< Joshua 5 >

1 and to be like/as to hear: hear all king [the] Amorite which in/on/with side: beyond [the] Jordan sea: west [to] and all king [the] Canaanite which upon [the] sea [obj] which to wither LORD [obj] water [the] Jordan from face: before son: descendant/people Israel till (to pass they *Q(K)*) and to melt heart their and not to be in/on/with them still spirit from face: because son: descendant/people Israel
Basi wafalme wote wa Waamori magharibi ya Yordani na wafalme wote wa Kanaani waliokuwa kwenye pwani waliposikia jinsi Bwana alivyoukausha Mto Yordani mbele ya Waisraeli hata tulipokwisha kuvuka, mioyo yao ikayeyuka kwa hofu, wala hawakuwa na ujasiri kuwakabili Waisraeli.
2 in/on/with time [the] he/she/it to say LORD to(wards) Joshua to make to/for you sword rock and to return: again to circumcise [obj] son: descendant/people Israel second
Wakati huo Bwana akamwambia Yoshua, “Tengeneza visu vya mawe magumu sana na uwatahiri Waisraeli tena.”
3 and to make to/for him Joshua sword rock and to circumcise [obj] son: descendant/people Israel to(wards) Gibeath-(haaraloth) [the] (Gilgal)-haaraloth
Kwa hiyo Yoshua akatengeneza visu vya mawe magumu sana na kutahiri Waisraeli huko Gibeath-Haaralothi.
4 and this [the] word: because which to circumcise Joshua all [the] people [the] to come out: come from Egypt [the] male all human [the] battle to die in/on/with wilderness in/on/with way: journey in/on/with to come out: come they from Egypt
Hii ndiyo sababu ya Yoshua kufanya hivyo: Wanaume wote waliotoka Misri, wote wenye umri wa kwenda vitani, walikufa jangwani wakiwa njiani baada ya kuondoka Misri.
5 for to circumcise to be all [the] people [the] to come out: come and all [the] people [the] born in/on/with wilderness in/on/with way: journey in/on/with to come out: come they from Egypt not to circumcise
Watu wote waliotoka Misri walikuwa wametahiriwa, lakini watu wote waliozaliwa jangwani wakiwa safarini toka Misri walikuwa hawajatahiriwa.
6 for forty year to go: walk son: descendant/people Israel in/on/with wilderness till to finish all [the] nation human [the] battle [the] to come out: come from Egypt which not to hear: obey in/on/with voice LORD which to swear LORD to/for them to/for lest to see: see them [obj] [the] land: country/planet which to swear LORD to/for father their to/for to give: give to/for us land: country/planet to flow: flowing milk and honey
Waisraeli walitembea jangwani miaka arobaini mpaka wanaume wote wale waliokuwa na umri wa kwenda vitani wakati waliondoka Misri walipokwisha kufa, kwa kuwa hawakumtii Bwana. Kwa maana Bwana alikuwa amewaapia kuwa wasingeweza kuona nchi ambayo alikuwa amewaahidi baba zao katika kuapa kutupatia, nchi inayotiririka maziwa na asali.
7 and [obj] son: child their to arise: raise underneath: instead them [obj] them to circumcise Joshua for uncircumcised to be for not to circumcise [obj] them in/on/with way: journey
Kwa hiyo akawainua wana wao baada yao na hawa ndio hao ambao Yoshua aliwatahiri. Walikuwa hawajatahiriwa bado kwa sababu walikuwa safarini.
8 and to be like/as as which to finish all [the] nation to/for to circumcise and to dwell underneath: stand them in/on/with camp till to live they
Baada ya taifa lote kutahiriwa, waliendelea kukaa kambini mpaka walipokuwa wamepona.
9 and to say LORD to(wards) Joshua [the] day to roll [obj] reproach Egypt from upon you and to call: call by name [the] place [the] he/she/it Gilgal till [the] day: today [the] this
Bwana akamwambia Yoshua, “Leo nimeiondoa aibu ya Wamisri kutoka kwenu.” Basi mahali pale pakaitwa Gilgali hadi leo.
10 and to camp son: descendant/people Israel in/on/with Gilgal and to make: do [obj] [the] Passover in/on/with four ten day to/for month in/on/with evening in/on/with plain Jericho
Jioni ya siku ya kumi na nne ya mwezi, wakiwa kambini huko Gilgali katika tambarare za Yeriko, Waisraeli wakaadhimisha Pasaka.
11 and to eat from produce [the] land: country/planet from morrow [the] Passover unleavened bread and to roast in/on/with bone: same [the] day [the] this
Siku iliyofuata Pasaka, katika siku ile ile, wakala mazao ya nchi, mikate isiyotiwa chachu na nafaka za kukaanga.
12 and to cease [the] manna from morrow in/on/with to eat they from produce [the] land: country/planet and not to be still to/for son: descendant/people Israel manna and to eat from produce land: country/planet Canaan in/on/with year [the] he/she/it
Mana ilikoma siku iliyofuata baada ya Waisraeli kula chakula kilichotoka katika nchi; hapakuwa na mana tena kwa ajili ya Waisraeli, ila mwaka huo walikula mazao ya nchi ya Kanaani.
13 and to be in/on/with to be Joshua in/on/with Jericho and to lift: look eye his and to see: see and behold man to stand: stand to/for before him and sword his to draw in/on/with hand his and to go: went Joshua to(wards) him and to say to/for him to/for us you(m. s.) if to/for enemy our
Basi wakati Yoshua alipokuwa karibu na Yeriko, akainua macho, akaona mtu aliyesimama mbele yake, akiwa na upanga mkononi uliofutwa kwenye ala. Yoshua akamwendea na kumuuliza, “Je, wewe uko upande wetu au upande wa adui zetu?”
14 and to say not for I ruler army LORD now to come (in): come and to fall: fall Joshua to(wards) face his land: soil [to] and to bow and to say to/for him what? lord my to speak: speak to(wards) servant/slave his
Akajibu, “La, siko upande wowote, lakini mimi nimekuja nikiwa jemadari wa jeshi la Bwana.” Yoshua akaanguka kifudifudi hadi chini, akasujudu, akamuuliza, “Je, Bwana, una ujumbe gani kwa mtumishi wako?”
15 and to say ruler army LORD to(wards) Joshua to slip sandal your from upon foot your for [the] place which you(m. s.) to stand: stand upon him holiness he/she/it and to make: do Joshua so
Jemadari wa jeshi la Bwana akajibu, “Vua viatu vyako, kwa maana mahali hapa unaposimama ni patakatifu.” Naye Yoshua akafanya hivyo.

< Joshua 5 >