< Isaiah 57 >

1 [the] righteous to perish and nothing man: anyone to set: put upon heart and human kindness to gather in/on/with nothing to understand for from face: before [the] distress: harm to gather [the] righteous
Mwenye haki hupotea, wala hakuna hata mmoja awazaye hilo moyoni mwake; watu wanaomcha Mungu huondolewa, wala hakuna hata mmoja anayeelewa kuwa wenye haki wameondolewa ili wasipatikane na maovu.
2 to come (in): come peace to rest upon bed their to go: walk straightforward his
Wale waendao kwa unyofu huwa na amani; hupata pumziko walalapo mautini.
3 and you(m. p.) to present: come here/thus son: child to divine seed: children to commit adultery and to fornicate
“Lakini ninyi: Njooni hapa, ninyi wana wa wachawi, ninyi wazao wa wazinzi na makahaba!
4 upon who? to delight upon who? to enlarge lip to prolong tongue not you(m. p.) youth transgression seed: children deception
Mnamdhihaki nani? Ni nani mnayemcheka kwa dharau, na kumtolea ndimi zenu? Je, ninyi si watoto wa waasi, uzao wa waongo?
5 [the] to warm in/on/with terebinth underneath: under all tree luxuriant to slaughter [the] youth in/on/with torrent: valley underneath: under cleft [the] crag
Mnawaka tamaa katikati ya mialoni na chini ya kila mti uliotanda matawi; mnawatoa kafara watoto wenu kwenye mabonde na chini ya majabali yenye mianya.
6 in/on/with smooth torrent: river portion your they(masc.) they(masc.) allotted your also to/for them to pour: pour drink offering to ascend: establish offering upon these to be sorry: relent
“Sanamu zilizo katikati ya mawe laini ya mabondeni ndizo fungu lenu; hizo ndizo sehemu yenu. Naam, kwa hizo mmemimina sadaka za vinywaji, na kutoa sadaka za nafaka. Katika haya yote, niendelee kuona huruma?
7 upon mountain: mount high and to lift: raise to set: make bed your also there to ascend: rise to/for to sacrifice sacrifice
Umeweka kitanda chako juu kwenye kilima kirefu kilichoinuka, huko ulikwenda kutoa dhabihu zako.
8 and after [the] door and [the] doorpost to set: make memorial your for from with me to reveal: uncover and to ascend: rise to enlarge bed your and to cut: make(covenant) to/for you from them to love: lover bed their hand: penis to see
Nyuma ya milango yako na miimo yako umeweka alama zako za kipagani. Kwa kuniacha mimi, ulifunua kitanda chako, umepanda juu yake na kukipanua sana; ulifanya patano na wale ambao unapenda vitanda vyao, nawe uliangalia uchi wao.
9 and to travel to/for king in/on/with oil and to multiply perfumery your and to send: depart (envoy your *L(abh)*) till from distant and to abase till hell: Sheol (Sheol h7585)
Ulikwenda kwa Moleki ukiwa na mafuta ya zeituni, na ukaongeza manukato yako. Ukawatuma wajumbe wako mbali sana, ukashuka kwenye kaburi lenyewe! (Sheol h7585)
10 in/on/with abundance way: journey your be weary/toil not to say to despair living thing hand: power your to find upon so not be weak: weak
Ulikuwa umechoshwa na njia zako zote, lakini hukusema, ‘Hakuna tumaini.’ Ulipata uhuisho wa nguvu zako, kwa sababu hiyo hukuzimia.
11 and [obj] who? be anxious and to fear: revere for to lie and [obj] me not to remember not to set: put upon heart your not I be silent and from forever: antiquity and [obj] me not to fear: revere
“Ni nani uliyemhofu hivyo na kumwogopa hata ukawa mwongo kwangu, wala hukunikumbuka au kutafakari hili moyoni mwako? Si ni kwa sababu nimekuwa kimya muda mrefu hata huniogopi?
12 I to tell righteousness your and [obj] deed your and not to gain you
Nitaifunua haki yako na matendo yako, nayo hayatakufaidi.
13 in/on/with to cry out you to rescue you collection your and [obj] all their to lift: bear spirit: breath to take: take vanity and [the] to seek refuge in/on/with me to inherit land: country/planet and to possess: possess mountain: mount holiness my
Utakapolia kwa kuhitaji msaada, sanamu zako ulizojikusanyia na zikuokoe! Upepo utazipeperusha zote, pumzi peke yake itazipeperusha, Lakini mtu atakayenifanya kimbilio lake, atairithi nchi na kuumiliki mlima wangu mtakatifu.”
14 and to say to build to build to turn way: road to exalt stumbling from way: road people my
Tena itasemwa: “Jengeni, jengeni, itengenezeni njia! Ondoeni vikwazo katika njia ya watu wangu.”
15 for thus to say to exalt and to lift: exalt to dwell perpetuity and holy name his height and holy to dwell and with contrite and low spirit to/for to live spirit low and to/for to live heart to crush
Kwa maana hili ndilo asemalo Aliye juu, yeye aliyeinuliwa sana, yeye aishiye milele, ambaye jina lake ni Mtakatifu: “Ninaishi mimi mahali palipoinuka na patakatifu, lakini pia pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na mwenye roho ya unyenyekevu, ili kuzihuisha roho za wanyenyekevu na kuihuisha mioyo yao waliotubu.
16 for not to/for forever: enduring to contend and not to/for perpetuity be angry for spirit from to/for face: before my to enfeeble and breath I to make
Sitaendelea kulaumu milele, wala sitakasirika siku zote, kwa kuwa roho ya mwanadamu ingezimia mbele zangu: yaani pumzi ya mwanadamu niliyemuumba.
17 in/on/with iniquity: crime unjust-gain his be angry and to smite him to hide and be angry and to go: went turning back in/on/with way: conduct heart his
Nilighadhibika na tamaa yake ya dhambi; nilimwadhibu, nikauficha uso wangu kwa hasira, na bado aliendelea katika njia zake za tamaa.
18 way: conduct his to see: see and to heal him and to lead him and to complete comfort to/for him and to/for mourning his
Nimeziona njia zake, lakini nitamponya, nitamwongoza na kumrudishia upya faraja,
19 to create (fruit *Q(K)*) lips peace peace to/for distant and to/for near to say LORD and to heal him
nikiumba sifa midomoni ya waombolezaji katika Israeli. Amani, amani, kwa wale walio mbali na kwa wale walio karibu,” asema Bwana. “Nami nitawaponya.”
20 and [the] wicked like/as sea to drive out: drive out for to quiet not be able and to drive out: drive out water his mire and mud
Bali waovu ni kama bahari ichafukayo, ambayo haiwezi kutulia, mawimbi yake hutupa takataka na matope.
21 nothing peace to say God my to/for wicked
Mungu wangu asema, “Hakuna amani kwa waovu.”

< Isaiah 57 >