< Leviticus 5 >

1 and soul: person for to sin and to hear: hear voice: [sound of] oath and he/she/it witness or to see: see or to know if not to tell and to lift: guilt iniquity: crime his
“‘Ikiwa mtu atakuwa ametenda dhambi kwa sababu hakusema alipotakiwa kutoa ushahidi hadharani kuhusu jambo aliloona au kujua habari zake, yeye anastahili adhabu.
2 or soul: person which to touch in/on/with all word: thing unclean or in/on/with carcass living thing unclean or in/on/with carcass animal unclean or in/on/with carcass swarm unclean and to conceal from him and he/she/it unclean and be guilty
“‘Au kama mtu akigusa kitu chochote ambacho ni najisi, iwe ni mizoga ya wanyama pori walio najisi, au ya wanyama wafugwao walio najisi, au ya viumbe vitambaavyo ardhini, hata akiwa hana habari, amekuwa najisi na mwenye hatia.
3 or for to touch in/on/with uncleanness man to/for all uncleanness his which to defile in/on/with her and to conceal from him and he/she/it to know and be guilty
“‘Au kama akigusa kitu kilicho kichafu kinachotokana na binadamu, kitu chochote kile kinachoweza kumfanya awe najisi, hata akiwa hana habari, atakapofahamu atakuwa na hatia.
4 or soul: person for to swear to/for to speak rashly in/on/with lips to/for be evil or to/for be good to/for all which to speak rashly [the] man in/on/with oath and to conceal from him and he/she/it to know and be guilty to/for one from these
“‘Au kama mtu ameapa kufanya kitu chochote bila kufikiri, kiwe chema au kibaya, kwa vyovyote mtu aweza kuapa bila kujali, hata akiwa hana habari, atakapofahamu atakuwa na hatia.
5 and to be for be guilty to/for one from these and to give thanks which to sin upon her
“‘Wakati mtu yeyote atakapokuwa na hatia katika mojawapo ya haya, lazima akiri ni kwa njia gani ametenda dhambi,
6 and to come (in): bring [obj] guilt (offering) his to/for LORD upon sin his which to sin female from [the] flock lamb or female goat goat to/for sin: sin offering and to atone upon him [the] priest from sin his
na kama adhabu ya dhambi aliyoitenda, lazima alete kwa Bwana kondoo jike au mbuzi jike kutoka kwenye kundi lake kama sadaka ya dhambi; naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi yake.
7 and if not to touch hand: themselves his sufficiency sheep and to come (in): bring [obj] guilt (offering) his which to sin two turtledove or two son: young animal dove to/for LORD one to/for sin: sin offering and one to/for burnt offering
“‘Lakini huyo mtu kama hataweza kumtoa mwana-kondoo, ataleta hua wawili au makinda mawili ya njiwa kwa Bwana kuwa adhabu kwa ajili ya dhambi yake, mmoja wa hao ndege kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na wa pili kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.
8 and to come (in): bring [obj] them to(wards) [the] priest and to present: bring [obj] which to/for sin: sin offering first and to nip [obj] head his from opposite neck his and not to separate
Atawaleta kwa kuhani, ambaye atamtoa kwanza ndege mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi. Atamvunja shingo na kuacha kichwa chake kikiningʼinia,
9 and to sprinkle from blood [the] sin: sin offering upon wall [the] altar and [the] to remain in/on/with blood to drain to(wards) foundation [the] altar sin: sin offering he/she/it
naye atanyunyiza sehemu ya hiyo damu ya sadaka ya dhambi kwenye pembe za madhabahu. Damu iliyobaki lazima ichuruzwe chini ya madhabahu. Hii ni sadaka ya dhambi.
10 and [obj] [the] second to make: offer burnt offering like/as justice: judgement and to atone upon him [the] priest from sin his which to sin and to forgive to/for him
Kisha kuhani atamtoa yule ndege wa pili kama sadaka ya kuteketezwa kwa kufuata utaratibu uliowekwa, na hivyo kufanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi aliyoitenda, naye atasamehewa.
11 and if not to overtake hand: expend his to/for two turtledove or to/for two son: young animal dove and to come (in): bring [obj] offering his which to sin tenth [the] ephah fine flour to/for sin: sin offering not to set: put upon her oil and not to give: put upon her frankincense for sin: sin offering he/she/it
“‘Ikiwa basi, hawezi kupata hua wawili au makinda mawili ya njiwa, ataleta sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kwa ajili ya sadaka ya dhambi. Kamwe asiweke mafuta wala uvumba juu yake, kwa sababu ni sadaka ya dhambi.
12 and to come (in): bring her to(wards) [the] priest and to grasp [the] priest from her fullness handful his [obj] memorial her and to offer: burn [the] altar [to] upon food offering LORD sin: sin offering he/she/it
Atauleta unga kwa kuhani, ambaye atachukua konzi moja kama sehemu ya kumbukumbu na atauteketeza kwenye madhabahu juu ya sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto. Hii ni sadaka ya dhambi.
13 and to atone upon him [the] priest upon sin his which to sin from one from these and to forgive to/for him and to be to/for priest like/as offering
Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi yoyote ya hizo alizotenda, naye atasamehewa. Sadaka iliyobaki itakuwa ya kuhani, kama ilivyokuwa ile sadaka ya nafaka.’”
14 and to speak: speak LORD to(wards) Moses to/for to say
Bwana akamwambia Mose:
15 soul: person for be unfaithful unfaithfulness and to sin in/on/with unintentionally from holiness LORD and to come (in): bring [obj] guilt (offering) his to/for LORD ram unblemished from [the] flock in/on/with valuation your silver: money shekel in/on/with shekel [the] holiness to/for guilt (offering)
“Mtu anapokiuka na kutenda dhambi pasipo kukusudia kuhusu mojawapo ya mambo matakatifu ya Bwana, huyo mtu ataleta kwa Bwana kama adhabu kondoo dume mmoja kutoka kundi lake, asiye na dosari na mwenye thamani halisi kifedha, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu. Hii ni sadaka ya hatia.
16 and [obj] which to sin from [the] holiness to complete and [obj] fifth his to add upon him and to give: give [obj] him to/for priest and [the] priest to atone upon him in/on/with ram [the] guilt (offering) and to forgive to/for him
Ni lazima alipe kwa yale aliyoshindwa kufanya kuhusu vitu vitakatifu, kwa kuongeza sehemu ya tano ya thamani ile na kuitoa yote kwa kuhani, ambaye atamfanyia upatanisho kwa huyo kondoo dume kama sadaka ya dhambi, naye atasamehewa.
17 and if soul: person for to sin and to make: do one from all commandment LORD which not to make: do and not to know and be guilty and to lift: guilt iniquity: crime his
“Kama mtu akifanya dhambi na kufanya yale yaliyokatazwa katika mojawapo ya amri za Bwana, hata ikiwa hajui, yeye ana hatia na anastahili adhabu.
18 and to come (in): bring ram unblemished from [the] flock in/on/with valuation your to/for guilt (offering) to(wards) [the] priest and to atone upon him [the] priest upon unintentionally his which to go astray and he/she/it not to know and to forgive to/for him
Atamletea kuhani kama sadaka ya hatia kondoo dume kutoka kundi lake, kondoo asiye na dosari na mwenye thamani halisi kifedha. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa kosa alilotenda bila kukusudia, naye atasamehewa.
19 guilt (offering) he/she/it be guilty be guilty to/for LORD
Hii ni sadaka ya hatia; amekuwa na hatia kwa kufanya kosa dhidi ya Bwana.”

< Leviticus 5 >