< Jeremiah 16 >

1 and to be word LORD to(wards) me to/for to say
Kisha neno la Bwana likanijia:
2 not to take: marry to/for you woman: wife and not to be to/for you son: child and daughter in/on/with place [the] this
“Kamwe usioe na kuwa na wana wala binti mahali hapa.”
3 for thus to say LORD upon [the] son: child and upon [the] daughter [the] born in/on/with place [the] this and upon mother their [the] to beget [obj] them and upon father their [the] to beget [obj] them in/on/with land: country/planet [the] this
Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana kuhusu wana na binti wazaliwao katika nchi hii, na kuhusu wale wanawake ambao ni mama zao, na wale wanaume ambao ni baba zao:
4 death disease to die not to mourn and not to bury to/for dung upon face: surface [the] land: soil to be and in/on/with sword and in/on/with famine to end: destroy and to be carcass their to/for food to/for bird [the] heaven and to/for animal [the] land: soil
“Watakufa kwa magonjwa ya kufisha. Hawataombolezewa wala kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyosambaa juu ya ardhi. Watakufa kwa upanga na kwa njaa, nazo maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani, na cha wanyama wa nchi.”
5 for thus to say LORD not to come (in): come house: home mourning and not to go: went to/for to mourn and not to wander to/for them for to gather [obj] peace my from with [the] people [the] this utterance LORD [obj] [the] kindness and [obj] [the] compassion
Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: “Usiingie katika nyumba ambayo kuna chakula cha matanga, usiende kuwaombolezea wala kuwahurumia, kwa sababu nimeziondoa baraka zangu, upendo wangu na huruma zangu kutoka kwa watu hawa,” asema Bwana.
6 and to die great: large and small in/on/with land: country/planet [the] this not to bury and not to mourn to/for them and not to cut and not to make bald to/for them
“Wakubwa na wadogo watakufa katika nchi hii. Hawatazikwa wala kuombolezewa, na hakuna atakayejikatakata au kunyoa nywele za kichwa chake kwa ajili yao.
7 and not to divide to/for them upon mourning to/for to be sorry: comfort him upon to die and not to water: drink [obj] them cup consolation upon father his and upon mother his
Hakuna yeyote atakayewapa chakula ili kuwafariji wale waombolezao kwa ajili ya wale waliokufa, hata akiwa amefiwa na baba au mama, wala hakuna yeyote atakayewapa kinywaji ili kuwafariji.
8 and house: home feast not to come (in): come to/for to dwell with them to/for to eat and to/for to drink
“Usiingie katika nyumba ambayo kuna karamu, na kuketi humo ili kula na kunywa.
9 for thus to say LORD Hosts God Israel look! I to cease from [the] place [the] this to/for eye your and in/on/with day your voice rejoicing and voice joy voice son-in-law and voice daughter-in-law: bride
Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliye Mungu wa Israeli: ‘Mbele ya macho yako na katika siku zako, nitakomesha sauti zote za shangwe na za furaha, na pia sauti za bibi arusi na bwana arusi mahali hapa.’
10 and to be for to tell to/for people [the] this [obj] all [the] word [the] these and to say to(wards) you upon what? to speak: promise LORD upon us [obj] all [the] distress: evil [the] great: large [the] this and what? iniquity: crime our and what? sin our which to sin to/for LORD God our
“Utakapowaambia watu hawa mambo haya yote na wakakuuliza, ‘Kwa nini Bwana ameamuru maafa makubwa kama haya dhidi yetu? Tumefanya kosa gani? Tumetenda dhambi gani dhidi ya Bwana, Mungu wetu?’
11 and to say to(wards) them upon which to leave: forsake father your [obj] me utterance LORD and to go: follow after God another and to serve: minister them and to bow to/for them and [obj] me to leave: forsake and [obj] instruction my not to keep: obey
Basi waambie, ‘Ni kwa sababu baba zenu waliniacha mimi, wakafuata miungu mingine ili kuitumikia na kuiabudu. Waliniacha mimi na hawakuishika sheria yangu,’ asema Bwana.
12 and you(m. p.) be evil to/for to make: do from father your and look! you to go: follow man: anyone after stubbornness heart his [the] bad: evil to/for lest to hear: obey to(wards) me
‘Lakini ninyi mmetenda uovu zaidi kuliko baba zenu. Tazama jinsi ambavyo kila mmoja wenu anafuata ukaidi wa moyo wake mbaya, badala ya kunitii mimi.
13 and to cast [obj] you from upon [the] land: country/planet [the] this upon [the] land: country/planet which not to know you(m. p.) and father your and to serve: minister there [obj] God another by day and night which not to give: give to/for you favor
Kwa hiyo nitawaondoa katika nchi hii na kuwatupa katika nchi ambayo ninyi wala baba zenu hamkuijua, nako huko mtaitumikia miungu mingine usiku na mchana, kwa maana sitawapa fadhili zangu huko.’
14 to/for so behold day to come (in): come utterance LORD and not to say still alive LORD which to ascend: establish [obj] son: descendant/people Israel from land: country/planet Egypt
“Hata hivyo, siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati ambapo watu hawatasema tena, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewapandisha Waisraeli kutoka Misri,’
15 that if: except if: except alive LORD which to ascend: establish [obj] son: descendant/people Israel from land: country/planet north and from all [the] land: country/planet which to banish them there [to] and to return: return them upon land: soil their which to give: give to/for father their
bali watasema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wana wa Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote alizokuwa amewafukuzia.’ Maana nitawarudisha katika nchi niliyowapa baba zao.
16 look! I to send: depart (to/for fisher *Q(K)*) many utterance LORD and to fish them and after so to send: depart to/for many hunter and to hunt them from upon all mountain: mount and from upon all hill and from cleft [the] crag
“Lakini sasa nitawaagiza wavuvi wengi,” asema Bwana, “nao watawavua. Baada ya hilo, nitawaagizia wawindaji wengi, nao watawawinda kwenye kila mlima na kilima, na katika nyufa za miamba.
17 for eye my upon all way: conduct their not to hide from to/for face of my and not to treasure iniquity: crime their from before eye my
Macho yangu yanaziona njia zao zote, hazikufichika kwangu, wala dhambi yao haikusitirika.
18 and to complete first second iniquity: crime their and sin their upon to profane/begin: profane they [obj] land: country/planet my in/on/with carcass abomination their and abomination their to fill [obj] inheritance my
Nitawalipiza maradufu kwa ajili ya uovu wao na dhambi yao, kwa sababu wameinajisi nchi yangu kwa maumbo yasiyo na uhai ya vinyago vyao vibaya, na kuujaza urithi wangu na sanamu za kuchukiza.”
19 LORD strength my and security my and refuge my in/on/with day distress to(wards) you nation to come (in): come from end land: country/planet and to say surely deception to inherit father our vanity and nothing in/on/with them to gain
Ee Bwana, nguvu zangu na ngome yangu, kimbilio langu wakati wa taabu, kwako mataifa yatakujia kutoka miisho ya dunia na kusema, “Baba zetu hawakuwa na chochote zaidi ya miungu ya uongo, sanamu zisizofaa kitu ambazo hazikuwafaidia lolote.
20 to make to/for him man God and they(masc.) not God
Je, watu hujitengenezea miungu yao wenyewe? Naam, lakini hao si miungu!”
21 to/for so look! I to know them in/on/with beat [the] this to know them [obj] hand: power my and [obj] might my and to know for name my LORD
“Kwa hiyo nitawafundisha: wakati huu nitawafundisha nguvu zangu na uwezo wangu. Ndipo watakapojua kuwa Jina langu ndimi Bwana.

< Jeremiah 16 >