< Joshua 1 >
1 and to be after death Moses servant/slave LORD and to say LORD to(wards) Joshua son: child Nun to minister Moses to/for to say
Baada ya kifo cha Mose mtumishi wa Bwana, Bwana akamwambia Yoshua mwana wa Nuni, msaidizi wa Mose:
2 Moses servant/slave my to die and now to arise: rise to pass [obj] [the] Jordan [the] this you(m. s.) and all [the] people [the] this to(wards) [the] land: country/planet which I to give: give to/for them to/for son: descendant/people Israel
“Mtumishi wangu Mose amekufa. Sasa basi, wewe pamoja na watu wote hawa, jiandaeni kuvuka huu Mto Yordani kuingia nchi ambayo karibu nitawapa wana wa Israeli.
3 all place which to tread palm: sole foot your in/on/with him to/for you to give: give him like/as as which to speak: promise to(wards) Moses
Kila mahali nyayo za miguu yenu zitakapokanyaga nimewapa, kama vile nilivyomwahidi Mose.
4 from [the] wilderness and [the] Lebanon [the] this and till [the] river [the] Great (Sea) river Euphrates all land: country/planet [the] Hittite and till [the] sea [the] Great (Sea) entrance [the] sun to be border: area your
Nchi yenu itaenea kuanzia jangwa hili hadi Lebanoni, tena kuanzia mto mkubwa wa Frati, yaani nchi yote ya Wahiti, hadi Bahari ile Kubwa iliyoko upande wa magharibi.
5 not to stand man: anyone to/for face: before your all day life your like/as as which to be with Moses to be with you not to slacken you and not to leave: forsake you
Hakuna mtu yeyote atakayeweza kushindana na wewe siku zote za maisha yako. Kama vile nilivyokuwa pamoja na Mose, ndivyo nitakavyokuwa pamoja na wewe, sitakuacha wala sitakupungukia.
6 to strengthen: strengthen and to strengthen for you(m. s.) to inherit [obj] [the] people [the] this [obj] [the] land: country/planet which to swear to/for father their to/for to give: give to/for them
“Uwe hodari na shujaa, kwa sababu wewe ndiwe utakayewaongoza watu hawa kuirithi nchi niliyowaapia baba zao kuwapa.
7 except to strengthen: strengthen and to strengthen much to/for to keep: careful to/for to make: do like/as all [the] instruction which to command you Moses servant/slave my not to turn aside: turn aside from him right and left because be prudent in/on/with all which to go: went
Uwe hodari na uwe na ushujaa mwingi. Uwe na bidii kutii sheria yote aliyokupa Mose mtumishi wangu, usiiache kwa kugeuka kuelekea kuume au kushoto, ili upate kufanikiwa popote uendako.
8 not to remove scroll: book [the] instruction [the] this from lip your and to mutter in/on/with him by day and night because to keep: careful to/for to make: do like/as all [the] to write in/on/with him for then to prosper [obj] way: journey your and then be prudent
Usiache Kitabu hiki cha Sheria kiondoke kinywani mwako; yatafakari maneno yake usiku na mchana, ili upate kuwa mwangalifu kufanya kila kitu sawasawa na yote yaliyoandikwa ndani yake. Ndipo utakapofanikiwa na kisha utastawi.
9 not to command you to strengthen: strengthen and to strengthen not to tremble and not to to be dismayed for with you LORD God your in/on/with all which to go: went
Je, si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na shujaa. Usihofu wala usivunjike moyo, kwa kuwa Bwana Mungu wako atakuwa pamoja nawe kokote uendako.”
10 and to command Joshua [obj] official [the] people to/for to say
Ndipo Yoshua akawaagiza maafisa wa watu akisema,
11 to pass in/on/with entrails: among [the] camp and to command [obj] [the] people to/for to say to establish: prepare to/for you provision for in/on/with still three day you(m. p.) to pass [obj] [the] Jordan [the] this to/for to come (in): come to/for to possess: take [obj] [the] land: country/planet which LORD God your to give: give to/for you to/for to possess: take her
“Pitieni katika kambi yote mkawaambie watu, ‘Wekeni tayari mahitaji yenu. Siku tatu kuanzia sasa mtavuka hii Yordani ili kuingia na kuimiliki nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa iwe yenu wenyewe.’”
12 and to/for Reubenite and to/for Gad and to/for half tribe [the] Manasseh to say Joshua to/for to say
Lakini kwa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase, Yoshua akasema,
13 to remember [obj] [the] word which to command [obj] you Moses servant/slave LORD to/for to say LORD God your to rest to/for you and to give: give to/for you [obj] [the] land: country/planet [the] this
“Kumbukeni agizo lile Mose mtumishi wa Bwana alilowapa: ‘Bwana Mungu wenu anawapa ninyi raha, naye amewapa nchi hii.’
14 woman: wife your child your and livestock your to dwell in/on/with land: country/planet which to give: give to/for you Moses in/on/with side: beyond [the] Jordan and you(m. p.) to pass armed to/for face: before brother: compatriot your all mighty man [the] strength and to help [obj] them
Wake zenu, watoto wenu na mifugo yenu watakaa katika nchi ile Mose aliyowapa mashariki ya Yordani, lakini mashujaa wenu wote, wakiwa wamevikwa silaha kikamilifu lazima wavuke mbele ya ndugu zenu. Imewapasa kuwasaidia ndugu zenu hadi
15 till which to rest LORD to/for brother: compatriot your like/as you and to possess: take also they(masc.) [obj] [the] land: country/planet which LORD God your to give: give to/for them and to return: return to/for land: country/planet possession your and to possess: take [obj] her which to give: give to/for you Moses servant/slave LORD in/on/with side: beyond [the] Jordan east [the] sun
Bwana awape nao raha, kama alivyokwisha kufanya kwa ajili yenu hadi wao pia watakapokuwa wamemiliki nchi ile Bwana Mungu wenu anayowapa. Baada ya hilo, mwaweza kurudi na kukalia nchi yenu wenyewe, ambayo Mose mtumishi wa Bwana aliwapa mashariki mwa Yordani kuelekea linakochomoza jua.”
16 and to answer [obj] Joshua to/for to say all which to command us to make: do and to(wards) all which to send: depart us to go: went
Ndipo wakamjibu Yoshua, “Chochote ambacho umetuagiza tutafanya na popote utakapotutuma tutakwenda.
17 like/as all which to hear: obey to(wards) Moses so to hear: obey to(wards) you except to be LORD God your with you like/as as which to be with Moses
Kama vile tulivyomtii Mose kikamilifu, ndivyo tutakavyokutii wewe. Bwana Mungu wako na awe pamoja nawe tu kama vile alivyokuwa pamoja na Mose.
18 all man which to rebel [obj] lip: word your and not to hear: obey [obj] word your to/for all which to command him to die except to strengthen: strengthen and to strengthen
Yeyote atakayeasi neno lako na kuacha kuyatii maneno yako, au chochote utakachowaamuru, atauawa. Uwe imara na hodari tu!”