< Ezekiel 1 >

1 and to be in/on/with thirty year in/on/with fourth in/on/with five to/for month and I in/on/with midst [the] captivity upon river Chebar to open [the] heaven and to see: see vision God
Katika mwaka wa thelathini, mwezi wa nne, siku ya tano ya mwezi, wakati nilipokuwa miongoni mwa hao waliokuwa uhamishoni kando ya Mto Kebari, mbingu zilifunguka nami nikaona maono ya Mungu.
2 in/on/with five to/for month he/she/it [the] year [the] fifth to/for captivity [the] king Jehoiachin
Katika siku ya tano ya mwezi, ilikuwa mwaka wa tano wa kuhamishwa kwa Mfalme Yehayakini,
3 to be to be word LORD to(wards) Ezekiel son: child Buzi [the] priest in/on/with land: country/planet Chaldea upon river Chebar and to be upon him there hand: power LORD
neno la Bwana lilimjia Ezekieli kuhani, mwana wa Buzi, kando ya Mto Kebari, katika nchi ya Wakaldayo. Huko mkono wa Bwana ulikuwa juu yake.
4 and to see: see and behold spirit: breath tempest to come (in): come from [the] north cloud great: large and fire to take: fire and brightness to/for him around and from midst her like/as eye: appearance [the] amber from midst [the] fire
Nilitazama, nikaona dhoruba kubwa ikitoka kaskazini, wingu kubwa sana pamoja likiwa na umeme wa radi likiwa limezungukwa na mwanga mkali. Katikati ya huo moto kulikuwa kama rangi ya manjano ya chuma kinapokuwa ndani ya moto.
5 and from midst her likeness four living thing and this appearance their likeness man to/for them
Katika ule moto kulikuwa na kitu kinachofanana na viumbe vinne vyenye uhai. Katika kuonekana kwake vilikuwa na umbo mfano wa mwanadamu,
6 and four face to/for one and four wing to/for one to/for them
lakini kila kimoja kilikuwa na nyuso nne na mabawa manne.
7 and foot their foot upright and palm: sole foot their like/as palm: sole foot calf and to shine like/as eye: appearance bronze burnished
Miguu yao ilikuwa imenyooka, nyayo za miguu yao zilikuwa kama kwato za miguu ya ndama, nazo zilimetameta kama shaba iliyosuguliwa.
8 (and hand *Q(K)*) man from underneath: under wing their upon four fourth their and face their and wing their to/for four their
Chini ya mabawa yao katika pande zao nne walikuwa na mikono ya mwanadamu. Wote wanne walikuwa na nyuso na mabawa,
9 to unite woman: another to(wards) sister her wing their not to turn: turn in/on/with to go: went they man: anyone to(wards) side: beyond face: before his to go: went
nayo mabawa yao yaligusana. Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja, hawakugeuka walipokuwa wanatembea.
10 and likeness face their face man and face lion to(wards) [the] right to/for four their and face cattle from [the] left to/for four their and face eagle to/for four their
Kuonekana kwa nyuso zao kulikuwa hivi: Kila mmoja wa wale wanne alikuwa na uso wa mwanadamu na kwa upande wa kulia kila mmoja alikuwa na uso wa simba, upande wa kushoto alikuwa na uso wa ngʼombe pia kila mmoja alikuwa na uso wa tai.
11 and face their and wing their to separate from to/for above [to] to/for man: anyone two to unite man: anyone and two to cover [obj] body their
Hivyo ndivyo zilivyokuwa nyuso zao. Mabawa yao yalikunjuliwa kuelekea juu, kila mmoja alikuwa na mabawa mawili ambayo kila moja liligusa bawa la mwenzake kila upande na mabawa mengine mawili yakifunika mwili wake.
12 and man: anyone to(wards) side: beyond face: before his to go: went to(wards) which to be there [to] [the] spirit to/for to go: went to go: went not to turn: turn in/on/with to go: went they
Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja. Popote roho alipotaka kwenda, ndipo walipokwenda pasipo kugeuka.
13 and likeness [the] living thing appearance their like/as coal fire to burn: burn like/as appearance [the] torch he/she/it to go: walk between: among [the] living thing and brightness to/for fire and from [the] fire to come out: come lightning
Kuonekana kwa vile viumbe hai katikati kulikuwa kama makaa ya mawe yanayowaka au kama mienge. Moto ule ulikuwa ukienda mbele na nyuma katikati ya vile viumbe, ulikuwa na mwangaza mkali na katikati ya ule moto kulitoka kimulimuli kama umeme wa radi.
14 and [the] living thing to run and to return: return like/as appearance [the] lightning
Vile viumbe vilipiga mbio kwenda na kurudi, kama vimulimuli vya umeme wa radi.
15 and to see: see [the] living thing and behold wheel one in/on/with land: country/planet beside [the] living thing to/for four face his
Nilipokuwa nikitazama vile viumbe hai, niliona gurudumu moja juu ya ardhi kando ya kila kiumbe kikiwa na nyuso zake nne.
16 appearance [the] wheel and deed: work their like/as eye: appearance jasper and likeness one to/for four their and appearance their and deed: work their like/as as which to be [the] wheel in/on/with midst [the] wheel
Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa hayo magurudumu na muundo wake: yalingʼaa kama zabarajadi, nayo yote manne yalifanana. Kila gurudumu lilikuwa na gurudumu jingine ndani yake.
17 upon four fourth their in/on/with to go: went they to go: went not to turn: turn in/on/with to go: went they
Yalipokwenda yalielekea upande wowote wa pande nne walipoelekea wale viumbe, magurudumu hayakuzunguka wakati viumbe vile vilipokwenda.
18 and back/rim/brow their and height to/for them and fear to/for them and back/rim/brow their full eye around to/for four their
Kingo zake zilikuwa ndefu kwenda juu na za kutisha, nazo zote nne zilijawa na macho pande zote.
19 and in/on/with to go: went [the] living thing to go: went [the] wheel beside them and in/on/with to lift: raise [the] living thing from upon [the] land: country/planet to lift: raise [the] wheel
Vile viumbe hai vilipokwenda, magurudumu yaliyokuwa kando yao yalisogea na wakati hivyo viumbe hai vilipoinuka kutoka ardhini magurudumu nayo yaliinuka.
20 upon which to be there [the] spirit to/for to go: went to go: went there [to] [the] spirit to/for to go: went and [the] wheel to lift: raise to/for close them for spirit [the] living thing in/on/with wheel
Mahali popote roho alipokwenda wale viumbe nao walikwenda, nayo magurudumu yaliinuka pamoja navyo, kwa sababu roho ya vile viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
21 in/on/with to go: went they to go: went and in/on/with to stand: stand they to stand: stand and in/on/with to lift: raise they from upon [the] land: country/planet to lift: raise [the] wheel to/for close them for spirit [the] living thing in/on/with wheel
Wakati viumbe vile viliposogea, nayo magurudumu yalisogea, viumbe viliposimama kimya, nayo pia yalisimama kimya, viumbe vilipoinuka juu ya nchi magurudumu yaliinuliwa pamoja navyo kwa kuwa roho ya hivyo viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
22 and likeness upon head [the] living thing expanse like/as eye: appearance [the] ice [the] to fear: revere to stretch upon head their from to/for above [to]
Juu ya vichwa vya hao viumbe hai palikuwa na kitu mfano wa eneo lililokuwa wazi, lililokuwa angavu kabisa na lenye kutisha.
23 and underneath: under [the] expanse wing their upright woman: another to(wards) sister her to/for man: anyone two to cover to/for them and to/for man: anyone two to cover to/for them [obj] body their
Chini ya hiyo nafasi mabawa yao yalitanda moja kuelekea jingine, kila mmoja alikuwa na mabawa mengine mawili yaliyofunika mwili wake.
24 and to hear: hear [obj] voice: sound wing their like/as voice: sound water many like/as voice: sound Almighty in/on/with to go: went they voice: sound tumult like/as voice: sound camp in/on/with to stand: stand they to slacken wing their
Viumbe wale waliposogea nilisikia sauti ya mabawa yao, kama ngurumo ya maji yaendayo kasi, kama sauti ya Mwenyezi, kama makelele ya jeshi. Waliposimama kimya walishusha mabawa yao.
25 and to be voice from upon to/for expanse which upon head their in/on/with to stand: stand they to slacken wing their
Ndipo ikaja sauti toka juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao, waliposimama mabawa yao yakiwa yameshushwa.
26 and from above to/for expanse which upon head their like/as appearance stone sapphire likeness throne and upon likeness [the] throne likeness like/as appearance man upon him from to/for above [to]
Juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi. Na juu ya kile kiti cha enzi kulikuwa na umbo mfano wa mwanadamu.
27 and to see: see like/as eye: appearance amber like/as appearance fire house: inside to/for her around from appearance loin his and to/for above [to] and from appearance loin his and to/for beneath to see: see like/as appearance fire and brightness to/for him around
Nikaona kwamba kutokana na kile nilichoona kama kiuno chake kuelekea juu alionekana kama chuma inayowaka kana kwamba imejaa moto na kuanzia kiuno kwenda chini alionekana kama moto na mwanga mkali ulimzunguka.
28 like/as appearance [the] bow which to be in/on/with cloud in/on/with day [the] rain so appearance [the] brightness around he/she/it appearance likeness glory LORD and to see: see and to fall: fall upon face my and to hear: hear voice to speak: speak
Kama vile kuonekana kwa upinde wa mvua mawinguni siku ya mvua, ndivyo ulivyokuwa ule mngʼao uliomzunguka. Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa utukufu wa Bwana. Nilipouona, nikaanguka kifudifudi, nikasikia sauti ya mtu anaongea.

< Ezekiel 1 >