< Ecclesiastes 6 >
1 there distress: evil which to see: see underneath: under [the] sun and many he/she/it upon [the] man
Nimeona ubaya mwingine chini ya jua, nao unalemea sana wanadamu:
2 man: anyone which to give: give to/for him [the] God riches and wealth and glory and nothing he lacking to/for soul: myself his from all which to desire and not to domineer him [the] God to/for to eat from him for man foreign to eat him this vanity and sickness bad: harmful he/she/it
Mungu humpa mwanadamu utajiri, mali na heshima, hivyo hakukosa chochote moyo wake unachokitamani. Lakini Mungu hamwezeshi kuvifurahia, badala yake mgeni ndiye anayevifurahia. Hili ni ubatili, ni ubaya unaosikitisha.
3 if to beget man: anyone hundred and year many to live and many which/that to be day year his and soul: appetite his not to satisfy from [the] welfare and also tomb not to be to/for him to say pleasant from him [the] miscarriage
Mtu anaweza kuwa na watoto mia moja naye akaishi miaka mingi, lakini haidhuru kuwa ataishi muda mrefu kiasi gani, kama hawezi kufurahia mafanikio yake na kwamba hapati mazishi ya heshima, ninasema afadhali mtoto aliyezaliwa akiwa amekufa kuliko yeye.
4 for in/on/with vanity to come (in): come and in/on/with darkness to go: went and in/on/with darkness name his to cover
Kuzaliwa kwake hakuna maana, huondokea gizani na gizani jina lake hufunikwa.
5 also sun not to see: see and not to know quietness to/for this from this
Ingawa hakuwahi kuliona jua wala kujua kitu chochote, yeye ana pumziko zaidi kuliko mtu huyo,
6 and except to live thousand year beat and welfare not to see: enjoy not to(wards) place one [the] all to go: went
Hata kama huyo mtu ataishi miaka elfu mara mbili na zaidi, lakini akashindwa kufurahia mafanikio yake, je, wote hawaendi sehemu moja?
7 all trouble [the] man to/for lip his and also [the] soul: appetite not to fill
Juhudi zote za binadamu ni kwa ajili ya kinywa chake, hata hivyo hamu yake kamwe haitoshelezwi.
8 for what? advantage to/for wise from [the] fool what? to/for afflicted to know to/for to go: walk before [the] alive
Mtu mwenye hekima ana faida gani zaidi ya mpumbavu? Mtu maskini anapata faida gani kwa kujua jinsi ya kujistahi mbele ya watu wengine?
9 pleasant appearance eye from to go: walk soul: appetite also this vanity and longing spirit: breath
Ni bora kile ambacho jicho linakiona kuliko hamu isiyotoshelezwa. Hili nalo ni ubatili, ni kukimbiza upepo.
10 what? which/that to be already to call: call by name his and to know which he/she/it man and not be able to/for to judge with (which/that mighty *Q(K)*) from him
Lolote lililopo limekwisha kupewa jina, naye mwanadamu alivyo ameshajulikana; hakuna mtu awezaye kushindana na mwenye nguvu kuliko yeye.
11 for there word to multiply to multiply vanity what? advantage to/for man
Maneno yanavyokuwa mengi, ndivyo yanavyokosa maana, Je, hilo linamfaidia vipi yeyote?
12 for who? to know what? pleasant to/for man in/on/with life number day life vanity his and to make: do them like/as shadow which who? to tell to/for man what? to be after him underneath: under [the] sun
Kwa maana ni nani anayejua lililo jema kwa ajili ya maisha ya mwanadamu, katika siku chache na za ubatili anazopita kama kivuli? Ni nani awezaye kumwambia yatakayotokea chini ya jua baada ya yeye kuondoka?