< Genesis 32 >

1 and Jacob to go: went to/for way: journey his and to fall on in/on/with him messenger: angel God
Yakobo pia akaondoka akaenda zake, nao malaika wa Mungu wakakutana naye.
2 and to say Jacob like/as as which to see: see them camp God this and to call: call by name [the] place [the] he/she/it Mahanaim
Yakobo alipowaona, akasema, “Hii ni kambi ya Mungu!” Kwa hiyo akapaita mahali pale Mahanaimu.
3 and to send: depart Jacob messenger to/for face: before his to(wards) Esau brother: male-sibling his land: country/planet [to] Seir land: country Edom
Yakobo akatuma wajumbe kumtangulia kwa Esau ndugu yake huko Seiri, katika nchi ya Edomu.
4 and to command [obj] them to/for to say thus to say [emph?] to/for lord my to/for Esau thus to say servant/slave your Jacob with Laban to sojourn and to delay till now
Akawaagiza akisema: “Hili ndilo mtakalomwambia bwana wangu Esau: ‘Mtumishi wako Yakobo anasema, nimekuwa nikiishi pamoja na Labani na nimekuwako huko mpaka sasa.
5 and to be to/for me cattle and donkey flock and servant/slave and maidservant and to send: depart [emph?] to/for to tell to/for lord my to/for to find favor in/on/with eye: seeing your
Ninao ngʼombe na punda, kondoo na mbuzi, watumishi wa kiume na wa kike. Sasa ninatuma ujumbe huu kwa bwana wangu, ili nipate kibali machoni pako.’”
6 and to return: return [the] messenger to(wards) Jacob to/for to say to come (in): come to(wards) brother: male-sibling your to(wards) Esau and also to go: come to/for to encounter: meet you and four hundred man with him
Wajumbe waliporudi kwa Yakobo, wakamwambia, “Tulikwenda kuonana na ndugu yako Esau, naye sasa anakuja kukulaki akifuatana na wanaume 400.”
7 and to fear Jacob much and be distressed to/for him and to divide [obj] [the] people which with him and [obj] [the] flock and [obj] [the] cattle and [the] camel to/for two camp
Kwa hofu kuu na huzuni, Yakobo akagawanya watu aliokuwa nao katika makundi mawili, pia akagawanya makundi ya kondoo na mbuzi, na vilevile ngʼombe na ngamia.
8 and to say if to come (in): come Esau to(wards) [the] camp [the] one and to smite him and to be [the] camp [the] to remain to/for survivor
Yakobo alifikiri, “Kama Esau akija na kushambulia kundi moja, kundi lililobaki litaweza likanusurika.”
9 and to say Jacob God father my Abraham and God father my Isaac LORD [the] to say to(wards) me to return: return to/for land: country/planet your and to/for relatives your and be good with you
Ndipo Yakobo akaomba, “Ee Mungu wa baba yangu Abrahamu, Mungu wa baba yangu Isaki, Ee Bwana, ambaye uliniambia, ‘Rudi katika nchi yako na jamaa yako, nami nitakufanya ustawi,’
10 be small from all [the] kindness and from all [the] truth: faithful which to make: do with servant/slave your for in/on/with rod my to pass [obj] [the] Jordan [the] this and now to be to/for two camp
mimi sistahili fadhili na uaminifu wako wote ulionitendea mimi mtumishi wako. Nilikuwa na fimbo tu mkononi mwangu nilipovuka mto huu wa Yordani, lakini sasa ninayo makundi mawili.
11 to rescue me please from hand: power brother: male-sibling my from hand: power Esau for afraid I [obj] him lest to come (in): come and to smite me mother upon son: child
Nakuomba, uniokoe na mkono wa ndugu yangu Esau, kwa maana ninaogopa kuwa atakuja kunishambulia, pia mama pamoja na watoto wao.
12 and you(m. s.) to say be good be good with you and to set: make [obj] seed: children your like/as sand [the] sea which not to recount from abundance
Lakini umeshasema, ‘Hakika nitakufanya ustawi na kuufanya uzao wako kuwa mwingi kama mchanga wa baharini ambao hauwezi kuhesabika!’”
13 and to lodge there in/on/with night [the] he/she/it and to take: take from [the] to come (in): bring in/on/with hand: to his offering: gift to/for Esau brother: male-sibling his
Akalala pale usiku ule, miongoni mwa vitu alivyokuwa navyo, akachagua zawadi kwa ajili ya Esau ndugu yake:
14 goat hundred and male goat twenty ewe hundred and ram twenty
Mbuzi waume ishirini na mbuzi wake 200, kondoo dume ishirini na kondoo wake 200.
15 camel to suckle and son: young animal their thirty heifer forty and bullock ten she-ass twenty and colt ten
Ngamia wake thelathini pamoja na ndama zao, ngʼombe wake arobaini na mafahali kumi, punda wake ishirini na punda waume kumi.
16 and to give: give in/on/with hand: to servant/slave his flock flock to/for alone him and to say to(wards) servant/slave his to pass to/for face: before my and space to set: put between flock and between flock
Akaviweka chini ya uangalizi wa watumishi wake, kila kundi peke yake na kuwaambia, “Nitangulieni na kuacha nafasi kati ya makundi.”
17 and to command [obj] [the] first to/for to say for to meet you Esau brother: male-sibling my and to ask you to/for to say to/for who? you(m. s.) and where? to go: went and to/for who? these to/for face: before your
Akamwagiza yule aliyetangulia kuwa, “Ndugu yangu Esau atakapokutana nawe na kukuuliza, ‘Wewe ni wa nani? Unakwenda wapi? Wanyama hawa wote mbele yako ni mali ya nani?’
18 and to say to/for servant/slave your to/for Jacob offering: gift he/she/it to send: depart to/for lord my to/for Esau and behold also he/she/it after us
Ndipo utakaposema, ‘Ni mali ya mtumishi wako Yakobo. Ni zawadi ambazo zimetumwa kwa bwana wangu Esau, naye anakuja nyuma yetu.’”
19 and to command also [obj] [the] second also [obj] [the] third also [obj] all [the] to go: follow after [the] flock to/for to say like/as Chronicles [the] this to speak: speak [emph?] to(wards) Esau in/on/with to find you [obj] him
Akamwagiza pia yule mtumishi wa kundi la pili, la tatu na yale mengine yote yaliyofuata akiwaambia, “Mtamwambia Esau maneno hayo hayo mtakapokutana naye.
20 and to say also behold servant/slave your Jacob after us for to say to atone face of his in/on/with offering: gift [the] to go: went to/for face: before my and after so to see: see face his perhaps to lift: kindness face: kindness my
Hakikisheni mmesema, ‘Mtumishi wako Yakobo anakuja nyuma yetu.’” Kwa kuwa alifikiri, “Nitaweza kumtuliza kwa zawadi hizi ninazotanguliza, hatimaye, nitakapomwona, huenda atanikubali.”
21 and to pass [the] offering: gift upon face: before his and he/she/it to lodge in/on/with night [the] he/she/it in/on/with camp
Kwa hiyo zawadi za Yakobo zilitangulia mbele yake, lakini yeye mwenyewe alilala kambini usiku ule.
22 and to arise: rise in/on/with night he/she/it and to take: take [obj] two woman: wife his and [obj] two maidservant his and [obj] one ten youth his and to pass [obj] ford Jabbok
Usiku ule Yakobo akaamka akawachukua wake zake wawili, watumishi wake wawili wa kike na wanawe kumi na mmoja na akavuka kivuko cha Yaboki.
23 and to take: take them and to pass them [obj] [the] torrent: river and to pass [obj] which to/for him
Baada ya kuwavusha ngʼambo ya kijito, alivusha pia mali zake zote.
24 and to remain Jacob to/for alone him and to wrestle man with him till to ascend: dawn [the] dawn
Kwa hiyo Yakobo akaachwa peke yake na mtu mmoja akashikana naye mweleka mpaka mapambazuko.
25 and to see: see for not be able to/for him and to touch in/on/with palm: dish thigh his and to dislocate/hang palm: dish thigh Jacob in/on/with to wrestle he with him
Yule mtu alipoona kuwa hawezi kumshinda, aligusa kiungio cha nyonga ya Yakobo kwa hiyo nyonga yake ikateguka wakati alipokuwa akishikana mweleka na yule mtu.
26 and to say to send: let go me for to ascend: dawn [the] dawn and to say not to send: let go you that if: except if: except to bless me
Ndipo yule mtu akasema, “Niache niende, kwa kuwa ni mapambazuko.” Lakini Yakobo akajibu, “Sitakuacha uende usiponibariki.”
27 and to say to(wards) him what? name your and to say Jacob
Yule mtu akamuuliza, “Jina lako nani?” Akajibu, “Yakobo.”
28 and to say not Jacob to say still name your that if: except if: except Israel for to strive with God and with human and be able
Ndipo yule mtu akasema, “Jina lako halitakuwa tena Yakobo, bali Israeli, kwa sababu umeshindana na Mungu na watu pia, nawe umeshinda.”
29 and to ask Jacob and to say to tell [emph?] please name your and to say to/for what? this to ask to/for name my and to bless [obj] him there
Yakobo akasema, “Tafadhali niambie jina lako.” Lakini akajibu, “Kwa nini kuniuliza Jina langu?” Ndipo akambariki huko.
30 and to call: call by Jacob name [the] place Peniel for to see: see God face to(wards) face and to rescue soul: life my
Kwa hiyo Yakobo akapaita mahali pale Penieli, akasema, “Ni kwa sababu nimemwona Mungu uso kwa uso na bado maisha yangu yameokoka.”
31 and to rise to/for him [the] sun like/as as which to pass [obj] Peniel and he/she/it to limp upon thigh his
Jua lilikuwa linachomoza Yakobo alipoondoka Penueli, naye alikuwa akichechemea kwa sababu ya nyonga yake.
32 upon so not to eat son: descendant/people Israel [obj] sinew [the] hamstring which upon palm: dish [the] thigh till [the] day: today [the] this for to touch in/on/with palm: dish thigh Jacob in/on/with sinew [the] hamstring
Kwa hiyo mpaka leo Waisraeli hawali mshipa ulioungana na kiungio cha nyonga, kwa sababu kiungio cha nyonga ya Yakobo kiliteguliwa karibu na mshipa huo.

< Genesis 32 >