< Isaiah 36 >
1 and to be in/on/with four ten year to/for king Hezekiah to ascend: rise Sennacherib king Assyria upon all city Judah [the] to gather/restrain/fortify and to capture them
Katika mwaka wa kumi na nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote ya Yuda yenye ngome na kuiteka.
2 and to send: depart king Assyria [obj] Rabshakeh Rabshakeh from Lachish Jerusalem [to] to(wards) [the] king Hezekiah in/on/with strength: soldiers heavy and to stand: stand in/on/with conduit [the] pool [the] high in/on/with highway Field (of the Launderer) Washer's
Kisha mfalme wa Ashuru akamtuma jemadari wa jeshi pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi hadi kwa Mfalme Hezekia huko Yerusalemu. Jemadari wa jeshi akasimama kwenye mfereji wa Bwawa la Juu, lililojengwa katika barabara iendayo kwenye Uwanja wa Dobi.
3 and to come out: come to(wards) him Eliakim son: child Hilkiah which upon [the] house: temple and Shebna [the] secretary and Joah son: child Asaph [the] to remember
Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi wakamwendea.
4 and to say to(wards) them Rabshakeh Rabshakeh to say please to(wards) Hezekiah thus to say [the] king [the] great: large king Assyria what? [the] trust [the] this which to trust
Jemadari wa jeshi akawaambia, “Mwambieni Hezekia, “‘Hili ndilo asemalo mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru: Ni wapi unapoweka hili tumaini lako?
5 to say surely word lip: words counsel and might to/for battle now upon who? to trust for to rebel in/on/with me
Unasema mnayo mikakati na nguvu za kijeshi, lakini unasema maneno matupu tu. Je, wewe unamtegemea nani, hata ukaniasi mimi?
6 behold to trust upon staff [the] branch: stem [the] to crush [the] this upon Egypt which to support man: anyone upon him and to come (in): come in/on/with palm his and to pierce her so Pharaoh king Egypt to/for all [the] to trust upon him
Tazama sasa, unaitegemea Misri, fimbo ile ya mwanzi uliopasuka, ambayo huuchoma na kuujeruhi mkono wa mtu akiiegemea! Hivyo ndivyo alivyo Farao mfalme wa Misri, kwa wote wanaomtegemea.
7 and for to say to(wards) me to(wards) LORD God our to trust not he/she/it which to turn aside: remove Hezekiah [obj] high place his and [obj] altar his and to say to/for Judah and to/for Jerusalem to/for face: before [the] altar [the] this to bow
Nawe kama ukiniambia, “Tunamtumainia Bwana Mungu wetu”: je, siyo yeye ambaye Hezekia aliondoa mahali pake pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu zake, akiwaambia Yuda na Yerusalemu, “Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu haya”?
8 and now to pledge please with lord my [the] king Assyria and to give: give to/for you thousand horse if be able to/for to give: put to/for you to ride upon them
“‘Njooni sasa, fanyeni mapatano na bwana wangu, mfalme wa Ashuru: Nitakupa farasi elfu mbili, kama unaweza kuwapandisha waendesha farasi juu yao!
9 and how? to return: turn back [obj] face governor one servant/slave lord my [the] small and to trust to/for you upon Egypt to/for chariot and to/for horseman
Utawezaje kumzuia hata afisa mmoja aliye mdogo kati ya maafisa wa bwana wangu, ijapo unategemea Misri kwa magari ya vita na wapanda farasi?
10 and now from beside LORD to ascend: rise upon [the] land: country/planet [the] this to/for to ruin her LORD to say to(wards) me to ascend: rise to(wards) [the] land: country/planet [the] this and to ruin her
Zaidi ya hayo, je, nimekuja kushambulia na kuangamiza nchi hii bila Bwana? Bwana mwenyewe ndiye aliniambia niishambulie nchi hii na kuiangamiza.’”
11 and to say Eliakim and Shebna and Joah to(wards) Rabshakeh Rabshakeh to speak: speak please to(wards) servant/slave your Aramaic for to hear: understand we and not to speak: speak to(wards) us Judahite in/on/with ear: hearing [the] people which upon [the] wall
Ndipo Eliakimu, Shebna na Yoa wakamwambia yule jemadari wa jeshi, “Tafadhali zungumza na watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaifahamu. Usiseme nasi kwa Kiebrania watu walioko juu ya ukuta wakiwa wanasikia.”
12 and to say Rabshakeh Rabshakeh to(wards) lord your and to(wards) you to send: depart me lord my to/for to speak: speak [obj] [the] word [the] these not upon [the] human [the] to dwell upon [the] wall to/for to eat [obj] (filth their *Q(K)*) and to/for to drink [obj] (water foot their *Q(K)*) with you
Lakini yule jemadari wa jeshi akajibu, “Je, bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Je, hakunituma pia kwa watu walioketi ukutani, ambao, kama ninyi, itawabidi kula mavi yao na kunywa mikojo yao wenyewe?”
13 and to stand: stand Rabshakeh Rabshakeh and to call: call out in/on/with voice great: large Judahite and to say to hear: hear [obj] word [the] king [the] great: large king Assyria
Kisha yule jemadari wa jeshi akasimama na kuita kwa lugha ya Kiebrania, akasema: “Sikieni maneno ya mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru!
14 thus to say [the] king not to deceive to/for you Hezekiah for not be able to/for to rescue [obj] you
Hili ndilo asemalo mfalme: Msikubali Hezekia awadanganye. Hawezi kuwaokoa!
15 and not to trust [obj] you Hezekiah to(wards) LORD to/for to say to rescue to rescue us LORD not to give: give [the] city [the] this in/on/with hand: power king Assyria
Msikubali Hezekia awashawishi kumtumaini Bwana kwa kuwaambia, ‘Hakika Bwana atatuokoa. Mji huu hautaangukia mikononi mwa mfalme wa Ashuru.’
16 not to hear: hear to(wards) Hezekiah for thus to say [the] king Assyria to make with me blessing and to come out: come to(wards) me and to eat man: anyone vine his and man: anyone fig his and to drink man: anyone water pit his
“Msimsikilize Hezekia. Hili ndilo mfalme wa Ashuru asemalo: Fanyeni amani nami na mje kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwa mzabibu wake na mtini wake mwenyewe, na kunywa maji kutoka kisima chake mwenyewe,
17 till to come (in): come I and to take: take [obj] you to(wards) land: country/planet like/as land: country/planet your land: country/planet grain and new wine land: country/planet food: bread and vineyard
mpaka nije nikawapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na ya mashamba ya mizabibu.
18 lest to incite [obj] you Hezekiah to/for to say LORD to rescue us to rescue God [the] nation man: anyone [obj] land: country/planet his from hand: power king Assyria
“Msikubali Hezekia awapotoshe asemapo, ‘Bwana atatuokoa.’ Je, yuko mungu wa taifa lolote aliyewahi kuokoa nchi yake kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru?
19 where? God Hamath and Arpad where? God Sepharvaim and for to rescue [obj] Samaria from hand: power my
Iko wapi miungu ya Hamathi na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu? Je, imeokoa Samaria kutoka mkononi mwangu?
20 who? in/on/with all God [the] land: country/planet [the] these which to rescue [obj] land: country/planet their from hand: power my for to rescue LORD [obj] Jerusalem from hand: power my
Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya nchi hizi ameweza kuokoa nchi yake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Bwana aiokoe Yerusalemu mkononi mwangu?”
21 and be quiet and not to answer [obj] him word for commandment [the] king he/she/it to/for to say not to answer him
Lakini wale watu wakakaa kimya, wala hawakujibu lolote, kwa kuwa mfalme alikuwa amewaamuru, “Msimjibu lolote.”
22 and to come (in): come Eliakim son: child Hilkiah which upon [the] house: temple and Shebna [the] secretary and Joah son: child Asaph [the] to remember to(wards) Hezekiah to tear garment and to tell to/for him [obj] word Rabshakeh Rabshakeh
Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna katibu, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wakamwendea Hezekia, nguo zao zikiwa zimeraruliwa, na kumwambia yale jemadari wa jeshi aliyoyasema.