< Genesis 24 >

1 and Abraham be old to come (in): advanced in/on/with day: year and LORD to bless [obj] Abraham in/on/with all
Wakati huu Abrahamu alikuwa mzee mwenye miaka mingi, naye Bwana alikuwa amembariki katika kila njia.
2 and to say Abraham to(wards) servant/slave his old house: household his [the] to rule in/on/with all which to/for him to set: put please hand: swear your underneath: swear thigh my
Akamwambia mtumishi wake mkuu wa vitu vyote katika nyumba yake, yule aliyekuwa msimamizi wa vitu vyote alivyokuwa navyo, “Weka mkono wako chini ya paja langu,
3 and to swear you in/on/with LORD God [the] heaven and God [the] land: country/planet which not to take: take woman: wife to/for son: child my from daughter [the] Canaanite which I to dwell in/on/with entrails: among his
Ninataka uape kwa Bwana, Mungu wa mbingu na Mungu wa nchi, kwamba hutamtwalia mwanangu mke kutoka binti za Wakanaani, ambao ninaishi miongoni mwao,
4 for to(wards) land: country/planet my and to(wards) relatives my to go: went and to take: take woman: wife to/for son: child my to/for Isaac
bali utakwenda katika nchi yangu na jamaa zangu umpatie Isaki mwanangu mke.”
5 and to say to(wards) him [the] servant/slave perhaps not be willing [the] woman to/for to go: follow after me to(wards) [the] land: country/planet [the] this to return: return to return: return [obj] son: child your to(wards) [the] land: country/planet which to come out: come from there
Yule mtumishi akamuuliza, “Je, kama huyo mwanamke atakataa kuja nami katika nchi hii? Je, nimpeleke mwanao katika hiyo nchi uliyotoka?”
6 and to say to(wards) him Abraham to keep: careful to/for you lest to return: return [obj] son: child my there [to]
Abrahamu akasema, “Hakikisha kwamba hutamrudisha mwanangu huko.
7 LORD God [the] heaven which to take: take me from house: household father my and from land: country/planet relatives my and which to speak: speak to/for me and which to swear to/for me to/for to say to/for seed: children your to give: give [obj] [the] land: country/planet [the] this he/she/it to send: depart messenger: angel his to/for face: before your and to take: take woman: wife to/for son: child my from there
Bwana, Mungu wa mbingu, aliyenitoa nyumbani kwa baba yangu na nchi yangu niliyozaliwa na aliyesema nami na akaniahidi kwa kiapo, akisema, ‘Nitawapa watoto wako nchi hii,’ atatuma malaika wake akutangulie ili umpatie mwanangu mke kutoka huko.
8 and if not be willing [the] woman to/for to go: follow after you and to clear from oath my this except [obj] son: child my not to return: return there [to]
Kama huyo mwanamke asipokubali kufuatana nawe, basi utafunguliwa kutoka kiapo nilichokuapisha. Ila usimrudishe mwanangu huko.”
9 and to set: put [the] servant/slave [obj] hand: swear his underneath: swear thigh Abraham lord his and to swear to/for him upon [the] word: thing [the] this
Basi yule mtumishi akaweka mkono wake chini ya paja la bwana wake Abrahamu akamwapia kuhusu shauri hili.
10 and to take: take [the] servant/slave ten camel from camel lord his and to go: went and all goodness lord his in/on/with hand: to his and to arise: rise and to go: went to(wards) Mesopotamia Mesopotamia to(wards) city Nahor
Ndipo huyo mtumishi akachukua ngamia kumi miongoni mwa ngamia za bwana wake, akaondoka, akiwa amechukua aina zote za vitu vizuri kutoka kwa bwana wake. Akaelekea Aramu-Naharaimu na kushika njia kwenda mji wa Nahori.
11 and to bless [the] camel from outside to/for city to(wards) well [the] water to/for time evening to/for time to come out: come [the] to draw
Akawapigisha ngamia magoti karibu na kisima cha maji nje ya mji, ilikuwa inaelekea jioni, wakati ambapo wanawake wanakuja kuteka maji.
12 and to say LORD God lord my Abraham to meet please to/for face of my [the] day and to make: do kindness with lord my Abraham
Kisha akaomba, “Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, nipatie ushindi leo, uonyeshe huruma kwa bwana wangu Abrahamu.
13 behold I to stand upon spring [the] water and daughter human [the] city to come out: come to/for to draw water
Tazama, nimesimama karibu na kisima hiki cha maji, nao binti za watu wa mji huu wanakuja kuteka maji.
14 and to be [the] maiden which to say to(wards) her to stretch please jar your and to drink and to say to drink and also camel your to water: watering [obj] her to rebuke to/for servant/slave your to/for Isaac and in/on/with her to know for to make: do kindness with lord my
Basi na iwe hivi, nitakapomwambia binti mmojawapo, ‘Tafadhali tua mtungi wako nipate kunywa maji,’ naye akisema, ‘Kunywa, nitawanywesha na ngamia wako pia.’ Basi na awe ndiye uliyemchagua kwa ajili ya mtumishi wako Isaki. Kwa hili nitajua umemhurumia bwana wangu.”
15 and to be he/she/it before to end: finish to/for to speak: speak and behold Rebekah to come out: come which to beget to/for Bethuel son: child Milcah woman: wife Nahor brother: male-sibling Abraham and jar her upon shoulder her
Ikawa kabla hajamaliza kuomba, Rebeka akatokea akiwa na mtungi begani mwake. Alikuwa binti wa Bethueli. Bethueli alikuwa mwana wa Milka aliyekuwa mke wa Nahori ndugu wa Abrahamu.
16 and [the] maiden pleasant appearance much virgin and man not to know her and to go down [the] spring [to] and to fill jar her and to ascend: rise
Huyu msichana alikuwa mzuri sana wa sura, bikira, ambaye hakuna mtu aliyekuwa amekutana naye kimwili. Aliteremka kisimani, akajaza mtungi wake akapanda juu.
17 and to run: run [the] servant/slave to/for to encounter: meet her and to say to swallow me please little water from jar your
Ndipo yule mtumishi akaharakisha kukutana naye akamwambia, “Tafadhali nipe maji kidogo katika mtungi wako.”
18 and to say to drink lord my and to hasten and to go down jar her upon hand her and to water: drink him
Yule msichana akasema, “Kunywa, bwana wangu.” Akashusha kwa haraka mtungi mkononi mwake na akampa, akanywa.
19 and to end: finish to/for to water: drink him and to say also to/for camel your to draw till if: until to end: finish to/for to drink
Baada ya kumpa yule mtumishi yale maji, akamwambia, “Nitateka maji kwa ajili ya ngamia zako pia mpaka wote watosheke.”
20 and to hasten and to uncover jar her to(wards) [the] trough and to run: run still to(wards) [the] well to/for to draw and to draw to/for all camel his
Akafanya haraka kumimina maji kwenye birika ya kunyweshea wanyama, akakimbia kisimani kuteka maji mengine na akateka ya kuwatosha ngamia wake wote.
21 and [the] man to gaze to/for her be quiet to/for to know to prosper LORD way: journey his if not
Pasipo kusema neno, yule mtumishi akamtazama kwa makini aone kama Bwana ameifanikisha safari yake, au la.
22 and to be like/as as which to end: finish [the] camel to/for to drink and to take: take [the] man ring gold bekah weight his and two bracelet upon hand: swear her ten gold weight their
Ikawa ngamia walipokwisha kunywa wote, yule mtumishi akampa huyo msichana pete ya puani ya dhahabu yenye uzito wa beka moja na bangili mbili za dhahabu zenye uzito wa shekeli kumi.
23 and to say daughter who? you(f. s.) to tell please to/for me there house: home father your place to/for us to/for to lodge
Kisha akamuuliza, “Wewe ni binti wa nani? Tafadhali uniambie, je, kuna nafasi katika nyumba ya baba yako tutakapoweza kulala?”
24 and to say to(wards) him daughter Bethuel I son: child Milcah which to beget to/for Nahor
Yule msichana akamjibu, “Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Milka aliyemzalia Nahori.”
25 and to say to(wards) him also straw also fodder many with us also place to/for to lodge
Akaendelea kusema, “Kwetu kuna majani mengi na malisho, tena kuna nafasi kwa ajili yenu kulala.”
26 and to bow [the] man and to bow to/for LORD
Yule mtumishi akasujudu na kumwabudu Bwana,
27 and to say to bless LORD God lord my Abraham which not to leave: forsake kindness his and truth: faithful his from from with lord my I in/on/with way: journey to lead me LORD house: home brother: male-relative lord my
akisema, “Atukuzwe Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye hakuondoa wema na uaminifu wake kwa bwana wangu. Mimi nami, Bwana ameniongoza safarini akanifikisha nyumbani kwa jamaa za bwana wangu.”
28 and to run: run [the] maiden and to tell to/for house: household mother her like/as word: thing [the] these
Yule msichana akakimbia akawaeleza watu wa nyumbani mwa mama yake kuhusu mambo haya.
29 and to/for Rebekah brother: male-sibling and name his Laban and to run: run Laban to(wards) [the] man [the] outside [to] to(wards) [the] spring
Rebeka alikuwa na kaka aliyeitwa Labani, huyo akaharakisha kukutana na yule mtumishi kule kisimani.
30 and to be like/as to see: see [obj] [the] ring and [obj] [the] bracelet upon hand sister his and like/as to hear: hear he [obj] word Rebekah sister his to/for to say thus to speak: speak to(wards) me [the] man and to come (in): come to(wards) [the] man and behold to stand: stand upon [the] camel upon [the] spring
Mara alipoiona ile pete puani, na bangili mikononi mwa dada yake na kusikia yale maneno Rebeka aliyoambiwa na huyo mtumishi, alimwendea huyo mtumishi, akamkuta amesimama karibu na ngamia wake pale karibu na kisima.
31 and to say to come (in): come to bless LORD to/for what? to stand: stand in/on/with outside and I to turn [the] house: home and place to/for camel
Akamwambia, “Karibu nyumbani wewe uliyebarikiwa na Bwana, kwa nini unasimama huko nje? Mimi nimekuandalia nyumba na mahali kwa ajili ya ngamia.”
32 and to come (in): come [the] man [the] house: home [to] and to open [the] camel and to give: give straw and fodder to/for camel and water to/for to wash: wash foot his and foot [the] human which with him
Hivyo yule mtumishi akaenda nyumbani, mizigo ikaondolewa juu ya ngamia. Majani na malisho yakaletwa kwa ajili ya ngamia na maji kwa ajili yake na watu wake ili kunawa miguu.
33 (and to set: put *Q(K)*) to/for face: before his to/for to eat and to say not to eat till if: surely no to speak: speak word: speaking my and to say to speak: speak
Ndipo chakula kikaandaliwa kwa ajili yake, lakini akasema, “Sitakula mpaka niwe nimewaambia yale niliyo nayo ya kusema.” Labani akasema, “Basi tuambie.”
34 and to say servant/slave Abraham I
Hivyo akasema, “Mimi ni mtumishi wa Abrahamu.
35 and LORD to bless [obj] lord my much and to magnify and to give: give to/for him flock and cattle and silver: money and gold and servant/slave and maidservant and camel and donkey
Bwana amembariki sana bwana wangu, amekuwa tajiri. Amempa kondoo na ngʼombe, fedha na dhahabu, watumishi wa kiume na wa kike, ngamia na punda.
36 and to beget Sarah woman: wife lord my son: child to/for lord my after old age her and to give: give to/for him [obj] all which to/for him
Sara mkewe bwana wangu amemzalia mwana katika uzee wake, naye amempa kila kitu alichokuwa nacho.
37 and to swear me lord my to/for to say not (to take: take *LA(bh)*) woman: wife to/for son: child my from daughter [the] Canaanite which I to dwell in/on/with land: country/planet his
Naye bwana wangu ameniapisha na akasema, ‘Kamwe usimtwalie mwanangu mke katika binti za Wakanaani, ambao ninaishi katika nchi yao,
38 if: surely yes not to(wards) house: household father my to go: went and to(wards) family my and to take: take woman: wife to/for son: child my
ila uende mpaka kwa jamaa ya baba yangu na ukoo wangu mwenyewe, ukamtwalie mwanangu mke huko.’
39 and to say to(wards) lord my perhaps not to go: follow [the] woman after me
“Kisha nikamuuliza bwana wangu, ‘Je, kama huyo mwanamke hatakubali kurudi nami?’
40 and to say to(wards) me LORD which to go: walk to/for face: before his to send: depart messenger: angel his with you and to prosper way: journey your and to take: take woman: wife to/for son: child my from family my and from house: household father my
“Akanijibu, ‘Bwana ambaye nimetembea mbele zake, atatuma malaika wake pamoja nawe, na kuifanikisha safari yako, ili uweze kupata mke kwa ajili ya mwanangu katika ukoo wangu na kutoka jamaa ya baba yangu.
41 then to clear from oath my for to come (in): come to(wards) family my and if not to give: give to/for you and to be innocent from oath my
Kisha, utakapokwenda kwenye ukoo wangu, utakuwa umefunguliwa kutoka kiapo changu hata kama wakikataa kukupa huyo binti, utakuwa umefunguliwa kutoka kiapo changu.’
42 and to come (in): come [the] day to(wards) [the] spring and to say LORD God lord my Abraham if there you please to prosper way: journey my which I to go: went upon her
“Nilipokuja kisimani leo nilisema, ‘Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ikikupendeza, naomba uifanikishe safari niliyoijia.
43 behold I to stand upon spring [the] water and to be [the] maiden [the] to come out: come to/for to draw and to say to(wards) her to water: drink me please little water from jar your
Tazama, ninasimama kando ya kisima hiki, kama mwanamwali akija kuteka maji nami nikimwambia, tafadhali niruhusu ninywe maji kidogo kutoka kwenye mtungi wako,
44 and to say to(wards) me also you(m. s.) to drink and also to/for camel your to draw he/she/it [the] woman which to rebuke LORD to/for son: child lord my
naye kama akiniambia, “Kunywa, nami nitateka maji kwa ajili ya ngamia wako pia,” basi huyo awe ndiye mke ambaye Bwana amemchagulia mwana wa bwana wangu.’
45 I before to end: finish to/for to speak: speak to(wards) heart my and behold Rebekah to come out: come and jar her upon shoulder her and to go down [the] spring [to] and to draw and to say to(wards) her to water: drink me please
“Kabla sijamaliza kuomba moyoni mwangu, Rebeka akatokea, amebeba mtungi begani mwake. Akashuka kisimani akateka maji, nami nikamwambia, ‘Tafadhali nipe maji ninywe.’
46 and to hasten and to go down jar her from upon her and to say to drink and also camel your to water: watering and to drink and also [the] camel to water: watering
“Akafanya haraka kushusha mtungi wake begani na kusema, ‘Kunywa na nitawanywesha ngamia wako pia,’ basi nikanywa, akawanywesha na ngamia pia.
47 and to ask [obj] her and to say daughter who? you(f. s.) and to say daughter Bethuel son: child Nahor which to beget to/for him Milcah and to set: put [the] ring upon face: nose her and [the] bracelet upon hand her
“Nikamuuliza, ‘Wewe ni binti wa nani?’ “Akasema, ‘Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Nahori, Milka aliyemzalia.’ “Ndipo nilipotia pete puani mwake na bangili mikononi mwake,
48 and to bow and to bow to/for LORD and to bless [obj] LORD God lord my Abraham which to lead me in/on/with way: journey truth: true to/for to take: take [obj] daughter brother: male-relative lord my to/for son: child his
nikasujudu na nikamwabudu Bwana. Nikamtukuza Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, aliyeniongoza katika njia sahihi ili nimtwalie mwana na bwana wangu mke katika jamaa zake.
49 and now if there you to make: do kindness and truth: faithful with lord my to tell to/for me and if not to tell to/for me and to turn upon right or upon left
Ikiwa mtaonyesha wema na uaminifu kwa bwana wangu, mniambie, la sivyo, mniambie, ili niweze kujua njia ya kugeukia.”
50 and to answer Laban and Bethuel and to say from LORD to come out: come [the] word: thing not be able to speak: speak to(wards) you bad: harmful or pleasant
Labani na Bethueli wakajibu, “Jambo hili limetoka kwa Bwana, hatuwezi kukuambia jambo lolote baya au jema.
51 behold Rebekah to/for face: before your to take: take and to go: went and to be woman: wife to/for son: child lord your like/as as which to speak: speak LORD
Rebeka yuko hapa, mchukue na uende, awe mke wa mwana wa bwana wako, sawasawa na Bwana alivyoongoza.”
52 and to be like/as as which to hear: hear servant/slave Abraham [obj] word their and to bow land: soil [to] to/for LORD
Ikawa huyo mtumishi wa Abrahamu aliposikia waliyosema, alisujudu mpaka nchi mbele za Bwana.
53 and to come out: send [the] servant/slave article/utensil silver: money and article/utensil gold and garment and to give: give to/for Rebekah and precious thing to give: give to/for brother: male-sibling her and to/for mother her
Ndipo huyo mtumishi akatoa vitu vilivyotengenezwa kwa dhahabu na kwa fedha pamoja na mavazi, akampa Rebeka, pia akawapa zawadi za thamani kubwa nduguye na mamaye.
54 and to eat and to drink he/she/it and [the] human which with him and to lodge and to arise: rise in/on/with morning and to say to send: depart me to/for lord my
Kisha yeye na wale watu waliokuwa pamoja naye wakala, wakanywa na kulala palepale. Walipoamka asubuhi, yule mtumishi, akasema, “Nipeni ruhusa nirudi kwa bwana wangu.”
55 and to say brother: male-sibling her and mother her to dwell [the] maiden with us day or ten (after *L(S)*) to go: went
Lakini ndugu yake Rebeka pamoja na mama yake wakajibu, “Acha binti akae kwetu siku kumi au zaidi, ndipo mwondoke.”
56 and to say to(wards) them not to delay [obj] me and LORD to prosper way: journey my to send: depart me and to go: went to/for lord my
Lakini yule mtumishi akawaambia, “Msinicheleweshe, kwa kuwa Bwana amefanikisha safari yangu, nipeni ruhusa nirudi kwa bwana wangu.”
57 and to say to call: call to to/for maiden and to ask [obj] lip her
Ndipo wakasema, “Acha tumwite huyo binti tumuulize, tusikie atakavyosema.”
58 and to call: call to to/for Rebekah and to say to(wards) her to go: went with [the] man [the] this and to say to go: went
Kwa hiyo wakamwita Rebeka na kumuuliza, “Je, utakwenda na mtu huyu?” Akasema, “Nitakwenda.”
59 and to send: depart [obj] Rebekah sister their and [obj] to suckle her and [obj] servant/slave Abraham and [obj] human his
Hivyo wakamwaga ndugu yao Rebeka aondoke, pamoja na mjakazi wake, mtumishi wa Abrahamu na watu wake.
60 and to bless [obj] Rebekah and to say to/for her sister our you(f. s.) to be to/for thousand myriad and to possess: take seed: children your [obj] gate to hate him
Wakambariki Rebeka, wakamwambia, “Ndugu yetu, uwe wewe kumi elfu, mara elfu nyingi, nao wazao wako wamiliki malango ya adui zao.”
61 and to arise: rise Rebekah and maiden her and to ride upon [the] camel and to go: follow after [the] man and to take: take [the] servant/slave [obj] Rebekah and to go: journey
Rebeka na vijakazi wake wakajiandaa, wakapanda ngamia zao wakafuatana na yule mtu. Hivyo yule mtumishi akamchukua Rebeka akaondoka.
62 and Isaac to come (in): come from to come (in): come Beer-lahai-roi Beer-lahai-roi Beer-lahai-roi and he/she/it to dwell in/on/with land: country/planet [the] Negeb
Basi Isaki alikuwa ametoka Beer-Lahai-Roi, kwa kuwa alikuwa anaishi nchi ya Negebu.
63 and to come out: come Isaac to/for to meditate in/on/with land: country to/for to turn evening and to lift: look eye his and to see: see and behold camel to come (in): come
Isaki akatoka kwenda shambani kutafakari wakati wa jioni, alipoinua macho yake, akaona ngamia wanakuja.
64 and to lift: look Rebekah [obj] eye her and to see: see [obj] Isaac and to fall: fall from upon [the] camel
Rebeka pia akainua macho akamwona Isaki. Akashuka kutoka kwenye ngamia wake
65 and to say to(wards) [the] servant/slave who? [the] man this [the] to go: walk in/on/with land: country to/for to encounter: meet us and to say [the] servant/slave he/she/it lord my and to take: take [the] shawl and to cover
na akamuuliza yule mtumishi, “Ni nani mtu yule aliye kule shambani anayekuja kutulaki?” Yule mtumishi akajibu, “Huyu ndiye bwana wangu.” Hivyo Rebeka akachukua shela yake akajifunika.
66 and to recount [the] servant/slave to/for Isaac [obj] all [the] word: thing which to make: do
Kisha yule mtumishi akamweleza Isaki mambo yote aliyoyatenda.
67 and to come (in): bring her Isaac [the] tent [to] Sarah mother his and to take: marry [obj] Rebekah and to be to/for him to/for woman: wife and to love: lover her and to be sorry: comfort Isaac after mother his
Ndipo Isaki akamwingiza Rebeka katika hema la Sara mama yake, Isaki akamchukua Rebeka, hivyo akawa mke wake. Isaki akampenda, akafarijika baada ya kifo cha mama yake.

< Genesis 24 >