< Leviticus 4 >

1 and to speak: speak LORD to(wards) Moses to/for to say
Bwana akamwambia Mose,
2 to speak: speak to(wards) son: descendant/people Israel to/for to say soul: person for to sin in/on/with unintentionally from all commandment LORD which not to make: do and to make: do from one from them
“Waambie Waisraeli: ‘Mtu yeyote afanyapo dhambi bila kukusudia na akatenda lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana:
3 if [the] priest [the] anointed to sin to/for guiltiness [the] people and to present: bring upon sin his which to sin bullock son: young animal cattle unblemished to/for LORD to/for sin: sin offering
“‘Ikiwa kuhani aliyetiwa mafuta amefanya dhambi na kuwaletea watu hatia, lazima alete kwa Bwana fahali mchanga asiye na dosari, kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya dhambi aliyotenda.
4 and to come (in): bring [obj] [the] bullock to(wards) entrance tent meeting to/for face: before LORD and to support [obj] hand his upon head [the] bullock and to slaughter [obj] [the] bullock to/for face: before LORD
Atamkabidhi huyo fahali kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha huyo fahali na kumchinja mbele za Bwana.
5 and to take: take [the] priest [the] anointed from blood [the] bullock and to come (in): bring [obj] him to(wards) tent meeting
Kisha kuhani huyo aliyetiwa mafuta atachukua sehemu ya damu ya huyo fahali na kuileta katika Hema la Kukutania.
6 and to dip [the] priest [obj] finger his in/on/with blood and to sprinkle from [the] blood seven beat to/for face: before LORD with face: before curtain [the] holiness
Atachovya kidole chake katika hiyo damu na kuinyunyiza sehemu yake mara saba mbele za Bwana mbele ya pazia la mahali patakatifu.
7 and to give: put [the] priest from [the] blood upon horn altar incense [the] spice to/for face: before LORD which in/on/with tent meeting and [obj] all blood [the] bullock to pour: pour to(wards) foundation altar [the] burnt offering which entrance tent meeting
Kisha kuhani atatia sehemu ya hiyo damu juu ya pembe za madhabahu ya kufukizia uvumba wenye harufu nzuri iliyoko mbele za Bwana katika Hema la Kukutania. Damu iliyobaki ya huyo fahali ataimwaga chini ya hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
8 and [obj] all fat bullock [the] sin: sin offering to exalt from him [obj] [the] fat [the] to cover upon [the] entrails: inner parts and [obj] all [the] fat which upon [the] entrails: inner parts
Atayaondoa mafuta yote ya fahali huyo wa sadaka ya dhambi, mafuta yale yanayofunika sehemu za ndani au zile zinazounganika nazo,
9 and [obj] two [the] kidney and [obj] [the] fat which upon them which upon [the] loin and [obj] [the] lobe upon [the] liver upon [the] kidney to turn aside: remove her
figo zote mbili na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yale yanayofunika ini ambayo atayaondoa pamoja na figo zote,
10 like/as as which to exalt from cattle sacrifice [the] peace offering and to offer: burn them [the] priest upon altar [the] burnt offering
kama vile mafuta yanayoondolewa kutoka kwenye maksai aliyetolewa sadaka ya amani. Kisha kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa.
11 and [obj] skin [the] bullock and [obj] all flesh his upon head his and upon leg his and entrails: inner parts his and refuse his
Lakini ngozi ya huyo fahali na nyama zake zote, pamoja na kichwa na miguu yake, sehemu za ndani na matumbo,
12 and to come out: send [obj] all [the] bullock to(wards) from outside to/for camp to(wards) place pure to(wards) pouring [the] ashes and to burn [obj] him upon tree: wood in/on/with fire upon pouring [the] ashes to burn
yaani sehemu nyingine zote zilizobaki za huyo fahali, lazima azitoe nje ya kambi mpaka mahali palipo safi kiibada, ambapo majivu hutupwa, naye atamchoma kwa moto juu ya kuni zilizoko juu ya lundo la majivu.
13 and if all congregation Israel to wander and to conceal word: thing from eye [the] assembly and to make: do one from all commandment LORD which not to make: do and be guilty
“‘Ikiwa jumuiya yote ya Israeli watatenda dhambi pasipo kukusudia na kufanya lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana, hata kama jumuiya haifahamu juu ya jambo hilo, wana hatia.
14 and to know [the] sin which to sin upon her and to present: bring [the] assembly bullock son: young animal cattle to/for sin: sin offering and to come (in): bring [obj] him to/for face: before tent meeting
Wanapotambua kuhusu dhambi waliyoitenda, lazima kusanyiko lilete fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi na kuikabidhi mbele ya Hema la Kukutania.
15 and to support old: elder [the] congregation [obj] hand their upon head [the] bullock to/for face: before LORD and to slaughter [obj] [the] bullock to/for face: before LORD
Wazee wa jumuiya wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo fahali aliye mbele za Bwana, naye fahali atachinjwa mbele za Bwana.
16 and to come (in): bring [the] priest [the] anointed from blood [the] bullock to(wards) tent meeting
Kisha kuhani aliyetiwa mafuta ataiingiza sehemu ya damu ya huyo fahali ndani ya Hema la Kukutania.
17 and to dip [the] priest finger his from [the] blood and to sprinkle seven beat to/for face: before LORD with face: before [the] curtain
Atachovya kidole chake kwenye damu na kuinyunyiza mara saba mbele za Bwana mbele ya hilo pazia.
18 and from [the] blood to give: put upon horn [the] altar which to/for face: before LORD which in/on/with tent meeting and [obj] all [the] blood to pour: pour to(wards) foundation altar [the] burnt offering which entrance tent meeting
Atatia sehemu ya hiyo damu juu ya pembe za madhabahu yaliyo mbele za Bwana katika Hema la Kukutania. Damu iliyobaki ataimwaga chini ya madhabahu ya kuteketezea sadaka, penye ingilio la Hema la Kukutania.
19 and [obj] all fat his to exalt from him and to offer: burn [the] altar [to]
Atayaondoa mafuta yote ya yule fahali na kuyateketeza juu ya madhabahu,
20 and to make: do to/for bullock like/as as which to make: do to/for bullock [the] sin: sin offering so to make: do to/for him and to atone upon them [the] priest and to forgive to/for them
naye atamfanyia fahali huyu kama alivyomfanyia yule fahali mwingine wa sadaka ya dhambi. Kwa njia hii kuhani atawafanyia watu upatanisho, nao watasamehewa.
21 and to come out: send [obj] [the] bullock to(wards) from outside to/for camp and to burn [obj] him like/as as which to burn [obj] [the] bullock [the] first sin: sin offering [the] assembly he/she/it
Kisha atamchukua yule fahali nje ya kambi na kumteketeza kama alivyomteketeza yule wa kwanza. Hii ni sadaka ya dhambi kwa ajili ya jumuiya.
22 which leader to sin and to make: do one from all commandment LORD God his which not to make: do in/on/with unintentionally and be guilty
“‘Wakati kiongozi ametenda dhambi bila kukusudia na kufanya yaliyokatazwa katika amri yoyote ya Bwana Mungu wake, ana hatia.
23 or to know to(wards) him sin his which to sin in/on/with her and to come (in): bring [obj] offering his he-goat goat male unblemished
Atakapofahamishwa dhambi aliyotenda, ni lazima alete mbuzi dume asiye na dosari kama sadaka yake.
24 and to support hand his upon head [the] he-goat and to slaughter [obj] him in/on/with place which to slaughter [obj] [the] burnt offering to/for face: before LORD sin: sin offering he/she/it
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha yule mbuzi na kumchinja mahali pale ambapo sadaka za kuteketezwa huchinjiwa mbele za Bwana. Hii ni sadaka ya dhambi.
25 and to take: take [the] priest from blood [the] sin: sin offering in/on/with finger his and to give: put upon horn altar [the] burnt offering and [obj] blood his to pour: pour to(wards) foundation altar [the] burnt offering
Kisha kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya dhambi kwa kidole chake na kuitia kwenye pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketeza, na kuimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu.
26 and [obj] all fat his to offer: burn [the] altar [to] like/as fat sacrifice [the] peace offering and to atone upon him [the] priest from sin his and to forgive to/for him
Atayateketeza mafuta yote juu ya madhabahu, kama alivyoteketeza mafuta ya sadaka ya amani. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho wa dhambi kwa ajili ya yule mtu, naye atasamehewa.
27 and if soul: person one to sin in/on/with unintentionally from people [the] land: soil in/on/with to make: do she one from commandment LORD which not to make: do and be guilty
“‘Kama mtu katika jumuiya ametenda dhambi pasipo kukusudia na kufanya lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana, yeye ana hatia.
28 or to know to(wards) him sin his which to sin and to come (in): bring offering his female goat goat unblemished female upon sin his which to sin
Atakapofahamishwa dhambi yake aliyoitenda, ni lazima alete mbuzi jike asiye na dosari kama sadaka yake kwa ajili ya dhambi aliyotenda.
29 and to support [obj] hand his upon head [the] sin: sin offering and to slaughter [obj] [the] sin: sin offering in/on/with place [the] burnt offering
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka ya dhambi na kumchinjia mahali pa kuteketezea sadaka.
30 and to take: take [the] priest from blood her in/on/with finger his and to give: put upon horn altar [the] burnt offering and [obj] all blood her to pour: pour to(wards) foundation [the] altar
Kisha kuhani atachukua sehemu ya ile damu kwa kidole chake na kuitia kwenye pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kuimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu.
31 and [obj] all fat her to turn aside: remove like/as as which to turn aside: remove fat from upon sacrifice [the] peace offering and to offer: burn [the] priest [the] altar [to] to/for aroma soothing to/for LORD and to atone upon him [the] priest and to forgive to/for him
Atayaondoa mafuta yote, kama vile mafuta yaondolewavyo kwenye sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake, naye atasamehewa.
32 and if lamb to come (in): bring offering his to/for sin: sin offering female unblemished to come (in): bring her
“‘Ikiwa ataleta mwana-kondoo kama sadaka yake ya dhambi, atamleta jike asiye na dosari.
33 and to support [obj] hand his upon head [the] sin: sin offering and to slaughter [obj] her to/for sin: sin offering in/on/with place which to slaughter [obj] [the] burnt offering
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha huyo mwana-kondoo na kumchinja kwa ajili ya sadaka ya dhambi mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa.
34 and to take: take [the] priest from blood [the] sin: sin offering in/on/with finger his and to give: put upon horn altar [the] burnt offering and [obj] all blood her to pour: pour to(wards) foundation [the] altar
Kisha kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya dhambi kwa kidole chake na kuitia juu ya pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa, na ile damu iliyobaki ataimwaga chini ya madhabahu.
35 and [obj] all fat her to turn aside: remove like/as as which to turn aside: remove fat [the] sheep from sacrifice [the] peace offering and to offer: burn [the] priest [obj] them [the] altar [to] upon food offering LORD and to atone upon him [the] priest upon sin his which to sin and to forgive to/for him
Ataondoa mafuta yote, kama vile mafuta yaondolewavyo kutoka kwenye mwana-kondoo wa sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya madhabahu juu ya zile sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi aliyoitenda, naye atasamehewa.

< Leviticus 4 >