao wataila kwenye ua wa Hema la Kukutania.
17 not to bake leaven portion their to give: give [obj] her from food offering my holiness holiness he/she/it like/as sin: sin offering and like/as guilt (offering)
Kamwe haitaokwa na chachu; nimewapa kama fungu lao la sadaka iliyotolewa kwangu kwa moto. Ni takatifu sana, kama vile ilivyo sadaka ya dhambi na ya hatia.
18 all male in/on/with son: descendant/people Aaron to eat her statute: decree forever: enduring to/for generation your from food offering LORD all which to touch in/on/with them to consecrate: consecate
Kila mwanaume mzao wa Aroni aweza kuila. Ni fungu lake la kawaida la sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto kwa vizazi vijavyo. Chochote kinachozigusa kitakuwa kitakatifu.’”
19 and to speak: speak LORD to(wards) Moses to/for to say
Tena Bwana akamwambia Mose,
20 this offering Aaron and son: child his which to present: bring to/for LORD in/on/with day to anoint [obj] him tenth [the] ephah fine flour offering continually half her in/on/with morning and half her in/on/with evening
“Hii ni sadaka ambayo Aroni na wanawe wanapaswa kuleta kwa Bwana siku atakapotiwa mafuta: sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kama sadaka ya kawaida ya nafaka. Nusu yake ataitoa asubuhi na nusu nyingine jioni.
21 upon griddle in/on/with oil to make to stir to come (in): bring her baked offering morsel to present: bring aroma soothing to/for LORD
Iandae kwa mafuta kwenye kikaango; ilete ikiwa imechanganywa vizuri, na utoe hiyo sadaka ya nafaka ikiwa imevunjwa vipande vipande kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
22 and [the] priest [the] anointed underneath: instead him from son: child his to make: offer [obj] her statute: decree forever: enduring to/for LORD entire to offer: burn
Mwanawe atakayeingia mahali pake kama kuhani aliyetiwa mafuta ndiye atakayeiandaa. Ni fungu la kawaida la Bwana, nalo litateketezwa kabisa.
23 and all offering priest entire to be not to eat
Kila sadaka ya nafaka ya kuhani itateketezwa kabisa; kamwe haitaliwa.”
24 and to speak: speak LORD to(wards) Moses to/for to say
Bwana akamwambia Mose,
25 to speak: speak to(wards) Aaron and to(wards) son: child his to/for to say this instruction [the] sin: sin offering in/on/with place which to slaughter [the] burnt offering to slaughter [the] sin: sin offering to/for face: before LORD holiness holiness he/she/it
“Mwambie Aroni na wanawe: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya dhambi: Sadaka ya dhambi itachinjiwa mbele za Bwana mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa, ni takatifu sana.
26 [the] priest [the] to sin [obj] her to eat her in/on/with place holy to eat in/on/with court tent meeting
Kuhani anayeitoa ndiye atakayeikula; itakuliwa katika mahali patakatifu, katika ua wa Hema la Kukutania.
27 all which to touch in/on/with flesh her to consecrate: consecate and which to sprinkle from blood her upon [the] garment which to sprinkle upon her to wash in/on/with place holy
Chochote kitakachogusa nyama yoyote ya hiyo sadaka kitakuwa kitakatifu, na kama hiyo damu itadondokea juu ya vazi, lazima uifulie mahali patakatifu.
28 and article/utensil earthenware which to boil in/on/with him to break and if in/on/with article/utensil bronze to boil and to polish and to overflow in/on/with water
Chungu cha udongo kitakachopikiwa nyama lazima kivunjwe, lakini kama imepikiwa kwenye chombo cha shaba, chombo hicho kitasuguliwa na kusuuzwa kwa maji.
29 all male in/on/with priest to eat [obj] her holiness holiness he/she/it
Kila mwanaume katika familia ya kuhani aweza kula nyama hiyo; ni takatifu sana.
30 and all sin: sin offering which to come (in): bring from blood her to(wards) tent meeting to/for to atone in/on/with Holy Place not to eat in/on/with fire to burn
Lakini kila sadaka ya dhambi ambayo damu yake imeletwa ndani ya Hema la Kukutania kufanya upatanisho katika Mahali Patakatifu kamwe haitaliwa; lazima iteketezwe.