< Job 34 >

1 and to answer Elihu and to say
Kisha Elihu akasema:
2 to hear: hear wise speech my and to know to listen to/for me
“Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima; nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.
3 for ear speech to test and palate to perceive to/for to eat
Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula.
4 justice to choose to/for us to know between: among us what? pleasant
Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa, nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.
5 for to say Job to justify and God to turn aside: remove justice my
“Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia, lakini Mungu ameninyima haki yangu.
6 upon justice my to lie be incurable arrow my without transgression
Ingawa niko sawa, ninaonekana mwongo; nami ingawa sina kosa, kidonda changu hakiponi.’
7 who? great man like/as Job to drink derision like/as water
Ni mtu gani aliye kama Ayubu, anywaye dharau kama maji?
8 and to journey to/for company with to work evil: wickedness and to/for to go: walk with human wickedness
Ashirikianaye na watenda mabaya na kuchangamana na watu waovu.
9 for to say not be useful great man in/on/with to accept he with God
Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote anapojitahidi kumpendeza Mungu.’
10 to/for so human heart to hear: hear to/for me forbid to/for God from wickedness and Almighty from injustice
“Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu. Kamwe Mungu hatendi uovu, Mwenyezi hafanyi kosa.
11 for work man to complete to/for him and like/as way man to find him
Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda; huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
12 also truly God not be wicked and Almighty not to pervert justice
Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa, kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
13 who? to reckon: overseer upon him land: country/planet [to] and who? to set: put world all her
Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia? Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
14 if to set: make to(wards) him heart his spirit his and breath his to(wards) him to gather
Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
15 to die all flesh together and man upon dust to return: return
wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.
16 and if understanding to hear: hear [emph?] this to listen [emph?] to/for voice: message speech my
“Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili; sikilizeni hili nisemalo.
17 also to hate justice to saddle/tie and if: surely no righteous mighty be wicked
Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala? Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?
18 to say to/for king Belial: worthless wicked to(wards) noble
Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’ nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’
19 which not to lift: kindness face: kindness ruler and not to recognize rich to/for face: before poor for deed: work hand his all their
yeye asiyependelea wakuu, wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?
20 moment to die and middle night to shake people and to pass and to turn aside: remove mighty: strong not in/on/with hand
Wanakufa ghafula, usiku wa manane; watu wanatikiswa nao hupita; wenye nguvu huondolewa bila mkono wa mwanadamu.
21 for eye his upon way: conduct man: anyone and all step his to see: see
“Macho yake yanazitazama njia za wanadamu; anaona kila hatua yao.
22 nothing darkness and nothing shadow to/for to hide there to work evil: wickedness
Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa, ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
23 for not upon man to set: consider still to/for to go: went to(wards) God in/on/with justice: judgement
Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana, ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
24 to shatter mighty not search and to stand: stand another underneath: instead them
Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi na kuwaweka wengine mahali pao.
25 to/for so to recognize work their and to overturn night and to crush
Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote, huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
26 underneath: because of wicked to slap them in/on/with place to see: see
Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
27 which upon so to turn aside: turn aside from after him and all way: conduct his not be prudent
kwa sababu wameacha kumfuata Mungu, nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
28 to/for to come (in): come upon him cry poor and cry afflicted to hear: hear
Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake, hivyo akasikia kilio cha wahitaji.
29 and he/she/it to quiet and who? be wicked and to hide face and who? to see him and upon nation and upon man unitedness
Lakini kama akinyamaza kimya, ni nani awezaye kumhukumu? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumwona? Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,
30 from to reign man profane from snare people
ili kumzuia mtu mwovu kutawala, au wale ambao huwategea watu mitego.
31 for to(wards) God to say to lift: bear not to destroy
“Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
32 beside to see you(m. s.) to show me if injustice to work not to add: again
Nifundishe nisichoweza kuona; kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
33 from from with you to complete her for to reject for you(m. s.) to choose and not I and what? to know to speak: promise
Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako, wakati wewe umekataa kutubu? Yakupasa wewe uamue, wala si mimi; sasa niambie lile ulijualo.
34 human heart to say to/for me and great man wise to hear: hear to/for me
“Wanadamu wenye ufahamu husema, wenye hekima wanaonisikia huniambia,
35 Job not in/on/with knowledge to speak: speak and word his not in/on/with be prudent
‘Ayubu huongea bila maarifa; maneno yake hayana busara.’
36 oh that! to test Job till perpetuity upon turn in/on/with human evil: wickedness
Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho, kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
37 for to add upon sin his transgression between us to slap and to multiply word his to/for God
Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”

< Job 34 >