< Isaiah 43 >

1 and now thus to say LORD to create you Jacob and to form: formed you Israel not to fear for to redeem: redeem you to call: call to in/on/with name your to/for me you(m. s.)
Lakini sasa hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyekuumba, ee Yakobo, yeye aliyekuhuluku, ee Israeli: “Usiogope kwa maana nimekukomboa, nimekuita wewe kwa jina lako, wewe u wangu.
2 for to pass in/on/with water with you I and in/on/with river not to overflow you for to go: walk in/at/by fire not to burn and flame not to burn: burn in/on/with you
Unapopita kwenye maji makuu, nitakuwa pamoja nawe, unapopita katika mito ya maji, hayatakugharikisha. Utakapopita katika moto, hutaungua, miali ya moto haitakuunguza.
3 for I LORD God your holy Israel to save you to give: give ransom your Egypt Cush and Seba underneath: instead you
Kwa kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wako. Ninaitoa Misri kuwa fidia yako, Kushi na Seba badala yako.
4 from whence be precious in/on/with eye my to honor: honour and I to love: lover you and to give: give man underneath: instead you and people underneath: instead soul: life your
Kwa kuwa wewe ni wa thamani na wa kuheshimiwa machoni pangu, nami kwa kuwa ninakupenda, nitatoa watu badala yako na mataifa badala ya maisha yako.
5 not to fear for with you I from east to come (in): bring seed: children your and from west to gather you
Usiogope, kwa kuwa mimi nipo pamoja nawe, nitawaleta watoto wako kutoka mashariki, na kukukusanya kutoka magharibi.
6 to say to/for north to give: give and to/for south not to restrain to come (in): bring son: child my from distant and daughter my from end [the] land: country/planet
Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’ nayo kusini, ‘Usiwazuie.’ Walete wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia:
7 all [the] to call: call by in/on/with name my and to/for glory my to create him to form: formed him also to make him
kila mmoja ambaye ameitwa kwa Jina langu, niliyemuumba kwa utukufu wangu, niliyemhuluku na kumfanya.”
8 to come out: send people blind and eye there and deaf and ear to/for them
Uwaongoze wale wenye macho lakini hawaoni, wenye masikio lakini hawasikii.
9 all [the] nation to gather together and to gather people who? in/on/with them to tell this and first: previous to hear: proclaim us to give: give witness their and to justify and to hear: hear and to say truth: true
Mataifa yote yanakutanika pamoja, na makabila yanakusanyika. Ni nani miongoni mwao aliyetangulia kutuambia haya, na kututangazia mambo yaliyopita? Walete mashahidi wao ili kuwathibitisha kuwa walikuwa sahihi, ili wengine waweze kusikia, waseme, “Ni kweli.”
10 you(m. p.) witness my utterance LORD and servant/slave my which to choose because to know and be faithful to/for me and to understand for I he/she/it to/for face: before my not to form: formed god and after me not to be
“Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “na mtumishi wangu niliyemchagua, ili mpate kunijua na kuniamini, na kutambua kwamba Mimi ndiye. Kabla yangu hakuna mungu aliyefanyizwa, wala hatakuwepo mwingine baada yangu.
11 I I LORD and nothing from beside me to save
Mimi, naam mimi, ndimi Bwana, zaidi yangu hakuna mwokozi.
12 I to tell and to save and to hear: proclaim and nothing in/on/with you be a stranger and you(m. p.) witness my utterance LORD and I God
Nimedhihirisha, kuokoa na kutangaza: Mimi, wala si mungu mgeni katikati yenu. Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “kwamba Mimi ndimi Mungu.
13 also from day: today I he/she/it and nothing from hand: power my to rescue to work and who? to return: turn back her
Naam, tangu siku za kale, Mimi ndiye. Hakuna hata mmoja awezaye kuokoa kutoka mkononi wangu. Mimi ninapotenda, ni nani awezaye kutangua?”
14 thus to say LORD to redeem: redeem your holy Israel because you to send: depart Babylon [to] and to go down fleeing all their and Chaldea in/on/with fleet cry their
Hili ndilo Bwana asemalo, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa ajili yenu nitatumana Babeli na kuwaleta Wakaldayo wote kama wakimbizi, katika meli walizozionea fahari.
15 I LORD holy your to create Israel king your
Mimi ndimi Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wako, Muumba wa Israeli, Mfalme wako.”
16 thus to say LORD [the] to give: make in/on/with sea way: journey and in/on/with water strong path
Hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyefanya njia baharini, mahali pa kupita kwenye maji mengi,
17 [the] to come out: send chariot and horse strength: soldiers and mighty together to lie down: lay down not to arise: rise to put out like/as flax to quench
aliyeyakokota magari ya vita na farasi, jeshi pamoja na askari wa msaada, nao wakalala huko, wala hawatainuka tena kamwe, wakakomeshwa, na wakazimika kama utambi:
18 not to remember first: previous and eastern: older not to understand
“Msiyakumbuke mambo yaliyopita, wala msiyatafakari mambo ya zamani.
19 look! I to make: do new now to spring not to know her also to set: make in/on/with wilderness way: road in/on/with wilderness river
Tazama, nitafanya jambo jipya! Sasa litachipuka, je, hamtalitambua? Nitafanya njia jangwani na vijito vya maji katika nchi kame.
20 to honor: honour me living thing [the] land: wildlife jackal and daughter ostrich for to give: give in/on/with wilderness water river in/on/with wilderness to/for to water: drink people my chosen my
Wanyama wa mwituni wataniheshimu, mbweha na bundi, kwa sababu ninawapatia maji jangwani, na vijito katika nchi kame, ili kuwapa watu wangu maji, wale niliowachagua,
21 people this to form: formed to/for me praise my to recount
watu wale niliowaumba kwa ajili yangu, ili wapate kutangaza sifa zangu.
22 and not [obj] me to call: call to Jacob for be weary/toil in/on/with me Israel
“Hata hivyo hukuniita mimi, ee Yakobo, hujajitaabisha kwa ajili yangu, ee Israeli.
23 not to come (in): bring to/for me sheep burnt offering your and sacrifice your not to honor: honour me not to serve: burden you in/on/with offering and not be weary/toil you in/on/with frankincense
Hujaniletea kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa dhabihu zako. Sikukulemea kwa sadaka za nafaka wala kukuchosha kwa kuhitaji uvumba.
24 not to buy to/for me in/on/with silver: money branch: stem and fat sacrifice your not to quench me surely to serve: burden me in/on/with sin your be weary/toil me in/on/with iniquity: crime your
Hukuninunulia uvumba wowote wenye manukato, wala hukunipa kwa ukarimu mafuta ya wanyama wa dhabihu zako. Lakini umenilemea kwa dhambi zako, na kunitaabisha kwa makosa yako.
25 I I he/she/it to wipe transgression your because me and sin your not to remember
“Mimi, naam mimi, ndimi nizifutaye dhambi zako, kwa ajili yangu mwenyewe, wala sizikumbuki dhambi zako tena.
26 to remember me to judge unitedness to recount you(m. s.) because to justify
Tafakari mambo yaliyopita, njoo na tuhojiane, leta shauri lako uweze kupewa haki yako.
27 father your [the] first to sin and to mock you to transgress in/on/with me
Baba yako wa kwanza alitenda dhambi, wasemaji wako wameasi dhidi yangu.
28 and to profane/begin: profane ruler holiness and to give: give to/for devoted thing Jacob and Israel to/for reviling
Kwa hiyo nitawaaibisha wakuu wa Hekalu lako, nami nitamtoa Yakobo aangamizwe, na Israeli adhihakiwe.

< Isaiah 43 >