< Judges 4 >
1 and to add: again son: descendant/people Israel to/for to make: do [the] bad: evil in/on/with eye: seeing LORD and Ehud to die
Baada ya Ehudi kufa, watu wa Israeli walifanya tena yaliyo mabaya machoni pa Bwana.
2 and to sell them LORD in/on/with hand: power Jabin king Canaan which to reign in/on/with Hazor and ruler army his Sisera and he/she/it to dwell in/on/with Harosheth (Harosheth)-hagoyim
Bwana akawatia mkononi mwa Yabini, mfalme wa Kanaani, aliyewala huko Hasori. Kamanda wa jeshi lake aitwaye Sisera, naye aliishi Harosheti ya Mataifa.
3 and to cry son: descendant/people Israel to(wards) LORD for nine hundred chariot iron to/for him and he/she/it to oppress [obj] son: descendant/people Israel in/on/with force twenty year
Wana wa Israeli wakamwomba Bwana awasaidie, kwa sababu Sisera alikuwa na magari ya chuma mia tisa na akawashinda wana wa Israeli kwa nguvu kwa miaka ishirini.
4 and Deborah woman: wife prophetess woman: wife Lappidoth he/she/it to judge [obj] Israel in/on/with time [the] he/she/it
Basi Debora, nabii wa kike (mke wa Lapidothi), alikuwa mwamuzi anayeongoza katika Israeli wakati huo.
5 and he/she/it to dwell underneath: under palm Deborah between [the] Ramah and between Bethel Bethel in/on/with mountain: hill country Ephraim and to ascend: rise to(wards) her son: descendant/people Israel to/for justice: judgement
Naye aliketi chini ya mtende wa Debora kati ya Rama na Betheli katika nchi ya mlima wa Efraimu, na watu wa Israeli walimwendea ili kutatua migogoro yao.
6 and to send: depart and to call: call to to/for Barak son: child Abinoam from Kedesh (Kedesh)-naphtali and to say to(wards) him not to command LORD God Israel to go: went and to draw in/on/with mountain: mount (Mount) Tabor and to take: take with you ten thousand man from son: descendant/people (Kedesh)-naphtali and from son: descendant/people Zebulun
Akamtuma Baraka mwana wa Abinoamu kutoka Kedeshi huko Naftali. Akamwambia, Bwana, Mungu wa Israeli, anakuamuru, Nenda katika mlima wa Tabori, uende pamoja nawe watu elfu kumi kutoka Naftali na Zabuloni.
7 and to draw to(wards) you to(wards) torrent: river Kishon [obj] Sisera ruler army Jabin and [obj] chariot his and [obj] crowd his and to give: give him in/on/with hand: power your
Nitamfukuza Sisera, jemadari wa jeshi la Yabini, akutane nawe karibu na mto Kishoni, pamoja na magari yake na jeshi lake, na nitakupa ushindi juu yake. '
8 and to say to(wards) her Barak if to go: went with me and to go: went and if not to go: went with me not to go: went
Baraka akamwambia, 'Ikiwa utakwenda nami, nitakwenda, lakini ikiwa huendi pamoja nami, sitaenda.'
9 and to say to go: went to go: went with you end for not to be beauty your upon [the] way: road which you(m. s.) to go: went for in/on/with hand: power woman to sell LORD [obj] Sisera and to arise: rise Deborah (and to go: went *L(abh)*) with Barak Kedesh [to]
Alisema, 'Nitakwenda nawe. Hata hivyo, njia unayoienda haitakupa heshima wewe, kwa kuwa Bwana atamuuza Sisera mkononi mwa mwanamke. Ndipo Debora akainuka, akaenda pamoja na Baraka Kedeshi.
10 and to cry out Barak [obj] Zebulun and [obj] Naphtali Kedesh [to] and to ascend: rise in/on/with foot his ten thousand man and to ascend: rise with him Deborah
Baraki akawaita wana wa Zebuloni na Naftali kusanyika Kedeshi. Watu elfu kumi walimfuata, na Debora akaenda pamoja naye.
11 and Heber [the] Kenite to separate from Kenite from son: descendant/people Hobab relative Moses and to stretch tent his till terebinth (in/on/with Zaanannim *Q(K)*) which with Kedesh
Heberi (Mkeni) alijitenganisha na Wakeni - walikuwa wazao wa Hobabu (mkwe wa Musa) - na akaweka hema yake mwaloni uliopo huko Saanaimu karibu na Kedesh.
12 and to tell to/for Sisera for to ascend: rise Barak son: child Abinoam mountain: mount (Mount) Tabor
Walipomwambia Sisera kwamba Baraka, mwana wa Abinoamu, alikuwa amekwenda mlima wa Tabori,
13 and to cry out Sisera [obj] all chariot his nine hundred chariot iron and [obj] all [the] people: soldiers which with him from Harosheth (Harosheth)-hagoyim to(wards) torrent: river Kishon
Sisera akawaita magari yake yote, magari ya farasi mia tisa, na askari wote waliokuwa pamoja naye, kutoka Haroshethi ya Mataifa mpaka Mto Kishoni.
14 and to say Deborah to(wards) Barak to arise: rise for this [the] day which to give: give LORD [obj] Sisera in/on/with hand: power your not LORD to come out: come to/for face: before your and to go down Barak from mountain: mount (Mount) Tabor and ten thousand man after him
Debora akamwambia Baraka, Nenda! Kwa maana hii ndiyo siku ambayo Bwana amekupa ushindi juu ya Sisera. Je! si Bwana anayekuongoza? Basi Baraka akashuka kutoka mlima wa Tabori na watu kumi elfu wakamfuata.
15 and to confuse LORD [obj] Sisera and [obj] all [the] chariot and [obj] all [the] camp to/for lip: edge sword to/for face: before Barak and to go down Sisera from upon [the] chariot and to flee in/on/with foot his
Bwana alifanya jeshi la Sisera kuchanganyikiwa, magari yake yote, na jeshi lake lote. Watu wa Baraka waliwashinda na Sisera akaanguka kutoka kwenye gari lake na kukimbia kwa miguu.
16 and Barak to pursue after [the] chariot and after [the] camp till Harosheth (Harosheth)-hagoyim and to fall: kill all camp Sisera to/for lip: edge sword not to remain till one
Lakini Baraka akayafuata magari na jeshi mpaka Haroshethi ya Mataifa, na jeshi lote la Sisera likauawa kwa upanga, wala hakuna mtu aliyeokoka.
17 and Sisera to flee in/on/with foot his to(wards) tent Jael (woman: wife *L(abh)*) Heber [the] Kenite for peace between Jabin king Hazor and between house: household Heber [the] Kenite
Lakini Sisera akakimbia kwa miguu mpaka hema ya Yaeli, mkewe Heberi Mkeni; kwa sababu kulikuwa na amani kati ya Yabini mfalme wa Hazori, na nyumba ya Heberi Mkeni.
18 and to come out: come Jael to/for to encounter: meet Sisera and to say to(wards) him to turn aside: turn aside [emph?] lord my to turn aside: turn aside [emph?] to(wards) me not to fear and to turn aside: turn aside to(wards) her [the] tent [to] and to cover him in/on/with rug
Jaeli akatoka kumlaki Sisera, akamwambia, karibu, bwana wangu; karibu kwangu, wala usiogope. Basi akakaribia kwake, akaingia hemani kwake, naye akamvika bushuti.
19 and to say to(wards) her to water: drink me please little water for to thirst and to open [obj] wineskin [the] milk and to water: drink him and to cover him
Akamwambia, Tafadhali nipe maji kidogo ninywe, kwa maana nina kiu. Alifungua mfuko wa ngozi ya maziwa akampa anywe, kisha akamfunika tena.
20 and to say to(wards) her to stand: stand entrance [the] tent and to be if man: anyone to come (in): come and to ask you and to say there here man: anyone and to say nothing
Akamwambia, “Simama mlangoni pa hema. Ikiwa mtu atakuja na kukuuliza, 'Je, kuna mtu hapa?', Sema 'Hapana'.”
21 and to take: take Jael woman: wife Heber [obj] peg [the] tent and to set: take [obj] [the] hammer in/on/with hand her and to come (in): come to(wards) him in/on/with secret and to blow [obj] [the] peg in/on/with temple his and to descend in/on/with land: soil and he/she/it to sleep and be faint and to die
Kisha Jaeli (mke wa Heberi) akachukua kigingi cha hema na nyundo mkononi mwake akamwendea kwa siri, kwa sababu alikuwa amelala usingizi mzito, naye akakitia kigingi cha hema upande wa kichwa chake akamchoma na kikapenya kushuka chini. Hivyo akafa.
22 and behold Barak to pursue [obj] Sisera and to come out: come Jael to/for to encounter: meet him and to say to/for him to go: come and to see: see you [obj] [the] man which you(m. s.) to seek and to come (in): come to(wards) her and behold Sisera to fall: kill to die and [the] peg in/on/with temple his
Baraka alipokuwa akimfuata Sisera, Jaeli alitoka kukutana naye akamwambia, “Njoo, nitakuonyesha mtu unayemtafuta.” Basi akaingia pamoja naye, tazama Sisera amekufa, na kigingi cha hema kando ya kichwa chake.
23 and be humble God in/on/with day [the] he/she/it [obj] Jabin king Canaan to/for face: before son: descendant/people Israel
Basi siku hiyo Mungu alimshinda Jabin, mfalme wa Kanaani, mbele ya watu wa Israeli.
24 and to go: continue hand: power son: descendant/people Israel to go: continue and severe upon Jabin king Canaan till which to cut: eliminate [obj] Jabin king Canaan
Uwezo wa watu wa Israeli ulikua na nguvu zaidi dhidi ya Jabin mfalme wa Kanaani, hata walipomwangamiza.