< Isaiah 25 >

1 LORD God my you(m. s.) to exalt you to give thanks name your for to make: do wonder counsel from distant faithfulness faithfulness
Ee Bwana, wewe ni Mungu wangu, nitakutukuza na kulisifu jina lako, kwa maana katika ukamilifu wa uaminifu umetenda mambo ya ajabu, mambo yaliyokusudiwa tangu zamani.
2 for to set: make from city to/for heap town to gather/restrain/fortify to/for ruin citadel: fortress be a stranger from city to/for forever: enduring not to build
Umeufanya mji kuwa lundo la kifusi, mji wenye ngome kuwa magofu, ngome imara ya wageni kuwa si mji tena, wala hautajengwa tena kamwe.
3 upon so to honor: honour you people strong town nation ruthless to fear you
Kwa hiyo mataifa yenye nguvu yatakuheshimu, miji ya mataifa katili itakuheshimu wewe.
4 for to be security to/for poor security to/for needy in/on/with distress to/for him refuge from storm shadow from drought for spirit: breath ruthless like/as storm wall
Umekuwa kimbilio la watu maskini, kimbilio la mhitaji katika taabu yake, hifadhi wakati wa dhoruba na kivuli wakati wa hari. Kwa maana pumzi ya wakatili ni kama dhoruba ipigayo ukuta
5 like/as drought in/on/with dryness roar be a stranger be humble drought in/on/with shadow cloud song ruthless to afflict
na kama joto la jangwani. Wewe wanyamazisha makelele ya wageni; kama vile hari ipunguzwavyo na kivuli cha wingu, ndivyo wimbo wa wakatili unyamazishwavyo.
6 and to make LORD Hosts to/for all [the] people in/on/with mountain: mount [the] this feast oil feast dreg oil be marrow dreg to refine
Juu ya mlima huu Bwana Mwenye Nguvu Zote ataandaa karamu ya vinono kwa mataifa yote, karamu ya mvinyo wa zamani, nyama nzuri sana na divai zilizo bora sana.
7 and to swallow up in/on/with mountain: mount [the] this face: surface [the] covering [the] to wrap upon all [the] people and [the] veil [the] to weave upon all [the] nation
Juu ya mlima huu ataharibu sitara ihifadhiyo mataifa yote, kile kifuniko kifunikacho mataifa yote,
8 to swallow up [the] death to/for perpetuity and to wipe Lord YHWH/God tears from upon all face and reproach people his to turn aside: remove from upon all [the] land: country/planet for LORD to speak: speak
yeye atameza mauti milele. Bwana Mwenyezi atafuta machozi katika nyuso zote; ataondoa aibu ya watu wake duniani kote. Bwana amesema hili.
9 and to say in/on/with day [the] he/she/it behold God our this to await to/for him and to save us this LORD to await to/for him to rejoice and to rejoice in/on/with salvation his
Katika siku ile watasema, “Hakika huyu ndiye Mungu wetu; tulimtumaini, naye akatuokoa. Huyu ndiye Bwana, tuliyemtumaini; sisi tushangilie na kufurahia katika wokovu wake.”
10 for to rest hand: power LORD in/on/with mountain: mount [the] this and to tread Moab underneath: stand him like/as to tread straw (in/at/by *Q(K)*) dunghill
Mkono wa Bwana utatulia juu ya mlima huu, bali Moabu atakanyagwa chini kama majani makavu yakanyagwavyo kwenye shimo la mbolea.
11 and to spread hand his in/on/with entrails: among his like/as as which to spread [the] to swim to/for to swim and to abase pride his with skill hand his
Watakunjua mikono yao katikati yake, kama vile mwogeleaji akunjuavyo mikono yake ili aogelee. Mungu atashusha kiburi chao licha ya ujanja wa mikono yao.
12 and fortification high refuge wall your to bow to abase to touch to/for land: soil till dust
Atabomoa kuta ndefu za maboma yako na kuziangusha chini, atazishusha chini ardhini, mpaka mavumbini kabisa.

< Isaiah 25 >