< Genesis 25 >
1 and to add Abraham and to take: marry woman: wife and name her Keturah
Abraham akaoa mke mwingine; jina lake aliitwa Ketura.
2 and to beget to/for him [obj] Zimran and [obj] Jokshan and [obj] Medan and [obj] Midian and [obj] Ishbak and [obj] Shuah
Akamzalia Zimrani, Jokshani, Medani, Midiani, Ishbaki, na Shua.
3 and Jokshan to beget [obj] Sheba and [obj] Dedan and son: descendant/people Dedan to be Asshurim and Letushim and Leummim
Jokshani akamzaa Sheba na Dedani. Wana wa Dedani walikuwa ni Waashuru, Waletushi, na Waleumi.
4 and son: descendant/people Midian Ephah and Epher and Hanoch and Abida and Eldaah all these son: descendant/people Keturah
Wana wa Midiani walikuwa ni Efa, Eferi, Hanoki, Abida, na Eldaa. Hawa wote walikuwa ni wana wa Ketura.
5 and to give: give Abraham [obj] all which to/for him to/for Isaac
Abraham akampatia Isaka vitu vyote alivyokuwa navyo.
6 and to/for son: child [the] concubine which to/for Abraham to give: give Abraham gift and to send: depart them from upon Isaac son: child his in/on/with still he alive east [to] to(wards) land: country/planet front: east
Ingawaje, wakati alipokua angali akiishi, aliwapatia zawadi wana wa masuria wake na kuwapeleka katika nchi ya mashariki, mbali na Isaka, mwanae.
7 and these day year life Abraham which to live hundred year and seventy year and five year
Hizi ndizo zilikuwa siku za miaka ya uhai wake Abraham alizoishi, miaka 175.
8 and to die and to die Abraham in/on/with greyheaded pleasant old and sated and to gather to(wards) kinsman his
Abraham akapumua pumzi ya mwisho na akafa katika uzee mwema, mzee aliye shiba siku, na akakusanywa kwa watu wake.
9 and to bury [obj] him Isaac and Ishmael son: child his to(wards) cave [the] Machpelah to(wards) land: country Ephron son: child Zohar [the] Hittite which upon face: before Mamre
Isaka na Ishmaili, wanae wakamzika katika pango la Makipela, katika shamba la Efron mwana wa Soari Mhiti, pango lililokuwa karibu na Mamre.
10 [the] land: country which to buy Abraham from with son: descendant/people Heth there [to] to bury Abraham and Sarah woman: wife his
Shamba hili Abraham alilinunua kwa watoto wa Hethi. Abraham akazikwa pale pamoja na Sara mkewe.
11 and to be after death Abraham and to bless God [obj] Isaac son: child his and to dwell Isaac with Beer-lahai-roi Beer-lahai-roi Beer-lahai-roi
Baada ya kifo cha Abraham, Mungu akambariki Isaka mwanae, na Isaka akaishi karibu na Beerlalahairoi.
12 and these generation Ishmael son: child Abraham which to beget Hagar [the] Egyptian maidservant Sarah to/for Abraham
Na sasa hawa ndio walikuwa wana wa Ishimaeli, mwana wa Abraham, ambaye Hajiri Mmisri mtumishi wake Sara, alizaa kwa Abraham.
13 and these name son: child Ishmael in/on/with name their to/for generation their firstborn Ishmael Nebaioth and Kedar and Adbeel and Mibsam
Haya ndiyo yalikuwa majina ya wana wa Ishimaeli, kuanzia mzaliwa wa kwanza: Nebayothi - mzaliwa wa kwanza wa Ishimaeli, Kedari, Adbeeli, Mibsamu,
14 and Mishma and Dumah and Massa
Mishma, Duma, Masa,
15 (Hadad *LA(BH)*) and Tema Jetur Naphish and Kedemah
Hadadi, Tema, Yeturi, Nafishi, na Kedema.
16 these they(masc.) son: child Ishmael and these name their in/on/with village their and in/on/with encampment their two ten leader to/for people their
Hawa ndio walikuwa wana wa Ishimaeli, na haya ndiyo majina yao, kwa vijiji vyao, na katika vituo vyao; Maseyidi kumi na wawili kufuatana na kabila zao.
17 and these year life Ishmael hundred year and thirty year and seven year and to die and to die and to gather to(wards) kinsman his
Hii ndiyo ilikuwa miaka ya Ishimaeli, miaka 137: akapumua pumzi yake ya mwisho na akafa, na akakusanywa pamoja na watu wake.
18 and to dwell from Havilah till Shur which upon face: before Egypt to come (in): towards you Assyria [to] upon face: before all brother: male-relative his to fall: fall
Walioshi toka Havila mpaka Shuri, ambayo iko karibu na Misri, kuelekea Ashuru. Waliishi kwa uadui kati yao.
19 and these generation Isaac son: child Abraham Abraham to beget [obj] Isaac
Haya ndiyo yalikuwa matukio kumuhusu Isaka, mwana wa Abraham: Abraham alimzaa Isaka.
20 and to be Isaac son: aged forty year in/on/with to take: marry he [obj] Rebekah daughter Bethuel [the] Aramean from Paddan (Paddan)-aram sister Laban [the] Aramean to/for him to/for woman: wife
Isaka alikuwa na umri wa miaka arobaini alipomuoa Rebeka, binti wa ethueli Mshami wa Padani Aramu, ndugu wa Labani Mshami.
21 and to pray Isaac to/for LORD to/for before woman: wife his for barren he/she/it and to pray to/for him LORD and to conceive Rebekah woman: wife his
Isaka akamwomba Yahwe kwa ajili ya mke wake kwa sababu alikuwa tasa, na Yahwe akajibu maombi yake, Rebeka mkewe akabeba mimba.
22 and to crush [the] son: child in/on/with entrails: among her and to say if so to/for what? this I and to go: went to/for to seek [obj] LORD
Watoto hawa walipokuwa tumboni mwake wakasumbuka, naye akasema, “Kwa nini jambo hili linatokea kwangu mimi?” Akaenda kumuuliza Yahwe kuhusu jambo hili.
23 and to say LORD to/for her two (nation *Q(k)*) in/on/with belly: womb your and two people from belly your to separate and people from people to strengthen and many to serve little
Yahwe akamwambia, “Mataifa mawili yako katika tumbo lako, na mataifa haya mawili yatatengana ndani yako. Taifa moja litakuwa lenye nguvu kuliko lingine, na yule mkubwa atamtumikia mdogo.
24 and to fill day her to/for to beget and behold twin in/on/with belly: womb her
Ulipo wadia wakati wa kujifungua, tazama, kulikuwa na mapacha ndani ya tumbo lake.
25 and to come out: produce [the] first red all his like/as clothing hair and to call: call by name his Esau
Wakwanza akatoka akiwa mwekundu mwili wote kama vazi la nywele. Wakamwita jina lake Esau.
26 and after so to come out: produce brother: male-sibling his and hand his to grasp in/on/with heel Esau and to call: call by name his Jacob and Isaac son: aged sixty year in/on/with to beget [obj] them
Baada ya hapo ndugu yake akatoka. Mkono wake ukiwa umeshika kisigino cha Esau. Akaitwa jina lake Yakobo. Isaka alikuwa na umri wa miaka sitini wakati mke wake alipo wazaa hawa watoto.
27 and to magnify [the] youth and to be Esau man to know wild game man land: country and Jacob man complete to dwell tent
Vijana hawa wakakua, Hesau akawa mwindaji hodari, mtu wa nyikani; lakini Yakobo alikuwa mtu mkimya, aliye tumia muda wake akiwa katika mahema.
28 and to love: lover Isaac [obj] Esau for wild game in/on/with lip his and Rebekah to love: lover [obj] Jacob
Kisha Isaka akampenda Esau kwa sababu alikula wanyama ambao alikuwa anawinda, lakini Rebeka akampenda Yakobo.
29 and to boil Jacob stew and to come (in): come Esau from [the] land: country and he/she/it faint
Yakobo akapika mchuzi. Esau akaja kutoka nyikani, akiwa dhaifu kutokana na njaa.
30 and to say Esau to(wards) Jacob to eat me please from [the] red stuff [the] red stuff [the] this for faint I upon so to call: call by name his Edom
Esau akamwambia Yakobo, “Nilishe mchuzi mwekundu. Tafadhari, nimechoka!” Na hii ndiyo sababu jina lake aliitwa Edomu.
31 and to say Jacob to sell [emph?] like/as day: today [obj] birthright your to/for me
Yakobo akasema, “Kwanza uniuzie haki yako ya mzaliwa wa kwanza.”
32 and to say Esau behold I to go: continue to/for to die and to/for what? this to/for me birthright
Esau akasema, “Tazama, nakaribia kufa. Ni nini kwangu haki ya mzaliwa wa kwanza?”
33 and to say Jacob to swear [emph?] to/for me like/as day: today and to swear to/for him and to sell [obj] birthright his to/for Jacob
Yakobo akasema, “Kwanza uape kwangu mimi,” kwa hiyo Esau akaapa kiapo na kwa njia hii akawa ameuza haki yake ya mzaliwa wa kwanza kwa Yakobo.
34 and Jacob to give: give to/for Esau food: bread and stew lentil and to eat and to drink and to arise: rise and to go: journey and to despise Esau [obj] [the] birthright
Yakobo akampatia Esau mkate pamoja na mchuzi wa dengu. Akala na kunywa, kisha akainuka na akaenda zake. Kwa njia hii Esau akawa ameidharau haki yake ya mzaliwa wa kwanza.