< Isaiah 9 >

1 for not gloom to/for which constraint to/for her like/as time [the] first: previous to lighten land: country/planet [to] Zebulun and land: country/planet [to] Naphtali and [the] last to honor: honour way: journey [the] sea side: beyond [the] Jordan Galilee [the] nation
Hata hivyo, hapatakuwepo huzuni tena kwa wale waliokuwa katika dhiki. Wakati uliopita aliidhili nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, lakini katika siku zijazo ataiheshimu Galilaya ya Mataifa, karibu na njia ya bahari, kando ya Yordani:
2 [the] people [the] to go: walk in/on/with darkness to see: see light great: large to dwell in/on/with land: country/planet shadow light to shine upon them
Watu wanaotembea katika giza wameona nuru kuu, wale wanaoishi katika nchi ya uvuli wa mauti, nuru imewazukia.
3 to multiply [the] nation (to/for him *Q(K)*) to magnify [the] joy to rejoice to/for face: before your like/as joy in/on/with harvest like/as as which to rejoice in/on/with to divide they spoil
Umelikuza taifa, na kuzidisha furaha yao, wanafurahia mbele zako, kama watu wanavyofurahia wakati wa mavuno, kama watu wafurahivyo wagawanyapo nyara.
4 for [obj] yoke burden his and [obj] tribe: rod shoulder his tribe: staff [the] to oppress in/on/with him to to be dismayed like/as day Midian
Kama vile siku ya kushindwa kwa Wamidiani, umevunja nira iliyowalemea, ile gongo mabegani mwao na fimbo yake yeye aliyewaonea.
5 for all boot to tread in/on/with quaking and mantle to roll in/on/with blood and to be to/for fire fuel fire
Kila kiatu cha askari kilichotumiwa vitani, na kila vazi lililovingirishwa katika damu vitawekwa kwa ajili ya kuchomwa, vitakuwa kuni za kuwasha moto.
6 for youth to beget to/for us son: child to give: give to/for us and to be [the] dominion upon shoulder his and to call: call by name his wonder to advise God mighty man father perpetuity ruler peace
Kwa maana, kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, tumepewa mtoto mwanaume, nao utawala utakuwa mabegani mwake. Naye ataitwa Mshauri wa Ajabu, Mungu Mwenye Nguvu, Baba wa Milele, Mfalme wa Amani.
7 (to/for abundance *Q(K)*) [the] dominion and to/for peace nothing end upon throne David and upon kingdom his to/for to establish: establish [obj] her and to/for to support her in/on/with justice and in/on/with righteousness from now and till forever: enduring jealousy LORD Hosts to make: do this
Kuongezeka kwa utawala wake na amani hakutakuwa na mwisho. Atatawala katika kiti cha enzi cha Daudi na juu ya ufalme wake, akiuthibitisha na kuutegemeza kwa haki na kwa adili, tangu wakati huo na hata milele. Wivu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote utatimiza haya.
8 word to send: depart Lord in/on/with Jacob and to fall: fall in/on/with Israel
Bwana ametuma ujumbe dhidi ya Yakobo, utamwangukia Israeli.
9 and to know [the] people all his Ephraim and to dwell Samaria in/on/with pride and in/on/with greatness heart to/for to say
Watu wote watajua hili: Efraimu na wakazi wa Samaria, wanaosema kwa kiburi na majivuno ya mioyo,
10 brick to fall: fall and cutting to build sycamore to cut down/off and cedar to pass
“Matofali yameanguka chini, lakini tutajenga tena kwa mawe yaliyochongwa, mitini imeangushwa, lakini tutapanda mierezi badala yake.”
11 and to exalt LORD [obj] enemy Rezin upon him and [obj] enemy his to cover
Lakini Bwana amemtia nguvu adui wa Resini dhidi yao na kuchochea watesi wao.
12 Syria from front: east and Philistine from back and to eat [obj] Israel in/on/with all lip in/on/with all this not to return: turn back face: anger his and still hand his to stretch
Waashuru kutoka upande wa mashariki na Wafilisti kutoka upande wa magharibi wameila Israeli kwa kinywa kilichopanuliwa. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
13 and [the] people not to return: turn back till [the] to smite him and [obj] LORD Hosts not to seek
Lakini watu hawajamrudia yeye aliyewapiga, wala hawajamtafuta Bwana Mwenye Nguvu Zote.
14 and to cut: cut LORD from Israel head and tail branch and bulrush day one
Kwa hiyo Bwana atakatilia mbali kutoka Israeli kichwa na mkia, tawi la mtende na tete katika siku moja.
15 old: elder and to lift: kindness face: kindness he/she/it [the] head: leader and prophet to show deception he/she/it [the] tail
Wazee na watu mashuhuri ndio vichwa, nao manabii wanaofundisha uongo ndio mkia.
16 and to be to bless [the] people [the] this to go astray and to bless his to swallow up
Wale wanaowaongoza watu hawa wanawapotosha, nao wale wanaoongozwa wamepotoka.
17 upon so upon youth his not to rejoice Lord and [obj] orphan his and [obj] widow his not to have compassion for all his profane and be evil and all lip to speak: speak folly in/on/with all this not to return: turn back face: anger his and still hand his to stretch
Kwa hiyo Bwana hatawafurahia vijana, wala hatawahurumia yatima na wajane, kwa kuwa kila mmoja wao hamchi Mungu, nao ni waovu, na kila kinywa kinanena upotovu. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
18 for to burn: burn like/as fire wickedness thorn and thornbush to eat and to kindle in/on/with thicket [the] wood and to roll up majesty smoke
Hakika uovu huwaka kama moto; huteketeza michongoma na miiba, huwasha moto vichaka vya msituni, hujiviringisha kuelekea juu kama nguzo ya moshi.
19 in/on/with fury LORD Hosts to burn land: country/planet and to be [the] people like/as fuel fire man: anyone to(wards) brother: compatriot his not to spare
Kwa hasira ya Bwana Mwenye Nguvu Zote nchi itachomwa kwa moto, nao watu watakuwa kuni za kuchochea moto. Hakuna mtu atakayemhurumia ndugu yake.
20 and to cut upon right and be hungry and to eat upon left and not to satisfy man: anyone flesh arm his to eat
Upande wa kuume watakuwa wakitafuna, lakini bado wataona njaa; upande wa kushoto watakuwa wakila, lakini hawatashiba. Kila mmoja atajilisha kwa nyama ya mtoto wake mwenyewe:
21 Manasseh [obj] Ephraim and Ephraim [obj] Manasseh together they(masc.) upon Judah in/on/with all this not to return: turn back face: anger his and still hand his to stretch
Manase atamla Efraimu, naye Efraimu atamla Manase; nao pamoja watakuwa kinyume na Yuda. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.

< Isaiah 9 >