< Isaiah 61 >
1 spirit Lord YHWH/God upon me because to anoint LORD [obj] me to/for to bear tidings poor to send: depart me to/for to saddle/tie to/for to break heart to/for to call: call out to/for to take captive liberty and to/for to bind opening opening
Roho wa Bwana Mwenyezi yu juu yangu, kwa sababu Bwana amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao;
2 to/for to call: call out year acceptance to/for LORD and day vengeance to/for God our to/for to be sorry: comfort all mourning
kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa, na siku ya kisasi ya Mungu wetu, kuwafariji wote waombolezao,
3 to/for to set: put to/for mourning Zion to/for to give: give to/for them headdress underneath: instead ashes oil rejoicing underneath: instead mourning mantle praise underneath: instead spirit faint and to call: call by to/for them terebinth [the] righteousness plantation LORD to/for to beautify
na kuwapa mahitaji wale wanaohuzunika katika Sayuni, ili kuwapa taji ya uzuri badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho ya kukata tamaa. Nao wataitwa mialoni ya haki, pando la Bwana, ili kuonyesha utukufu wake.
4 and to build desolation forever: antiquity be desolate: destroyed first: previous to arise: establish and to renew city desolation be desolate: destroyed generation and generation
Watajenga upya magofu ya zamani na kupatengeneza mahali palipoachwa ukiwa zamani; watafanya upya miji iliyoharibiwa, iliyoachwa ukiwa kwa vizazi vingi.
5 and to stand: stand be a stranger and to pasture flock your and son: type of foreign farmer your and to tend vineyards your
Wageni watayachunga makundi yenu, wageni watafanya kazi katika mashamba yenu, na kutunza mashamba yenu ya mizabibu.
6 and you(m. p.) priest LORD to call: call by to minister God our to say to/for you strength: rich nation to eat and in/on/with glory their to exchange
Nanyi mtaitwa makuhani wa Bwana, mtaitwa watumishi wa Mungu wetu. Mtakula utajiri wa mataifa, nanyi katika utajiri wao mtajisifu.
7 underneath: instead shame your second and shame to sing portion their to/for so in/on/with land: country/planet their second to possess: possess joy forever: enduring to be to/for them
Badala ya aibu yao watu wangu watapokea sehemu maradufu, na badala ya fedheha watafurahia katika urithi wao; hivyo watarithi sehemu maradufu katika nchi yao, nayo furaha ya milele itakuwa yao.
8 for I LORD to love: lover justice to hate robbery in/on/with injustice and to give: give wages their in/on/with truth: faithful and covenant forever: enduring to cut: make(covenant) to/for them
“Kwa maana Mimi, Bwana, napenda haki, na ninachukia unyangʼanyi na uovu. Katika uaminifu wangu nitawapa malipo yao na kufanya agano la milele nao.
9 and to know in/on/with nation seed: children their and offspring their in/on/with midst [the] people all to see: see them to recognize them for they(masc.) seed: children to bless LORD
Wazao wao watajulikana miongoni mwa mataifa, na uzao wao miongoni mwa kabila za watu. Wale wote watakaowaona watatambua kuwa ni taifa ambalo Bwana amelibariki.”
10 to rejoice to rejoice in/on/with LORD to rejoice soul my in/on/with God my for to clothe me garment salvation robe righteousness to cover me like/as son-in-law to minister headdress and like/as daughter-in-law: bride to adorn article/utensil her
Ninafurahia sana katika Bwana, nafsi yangu inashangilia katika Mungu wangu. Kwa maana amenivika mavazi ya wokovu, na kunipamba kwa joho la haki, kama vile bwana arusi apambavyo kichwa chake kama kuhani, na kama bibi arusi ajipambavyo kwa vito vyake vya thamani.
11 for like/as land: country/planet to come out: produce branch her and like/as garden sowing her to spring so Lord YHWH/God to spring righteousness and praise before all [the] nation
Kwa maana kama vile ardhi ifanyavyo chipukizi kuota, na bustani isababishavyo mbegu kuota, ndivyo Bwana Mwenyezi atafanya haki na sifa zichipuke mbele ya mataifa yote.