< Deuteronomy 26 >

1 and to be for to come (in): come to(wards) [the] land: country/planet which LORD God your to give: give to/for you inheritance and to possess: take her and to dwell in/on/with her
Mtakapokuwa mmeingia nchi ile ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi na mtakapokuwa mmeimiliki na kukaa ndani yake,
2 and to take: take from first: beginning all fruit [the] land: soil which to come (in): bring from land: country/planet your which LORD God your to give: give to/for you and to set: put in/on/with basket and to go: went to(wards) [the] place which to choose LORD God your to/for to dwell name his there
chukueni baadhi ya mavuno ya kwanza ya yale yote mtakayozalisha kutoka udongo wa nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa na mweke kwenye kapu. Kisha uende mahali ambapo Bwana Mungu wako atapachagua kuwa makao kwa ajili ya Jina lake
3 and to come (in): come to(wards) [the] priest which to be in/on/with day [the] they(masc.) and to say to(wards) him to tell [the] day to/for LORD God your for to come (in): come to(wards) [the] land: country/planet which to swear LORD to/for father our to/for to give: give to/for us
na umwambie kuhani atakayekuwepo kwa wakati huo, “Ninatangaza leo kwa Bwana Mungu wako kwamba nimekuja katika nchi ambayo Bwana aliwaapia baba zetu kwamba atatupa.”
4 and to take: take [the] priest [the] basket from hand your and to rest him to/for face: before altar LORD God your
Kuhani atapokea lile kapu mikononi mwako na kuliweka chini mbele ya madhabahu ya Bwana Mungu wako.
5 and to answer and to say to/for face: before LORD God your Aramean to perish father my and to go down Egypt [to] and to sojourn there in/on/with man little and to be there to/for nation great: large mighty and many
Kisha utatangaza mbele za Bwana Mungu wako: “Baba yangu alikuwa Mwaramu aliyekuwa anatangatanga, akaenda Misri pamoja na watu wachache, akaishi huko hadi akawa taifa kubwa, lenye nguvu na watu wengi.
6 and be evil [obj] us [the] Egyptian and to afflict us and to give: put upon us service: work severe
Lakini Wamisri walituonea na kututaabisha, wakitufanyisha kazi ngumu.
7 and to cry to(wards) LORD God father our and to hear: hear LORD [obj] voice our and to see: see [obj] affliction our and [obj] trouble our and [obj] oppression our
Kisha tulimlilia Bwana, Mungu wa baba zetu, naye Bwana akasikia sauti yetu na akaona huzuni yetu, taabu yetu na mateso yetu.
8 and to come out: send us LORD from Egypt in/on/with hand strong and in/on/with arm to stretch and in/on/with fear great: large and in/on/with sign: miraculous and in/on/with wonder
Kwa hiyo Bwana akatutoa nchi ya Misri kwa mkono wenye nguvu na ulionyooshwa, pamoja na utisho mkuu, ishara za miujiza na maajabu.
9 and to come (in): bring us to(wards) [the] place [the] this and to give: give to/for us [obj] [the] land: country/planet [the] this land: country/planet to flow: flowing milk and honey
Akatuleta mahali hapa akatupa nchi hii, nchi inayotiririka maziwa na asali;
10 and now behold to come (in): bring [obj] first: beginning fruit [the] land: soil which to give: give to/for me LORD and to rest him to/for face: before LORD God your and to bow to/for face: before LORD God your
nami sasa ninaleta malimbuko ya ardhi ambayo wewe, Ee Bwana, umenipa.” Weka kapu mbele za Bwana Mungu wako na usujudu mbele zake.
11 and to rejoice in/on/with all [the] good which to give: give to/for you LORD God your and to/for house: home your you(m. s.) and [the] Levi and [the] sojourner which in/on/with entrails: among your
Kisha wewe pamoja na Walawi na wageni wote walioko miongoni mwenu mtafurahi katika vitu vyote vizuri ambavyo Bwana Mungu wenu amewapa pamoja na wa nyumbani mwenu.
12 for to end: finish to/for to tithe [obj] all tithe produce your in/on/with year [the] third year [the] tithe and to give: give to/for Levi to/for sojourner to/for orphan and to/for widow and to eat in/on/with gate: town your and to satisfy
Wakati utakapokuwa umeshatoa zaka zote za mazao yako katika mwaka wa tatu, ambao ni mwaka wa zaka, utampa Mlawi, mgeni, yatima na mjane, ili waweze kula katika miji yenu na kushiba.
13 and to say to/for face: before LORD God your to burn: purge [the] holiness from [the] house: home and also to give: give him to/for Levi and to/for sojourner to/for orphan and to/for widow like/as all commandment your which to command me not to pass: trespass from commandment your and not to forget
Kisha umwambie Bwana Mungu wako: “Nimeondoa katika nyumba yangu ile sehemu iliyowekwa wakfu na nimempa Mlawi, mgeni, yatima na mjane, kulingana na yote uliyoamuru. Sijazihalifu amri zako wala kusahau hata mojawapo.
14 not to eat in/on/with evil: trouble my from him and not to burn: purge from him in/on/with unclean and not to give: give from him to/for to die to hear: obey in/on/with voice LORD God my to make: do like/as all which to command me
Sijala sehemu iliyowekwa wakfu wakati nilipokuwa nikiomboleza, wala sijaondoa mojawapo wakati nilipokuwa najisi, wala sijatoa sehemu yake yoyote kwa wafu. Nimemtii Bwana Mungu wangu; nimefanya kila kitu ulichoniamuru.
15 to look [emph?] from habitation holiness your from [the] heaven and to bless [obj] people your [obj] Israel and [obj] [the] land: soil which to give: give to/for us like/as as which to swear to/for father our land: country/planet to flow: flowing milk and honey
Angalia chini kutoka mbinguni, maskani yako matakatifu, uwabariki watu wako Israeli pamoja na nchi uliyotupa kama ulivyoahidi kwa kiapo kwa baba zetu, nchi inayotiririka maziwa na asali.”
16 [the] day: today [the] this LORD God your to command you to/for to make: do [obj] [the] statute: decree [the] these and [obj] [the] justice: judgement and to keep: careful and to make: do [obj] them in/on/with all heart your and in/on/with all soul your
Bwana Mungu wako anakuagiza leo kufuata amri hizi na sheria; zishike kwa bidii kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote.
17 [obj] LORD to say [the] day to/for to be to/for you to/for God and to/for to go: walk in/on/with way: conduct his and to/for to keep: obey statute: decree his and commandment his and justice: judgement his and to/for to hear: obey in/on/with voice his
Umetangaza leo kwamba Bwana ndiye Mungu wako na kwamba utafuata njia zake, kwamba utayashika maagizo yake, amri zake na sheria zake nawe utamtii.
18 and LORD to say you [the] day to/for to be to/for him to/for people possession like/as as which to speak: promise to/for you and to/for to keep: obey all commandment his
Naye Bwana ametangaza leo kwamba ninyi ni taifa lake, hazina yake ya thamani kama alivyoahidi, ili kwamba mpate kuyashika maagizo yake yote.
19 and to/for to give: put you high upon all [the] nation which to make to/for praise and to/for name and to/for beauty and to/for to be you people holy to/for LORD God your like/as as which to speak: promise
Ametangaza kwamba atawaweka juu kuliko mataifa mengine aliyoyafanya katika sifa, kuwa fahari na heshima, na kwamba mtakuwa taifa takatifu kwa Bwana Mungu wenu, kama alivyoahidi.

< Deuteronomy 26 >