< Jeremiah 28 >

1 and to be in/on/with year [the] he/she/it in/on/with first: beginning kingdom Zedekiah king Judah (in/on/with year *Q(K)*) [the] fourth in/on/with month [the] fifth to say to(wards) me Hananiah son: child Azzur [the] prophet which from Gibeon in/on/with house: temple LORD to/for eye: before(the eyes) [the] priest and all [the] people to/for to say
Katika mwezi wa tano wa mwaka ule ule, yaani mwaka wa nne, mwanzoni mwa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, nabii Hanania mwana wa Azuri, ambaye alitoka Gibeoni, akaniambia katika nyumba ya Bwana mbele ya makuhani na watu wote:
2 thus to say LORD Hosts God Israel to/for to say to break [obj] yoke king Babylon
“Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli asemalo: ‘Nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.
3 in/on/with still year day I to return: return to(wards) [the] place [the] this [obj] all article/utensil house: temple LORD which to take: take Nebuchadnezzar king Babylon from [the] place [the] this and to come (in): bring them Babylon
Katika muda wa miaka miwili nitavirudisha mahali hapa vyombo vyote vya nyumba ya Bwana ambavyo Nebukadneza mfalme wa Babeli aliviondoa kutoka hapa na kuvipeleka Babeli.
4 and [obj] Jeconiah son: child Jehoiakim king Judah and [obj] all captivity Judah [the] to come (in): come Babylon [to] I to return: return to(wards) [the] place [the] this utterance LORD for to break [obj] yoke king Babylon
Pia nitamrudisha mahali hapa Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, pamoja na wote waliohamishwa kutoka Yuda ambao walikwenda Babeli,’ asema Bwana, ‘kwa kuwa nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.’”
5 and to say Jeremiah [the] prophet to(wards) Hananiah [the] prophet to/for eye: before(the eyes) [the] priest and to/for eye: before(the eyes) all [the] people [the] to stand: stand in/on/with house: temple LORD
Ndipo nabii Yeremia akamjibu nabii Hanania mbele ya makuhani na watu wote waliokuwa wamesimama ndani ya nyumba ya Bwana.
6 and to say Jeremiah [the] prophet amen so to make: do LORD to arise: establish LORD [obj] word your which to prophesy to/for to return: return article/utensil house: temple LORD and all [the] captivity from Babylon to(wards) [the] place [the] this
Akasema, “Amen! Bwana na afanye hivyo! Bwana na ayatimize maneno uliyotoa unabii kwa kuvirudisha mahali hapa kutoka Babeli vyombo vya nyumba ya Bwana pamoja na wote waliohamishwa.
7 surely to hear: hear please [the] word [the] this which I to speak: speak in/on/with ear: hearing your and in/on/with ear: hearing all [the] people
Hata hivyo, nisikilize nikuambie yale nitakayoyasema masikioni mwako na masikioni mwa watu hawa wote:
8 [the] prophet which to be to/for face: before my and to/for face: before your from [the] forever: antiquity and to prophesy to(wards) land: country/planet many and upon kingdom great: large to/for battle and to/for distress: harm and to/for pestilence
Tangu mwanzo, manabii waliokutangulia wewe na mimi walitabiri vita, maafa na tauni dhidi ya nchi nyingi na falme kubwa.
9 [the] prophet which to prophesy to/for peace in/on/with to come (in): come word [the] prophet to know [the] prophet which to send: depart him LORD in/on/with truth: true
Lakini nabii atakayetabiri amani atatambuliwa kuwa kweli ametumwa na Bwana ikiwa unabii wake utatimia.”
10 and to take: take Hananiah [the] prophet [obj] [the] yoke from upon neck Jeremiah [the] prophet and to break him
Kisha nabii Hanania akaiondoa nira iliyokuwa shingoni mwa Yeremia na kuivunja,
11 and to say Hananiah to/for eye: before(the eyes) all [the] people to/for to say thus to say LORD thus to break [obj] yoke Nebuchadnezzar king Babylon in/on/with still year day (from upon *L(abh)*) neck all [the] nation and to go: went Jeremiah [the] prophet to/for way: journey his
naye akasema mbele ya watu wote, “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Vivi hivi ndivyo nitakavyoivunja nira ya Nebukadneza mfalme wa Babeli kutoka kwenye shingo za mataifa katika muda huu wa miaka miwili.’” Alipofanya hivi, nabii Yeremia akaondoka zake.
12 and to be word LORD to(wards) Jeremiah after to break Hananiah [the] prophet [obj] [the] yoke from upon neck Jeremiah [the] prophet to/for to say
Kitambo kidogo baada ya nabii Hanania kuivunja nira kutoka shingo ya nabii Yeremia, neno la Bwana likamjia Yeremia:
13 to go: went and to say to(wards) Hananiah to/for to say thus to say LORD yoke tree: wood to break and to make underneath: instead them yoke iron
“Nenda ukamwambie Hanania, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Umevunja nira ya mti, lakini badala yake utapata nira ya chuma.
14 for thus to say LORD Hosts God Israel yoke iron to give: put upon neck all [the] nation [the] these to/for to serve [obj] Nebuchadnezzar king Babylon and to serve him and also [obj] living thing [the] land: country to give: give to/for him
Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Nitaweka nira ya chuma kwenye shingo za mataifa haya yote ili kufanya yamtumikie Nebukadneza mfalme wa Babeli, nao watamtumikia. Nitampa kutawala hata wanyama wa mwituni.’”
15 and to say Jeremiah [the] prophet to(wards) Hananiah [the] prophet to hear: hear please Hananiah not to send: depart you LORD and you(m. s.) to trust [obj] [the] people [the] this upon deception
Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania, “Sikiliza Hanania! Bwana hajakutuma, lakini wewe umelishawishi taifa hili kuamini uongo.
16 to/for so thus to say LORD look! I to send: depart you from upon face: surface [the] land: planet [the] year you(m. s.) to die for revolt to speak: speak to(wards) LORD
Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: ‘Hivi karibuni nitakuondoa kutoka juu ya uso wa dunia. Mwaka huu utakufa, kwa sababu umetangaza uasi dhidi ya Bwana.’”
17 and to die Hananiah [the] prophet in/on/with year [the] he/she/it in/on/with month [the] seventh
Katika mwezi wa saba wa mwaka ule ule, nabii Hanania akafa.

< Jeremiah 28 >