< Job 30 >

1 and now to laugh upon me little from me to/for day: old which to reject father their to/for to set: make with dog flock my
“Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
2 also strength hand their to/for what? to/for me upon them to perish vigor
Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
3 in/on/with poverty and in/on/with famine solitary [the] to gnaw dryness last night devastation and desolation
Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
4 [the] to pluck mallow upon bush and root broom food their
Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
5 from midst to drive out: drive out to shout upon them like/as thief
Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
6 in/on/with dreadful torrent: river to/for to dwell hole dust and rock
Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
7 between bush to bray underneath: under nettle to attach
Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
8 son: type of foolish also son: child without name to whip from [the] land: country/planet
Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
9 and now music their to be and to be to/for them to/for speech
“Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
10 to abhor me to remove from me and from face my not to withhold spittle
Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
11 for (cord my *Q(K)*) to open and to afflict me and bridle from face my to send: depart
Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
12 upon right brood to arise: rise foot my to send: depart and to build upon me way calamity their
Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
13 to break path my to/for desire my to gain not to help to/for them
Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
14 like/as breach broad: wide to come underneath: stand devastation to roll
Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
15 to overturn upon me terror to pursue like/as spirit: breath honor my and like/as cloud to pass salvation my
Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
16 and now upon me to pour: pour soul my to grasp me day affliction
“Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
17 night bone my to dig from upon me and to gnaw me not to lie down: sleep [emph?]
Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
18 in/on/with many strength to search clothing my like/as lip: edge tunic my to gird me
Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
19 to shoot me to/for clay and to liken like/as dust and ashes
Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
20 to cry to(wards) you and not to answer me to stand: stand and to understand in/on/with me
“Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
21 to overturn to/for cruel to/for me in/on/with strength hand: power your to hate me
Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
22 to lift: raise me to(wards) spirit: breath to ride me and to melt me (wisdom *Q(K)*)
Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
23 for to know death to return: return me and house: home meeting: time appointed to/for all alive
Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
24 surely not in/on/with ruin to send: reach hand if: surely yes in/on/with disaster his to/for them cry
“Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
25 if: surely no not to weep to/for severe day be grieved soul my to/for needy
Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
26 for good to await and to come (in): come bad: evil and to wait: hope to/for light and to come (in): come darkness
Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
27 belly my to boil and not to silence: stationary to meet me day affliction
Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
28 be dark to go: walk in/on/with not heat to arise: establish in/on/with assembly to cry
Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
29 brother: male-sibling to be to/for jackal and neighbor to/for daughter ostrich
Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
30 skin my be black from upon me and bone my to scorch from drought
Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
31 and to be to/for mourning lyre my and pipe my to/for voice to weep
Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.

< Job 30 >